< 1 Nyakati 6 >

1 Wana wa Levi walikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
The sons of Levi; Gershon, Kohath, and Merari.
2 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
And the sons of Kohath; Amram, Izhar, and Hebron, and Uzziel.
3 Wana wa Amramu walikuwa Aruni, Musa, Miriamu. Wana wa Aruni walikuwa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.
And the children of Amram; Aaron, and Moses, and Miriam. The sons also of Aaron; Nadab, and Abihu, Eleazar, and Ithamar.
4 Eleazari akawa baba wa Finehasi, na Finehasi akawa baba wa Abishua.
Eleazar brings forth Phinehas, Phinehas brings forth Abishua,
5 Abishua akawa baba wa Buki, na Buki akawa baba wa Uzi.
And Abishua brings forth Bukki, and Bukki brings forth Uzzi,
6 Uzi akawa baba wa Zerahia, na Zerahia akawa baba wa Meraioti.
And Uzzi brings forth Zerahiah, and Zerahiah brings forth Meraioth,
7 Meraioti akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
Meraioth brings forth Amariah, and Amariah brings forth Ahitub,
8 Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Ahimazi.
And Ahitub brings forth Zadok, and Zadok brings forth Ahimaaz,
9 Ahimazi akawa baba wa Azaria, na Azaria akawa baba wa Yohanani.
And Ahimaaz brings forth Azariah, and Azariah brings forth Johanan,
10 Yohanani akawa baba wa Azaria, aliye hudumu katika hekalu alilo lijenga Sulemani ndaniya Yerusalemu.
And Johanan brings forth Azariah, (he it is that executed the priest's office in the temple that Solomon built in Jerusalem: )
11 Azaria akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
And Azariah brings forth Amariah, and Amariah brings forth Ahitub,
12 Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Shalumu.
And Ahitub brings forth Zadok, and Zadok brings forth Shallum,
13 Shalumu akawa baba wa Hilikia, na Hilikia akawa baba wa Azaria.
And Shallum brings forth Hilkiah, and Hilkiah brings forth Azariah,
14 Azaria akawa baba Seraia, na Seraia akawa baba wa Yehozadaki.
And Azariah brings forth Seraiah, and Seraiah brings forth Jehozadak,
15 Yehozadaki akaenda matekani Yahweh alipo wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.
And Jehozadak went into captivity, when the LORD carried away Judah and Jerusalem by the hand of Nebuchadnezzar.
16 Wana wa Levi walikuwa Gerishomu, Kohathi, na Merari.
The sons of Levi; Gershom, Kohath, and Merari.
17 Wana wa Gerishomu walikuwa Libini na Shimei.
And these be the names of the sons of Gershom; Libni, and Shimei.
18 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
And the sons of Kohath were, Amram, and Izhar, and Hebron, and Uzziel.
19 Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Hawa walikuwa koo za Walawi kwa familia za baba zao.
The sons of Merari; Mahli, and Mushi. And these are the families of the Levites according to their fathers.
20 Uzao wa Gerishomu ulianza na mwanae Libini. Mwana wa Libini alikuwa Jahathi. Mwanae alikuwa Zima.
Of Gershom; Libni his son, Jahath his son, Zimmah his son,
21 Mwanae alikuwa Yoa. Mwanae alikuwa alikuwa Ido. Mwanae alikuwa Zera. Mwanae alikuwa Yeatherai.
Joah his son, Iddo his son, Zerah his son, Jeaterai his son.
22 Uzao wa Kohathi ulianza na mwanae Aminadabu. Mwanae alikuwa Kora. Mwanae alikuwa Asiri.
The sons of Kohath; Amminadab his son, Korah his son, Assir his son,
23 Mwanae alikuwa Elikana. Mwanae alikuwa Ebiasa. Mwanae alikuwa Asiri.
Elkanah his son, and Ebiasaph his son, and Assir his son,
24 Mwanae alikuwa Tahathi. Mwanae alikuwa Urieli. Mwanae alikuwa uzia. Mwanae alikuwa Shauli.
Tahath his son, Uriel his son, Uzziah his son, and Shaul his son.
25 Wana wa Elikana walikuwa Amasai, Ahimothi, na Elikana.
And the sons of Elkanah; Amasai, and Ahimoth.
26 Mwana wa huyu Elikana wa pili alikuwa Zofai. Mwanae alikuwa Nahathi.
As for Elkanah: the sons of Elkanah; Zophai his son, and Nahath his son,
27 Mwanae alikuwa Eliabu. Mwanae alikuwa Yehoramu. Mwanae alikuwa Elikana.
Eliab his son, Jeroham his son, Elkanah his son.
28 Wana wa Samwali walikuwa mzaliwa wa kwanza, Yoeli, na Abija, wa pili.
And the sons of Samuel; the firstborn Vashni, and Abiah.
29 Mwana wa Merari alikuwa Mahili. Mwanae alikuwa Libini.
The sons of Merari; Mahli, Libni his son, Shimei his son, Uzza his son,
30 Mwanae alikuwa Shimei. Mwanae alikuwa Uza. Mwanae alikuwa Shimea. Mwanae alikuwa Hagia. Mwana alikuwa Asaia.
Shimea his son, Haggiah his son, Asaiah his son.
31 Haya ndio majina ya wanaume ambao Daudi waliwaeka kusimamia muziki katika nyumba ya Yahweh, baada ya sanduku kuja hapo.
And these are they whom David set over the service of song in the house of the LORD, after that the ark had rest.
32 Walitumika kwa kuimba mbele ya hema, hema la kukutania, mpaka Sulemani alipo jenga nyumba ya Yahweh ndani ya Yerusalemu. Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa.
And they ministered before the dwelling place of the tabernacle of the congregation with singing, until Solomon had built the house of the LORD in Jerusalem: and then they waited on their office according to their order.
33 Hawa walitumika pamoja na wana wao. Katika makabila ya Wakohathi alitoka Hemani mwana muziki. Babu zake walikuwa hawa, kurudi nyuma ya wakati: Hemani alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Samweli.
And these are they that waited with their children. Of the sons of the Kohathites: Heman a singer, the son of Joel, the son of Shemuel,
34 Samweli alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Yerohamu. Yerohamu alikuwa mwana wa Elieli. Elieli alikuwa mwana wa Toa.
The son of Elkanah, the son of Jeroham, the son of Eliel, the son of Toah,
35 Toa alikuwa mwana wa Zufi. Zufi alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Mahathi. Mahathi alikuwa mwana wa Amasai. Amasai alikuwa mwana wa Elikana.
The son of Zuph, the son of Elkanah, the son of Mahath, the son of Amasai,
36 Elikana alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Azaria. Azaria alikuwa mwana wa Zefania.
The son of Elkanah, the son of Joel, the son of Azariah, the son of Zephaniah,
37 Zefania alikuwa mwana wa Tahathi. Tahathi alikuwa mwana wa Asiri. Asiri alikuwa mwana wa Ebiasa. Ebiasa alikuwa mwana wa Kora.
The son of Tahath, the son of Assir, the son of Ebiasaph, the son of Korah,
38 Kora alikuwa mwana wa Izhari. Izhari alikuwa mwana wa Kohathi. Kohathi alikuwa mwana wa Levi. Levi alikuwa mwana wa Israeli.
The son of Izhar, the son of Kohath, the son of Levi, the son of Israel.
39 Msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliye simama mkono wake wa kuume. Asafu alikuwa mwana Berekia. Berekia alikuwa mwana wa Shimea.
And his brother Asaph, who stood on his right hand, even Asaph the son of Berachiah, the son of Shimea,
40 Shimea alikuwa mwana Mikaeli. Mikaeli alikuwa mwana wa Baaseia. Baaseia alikuwa mwana wa Malikiya.
The son of Michael, the son of Baaseiah, the son of Malchiah,
41 Malikiya alikuwa mwana wa Ethini. Ethini alikuwa mwana wa Zera. Zera alikuwa mwana wa Adaia.
The son of Ethni, the son of Zerah, the son of Adaiah,
42 Adaia alikuwa mwana wa Ethani. Ethani alikuwa mwana wa Zima. Zima alikuwa mwana wa Shimei.
The son of Ethan, the son of Zimmah, the son of Shimei,
43 Shimei alikuwa mwana wa Yahathi. Yahathi alikuwa mwana wa Gerishomu. Gerishomu alikuwa mwana wa Levi.
The son of Jahath, the son of Gershom, the son of Levi.
44 Upande wa mkono wa koshoto wa Hemani walikuwa wasaidizi wake wana wa Merari. Alikuwa Ethani mwana wa Kishi. Kishi alikuwa mwana wa Abdi. Abdi alikuwa mwana wa Maluki.
And their brethren the sons of Merari stood on the left hand: Ethan the son of Kishi, the son of Abdi, the son of Malluch,
45 Maluki alikuwa mwana wa Hashabia. Hashabia alikuwa mwana wa Amazia. Amazia alikuwa mwana wa Hilikia.
The son of Hashabiah, the son of Amaziah, the son of Hilkiah,
46 Hilikia alikuwa mwana wa Amzi. Amzi alikuwa mwana wa Bani. Bani alikuwa mwana wa Shemeri.
The son of Amzi, the son of Bani, the son of Shamer,
47 Shemeri alikuwa mwana wa Mahili. Mahili alikuwa mwana wa Mushi. Mushi alikuwa mwana wa Merari. Merari alikuwa mwana wa Levi.
The son of Mahli, the son of Mushi, the son of Merari, the son of Levi.
48 Walawi, alipangiwa kufanya kazi zote za hema, nyumba ya Mungu.
Their brethren also the Levites were appointed unto all manner of service of the tabernacle of the house of God.
49 Aruni na wana wake walitoa sadaka katika madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketeza; na sadaka katika madhabahu ya uvumba kwa kazi zote katika pa patakatifu. Hizi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli, kwa kadiri ya yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu aliwaamuru.
But Aaron and his sons offered upon the altar of the burnt offering, and on the altar of incense, and were appointed for all the work of the place most holy, and to make an atonement for Israel, according to all that Moses the servant of God had commanded.
50 Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo: Mwana wa Aruni alikuwa Eleazari. Mwana Eleazari alikuwa Finehasi. Mwana wa Finehasi alikuwa Abishua.
And these are the sons of Aaron; Eleazar his son, Phinehas his son, Abishua his son,
51 Mwana wa Abishua alikuwa Buki. Mwana wa Buki alikuwa Uzi. Mwana wa Buki alikuwa Zerahia.
Bukki his son, Uzzi his son, Zerahiah his son,
52 Mwana wa Zerahia alikuwa Meraiothi. Mwana wa Meraiothi alikuwa Amaria. Mwana wa Amaria alikuwa Ahitubi.
Meraioth his son, Amariah his son, Ahitub his son,
53 Mwana wa Ahitubi alikuwa Zadoki. Mwana wa Zadoki alikuwa Ahimazi.
Zadok his son, Ahimaaz his son.
54 Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao).
Now these are their dwelling places throughout their castles in their coasts, of the sons of Aaron, of the families of the Kohathites: for theirs was the lot.
55 Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda na nchi ya malisho,
And they gave them Hebron in the land of Judah, and the suburbs thereof round about it.
56 lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
But the fields of the city, and the villages thereof, they gave to Caleb the son of Jephunneh.
57 Kwa wazao wa Aruni waliwapa: Hebroni ( mji wa makimblio), na Libina pamoja na nchi ya malisho, Yatiri, Eshitemoa pamoja na nchi ya malisho,
And to the sons of Aaron they gave the cities of Judah, namely, Hebron, the city of refuge, and Libnah with her suburbs, and Jattir, and Eshtemoa, with their suburbs,
58 Hileni pamoja na nchi ya malisho, na Debiri pamoja na nchi ya malisho.
And Hilen with her suburbs, Debir with her suburbs,
59 Waliwapa uzao wa Aruni: Ashani pamoja na nchi ya malisho na Bethi Shemeshi pamoja na nchi ya malisho;
And Ashan with her suburbs, and Bethshemesh with her suburbs:
60 na kutoka katika kabila la Benjamini walipewa Geba pamoja na nchi ya malisho, Alemethi pamoja na nchi ya malisho, na Anothothi na nchi ya malisho. Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu.
And out of the tribe of Benjamin; Geba with her suburbs, and Alemeth with her suburbs, and Anathoth with her suburbs. All their cities throughout their families were thirteen cities.
61 Uzao mwengine wa Kohathi waliwapa kwa sehemu miji kumi kutoka kwa kabila la Manase.
And unto the sons of Kohath, which were left of the family of that tribe, were cities given out of the half tribe, namely, out of the half tribe of Manasseh, by lot, ten cities.
62 Kwa uzao wa Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri, Naftali, na nusu ya kabila la Manase huko Bashani.
And to the sons of Gershom throughout their families out of the tribe of Issachar, and out of the tribe of Asher, and out of the tribe of Naphtali, and out of the tribe of Manasseh in Bashan, thirteen cities.
63 Kwa uzao wa Merari walipewa miji kumi, kulingana na koo zao, kutoka kwa makabila ya Rubeni, Gadi, na Zebuluni.
Unto the sons of Merari were given by lot, throughout their families, out of the tribe of Reuben, and out of the tribe of Gad, and out of the tribe of Zebulun, twelve cities.
64 Hivyo watu wa Israeli walitoa hii miji pamoja na nchi za malisho kwa Walawi.
And the children of Israel gave to the Levites these cities with their suburbs.
65 Walitoa kwa sehemu miji iliyo tajwa awali kutoka katika kabila la Yuda, Simeoni, na Benjamini.
And they gave by lot out of the tribe of the children of Judah, and out of the tribe of the children of Simeon, and out of the tribe of the children of Benjamin, these cities, which are called by their names.
66 Kwa baadhi ya koo za Wakohathi walitoa miji kutoka kwa kabila la Efraimu.
And the residue of the families of the sons of Kohath had cities of their coasts out of the tribe of Ephraim.
67 Waliwapa: Shekemu ( mji wa makimbilio) pamoja na nchi ya malisho katika milima ya Efraimu, Gezeri na nchi ya malisho,
And they gave unto them, of the cities of refuge, Shechem in mount Ephraim with her suburbs; they gave also Gezer with her suburbs,
68 Jokimeamu pamoja na nchi ya malisho, Bethi Horoni pamoja na nchi ya malisho,
And Jokmeam with her suburbs, and Bethhoron with her suburbs,
69 Aiyaloni pamoja na nchi ya malisho, na Gathi Rimoni pamoja na nchi ya malisho.
And Aijalon with her suburbs, and Gathrimmon with her suburbs:
70 Nusu ya kabila la Manase waliwapa Wakohathi: Aneri pamoja na nchi ya malisho na Bileamu pamoja na nchi ya malisho. Hizi zikawa mali za koo za Wakohathi.
And out of the half tribe of Manasseh; Aner with her suburbs, and Bileam with her suburbs, for the family of the remnant of the sons of Kohath.
71 Kwa uzao wa Gerishomu kutoka koo za nusu ya kabila la Manase, waliwapa: Golani huko Baashani na nchi ya malisho na Ashitarothi pamoja na nchi ya malisho.
Unto the sons of Gershom were given out of the family of the half tribe of Manasseh, Golan in Bashan with her suburbs, and Ashtaroth with her suburbs:
72 Kabila la Isakari liliwapa uzao wa Gerishomu: Kedeshi pamoja na nchi ya malisho, Dabera pamoja na nchi ya malisho,
And out of the tribe of Issachar; Kedesh with her suburbs, Daberath with her suburbs,
73 Ramothi pamoja na nchi ya malisho, na Anemu pamoja na nchi ya malisho.
And Ramoth with her suburbs, and Anem with her suburbs:
74 Isakari alipokea kutoka kwa kabila la Asheri: Mashali pamoja na nchi ya malisho, Abdoni pamoja na nchi ya malisho,
And out of the tribe of Asher; Mashal with her suburbs, and Abdon with her suburbs,
75 Hukoki pamoja na nchi ya malisho, na Rehobu pamoja na nchi ya malisho.
And Hukok with her suburbs, and Rehob with her suburbs:
76 Walipokea kutoka kabila la Naftali: Kedeshi iliyo Galileya pamoja na nchi ya malisho, Hamoni pamoja na nchi ya malisho, na Kiriathaimu pamoja na nchi ya malisho.
And out of the tribe of Naphtali; Kedesh in Galilee with her suburbs, and Hammon with her suburbs, and Kirjathaim with her suburbs.
77 Kwa Walawi wengine, uzao wa Merari, walipewa kutoka kabila la Zebuluni: Rimono pamoja na nchi ya malisho na Tabori pamoja na nchi ya malisho.
Unto the rest of the children of Merari were given out of the tribe of Zebulun, Rimmon with her suburbs, Tabor with her suburbs:
78 Kwa wao pia walipewa, upande wa pili wa Yordani huko Yeriko, kwa upande wa mashariki mwa mto: Bezeri katika jangwa pamoja na nchi ya malisho, Yahzahi pamoja na nchi ya malisho,
And on the other side Jordan by Jericho, on the east side of Jordan, were given them out of the tribe of Reuben, Bezer in the wilderness with her suburbs, and Jahzah with her suburbs,
79 Kedemothi pamoka na nchi ya malisho, ma Mefathi pamoja na nchi ya malisho. Hizi zilitolewa kutoka kabila la Rubeni.
Kedemoth also with her suburbs, and Mephaath with her suburbs:
80 Walawi walipokea kutoka kabila la Gadi: Ramothi ya Gileadi pamoja na nchi ya malisho, Mahanaimu pamoja na nchi ya malisho,
And out of the tribe of Gad; Ramoth in Gilead with her suburbs, and Mahanaim with her suburbs,
81 Heshiboni pamoja na nchi ya malisho, na Yazeri pamoja na nchi ya malisho.
And Heshbon with her suburbs, and Jazer with her suburbs.

< 1 Nyakati 6 >