< 1 Nyakati 6 >
1 Wana wa Levi walikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
The sons of Levi were Gerson, Caath, and Merari.
2 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
The sons of Caath: Amram, Isaar, Hebron, and Oziel.
3 Wana wa Amramu walikuwa Aruni, Musa, Miriamu. Wana wa Aruni walikuwa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.
The children of Amram: Aaron, Moses, and Mary. The sons of Aaron: Nadab and Abiu, Eleazar and Ithamar.
4 Eleazari akawa baba wa Finehasi, na Finehasi akawa baba wa Abishua.
Eleazar beget Phinees, and Phinees beget Abisue,
5 Abishua akawa baba wa Buki, na Buki akawa baba wa Uzi.
And Abisue beget Bocci, and Bocci begot Ozi.
6 Uzi akawa baba wa Zerahia, na Zerahia akawa baba wa Meraioti.
Ozi beget Zaraias, and Zaraias beget Maraioth.
7 Meraioti akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
And Maraioth beget Amarias, and Amarias beget Achitob.
8 Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Ahimazi.
Achitob beget Sadoc, and Sadoc begot Achimaas.
9 Ahimazi akawa baba wa Azaria, na Azaria akawa baba wa Yohanani.
Achimaas beget Azarias, Azarias begot Johanan,
10 Yohanani akawa baba wa Azaria, aliye hudumu katika hekalu alilo lijenga Sulemani ndaniya Yerusalemu.
Johanan beget Azarias. This is he that executed the priestly office in the house which Solomon built in Jerusalem.
11 Azaria akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
And Azarias beget Amarias, and Amarias beget Achitob.
12 Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Shalumu.
And Achitob beget Sadoc, and Sadoc beget Sellum,
13 Shalumu akawa baba wa Hilikia, na Hilikia akawa baba wa Azaria.
Sellum beget Helcias, and Helcias beget Azarias,
14 Azaria akawa baba Seraia, na Seraia akawa baba wa Yehozadaki.
Azarias beget Saraias, and Saraias beget Josedec.
15 Yehozadaki akaenda matekani Yahweh alipo wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.
Now Josedec went out, when the Lord carried away Juda, and Jerusalem, by the hands of Nabuchodonosor.
16 Wana wa Levi walikuwa Gerishomu, Kohathi, na Merari.
So the sons of Levi were Gerson, Caath, and Merari.
17 Wana wa Gerishomu walikuwa Libini na Shimei.
And these are the names of the sons of Gerson: Lobni and Semei.
18 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
The sons of Caath: Amram, and Isaar, and Hebron, and Oziel.
19 Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Hawa walikuwa koo za Walawi kwa familia za baba zao.
The sons of Merari: Moholi and Musi. And these are the kindreds of Levi according to their families.
20 Uzao wa Gerishomu ulianza na mwanae Libini. Mwana wa Libini alikuwa Jahathi. Mwanae alikuwa Zima.
Of Gerson: Lobni his son, Jahath his son, Zamma his son,
21 Mwanae alikuwa Yoa. Mwanae alikuwa alikuwa Ido. Mwanae alikuwa Zera. Mwanae alikuwa Yeatherai.
Joah his son, Addo his son, Zara his son, Jethrai his son.
22 Uzao wa Kohathi ulianza na mwanae Aminadabu. Mwanae alikuwa Kora. Mwanae alikuwa Asiri.
The sons of Caath, Aminadab his son, Core his son, Asir his son,
23 Mwanae alikuwa Elikana. Mwanae alikuwa Ebiasa. Mwanae alikuwa Asiri.
Elcana his son, Abiasaph his son, Asir his son,
24 Mwanae alikuwa Tahathi. Mwanae alikuwa Urieli. Mwanae alikuwa uzia. Mwanae alikuwa Shauli.
Thahath his son, Uriel his son, Ozias his son, Saul his son.
25 Wana wa Elikana walikuwa Amasai, Ahimothi, na Elikana.
The sons of Elcana: Amasai, and Achimoth.
26 Mwana wa huyu Elikana wa pili alikuwa Zofai. Mwanae alikuwa Nahathi.
And Elcana. The sons of Elcana: Sophai his son, Nahath his son,
27 Mwanae alikuwa Eliabu. Mwanae alikuwa Yehoramu. Mwanae alikuwa Elikana.
Eliab his son, Jeroham his son, Elcana his son.
28 Wana wa Samwali walikuwa mzaliwa wa kwanza, Yoeli, na Abija, wa pili.
The sons of Samuel: the firstborn Vasseni, and Abia.
29 Mwana wa Merari alikuwa Mahili. Mwanae alikuwa Libini.
And the sons of Merari, Moholi: Lobni his son, Semei his son, Oza his son,
30 Mwanae alikuwa Shimei. Mwanae alikuwa Uza. Mwanae alikuwa Shimea. Mwanae alikuwa Hagia. Mwana alikuwa Asaia.
Sammaa his son, Haggia his son, Asaia his son.
31 Haya ndio majina ya wanaume ambao Daudi waliwaeka kusimamia muziki katika nyumba ya Yahweh, baada ya sanduku kuja hapo.
These are they, whom David set over the singing men of the house of the Lord, after that the ark was placed:
32 Walitumika kwa kuimba mbele ya hema, hema la kukutania, mpaka Sulemani alipo jenga nyumba ya Yahweh ndani ya Yerusalemu. Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa.
And they ministered before the tabernacle of the testimony, with singing, until Solomon built the house of the Lord in Jerusalem, and they stood according to their order in the ministry.
33 Hawa walitumika pamoja na wana wao. Katika makabila ya Wakohathi alitoka Hemani mwana muziki. Babu zake walikuwa hawa, kurudi nyuma ya wakati: Hemani alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Samweli.
And these are they that stood with their sons, of the sons of Caath, Hemam a singer, the son of Joel, the son of Sammuel,
34 Samweli alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Yerohamu. Yerohamu alikuwa mwana wa Elieli. Elieli alikuwa mwana wa Toa.
The son of Elcana, the son of Jeroham, the son of Eliel, the son of Thohu,
35 Toa alikuwa mwana wa Zufi. Zufi alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Mahathi. Mahathi alikuwa mwana wa Amasai. Amasai alikuwa mwana wa Elikana.
The son of Suph, the son of Elcana, the son of Mahath, the son of Amasai,
36 Elikana alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Azaria. Azaria alikuwa mwana wa Zefania.
The son of Elcana, the son of Johel, the son of Azarias, the son of Sophonias,
37 Zefania alikuwa mwana wa Tahathi. Tahathi alikuwa mwana wa Asiri. Asiri alikuwa mwana wa Ebiasa. Ebiasa alikuwa mwana wa Kora.
The son of Thahath, the son of Asir, the son or Abiasaph, the son of Core,
38 Kora alikuwa mwana wa Izhari. Izhari alikuwa mwana wa Kohathi. Kohathi alikuwa mwana wa Levi. Levi alikuwa mwana wa Israeli.
The son of Isaar, the son of Caath, the son of Levi, the son of Israel.
39 Msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliye simama mkono wake wa kuume. Asafu alikuwa mwana Berekia. Berekia alikuwa mwana wa Shimea.
And his brother Asaph, who stood on his right hand, Asaph the son of Barachias, the son of Samaa.
40 Shimea alikuwa mwana Mikaeli. Mikaeli alikuwa mwana wa Baaseia. Baaseia alikuwa mwana wa Malikiya.
The son of Michael, the son of Basaia, the son of Melchia.
41 Malikiya alikuwa mwana wa Ethini. Ethini alikuwa mwana wa Zera. Zera alikuwa mwana wa Adaia.
The son of Athanai, the son of Zara, the son of Adaia.
42 Adaia alikuwa mwana wa Ethani. Ethani alikuwa mwana wa Zima. Zima alikuwa mwana wa Shimei.
The son of Ethan, the son of Zamma, the son of Semei.
43 Shimei alikuwa mwana wa Yahathi. Yahathi alikuwa mwana wa Gerishomu. Gerishomu alikuwa mwana wa Levi.
The son of Jeth, the son of Gerson, the son of Levi.
44 Upande wa mkono wa koshoto wa Hemani walikuwa wasaidizi wake wana wa Merari. Alikuwa Ethani mwana wa Kishi. Kishi alikuwa mwana wa Abdi. Abdi alikuwa mwana wa Maluki.
And the sons of Merari their brethren, on the left hand, Ethan the son of Cusi, the son of Abdi, the son of Meloch,
45 Maluki alikuwa mwana wa Hashabia. Hashabia alikuwa mwana wa Amazia. Amazia alikuwa mwana wa Hilikia.
The son of Hasabia, the son of Amasai, the son of Helcias,
46 Hilikia alikuwa mwana wa Amzi. Amzi alikuwa mwana wa Bani. Bani alikuwa mwana wa Shemeri.
The son of Amasai, the son of Boni, the son of Somer,
47 Shemeri alikuwa mwana wa Mahili. Mahili alikuwa mwana wa Mushi. Mushi alikuwa mwana wa Merari. Merari alikuwa mwana wa Levi.
The son of Moholi, the son of Mud, the son of Merari, the son of Levi.
48 Walawi, alipangiwa kufanya kazi zote za hema, nyumba ya Mungu.
Their brethren also the Levites, who were appointed for all the ministry of the tabernacle of the house of the Lord.
49 Aruni na wana wake walitoa sadaka katika madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketeza; na sadaka katika madhabahu ya uvumba kwa kazi zote katika pa patakatifu. Hizi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli, kwa kadiri ya yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu aliwaamuru.
But Aaron and his sons offered burnt offerings upon the altar of holocausts, and upon the altar of incense, for very work of the holy of holies: and to pray for Israel according to all that Moses the servant of God had commanded.
50 Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo: Mwana wa Aruni alikuwa Eleazari. Mwana Eleazari alikuwa Finehasi. Mwana wa Finehasi alikuwa Abishua.
And these are the sons of Aaron: Eleazar his son, Phinees his son, Abisue his son,
51 Mwana wa Abishua alikuwa Buki. Mwana wa Buki alikuwa Uzi. Mwana wa Buki alikuwa Zerahia.
Bocci his son, Ozi his son, Zarahia his son,
52 Mwana wa Zerahia alikuwa Meraiothi. Mwana wa Meraiothi alikuwa Amaria. Mwana wa Amaria alikuwa Ahitubi.
Meraioth his son, Amarias his son, Achitob his son,
53 Mwana wa Ahitubi alikuwa Zadoki. Mwana wa Zadoki alikuwa Ahimazi.
Sadoc his son, Achimaas his son.
54 Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao).
And these are their dwelling places by the towns and confines, to wit, of the sons of Aaron, of the families of the Caathites: for they fell to them by lot.
55 Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda na nchi ya malisho,
And they gave them Hebron in the land of Juda, and the suburbs thereof round about:
56 lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
But the fields of the city, and the villages to Caleb son of Jephone.
57 Kwa wazao wa Aruni waliwapa: Hebroni ( mji wa makimblio), na Libina pamoja na nchi ya malisho, Yatiri, Eshitemoa pamoja na nchi ya malisho,
And to the sons of Aaron they gave the cities for refuge Hebron, and Lobna, and the suburbs thereof,
58 Hileni pamoja na nchi ya malisho, na Debiri pamoja na nchi ya malisho.
And Jether and Esthemo, with their suburbs, and Helon, and Dabir with their suburbs:
59 Waliwapa uzao wa Aruni: Ashani pamoja na nchi ya malisho na Bethi Shemeshi pamoja na nchi ya malisho;
Asan also, and Bethsames, with their suburbs.
60 na kutoka katika kabila la Benjamini walipewa Geba pamoja na nchi ya malisho, Alemethi pamoja na nchi ya malisho, na Anothothi na nchi ya malisho. Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu.
And out of the tribe of Benjamin: Gabee and its suburbs, Almath with its suburbs, Anathoth also with its suburbs: all their cities throughout their families were thirteen.
61 Uzao mwengine wa Kohathi waliwapa kwa sehemu miji kumi kutoka kwa kabila la Manase.
And to the sons of Caath that remained of their kindred they gave out of the half tribe of Manasses ten cities in possession.
62 Kwa uzao wa Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri, Naftali, na nusu ya kabila la Manase huko Bashani.
And to the sons of Gerson by their families out of the tribe of Issachar, and out of the tribe of Aser, and out of the tribe of Nephtali, and out of the tribe of Manasses in Basan, thirteen cities.
63 Kwa uzao wa Merari walipewa miji kumi, kulingana na koo zao, kutoka kwa makabila ya Rubeni, Gadi, na Zebuluni.
And to the sons of Merari by their families out of the tribe of Ruben, and out of the tribe of Gad, and out of the tribe of Zabulon, they gave by lot twelve cities.
64 Hivyo watu wa Israeli walitoa hii miji pamoja na nchi za malisho kwa Walawi.
And the children of Israel gave to the Levites the cities, and their suburbs.
65 Walitoa kwa sehemu miji iliyo tajwa awali kutoka katika kabila la Yuda, Simeoni, na Benjamini.
And they gave them by lot, out of the tribe of the sons of Juda, and out of the tribe of the sons of Simeon, and out of the tribe of the sons of Benjamin, these cities which they called by their names.
66 Kwa baadhi ya koo za Wakohathi walitoa miji kutoka kwa kabila la Efraimu.
And to them that were of the kindred of the sons of Caath, and the cities in their borders were of the tribe of Ephraim.
67 Waliwapa: Shekemu ( mji wa makimbilio) pamoja na nchi ya malisho katika milima ya Efraimu, Gezeri na nchi ya malisho,
And they gave the cities of refuge Sichem with its suburbs in mount Ephraim, and Gazer with its suburbs,
68 Jokimeamu pamoja na nchi ya malisho, Bethi Horoni pamoja na nchi ya malisho,
Jecmaan also with its suburbs, and Beth-horon in like manner,
69 Aiyaloni pamoja na nchi ya malisho, na Gathi Rimoni pamoja na nchi ya malisho.
Helon also with its suburbs, and Gethremmon in like manner,
70 Nusu ya kabila la Manase waliwapa Wakohathi: Aneri pamoja na nchi ya malisho na Bileamu pamoja na nchi ya malisho. Hizi zikawa mali za koo za Wakohathi.
And out of the half tribe of Manasses, Aner and its suburbs, Baalam and its suburbs: to wit, to them that were left of the family of the sons of Caath.
71 Kwa uzao wa Gerishomu kutoka koo za nusu ya kabila la Manase, waliwapa: Golani huko Baashani na nchi ya malisho na Ashitarothi pamoja na nchi ya malisho.
And to the sons of Gersom, out of the kindred of the half tribe of Manasses, Gaulon, in Basan, and its suburbs, and Astharoth with its suburbs.
72 Kabila la Isakari liliwapa uzao wa Gerishomu: Kedeshi pamoja na nchi ya malisho, Dabera pamoja na nchi ya malisho,
Out of the tribe of Issachar, Cedes and its suburbs, and Dabereth with its suburbs;
73 Ramothi pamoja na nchi ya malisho, na Anemu pamoja na nchi ya malisho.
Ramoth also and its suburbs, and Anem with its suburbs.
74 Isakari alipokea kutoka kwa kabila la Asheri: Mashali pamoja na nchi ya malisho, Abdoni pamoja na nchi ya malisho,
And out of the tribe of Aser: Masal with its suburbs, and Abdon in like manner;
75 Hukoki pamoja na nchi ya malisho, na Rehobu pamoja na nchi ya malisho.
Hucac also and its suburbs, and Rohol with its suburbs.
76 Walipokea kutoka kabila la Naftali: Kedeshi iliyo Galileya pamoja na nchi ya malisho, Hamoni pamoja na nchi ya malisho, na Kiriathaimu pamoja na nchi ya malisho.
And out of the tribe of Nephtali, Cedes in Galilee and its suburbs, Hamon with its suburbs, and Cariathaim, and its suburbs.
77 Kwa Walawi wengine, uzao wa Merari, walipewa kutoka kabila la Zebuluni: Rimono pamoja na nchi ya malisho na Tabori pamoja na nchi ya malisho.
And to the sons of Merari that remained: out of the tribe of Zabulon, Remmono and its suburbs, and Thabor with its suburbs.
78 Kwa wao pia walipewa, upande wa pili wa Yordani huko Yeriko, kwa upande wa mashariki mwa mto: Bezeri katika jangwa pamoja na nchi ya malisho, Yahzahi pamoja na nchi ya malisho,
Beyond the Jordan also over against Jericho, on the east side of the Jordan, out of the tribe of Ruben, Bosor in the wilderness with its suburbs, and Jassa with its suburbs;
79 Kedemothi pamoka na nchi ya malisho, ma Mefathi pamoja na nchi ya malisho. Hizi zilitolewa kutoka kabila la Rubeni.
Cademoth also and its suburbs, and Mephaath with its suburbs;
80 Walawi walipokea kutoka kabila la Gadi: Ramothi ya Gileadi pamoja na nchi ya malisho, Mahanaimu pamoja na nchi ya malisho,
Moreover also out of the tribe of Gad, Ramoth in Galaad and its suburbs, and Manaim with its suburbs;
81 Heshiboni pamoja na nchi ya malisho, na Yazeri pamoja na nchi ya malisho.
Hesebon also with its suburbs, and Jazer with its suburbs.