< 1 Nyakati 6 >
1 Wana wa Levi walikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
The sons of Levi: Gershon, Kohath, and Merari.
2 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
The sons of Kohath: Amram, Izhar, Hebron, and Uzziel.
3 Wana wa Amramu walikuwa Aruni, Musa, Miriamu. Wana wa Aruni walikuwa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.
The children of Amram: Aaron, Moses, and Miriam. The sons of Aaron: Nadab, Abihu, Eleazar, and Ithamar.
4 Eleazari akawa baba wa Finehasi, na Finehasi akawa baba wa Abishua.
Eleazar was the father of Phinehas, Phinehas was the father of Abishua,
5 Abishua akawa baba wa Buki, na Buki akawa baba wa Uzi.
Abishua was the father of Bukki, Bukki was the father of Uzzi,
6 Uzi akawa baba wa Zerahia, na Zerahia akawa baba wa Meraioti.
Uzzi was the father of Zerahiah, Zerahiah was the father of Meraioth,
7 Meraioti akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
Meraioth was the father of Amariah, Amariah was the father of Ahitub,
8 Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Ahimazi.
Ahitub was the father of Zadok, Zadok was the father of Ahimaaz,
9 Ahimazi akawa baba wa Azaria, na Azaria akawa baba wa Yohanani.
Ahimaaz was the father of Azariah, Azariah was the father of Johanan,
10 Yohanani akawa baba wa Azaria, aliye hudumu katika hekalu alilo lijenga Sulemani ndaniya Yerusalemu.
Johanan was the father of Azariah, who served as priest in the temple that Solomon built in Jerusalem,
11 Azaria akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
Azariah was the father of Amariah, Amariah was the father of Ahitub,
12 Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Shalumu.
Ahitub was the father of Zadok, Zadok was the father of Shallum,
13 Shalumu akawa baba wa Hilikia, na Hilikia akawa baba wa Azaria.
Shallum was the father of Hilkiah, Hilkiah was the father of Azariah,
14 Azaria akawa baba Seraia, na Seraia akawa baba wa Yehozadaki.
Azariah was the father of Seraiah, and Seraiah was the father of Jehozadak.
15 Yehozadaki akaenda matekani Yahweh alipo wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.
Jehozadak went into captivity when the LORD sent Judah and Jerusalem into exile by the hand of Nebuchadnezzar.
16 Wana wa Levi walikuwa Gerishomu, Kohathi, na Merari.
The sons of Levi: Gershom, Kohath, and Merari.
17 Wana wa Gerishomu walikuwa Libini na Shimei.
These are the names of the sons of Gershom: Libni and Shimei.
18 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
The sons of Kohath: Amram, Izhar, Hebron, and Uzziel.
19 Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Hawa walikuwa koo za Walawi kwa familia za baba zao.
The sons of Merari: Mahli and Mushi. These are the clans of the Levites listed according to their fathers:
20 Uzao wa Gerishomu ulianza na mwanae Libini. Mwana wa Libini alikuwa Jahathi. Mwanae alikuwa Zima.
Of Gershom: Libni his son, Jahath his son, Zimmah his son,
21 Mwanae alikuwa Yoa. Mwanae alikuwa alikuwa Ido. Mwanae alikuwa Zera. Mwanae alikuwa Yeatherai.
Joah his son, Iddo his son, Zerah his son, and Jeatherai his son.
22 Uzao wa Kohathi ulianza na mwanae Aminadabu. Mwanae alikuwa Kora. Mwanae alikuwa Asiri.
The descendants of Kohath: Amminadab his son, Korah his son, Assir his son,
23 Mwanae alikuwa Elikana. Mwanae alikuwa Ebiasa. Mwanae alikuwa Asiri.
Elkanah his son, Ebiasaph his son, Assir his son,
24 Mwanae alikuwa Tahathi. Mwanae alikuwa Urieli. Mwanae alikuwa uzia. Mwanae alikuwa Shauli.
Tahath his son, Uriel his son, Uzziah his son, and Shaul his son.
25 Wana wa Elikana walikuwa Amasai, Ahimothi, na Elikana.
The descendants of Elkanah: Amasai, Ahimoth,
26 Mwana wa huyu Elikana wa pili alikuwa Zofai. Mwanae alikuwa Nahathi.
Elkanah his son, Zophai his son, Nahath his son,
27 Mwanae alikuwa Eliabu. Mwanae alikuwa Yehoramu. Mwanae alikuwa Elikana.
Eliab his son, Jeroham his son, and Elkanah his son.
28 Wana wa Samwali walikuwa mzaliwa wa kwanza, Yoeli, na Abija, wa pili.
The sons of Samuel: Joel his firstborn and Abijah his second son.
29 Mwana wa Merari alikuwa Mahili. Mwanae alikuwa Libini.
The descendants of Merari: Mahli, Libni his son, Shimei his son, Uzzah his son,
30 Mwanae alikuwa Shimei. Mwanae alikuwa Uza. Mwanae alikuwa Shimea. Mwanae alikuwa Hagia. Mwana alikuwa Asaia.
Shimea his son, Haggiah his son, and Asaiah his son.
31 Haya ndio majina ya wanaume ambao Daudi waliwaeka kusimamia muziki katika nyumba ya Yahweh, baada ya sanduku kuja hapo.
These are the men David put in charge of the music in the house of the LORD after the ark rested there.
32 Walitumika kwa kuimba mbele ya hema, hema la kukutania, mpaka Sulemani alipo jenga nyumba ya Yahweh ndani ya Yerusalemu. Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa.
They ministered with song before the tabernacle, the Tent of Meeting, until Solomon built the house of the LORD in Jerusalem. And they performed their duties according to the regulations given them.
33 Hawa walitumika pamoja na wana wao. Katika makabila ya Wakohathi alitoka Hemani mwana muziki. Babu zake walikuwa hawa, kurudi nyuma ya wakati: Hemani alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Samweli.
These are the men who served, together with their sons. From the Kohathites: Heman the singer, the son of Joel, the son of Samuel,
34 Samweli alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Yerohamu. Yerohamu alikuwa mwana wa Elieli. Elieli alikuwa mwana wa Toa.
the son of Elkanah, the son of Jeroham, the son of Eliel, the son of Toah,
35 Toa alikuwa mwana wa Zufi. Zufi alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Mahathi. Mahathi alikuwa mwana wa Amasai. Amasai alikuwa mwana wa Elikana.
the son of Zuph, the son of Elkanah, the son of Mahath, the son of Amasai,
36 Elikana alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Azaria. Azaria alikuwa mwana wa Zefania.
the son of Elkanah, the son of Joel, the son of Azariah, the son of Zephaniah,
37 Zefania alikuwa mwana wa Tahathi. Tahathi alikuwa mwana wa Asiri. Asiri alikuwa mwana wa Ebiasa. Ebiasa alikuwa mwana wa Kora.
the son of Tahath, the son of Assir, the son of Ebiasaph, the son of Korah,
38 Kora alikuwa mwana wa Izhari. Izhari alikuwa mwana wa Kohathi. Kohathi alikuwa mwana wa Levi. Levi alikuwa mwana wa Israeli.
the son of Izhar, the son of Kohath, the son of Levi, the son of Israel.
39 Msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliye simama mkono wake wa kuume. Asafu alikuwa mwana Berekia. Berekia alikuwa mwana wa Shimea.
Heman’s kinsman was Asaph, who served at his right hand: Asaph the son of Berechiah, the son of Shimea,
40 Shimea alikuwa mwana Mikaeli. Mikaeli alikuwa mwana wa Baaseia. Baaseia alikuwa mwana wa Malikiya.
the son of Michael, the son of Baaseiah, the son of Malchijah,
41 Malikiya alikuwa mwana wa Ethini. Ethini alikuwa mwana wa Zera. Zera alikuwa mwana wa Adaia.
the son of Ethni, the son of Zerah, the son of Adaiah,
42 Adaia alikuwa mwana wa Ethani. Ethani alikuwa mwana wa Zima. Zima alikuwa mwana wa Shimei.
the son of Ethan, the son of Zimmah, the son of Shimei,
43 Shimei alikuwa mwana wa Yahathi. Yahathi alikuwa mwana wa Gerishomu. Gerishomu alikuwa mwana wa Levi.
the son of Jahath, the son of Gershom, the son of Levi.
44 Upande wa mkono wa koshoto wa Hemani walikuwa wasaidizi wake wana wa Merari. Alikuwa Ethani mwana wa Kishi. Kishi alikuwa mwana wa Abdi. Abdi alikuwa mwana wa Maluki.
On the left were their kinsmen, the sons of Merari: Ethan the son of Kishi, the son of Abdi, the son of Malluch,
45 Maluki alikuwa mwana wa Hashabia. Hashabia alikuwa mwana wa Amazia. Amazia alikuwa mwana wa Hilikia.
the son of Hashabiah, the son of Amaziah, the son of Hilkiah,
46 Hilikia alikuwa mwana wa Amzi. Amzi alikuwa mwana wa Bani. Bani alikuwa mwana wa Shemeri.
the son of Amzi, the son of Bani, the son of Shemer,
47 Shemeri alikuwa mwana wa Mahili. Mahili alikuwa mwana wa Mushi. Mushi alikuwa mwana wa Merari. Merari alikuwa mwana wa Levi.
the son of Mahli, the son of Mushi, the son of Merari, the son of Levi.
48 Walawi, alipangiwa kufanya kazi zote za hema, nyumba ya Mungu.
Their fellow Levites were assigned to every kind of service of the tabernacle, the house of God.
49 Aruni na wana wake walitoa sadaka katika madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketeza; na sadaka katika madhabahu ya uvumba kwa kazi zote katika pa patakatifu. Hizi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli, kwa kadiri ya yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu aliwaamuru.
But Aaron and his sons did all the work of the Most Holy Place. They presented the offerings on the altar of burnt offering and on the altar of incense to make atonement for Israel, according to all that Moses the servant of God had commanded.
50 Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo: Mwana wa Aruni alikuwa Eleazari. Mwana Eleazari alikuwa Finehasi. Mwana wa Finehasi alikuwa Abishua.
These were the descendants of Aaron: Eleazar his son, Phinehas his son, Abishua his son,
51 Mwana wa Abishua alikuwa Buki. Mwana wa Buki alikuwa Uzi. Mwana wa Buki alikuwa Zerahia.
Bukki his son, Uzzi his son, Zerahiah his son,
52 Mwana wa Zerahia alikuwa Meraiothi. Mwana wa Meraiothi alikuwa Amaria. Mwana wa Amaria alikuwa Ahitubi.
Meraioth his son, Amariah his son, Ahitub his son,
53 Mwana wa Ahitubi alikuwa Zadoki. Mwana wa Zadoki alikuwa Ahimazi.
Zadok his son, and Ahimaaz his son.
54 Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao).
Now these were the territories assigned to the descendants of Aaron from the Kohathite clan for their settlements, because the first lot fell to them:
55 Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda na nchi ya malisho,
They were given Hebron in the land of Judah and its surrounding pasturelands.
56 lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
But the fields and villages around the city were given to Caleb son of Jephunneh.
57 Kwa wazao wa Aruni waliwapa: Hebroni ( mji wa makimblio), na Libina pamoja na nchi ya malisho, Yatiri, Eshitemoa pamoja na nchi ya malisho,
So the descendants of Aaron were given Hebron (a city of refuge), Libnah, Jattir, Eshtemoa,
58 Hileni pamoja na nchi ya malisho, na Debiri pamoja na nchi ya malisho.
Hilen, Debir,
59 Waliwapa uzao wa Aruni: Ashani pamoja na nchi ya malisho na Bethi Shemeshi pamoja na nchi ya malisho;
Ashan, Juttah, and Beth-shemesh, together with their pasturelands.
60 na kutoka katika kabila la Benjamini walipewa Geba pamoja na nchi ya malisho, Alemethi pamoja na nchi ya malisho, na Anothothi na nchi ya malisho. Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu.
And from the tribe of Benjamin they were given Gibeon, Geba, Alemeth, and Anathoth, together with their pasturelands. So they had thirteen cities in all among their families.
61 Uzao mwengine wa Kohathi waliwapa kwa sehemu miji kumi kutoka kwa kabila la Manase.
To the rest of the Kohathites, ten cities were allotted from the half-tribe of Manasseh.
62 Kwa uzao wa Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri, Naftali, na nusu ya kabila la Manase huko Bashani.
The Gershomites, according to their clans, were allotted thirteen cities from the tribes of Issachar, Asher, Naphtali, and Manasseh in Bashan.
63 Kwa uzao wa Merari walipewa miji kumi, kulingana na koo zao, kutoka kwa makabila ya Rubeni, Gadi, na Zebuluni.
The Merarites, according to their families, were allotted twelve cities from the tribes of Reuben, Gad, and Zebulun.
64 Hivyo watu wa Israeli walitoa hii miji pamoja na nchi za malisho kwa Walawi.
So the Israelites gave to the Levites these cities and their pasturelands.
65 Walitoa kwa sehemu miji iliyo tajwa awali kutoka katika kabila la Yuda, Simeoni, na Benjamini.
They assigned by lot the cities named above from the tribes of Judah, Simeon, and Benjamin.
66 Kwa baadhi ya koo za Wakohathi walitoa miji kutoka kwa kabila la Efraimu.
And some of the clans of the Kohathites were given cities from the tribe of Ephraim for their territory:
67 Waliwapa: Shekemu ( mji wa makimbilio) pamoja na nchi ya malisho katika milima ya Efraimu, Gezeri na nchi ya malisho,
They were given Shechem (a city of refuge) with its pasturelands in the hill country of Ephraim, and Gezer,
68 Jokimeamu pamoja na nchi ya malisho, Bethi Horoni pamoja na nchi ya malisho,
Jokmeam, Beth-horon,
69 Aiyaloni pamoja na nchi ya malisho, na Gathi Rimoni pamoja na nchi ya malisho.
Aijalon, and Gath-rimmon, together with their pasturelands.
70 Nusu ya kabila la Manase waliwapa Wakohathi: Aneri pamoja na nchi ya malisho na Bileamu pamoja na nchi ya malisho. Hizi zikawa mali za koo za Wakohathi.
And from the half-tribe of Manasseh the remaining clans of the Kohathites were given Aner and Bileam, together with their pasturelands.
71 Kwa uzao wa Gerishomu kutoka koo za nusu ya kabila la Manase, waliwapa: Golani huko Baashani na nchi ya malisho na Ashitarothi pamoja na nchi ya malisho.
The Gershomites received the following: From the clan of the half-tribe of Manasseh they were given Golan in Bashan and also Ashtaroth, together with their pasturelands.
72 Kabila la Isakari liliwapa uzao wa Gerishomu: Kedeshi pamoja na nchi ya malisho, Dabera pamoja na nchi ya malisho,
From the tribe of Issachar they were given Kedesh, Daberath,
73 Ramothi pamoja na nchi ya malisho, na Anemu pamoja na nchi ya malisho.
Ramoth, and Anem, together with their pasturelands.
74 Isakari alipokea kutoka kwa kabila la Asheri: Mashali pamoja na nchi ya malisho, Abdoni pamoja na nchi ya malisho,
From the tribe of Asher they were given Mashal, Abdon,
75 Hukoki pamoja na nchi ya malisho, na Rehobu pamoja na nchi ya malisho.
Hukok, and Rehob, together with their pasturelands.
76 Walipokea kutoka kabila la Naftali: Kedeshi iliyo Galileya pamoja na nchi ya malisho, Hamoni pamoja na nchi ya malisho, na Kiriathaimu pamoja na nchi ya malisho.
And from the tribe of Naphtali they were given Kedesh in Galilee, Hammon, and Kiriathaim, together with their pasturelands.
77 Kwa Walawi wengine, uzao wa Merari, walipewa kutoka kabila la Zebuluni: Rimono pamoja na nchi ya malisho na Tabori pamoja na nchi ya malisho.
The Merarites (the rest of the Levites) received the following: From the tribe of Zebulun they were given Rimmono and Tabor, together with their pasturelands.
78 Kwa wao pia walipewa, upande wa pili wa Yordani huko Yeriko, kwa upande wa mashariki mwa mto: Bezeri katika jangwa pamoja na nchi ya malisho, Yahzahi pamoja na nchi ya malisho,
From the tribe of Reuben east of the Jordan opposite Jericho they were given Bezer in the wilderness, Jahzah,
79 Kedemothi pamoka na nchi ya malisho, ma Mefathi pamoja na nchi ya malisho. Hizi zilitolewa kutoka kabila la Rubeni.
Kedemoth, and Mephaath, together with their pasturelands.
80 Walawi walipokea kutoka kabila la Gadi: Ramothi ya Gileadi pamoja na nchi ya malisho, Mahanaimu pamoja na nchi ya malisho,
And from the tribe of Gad they were given Ramoth in Gilead, Mahanaim,
81 Heshiboni pamoja na nchi ya malisho, na Yazeri pamoja na nchi ya malisho.
Heshbon, and Jazer, together with their pasturelands.