< 1 Nyakati 28 >
1 Daudi akakusanya waamuzi wote wa Israeli Yerusalemu: waamuzi wa makabila, maafisa wa vitengo walio mtumikia mfalme katika kazi walizo pangiwa, wakuu wa maelfu na mamia, wasimamizi wa mali zote za mfalme na mwanae, na maafisa na wanaume wa mapambano, ukijumuisha wale wenye ujuzi sana.
David assembla à Jérusalem tous les chefs d'Israël, les chefs des tribus, les chefs des troupes qui servaient le roi par divisions, les chefs de milliers, les chefs de centaines, et les chefs de tous les biens et de toutes les possessions du roi et de ses fils, avec les officiers et les hommes forts, tous les vaillants hommes.
2 Daudi mfalme akainuka kwa miguu yake na kusema, “Sikilizeni mimi, kaka zangu na watu wangu. Ilikuwa dhumuni langu kujenga hekalu kwa ajili ya sanduku la agano la Yahweh; stuli ya miguu kwa ajili ya Mungu wetu, na nimefanya maandalizi kuijenga.
Alors le roi David se leva sur ses pieds et dit: « Écoutez-moi, mes frères et mon peuple! Moi, j'avais à cœur de bâtir une maison de repos pour l'arche de l'alliance de Yahvé et pour le marchepied de notre Dieu, et j'avais préparé la construction.
3 Lakini Mungu akaniambia, 'Hautajenga hekalu kwa ajili ya jina la langu, kwasababu wewe ni mwanaume wa vita na umemwaga damu.'
Mais Dieu me dit: « Tu ne bâtiras pas une maison à mon nom, car tu es un homme de guerre et tu as versé du sang.
4 Bado Yahweh, Mungu wa Israeli, alinichagua kutoka katika familia ya baba yangu kuwa mfalme wa Israeli milele. Amechagua kabila la Yuda kama kiongozi. Katika kabila la Yuda, na nyumba ya baba yangu, kutoka kwa wana wa baba yangu, amenichagua kuwa mfalme wa Israeli.
Mais Yahvé, le Dieu d'Israël, m'a choisi parmi toute la maison de mon père pour être roi d'Israël à jamais. Car il a choisi Juda comme prince; et dans la maison de Juda, la maison de mon père, et parmi les fils de mon père, il a pris plaisir à me faire régner sur tout Israël.
5 Kutoka kwa wana wengi ambao Yahweh amenipa, amemchagua Sulemani, mwanangu, kuketi katika kiti cha enzi cha ufalme wa Yahweh, juu ya Israeli.
De tous mes fils (car l'Éternel m'a donné beaucoup de fils), il a choisi Salomon, mon fils, pour s'asseoir sur le trône du royaume de l'Éternel sur Israël.
6 Aliniambia, 'Sulemani mwanae atanijengea nyumba yangu na nyuani mwangu, kwa kuwa nimemchagua kuwa mwana wangu, nami nitakuwa baba yake.
Il m'a dit: « Salomon, ton fils, bâtira ma maison et mes parvis, car je l'ai choisi comme mon fils et je serai son père.
7 Nitaimarisha ufalme wake, akidumu kutii sheria na amri zangu, kama ulivyo siku ya leo.'
J'établirai son royaume pour toujours, s'il continue à pratiquer mes commandements et mes ordonnances, comme il le fait aujourd'hui.
8 Kisha sasa, katika macho ya Waisraeli wote, ili kusanyiko la yahweh, na katika uwepo wa Mungu wetu, nyinyi nyote lazima mshike na kufanya amri zote za Yahweh Mungu wenu. Fanyeni hivi ili mmiliki nchi nzuri na kuacha urithi wa watoto wenu baada yenu milele.
Maintenant, en présence de tout Israël, de l'assemblée de l'Éternel, et en présence de notre Dieu, observez et recherchez tous les commandements de l'Éternel, votre Dieu, afin de posséder ce bon pays et de le laisser en héritage à vos enfants après vous pour toujours.
9 Kwako wewe, Sulemani mwanangu, mtii Mungu wa baba yako, mtumikie kwa moyo wako wote na roho ya utayari. Fanya hivi kwasababu yahweh anachunguza mioyo yote na kufahamu amasa ya kila wazo la mtu. Ukimtafuta, ataonekana kwako, lakini ukimtelekeza, atakukataa milele.
Toi, Salomon, mon fils, connais le Dieu de ton père, et sers-le d'un cœur parfait et d'un esprit bien disposé; car Yahvé sonde tous les cœurs et comprend toutes les imaginations des pensées. Si tu le cherches, tu le trouveras, mais si tu l'abandonnes, il te rejettera pour toujours.
10 Elewa kuwa Yahweh amekuchagua kujenga hekalu ili kama sehemu yake takatifu. Kuwa imara na ufanye.”
Prends garde maintenant, car Yahvé t'a choisi pour construire une maison pour le sanctuaire. Sois fort, et fais-le. »
11 Kisha Daudi akamkabidhi Sulemani mwanae mipango ya baraza la hekalu, jengo la hekalu, vyumba vya hifadhi, vyumba vya juu, vyumba vya ndani, na chumba chenye mfuniko wa maombezi.
David donna à Salomon, son fils, les plans du portique du temple, de ses maisons, de ses trésors, de ses salles supérieures, de ses salles intérieures, de la place du propitiatoire,
12 Alimpatia mipango aliyo chora ya nyuani kwa ajili ya nyumba ya Yahweh, vyumba vyote vilivyo zunguka, vyumba vya hifadhi katika nyumba ya Mungu, na hazina za vitu vya Yahweh.
et les plans de tout ce qu'il avait reçu de l'Esprit, pour les parvis de la maison de l'Éternel, pour toutes les salles environnantes, pour les trésors de la maison de Dieu et pour les trésors des choses consacrées;
13 Alimpatia masharti kwa vitengo vya makuhani na Walawi, kwa majukumu walio pangiwa katika nyumba ya Yahweh, na kwa vyombo vyote vinavyo tumika katika nyumba ya Yahweh.
aussi pour les divisions des prêtres et des lévites, pour tout le travail du service de la maison de l'Éternel, et pour tous les ustensiles de service de la maison de l'Éternel -
14 Alimpa uzito wote wa vifaa vya dhahabu kwa kila huduma na vifaa vyote vya fedha, na vitu vyote kwa kila namna ya huduma.
au poids d'or pour les ustensiles de service de toute espèce, au poids d'argent pour tous les ustensiles de service de toute espèce;
15 Haya maelekezo yalitolewa kwa uzito, ukijumuisha maelekezo yote ya vinara vya taa vya dhahabu na taa za dhahabu, maelekezo kwa uzito kwa kila vinara vya taa, kwa vinara vya taa vya fedha, na maelekezo kwa matumizi sahihi ya vinara vya taa vyote.
de l'or, au poids, pour les chandeliers d'or et pour leurs lampes, d'or, au poids, pour chaque chandelier et pour ses lampes; et de l'argent, au poids, pour chaque chandelier et pour ses lampes, selon l'usage de chaque chandelier;
16 Alitoa uzito wa dhahabu kwa meza za mkate wa uwepo, kwa kila meza, na uzito wa fedha kwa meza za fedha.
de l'or, au poids, pour les tables de pain de proposition, pour chaque table; et de l'argent, pour les tables d'argent;
17 Alitoa uzito wa dhahabu safi kwa uma za nyama, bakuli, na vikombe. Alitoa uzito kwa kila bakuli ya dhahabu, na uzito kwa kila bakuli ya fedha.
les fourchettes, les bassins et les tasses d'or pur; les coupes d'or, au poids de chaque coupe; les coupes d'argent, au poids de chaque coupe;
18 Alitoa uzito wa dhahabu ya kutakasika kwa madhabahu ya uvumba, na kwa dhahabu kwa ajili ya mchoro wa makerubi waliye tanda mabawa yao na kufunika sanduku la agano la Yahweh.
l'or pur pour l'autel des parfums; l'or pour les plans du char et les chérubins qui couvrent l'arche de l'alliance de Yahvé.
19 Daudi akasema, “Nimeeka haya katika maandishi kama Yahweh alivyo ni elekeza na kunipa kuelewa kuhusu mchoro.”
« Tout cela, dit David, m'a été expliqué par écrit, de la main de l'Éternel, tous les ouvrages de ce modèle. »
20 Daudi akasema kwa Sulemani mwanae, “Kuwa hodari na mjasiri. Fanya kazi. Usiogope au kuwa na wasiwasi, kwa kuwa Yahweh Mungu, Mungu wangu, yupo nawe. Hatakuacha wala kukutelekeza mpaka kazi ya huduma ya hekalu la Yahweh imekamilika.
David dit à Salomon, son fils: « Sois fort et courageux, et fais-le. N'aie pas peur et ne t'effraie pas, car Yahvé Dieu, mon Dieu, est avec toi. Il ne te décevra pas et ne t'abandonnera pas, jusqu'à ce que soit achevé tout le travail pour le service de la maison de l'Éternel.
21 Ona, hivi ni vitengo vya makuhani na Walawi kwa huduma katika hekalu la Mungu. Watakuwa nawe, pamoja na wanaume walio tayari na wenye ujuzi, kukusaidia katika kazi na kutenda huduma. Waamuzi na watu wote wako tayari kufuata amri zako.”
Voici la répartition des prêtres et des lévites pour tout le service de la maison de Dieu. Tous les hommes de bonne volonté, qui ont de l'habileté pour quelque service que ce soit, seront avec vous pour toutes sortes de travaux. Les chefs et tout le peuple seront entièrement à tes ordres. »