< 1 Nyakati 28 >

1 Daudi akakusanya waamuzi wote wa Israeli Yerusalemu: waamuzi wa makabila, maafisa wa vitengo walio mtumikia mfalme katika kazi walizo pangiwa, wakuu wa maelfu na mamia, wasimamizi wa mali zote za mfalme na mwanae, na maafisa na wanaume wa mapambano, ukijumuisha wale wenye ujuzi sana.
And David assembled all the princes of Israel, the princes of the tribes, and the captains of the companies that served the king by course, and the captains of thousands, and the captains of hundreds, and the rulers over all the substance and cattle of the king and of his sons, with the officers, and the mighty men, even all the mighty men of valour, unto Jerusalem.
2 Daudi mfalme akainuka kwa miguu yake na kusema, “Sikilizeni mimi, kaka zangu na watu wangu. Ilikuwa dhumuni langu kujenga hekalu kwa ajili ya sanduku la agano la Yahweh; stuli ya miguu kwa ajili ya Mungu wetu, na nimefanya maandalizi kuijenga.
Then David the king stood up upon his feet, and said: 'Hear me, my brethren, and my people; as for me, it was in my heart to build a house of rest for the ark of the covenant of the LORD, and for the footstool of our God; and I had made ready for the building.
3 Lakini Mungu akaniambia, 'Hautajenga hekalu kwa ajili ya jina la langu, kwasababu wewe ni mwanaume wa vita na umemwaga damu.'
But God said unto me: Thou shalt not build a house for My name, because thou art a man of war, and hast shed blood.
4 Bado Yahweh, Mungu wa Israeli, alinichagua kutoka katika familia ya baba yangu kuwa mfalme wa Israeli milele. Amechagua kabila la Yuda kama kiongozi. Katika kabila la Yuda, na nyumba ya baba yangu, kutoka kwa wana wa baba yangu, amenichagua kuwa mfalme wa Israeli.
Howbeit the LORD, the God of Israel, chose me out of all the house of my father to be king over Israel for ever; for He hath chosen Judah to be prince, and in the house of Judah, the house of my father, and among the sons of my father He took pleasure in me to make me king over all Israel;
5 Kutoka kwa wana wengi ambao Yahweh amenipa, amemchagua Sulemani, mwanangu, kuketi katika kiti cha enzi cha ufalme wa Yahweh, juu ya Israeli.
and of all my sons — for the LORD hath given me many sons — He hath chosen Solomon my son to sit upon the throne of the kingdom of the LORD over Israel.
6 Aliniambia, 'Sulemani mwanae atanijengea nyumba yangu na nyuani mwangu, kwa kuwa nimemchagua kuwa mwana wangu, nami nitakuwa baba yake.
And He said unto me: Solomon thy son, he shall build My house and My courts; for I have chosen him to be to Me for a son, and I will be to him for a father.
7 Nitaimarisha ufalme wake, akidumu kutii sheria na amri zangu, kama ulivyo siku ya leo.'
And I will establish his kingdom for ever, if he be constant to do My commandments and Mine ordinances, as at this day.
8 Kisha sasa, katika macho ya Waisraeli wote, ili kusanyiko la yahweh, na katika uwepo wa Mungu wetu, nyinyi nyote lazima mshike na kufanya amri zote za Yahweh Mungu wenu. Fanyeni hivi ili mmiliki nchi nzuri na kuacha urithi wa watoto wenu baada yenu milele.
Now therefore, in the sight of all Israel, the congregation of the LORD, and in the hearing of our God, observe and seek out all the commandments of the LORD your God; that ye may possess this good land, and leave it for an inheritance to your children after you for ever.
9 Kwako wewe, Sulemani mwanangu, mtii Mungu wa baba yako, mtumikie kwa moyo wako wote na roho ya utayari. Fanya hivi kwasababu yahweh anachunguza mioyo yote na kufahamu amasa ya kila wazo la mtu. Ukimtafuta, ataonekana kwako, lakini ukimtelekeza, atakukataa milele.
And thou, Solomon my son, know thou the God of thy father, and serve Him with a whole heart and with a willing mind; for the LORD searcheth all hearts, and understandeth all the imaginations of the thoughts; if thou seek Him, He will be found of thee; but if thou forsake Him, He will cast thee off for ever.
10 Elewa kuwa Yahweh amekuchagua kujenga hekalu ili kama sehemu yake takatifu. Kuwa imara na ufanye.”
Take heed now; for the LORD hath chosen thee to build a house for the sanctuary; be strong, and do it.'
11 Kisha Daudi akamkabidhi Sulemani mwanae mipango ya baraza la hekalu, jengo la hekalu, vyumba vya hifadhi, vyumba vya juu, vyumba vya ndani, na chumba chenye mfuniko wa maombezi.
Then David gave to Solomon his son the pattern of the porch of the temple, and of the houses thereof, and of the treasuries thereof, and of the upper rooms thereof, and of the inner chambers thereof, and of the place of the ark-cover;
12 Alimpatia mipango aliyo chora ya nyuani kwa ajili ya nyumba ya Yahweh, vyumba vyote vilivyo zunguka, vyumba vya hifadhi katika nyumba ya Mungu, na hazina za vitu vya Yahweh.
and the pattern of all that he had by the spirit, for the courts of the house of the LORD, and for all the chambers round about, for the treasuries of the house of God, and for the treasuries of the hallowed things;
13 Alimpatia masharti kwa vitengo vya makuhani na Walawi, kwa majukumu walio pangiwa katika nyumba ya Yahweh, na kwa vyombo vyote vinavyo tumika katika nyumba ya Yahweh.
also for the courses of the priests and the Levites, and for all the work of the service of the house of the LORD, and for all the vessels of service in the house of the LORD:
14 Alimpa uzito wote wa vifaa vya dhahabu kwa kila huduma na vifaa vyote vya fedha, na vitu vyote kwa kila namna ya huduma.
of gold by weight for the vessels of gold, for all vessels of every kind of service; of silver for all the vessels of silver by weight, for all vessels of every kind of service;
15 Haya maelekezo yalitolewa kwa uzito, ukijumuisha maelekezo yote ya vinara vya taa vya dhahabu na taa za dhahabu, maelekezo kwa uzito kwa kila vinara vya taa, kwa vinara vya taa vya fedha, na maelekezo kwa matumizi sahihi ya vinara vya taa vyote.
by weight also for the candlesticks of gold, and for the lamps thereof, of gold, by weight for every candlestick and for the lamps thereof; and for the candlesticks of silver, silver by weight for every candlestick and for the lamps thereof, according to the use of every candlestick;
16 Alitoa uzito wa dhahabu kwa meza za mkate wa uwepo, kwa kila meza, na uzito wa fedha kwa meza za fedha.
and the gold by weight for the tables of showbread, for every table; and silver for the tables of silver;
17 Alitoa uzito wa dhahabu safi kwa uma za nyama, bakuli, na vikombe. Alitoa uzito kwa kila bakuli ya dhahabu, na uzito kwa kila bakuli ya fedha.
and the flesh-hooks, and the basins, and the jars, of pure gold; and for the golden bowls by weight for every bowl; and for the silver bowls by weight for every bowl;
18 Alitoa uzito wa dhahabu ya kutakasika kwa madhabahu ya uvumba, na kwa dhahabu kwa ajili ya mchoro wa makerubi waliye tanda mabawa yao na kufunika sanduku la agano la Yahweh.
and for the altar of incense refined gold by weight; and gold for the pattern of the chariot, even the cherubim, that spread out their wings, and covered the ark of the covenant of the LORD.
19 Daudi akasema, “Nimeeka haya katika maandishi kama Yahweh alivyo ni elekeza na kunipa kuelewa kuhusu mchoro.”
'All this do I give thee in writing, as the LORD hath made me wise by His hand upon me, even all the works of this pattern.'
20 Daudi akasema kwa Sulemani mwanae, “Kuwa hodari na mjasiri. Fanya kazi. Usiogope au kuwa na wasiwasi, kwa kuwa Yahweh Mungu, Mungu wangu, yupo nawe. Hatakuacha wala kukutelekeza mpaka kazi ya huduma ya hekalu la Yahweh imekamilika.
And David said to Solomon his son: 'Be strong and of good courage, and do it; fear not, nor be dismayed; for the LORD God, even my God, is with thee; He will not fail thee, nor forsake thee, until all the work for the service of the house of the LORD be finished.
21 Ona, hivi ni vitengo vya makuhani na Walawi kwa huduma katika hekalu la Mungu. Watakuwa nawe, pamoja na wanaume walio tayari na wenye ujuzi, kukusaidia katika kazi na kutenda huduma. Waamuzi na watu wote wako tayari kufuata amri zako.”
And, behold, there are the courses of the priests and the Levites, for all the service of the house of God; and there shall be with thee in all manner of work every willing man that hath skill, for any manner of service; also the captains and all the people will be wholly at thy commandment.'

< 1 Nyakati 28 >