< 1 Nyakati 28 >

1 Daudi akakusanya waamuzi wote wa Israeli Yerusalemu: waamuzi wa makabila, maafisa wa vitengo walio mtumikia mfalme katika kazi walizo pangiwa, wakuu wa maelfu na mamia, wasimamizi wa mali zote za mfalme na mwanae, na maafisa na wanaume wa mapambano, ukijumuisha wale wenye ujuzi sana.
And so David called together all the leaders of Israel, the rulers of the tribes, and those in charge of the companies, who were ministering to the king, and also the tribunes and centurions, and those in charge of the substance and possessions of the king, and his sons, with the eunuchs and the powerful and those most experienced in the army, at Jerusalem.
2 Daudi mfalme akainuka kwa miguu yake na kusema, “Sikilizeni mimi, kaka zangu na watu wangu. Ilikuwa dhumuni langu kujenga hekalu kwa ajili ya sanduku la agano la Yahweh; stuli ya miguu kwa ajili ya Mungu wetu, na nimefanya maandalizi kuijenga.
And when the king had risen up and was standing, he said: “Listen to me, my brothers and my people. I thought that I would build a house, in which the ark of the covenant of the Lord, the footstool of our God, might rest. And so I prepared everything for its building.
3 Lakini Mungu akaniambia, 'Hautajenga hekalu kwa ajili ya jina la langu, kwasababu wewe ni mwanaume wa vita na umemwaga damu.'
But God said to me: ‘You shall not build a house to my name, because you are a man of war, and have shed blood.’
4 Bado Yahweh, Mungu wa Israeli, alinichagua kutoka katika familia ya baba yangu kuwa mfalme wa Israeli milele. Amechagua kabila la Yuda kama kiongozi. Katika kabila la Yuda, na nyumba ya baba yangu, kutoka kwa wana wa baba yangu, amenichagua kuwa mfalme wa Israeli.
Now the Lord God of Israel chose me, out of the entire house of my father, so that I would be king over Israel forever. For from Judah he chose leaders; then from the house of Judah he chose the house of my father; and from the sons of my father, it pleased him to choose me as king over all of Israel.
5 Kutoka kwa wana wengi ambao Yahweh amenipa, amemchagua Sulemani, mwanangu, kuketi katika kiti cha enzi cha ufalme wa Yahweh, juu ya Israeli.
Then too, among my sons (for the Lord has given me many sons) he chose Solomon my son, so that he would sit upon the throne of the kingdom of the Lord, over Israel.
6 Aliniambia, 'Sulemani mwanae atanijengea nyumba yangu na nyuani mwangu, kwa kuwa nimemchagua kuwa mwana wangu, nami nitakuwa baba yake.
And he said to me: ‘Solomon your son shall build my house and my courts. For I have chosen him to be to me as a son, and I will be to him as a father.
7 Nitaimarisha ufalme wake, akidumu kutii sheria na amri zangu, kama ulivyo siku ya leo.'
And I will make firm his kingdom, even unto eternity, if he will persevere in doing my precepts and judgments, as also today.’
8 Kisha sasa, katika macho ya Waisraeli wote, ili kusanyiko la yahweh, na katika uwepo wa Mungu wetu, nyinyi nyote lazima mshike na kufanya amri zote za Yahweh Mungu wenu. Fanyeni hivi ili mmiliki nchi nzuri na kuacha urithi wa watoto wenu baada yenu milele.
Now therefore, before the entire assembly of Israel, in the hearing of our God, keep and seek all the commandments of the Lord our God, so that you may possess the good land, and may bequeath it to your sons after you, even forever.
9 Kwako wewe, Sulemani mwanangu, mtii Mungu wa baba yako, mtumikie kwa moyo wako wote na roho ya utayari. Fanya hivi kwasababu yahweh anachunguza mioyo yote na kufahamu amasa ya kila wazo la mtu. Ukimtafuta, ataonekana kwako, lakini ukimtelekeza, atakukataa milele.
And as for you, my son Solomon, know the God of your father, and serve him with a perfect heart and a willing mind. For the Lord searches all hearts, and understands the thoughts of all minds. If you seek him, you will find him. But if you abandon him, he will cast you aside for eternity.
10 Elewa kuwa Yahweh amekuchagua kujenga hekalu ili kama sehemu yake takatifu. Kuwa imara na ufanye.”
Now therefore, since the Lord has chosen you, so that you would build the house of the Sanctuary, be strengthened and accomplish it.”
11 Kisha Daudi akamkabidhi Sulemani mwanae mipango ya baraza la hekalu, jengo la hekalu, vyumba vya hifadhi, vyumba vya juu, vyumba vya ndani, na chumba chenye mfuniko wa maombezi.
Then David gave to his son Solomon a description of the portico, and the temple, and the storerooms, and the upper floor, and the innermost rooms, and the house of propitiation,
12 Alimpatia mipango aliyo chora ya nyuani kwa ajili ya nyumba ya Yahweh, vyumba vyote vilivyo zunguka, vyumba vya hifadhi katika nyumba ya Mungu, na hazina za vitu vya Yahweh.
and indeed also of all the courts that he had planned, and the outer rooms on all sides, for the treasuries of the house of the Lord, and for the treasuries of the holy things,
13 Alimpatia masharti kwa vitengo vya makuhani na Walawi, kwa majukumu walio pangiwa katika nyumba ya Yahweh, na kwa vyombo vyote vinavyo tumika katika nyumba ya Yahweh.
and for the divisions of the priests and the Levites: concerning all the works of the house of the Lord and all the items in the ministry of the temple of the Lord.
14 Alimpa uzito wote wa vifaa vya dhahabu kwa kila huduma na vifaa vyote vya fedha, na vitu vyote kwa kila namna ya huduma.
There was gold by weight for every vessel of the ministry, and also silver by weight for the diversity of vessels and equipment.
15 Haya maelekezo yalitolewa kwa uzito, ukijumuisha maelekezo yote ya vinara vya taa vya dhahabu na taa za dhahabu, maelekezo kwa uzito kwa kila vinara vya taa, kwa vinara vya taa vya fedha, na maelekezo kwa matumizi sahihi ya vinara vya taa vyote.
Then too, he distributed gold for the lampstands and their lamps, according to the measure of each of the lampstands with their lamps. Similarly also, he distributed silver by weight for the silver lampstands with their lamps, according to the diversity of their measure.
16 Alitoa uzito wa dhahabu kwa meza za mkate wa uwepo, kwa kila meza, na uzito wa fedha kwa meza za fedha.
Also, he gave gold for the tables of the presence, according to the diversity of the tables; similarly too, he gave silver for the other tables of silver.
17 Alitoa uzito wa dhahabu safi kwa uma za nyama, bakuli, na vikombe. Alitoa uzito kwa kila bakuli ya dhahabu, na uzito kwa kila bakuli ya fedha.
Also, he distributed from the purest gold for the small hooks and the bowls and the censors, as well as for the little lions of gold, in accord with the precise measure of the weight, for lion after lion. Similarly too, for the lions of silver, he set aside a different weight of silver.
18 Alitoa uzito wa dhahabu ya kutakasika kwa madhabahu ya uvumba, na kwa dhahabu kwa ajili ya mchoro wa makerubi waliye tanda mabawa yao na kufunika sanduku la agano la Yahweh.
Then, for the altar on which the incense was burned, he gave the purest gold. And from the same he made the likeness of the chariot of the Cherubim, with extended wings, which is veiling the ark of the covenant of the Lord.
19 Daudi akasema, “Nimeeka haya katika maandishi kama Yahweh alivyo ni elekeza na kunipa kuelewa kuhusu mchoro.”
“All these things,” he said, “came to me written by the hand of the Lord, so that I would understand all the works of the pattern.”
20 Daudi akasema kwa Sulemani mwanae, “Kuwa hodari na mjasiri. Fanya kazi. Usiogope au kuwa na wasiwasi, kwa kuwa Yahweh Mungu, Mungu wangu, yupo nawe. Hatakuacha wala kukutelekeza mpaka kazi ya huduma ya hekalu la Yahweh imekamilika.
David also said to his son Solomon: “Act manfully, and be strengthened, and carry it out. You should not be afraid, and you should not be dismayed. For the Lord my God will be with you, and he will not send you away, nor will he abandon you, until you have perfected the entire work of the ministry of the house of the Lord.
21 Ona, hivi ni vitengo vya makuhani na Walawi kwa huduma katika hekalu la Mungu. Watakuwa nawe, pamoja na wanaume walio tayari na wenye ujuzi, kukusaidia katika kazi na kutenda huduma. Waamuzi na watu wote wako tayari kufuata amri zako.”
Behold, the divisions of the priests and the Levites, for every ministry of the house of the Lord, are standing before you. And they have been prepared, and so they know, both the leaders and the people, how to carry out all your precepts.”

< 1 Nyakati 28 >