< 1 Nyakati 27 >
1 Hii ni orodha ya familia za viongozi wa Israeli, wakuu wa maelfu na mamia, pamoja na maafisa wa jeshi walio mtumikia mfalme kwa namna tofauti. Kila kikosi cha jeshi kilitumika mwenzi hadi mwezi kwa mwaka mzima. Kila kikosi kilikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
Now the children of Israel after their number, the heads of fathers’ households and the captains of thousands and of hundreds, and their officers who served the king in any matter of the divisions which came in and went out month by month throughout all the months of the year—of every division were twenty-four thousand.
2 Kwa mwezi wa kwanza wa kikosi alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Katika kikosi chake kulikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
Over the first division for the first month was Jashobeam the son of Zabdiel. In his division were twenty-four thousand.
3 Alikuwa miongoni mwa uzao wa Perezi na mhusika wa maafisa wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
He was of the children of Perez, the chief of all the captains of the army for the first month.
4 Juu ya kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai, wa ukoo wa uliotoka kwa Ahoa. Mikilothi alikuwa wa pili kwa cheo. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
Over the division of the second month was Dodai the Ahohite and his division, and Mikloth the ruler; and in his division were twenty-four thousand.
5 Mkuu wa jeshi wa mwezi wa tatu alikuwa Benaia mwana wa Yehoiada, kuhani na kiongozi. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The third captain of the army for the third month was Benaiah, the son of Jehoiada the chief priest. In his division were twenty-four thousand.
6 Huyu ni Benaia aliye kuwa kiongozi wa wale thelathini na juu ya wale thelathini. Amizabadi mwanae alikuwa katika kikosi chake.
This is that Benaiah who was the mighty man of the thirty and over the thirty. Of his division was Ammizabad his son.
7 Mkuu kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli kaka wa Yoabu. Zebadia mwanae akawa mkuu baada yake. Katika kikosi chake kulikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
The fourth captain for the fourth month was Asahel the brother of Joab, and Zebadiah his son after him. In his division were twenty-four thousand.
8 Mkuu kwa mwezi wa tano alikuwa Shamihuthi, mzao wa Izra. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The fifth captain for the fifth month was Shamhuth the Izrahite. In his division were twenty-four thousand.
9 Mkuu kwa mwezi wa sita alikuwa Ira mwana wa Ikeshi, kutoka Tekoa. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The sixth captain for the sixth month was Ira the son of Ikkesh the Tekoite. In his division were twenty-four thousand.
10 Mkuu kwa mwezi wa saba alikuwa Helezi Mpeloni, kutoka watu wa Efraimu. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The seventh captain for the seventh month was Helez the Pelonite, of the children of Ephraim. In his division were twenty-four thousand.
11 Mkuu kwa mwezi wa nane alikuwa Sibekai Mhushathi, kutoka ukoo ulitoka kwa Zera. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The eighth captain for the eighth month was Sibbecai the Hushathite, of the Zerahites. In his division were twenty-four thousand.
12 Mkuu kwa mwezi wa tisa alikuwa Abi Ezeri Manathothi, kutoka kwa kabila la Benjamini. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The ninth captain for the ninth month was Abiezer the Anathothite, of the Benjamites. In his division were twenty-four thousand.
13 Mkuu kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai kutoka mji wa Netofa, kutoka ukoo ulio toka kwa Zera. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The tenth captain for the tenth month was Maharai the Netophathite, of the Zerahites. In his division were twenty-four thousand.
14 Mkuu kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaia kutoka mji wa Pirathoni, kutoka kabila la Efraimu. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The eleventh captain for the eleventh month was Benaiah the Pirathonite, of the children of Ephraim. In his division were twenty-four thousand.
15 Mkuu kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Helidai kutoka mji wa Netopafa, kutoka ukoo uliotoka kwa Othinieli. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The twelfth captain for the twelfth month was Heldai the Netophathite, of Othniel. In his division were twenty-four thousand.
16 Hawa walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli: Kwa kabila la Rubeni, Eliezeri mwana wa Zikri alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Simeoni, Shefatia mwana wa Maka alikuwa kiongozi.
Furthermore over the tribes of Israel: of the Reubenites, Eliezer the son of Zichri was the ruler; of the Simeonites, Shephatiah the son of Maacah;
17 Kwa kabila la Lawi, Hashinia mwana wa Kemueli alikuwa kiongozi, na Zadoki aliongoza uzao wa Aruni.
of Levi, Hashabiah the son of Kemuel; of Aaron, Zadok;
18 Kwa kabila la Yuda, Elihu, mmoja wa kaka zake Daudi, alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Isakari, Omri mwana wa Mikaeli alikuwa kiongozi.
of Judah, Elihu, one of the brothers of David; of Issachar, Omri the son of Michael;
19 Kwa kabila la Zebuluni, Ishimaia mwana wa Obadia alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Naftali, Yeremothi mwana wa Azirieli alikuwa kiongozi.
of Zebulun, Ishmaiah the son of Obadiah; of Naphtali, Jeremoth the son of Azriel;
20 Kwa kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Azazia alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Manase, Yoeli mwana wa Pedaia alikuwa kiongozi.
of the children of Ephraim, Hoshea the son of Azaziah; of the half-tribe of Manasseh, Joel the son of Pedaiah;
21 Kwa nusu kabila la Manase lililo Gileadi, Ido mwana wa Zekaria alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Benjamini, Yaasieli mwana wa Abneri alikuwa kiongozi.
of the half-tribe of Manasseh in Gilead, Iddo the son of Zechariah; of Benjamin, Jaasiel the son of Abner;
22 Kwa kabila la Dani, Azareli mwana wa Yerohamu alikuwa kiongozi. Hawa walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli.
of Dan, Azarel the son of Jeroham. These were the captains of the tribes of Israel.
23 Daudi hakuwa hesabu wenye umri wa miaka ishirini au chini zaidi, kwasababu Yahweh alihaidi kuongeza Israeli kama nyota za mbinguni.
But David didn’t take the number of them from twenty years old and under, because Yahweh had said he would increase Israel like the stars of the sky.
24 Yoabu mwana wa Zeruia alianza kuhesabu wanaume, lakini hakumaliza. Gadhabu iliangukia Israeli kwa hili. Hii idadi haikuandikwa kwenye nyakati za mfalme Daudi.
Joab the son of Zeruiah began to take a census, but didn’t finish; and wrath came on Israel for this. The number wasn’t put into the account in the chronicles of King David.
25 Azimavethi mwana wa Adieli alikuwa mhusika wa hazina za mfalme. Yonathani mwana wa Uzia alikuwa juu ya nyumba za ghala katika mashamba, kwenye miji, na vijijini, na kwenye minara iliyo imarishwa.
Over the king’s treasures was Azmaveth the son of Adiel. Over the treasures in the fields, in the cities, in the villages, and in the towers was Jonathan the son of Uzziah;
26 Ezri mwana wa Kelubi alikuwa juu ya mashamba, hao walio lima ardhi.
Over those who did the work of the field for tillage of the ground was Ezri the son of Chelub.
27 Shimei kutoka Rama alikuwa juu ya mashamba ya mizabibu, na Zabdi kutoka Shefamu alikuwa juu ya mizabibu na mhifadhi wa mvinyo.
Over the vineyards was Shimei the Ramathite. Over the increase of the vineyards for the wine cellars was Zabdi the Shiphmite.
28 Mwangalizi wa miti mizeituni na miti ya mikuyu iliyo kuwa bondeni alikuwa Baali Hanani kutoka Gederi, na juu ya nyumba za ghala za mafuta alikuwa Yoashi.
Over the olive trees and the sycamore trees that were in the lowland was Baal Hanan the Gederite. Over the cellars of oil was Joash.
29 Juu ya mifugo iliyo kuwa inalishwa huko Sharoni alikuwa Shitrai kutoka Sharoni, na juu ya mifugo iliyo kuwa mabondeni alikuwa Shafati mwana wa Adlai.
Over the herds that fed in Sharon was Shitrai the Sharonite. Over the herds that were in the valleys was Shaphat the son of Adlai.
30 Msimamizi wa ngamia alikuwa Obili Mishimaeli, na juu ya punda wakike alikuwa Yehideia kutoka Meronothi. Juu ya mifugo alikuwa Yazizi Mhagri.
Over the camels was Obil the Ishmaelite. Over the donkeys was Jehdeiah the Meronothite. Over the flocks was Jaziz the Hagrite.
31 Hawa wote walikuwa wasimamizi wa mali za Mfalme Daudi.
All these were the rulers of the property which was King David’s.
32 Yonathani, mjomba wake Daudi alikuwa mshauri, sababu alikuwa na busara na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakimoni aliwajali watoto wa mfalme.
Also Jonathan, David’s uncle, was a counselor, a man of understanding, and a scribe. Jehiel the son of Hachmoni was with the king’s sons.
33 Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme, na Hushai kutoka watu wa Waariki alikuwa mshauri wake wa siri.
Ahithophel was the king’s counselor. Hushai the Archite was the king’s friend.
34 Nafasi ya Ahithofeli ilichukuliwa na Yehoiada mwana wa Benaia, na Abiathari. Yoabu alikuwa mkuu wa jeshi la mfalme.
After Ahithophel was Jehoiada the son of Benaiah, and Abiathar. Joab was the captain of the king’s army.