< 1 Nyakati 27 >

1 Hii ni orodha ya familia za viongozi wa Israeli, wakuu wa maelfu na mamia, pamoja na maafisa wa jeshi walio mtumikia mfalme kwa namna tofauti. Kila kikosi cha jeshi kilitumika mwenzi hadi mwezi kwa mwaka mzima. Kila kikosi kilikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
And the sons of Israel, after their number, heads of the fathers, and princes of the thousands and of the hundreds, and their officers, those serving the king in any matter of the divisions, that are coming in and going out month by month throughout all months of the year, [are] twenty-four thousand in each division.
2 Kwa mwezi wa kwanza wa kikosi alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Katika kikosi chake kulikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
Over the first division for the first month [is] Jashobeam son of Zabdiel, and twenty-four thousand [are] on his division;
3 Alikuwa miongoni mwa uzao wa Perezi na mhusika wa maafisa wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
[he was] of the sons of Perez, [and] the head of all princes of the hosts for the first month.
4 Juu ya kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai, wa ukoo wa uliotoka kwa Ahoa. Mikilothi alikuwa wa pili kwa cheo. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
And over the division of the second month [is] Dodai the Ahohite, and Mikloth [is] also president of his division, and twenty-four thousand [are] on his division.
5 Mkuu wa jeshi wa mwezi wa tatu alikuwa Benaia mwana wa Yehoiada, kuhani na kiongozi. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
Head of the third host, for the third month, [is] Benaiah son of Jehoiada, the head priest, and twenty-four thousand [are] on his division.
6 Huyu ni Benaia aliye kuwa kiongozi wa wale thelathini na juu ya wale thelathini. Amizabadi mwanae alikuwa katika kikosi chake.
This Benaiah [is] a mighty one of the thirty, and over the thirty, and his son Ammizabad [is in] his division.
7 Mkuu kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli kaka wa Yoabu. Zebadia mwanae akawa mkuu baada yake. Katika kikosi chake kulikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
The fourth, for the fourth month, [is] Asahel brother of Joab, and his son Zebadiah after him, and twenty-four thousand [are] on his division.
8 Mkuu kwa mwezi wa tano alikuwa Shamihuthi, mzao wa Izra. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The fifth, for the fifth month, [is] the prince Shamhuth the Izrahite, and twenty-four thousand [are] on his division.
9 Mkuu kwa mwezi wa sita alikuwa Ira mwana wa Ikeshi, kutoka Tekoa. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The sixth, for the sixth month, [is] Ira son of Ikkesh the Tekoite, and twenty-four thousand [are] on his division.
10 Mkuu kwa mwezi wa saba alikuwa Helezi Mpeloni, kutoka watu wa Efraimu. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The seventh, for the seventh month, [is] Helez the Pelonite, of the sons of Ephraim, and twenty-four thousand [are] on his division.
11 Mkuu kwa mwezi wa nane alikuwa Sibekai Mhushathi, kutoka ukoo ulitoka kwa Zera. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The eighth, for the eighth month, [is] Sibbecai the Hushathite, of the Zerahite, and twenty-four thousand [are] on his division.
12 Mkuu kwa mwezi wa tisa alikuwa Abi Ezeri Manathothi, kutoka kwa kabila la Benjamini. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The ninth, for the ninth month, [is] Abiezer the Antothite, of the Benjamite, and twenty-four thousand [are] on his division.
13 Mkuu kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai kutoka mji wa Netofa, kutoka ukoo ulio toka kwa Zera. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The tenth, for the tenth month, [is] Maharai the Netophathite, of the Zerahite, and twenty-four thousand [are] on his division.
14 Mkuu kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaia kutoka mji wa Pirathoni, kutoka kabila la Efraimu. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
Eleventh, for the eleventh month, [is] Benaiah the Pirathonite, of the sons of Ephraim, and twenty-four thousand [are] on his division.
15 Mkuu kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Helidai kutoka mji wa Netopafa, kutoka ukoo uliotoka kwa Othinieli. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The twelfth, for the twelfth month, [is] Heldai the Netophathite, of Othniel, and twenty-four thousand [are] on his division.
16 Hawa walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli: Kwa kabila la Rubeni, Eliezeri mwana wa Zikri alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Simeoni, Shefatia mwana wa Maka alikuwa kiongozi.
And over the tribes of Israel: the leader of the Reubenite [is] Eliezer son of Zichri; of the Simeonite, Shephatiah son of Maachah;
17 Kwa kabila la Lawi, Hashinia mwana wa Kemueli alikuwa kiongozi, na Zadoki aliongoza uzao wa Aruni.
of the Levite, Hashabiah son of Kemuel; of the Aaronite, Zadok;
18 Kwa kabila la Yuda, Elihu, mmoja wa kaka zake Daudi, alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Isakari, Omri mwana wa Mikaeli alikuwa kiongozi.
of Judah, Elihu, of the brothers of David; of Issachar, Omri son of Michael;
19 Kwa kabila la Zebuluni, Ishimaia mwana wa Obadia alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Naftali, Yeremothi mwana wa Azirieli alikuwa kiongozi.
of Zebulun, Ishmaiah son of Obadiah; of Naphtali, Jerimoth son of Azriel;
20 Kwa kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Azazia alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Manase, Yoeli mwana wa Pedaia alikuwa kiongozi.
of the sons of Ephraim, Hoshea son of Azaziah; of the half of the tribe of Manasseh, Joel son of Pedaiah;
21 Kwa nusu kabila la Manase lililo Gileadi, Ido mwana wa Zekaria alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Benjamini, Yaasieli mwana wa Abneri alikuwa kiongozi.
of the half of Manasseh in Gilead, Iddo son of Zechariah; of Benjamin, Jaasiel son of Abner; of Dan, Azareel son of Jeroham.
22 Kwa kabila la Dani, Azareli mwana wa Yerohamu alikuwa kiongozi. Hawa walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli.
These [are the] heads of the tribes of Israel.
23 Daudi hakuwa hesabu wenye umri wa miaka ishirini au chini zaidi, kwasababu Yahweh alihaidi kuongeza Israeli kama nyota za mbinguni.
But David has not taken up their number from a son of twenty years and under, for YHWH had said [He would] multiply Israel as the stars of the heavens.
24 Yoabu mwana wa Zeruia alianza kuhesabu wanaume, lakini hakumaliza. Gadhabu iliangukia Israeli kwa hili. Hii idadi haikuandikwa kwenye nyakati za mfalme Daudi.
Joab son of Zeruiah has begun to number, but has not finished; and there is wrath against Israel for this, and the number has not gone up in the account of the Chronicles of King David.
25 Azimavethi mwana wa Adieli alikuwa mhusika wa hazina za mfalme. Yonathani mwana wa Uzia alikuwa juu ya nyumba za ghala katika mashamba, kwenye miji, na vijijini, na kwenye minara iliyo imarishwa.
And Azmaveth son of Adiel [is] over the treasures of the king; and Jonathan son of Uzziah [is] over the treasures in the field, in the cities, and in the villages, and in the towers;
26 Ezri mwana wa Kelubi alikuwa juu ya mashamba, hao walio lima ardhi.
and Ezri son of Chelub [is] over workmen of the field for the service of the ground;
27 Shimei kutoka Rama alikuwa juu ya mashamba ya mizabibu, na Zabdi kutoka Shefamu alikuwa juu ya mizabibu na mhifadhi wa mvinyo.
and Shimei the Ramathite [is] over the vineyards; and Zabdi the Shiphmite [is] over what [is] in the vineyards for the treasures of wine;
28 Mwangalizi wa miti mizeituni na miti ya mikuyu iliyo kuwa bondeni alikuwa Baali Hanani kutoka Gederi, na juu ya nyumba za ghala za mafuta alikuwa Yoashi.
and Ba‘al-Hanan the Gederite [is] over the olives and the sycamores that [are] in the low country; and Joash [is] over the treasures of oil;
29 Juu ya mifugo iliyo kuwa inalishwa huko Sharoni alikuwa Shitrai kutoka Sharoni, na juu ya mifugo iliyo kuwa mabondeni alikuwa Shafati mwana wa Adlai.
and Shitrai the Sharonite [is] over the herds that are feeding in Sharon; and Shaphat son of Adlai [is] over the herds in the valleys;
30 Msimamizi wa ngamia alikuwa Obili Mishimaeli, na juu ya punda wakike alikuwa Yehideia kutoka Meronothi. Juu ya mifugo alikuwa Yazizi Mhagri.
and Obil the Ishmaelite [is] over the camels; and Jehdeiah the Meronothite [is] over the donkeys;
31 Hawa wote walikuwa wasimamizi wa mali za Mfalme Daudi.
and Jaziz the Hagerite [is] over the flock; all these [are] heads of the substance that King David has.
32 Yonathani, mjomba wake Daudi alikuwa mshauri, sababu alikuwa na busara na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakimoni aliwajali watoto wa mfalme.
And Jonathan, David’s uncle, [is] counselor, a man of understanding, [and] he is also a scribe; and Jehiel son of Hachmoni [is] with the sons of the king;
33 Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme, na Hushai kutoka watu wa Waariki alikuwa mshauri wake wa siri.
and Ahithophel [is] counselor to the king; and Hushai the Archite [is] the friend of the king;
34 Nafasi ya Ahithofeli ilichukuliwa na Yehoiada mwana wa Benaia, na Abiathari. Yoabu alikuwa mkuu wa jeshi la mfalme.
and after Ahithophel [is] Jehoiada son of Benaiah, and Abiathar; and the head of the host of the king [is] Joab.

< 1 Nyakati 27 >