< 1 Nyakati 27 >

1 Hii ni orodha ya familia za viongozi wa Israeli, wakuu wa maelfu na mamia, pamoja na maafisa wa jeshi walio mtumikia mfalme kwa namna tofauti. Kila kikosi cha jeshi kilitumika mwenzi hadi mwezi kwa mwaka mzima. Kila kikosi kilikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
And [these] are the children of Israel after their number, the chief fathers and captains of thousands and hundreds, and their officers that served the king in every matter of the divisions, which came in and went out month by month throughout the months of the year; in every division were twenty-four thousand.
2 Kwa mwezi wa kwanza wa kikosi alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Katika kikosi chake kulikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
Over the first division for the first month was Jashobeam the son of Zabdiel; and in his division were twenty-four thousand.
3 Alikuwa miongoni mwa uzao wa Perezi na mhusika wa maafisa wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
He was of the children of Pherez, the head of all the captains of the hosts for the first month.
4 Juu ya kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai, wa ukoo wa uliotoka kwa Ahoa. Mikilothi alikuwa wa pili kwa cheo. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
And over the division of the second month was Dodai the Ahohite; and in his division was Mikloth ruler; and in his division were twenty-four thousand.
5 Mkuu wa jeshi wa mwezi wa tatu alikuwa Benaia mwana wa Yehoiada, kuhani na kiongozi. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The third captain of the host for the third month was Benaiah (the son of Jehoiada, a principal officer): [he was] head; and in his division were twenty-four thousand.
6 Huyu ni Benaia aliye kuwa kiongozi wa wale thelathini na juu ya wale thelathini. Amizabadi mwanae alikuwa katika kikosi chake.
This Benaiah was a mighty man among the thirty, and above the thirty; and in his division was Ammizabad his son.
7 Mkuu kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli kaka wa Yoabu. Zebadia mwanae akawa mkuu baada yake. Katika kikosi chake kulikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
The fourth for the fourth month was Asahel the brother of Joab, and Zebadiah his son after him; and in his division were twenty-four thousand.
8 Mkuu kwa mwezi wa tano alikuwa Shamihuthi, mzao wa Izra. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The fifth for the fifth month was the captain Shamhuth the Jizrahite; and in his division were twenty-four thousand.
9 Mkuu kwa mwezi wa sita alikuwa Ira mwana wa Ikeshi, kutoka Tekoa. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The sixth for the sixth month was Ira the son of Ikkesh the Tekoite; and in his division were twenty-four thousand.
10 Mkuu kwa mwezi wa saba alikuwa Helezi Mpeloni, kutoka watu wa Efraimu. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The seventh for the seventh month was Helez the Pelonite, of the children of Ephraim; and in his division were twenty-four thousand.
11 Mkuu kwa mwezi wa nane alikuwa Sibekai Mhushathi, kutoka ukoo ulitoka kwa Zera. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The eighth for the eighth month was Sibbechai the Hushathite, of the Zarhites; and in his division were twenty-four thousand.
12 Mkuu kwa mwezi wa tisa alikuwa Abi Ezeri Manathothi, kutoka kwa kabila la Benjamini. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The ninth for the ninth month was Abiezer the Anathothite, of the Benjaminites; and in his division were twenty-four thousand.
13 Mkuu kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai kutoka mji wa Netofa, kutoka ukoo ulio toka kwa Zera. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The tenth for the tenth month was Maharai the Netophathite, of the Zarhites; and in his division were twenty-four thousand.
14 Mkuu kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaia kutoka mji wa Pirathoni, kutoka kabila la Efraimu. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The eleventh for the eleventh month was Benaiah the Pirathonite, of the children of Ephraim; and in his division were twenty-four thousand.
15 Mkuu kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Helidai kutoka mji wa Netopafa, kutoka ukoo uliotoka kwa Othinieli. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The twelfth for the twelfth month was Heldai the Netophathite, of Othniel; and in his division were twenty-four thousand.
16 Hawa walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli: Kwa kabila la Rubeni, Eliezeri mwana wa Zikri alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Simeoni, Shefatia mwana wa Maka alikuwa kiongozi.
And over the tribes of Israel were: for the Reubenites Eliezer the son of Zichri was the prince; for the Simeonites, Shephatiah the son of Maachah;
17 Kwa kabila la Lawi, Hashinia mwana wa Kemueli alikuwa kiongozi, na Zadoki aliongoza uzao wa Aruni.
for the Levites, Hashabiah the son of Kemuel; for Aaron, Zadok;
18 Kwa kabila la Yuda, Elihu, mmoja wa kaka zake Daudi, alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Isakari, Omri mwana wa Mikaeli alikuwa kiongozi.
for Judah, Elihu of the brethren of David; for Issachar, Omri the son of Michael;
19 Kwa kabila la Zebuluni, Ishimaia mwana wa Obadia alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Naftali, Yeremothi mwana wa Azirieli alikuwa kiongozi.
for Zebulun, Jishmaiah the son of Obadiah; for Naphtali, Jerimoth the son of Azriel;
20 Kwa kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Azazia alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Manase, Yoeli mwana wa Pedaia alikuwa kiongozi.
for the children of Ephraim, Hosea the son of Azaziah; for the half tribe of Manasseh, Joel the son of Pedaiah;
21 Kwa nusu kabila la Manase lililo Gileadi, Ido mwana wa Zekaria alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Benjamini, Yaasieli mwana wa Abneri alikuwa kiongozi.
for the half [tribe] of Manasseh in Gilead, Jiddo the son of Zechariah; for Benjamin, Jaasiel the son of Abner;
22 Kwa kabila la Dani, Azareli mwana wa Yerohamu alikuwa kiongozi. Hawa walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli.
for Dan, Azareel the son of Jeroham. These were the princes of the tribes of Israel.
23 Daudi hakuwa hesabu wenye umri wa miaka ishirini au chini zaidi, kwasababu Yahweh alihaidi kuongeza Israeli kama nyota za mbinguni.
And David took not their number from twenty years old and under; for Jehovah had said he would increase Israel as the stars of heaven.
24 Yoabu mwana wa Zeruia alianza kuhesabu wanaume, lakini hakumaliza. Gadhabu iliangukia Israeli kwa hili. Hii idadi haikuandikwa kwenye nyakati za mfalme Daudi.
Joab the son of Zeruiah began to number, but he did not finish; and there fell wrath for it upon Israel; and the number was not put in the account of the chronicles of king David.
25 Azimavethi mwana wa Adieli alikuwa mhusika wa hazina za mfalme. Yonathani mwana wa Uzia alikuwa juu ya nyumba za ghala katika mashamba, kwenye miji, na vijijini, na kwenye minara iliyo imarishwa.
And over the king's treasures was Azmaveth the son of Adiel; and over the storehouses in the country, in the cities, and in the villages, and in the towers was Jonathan the son of Uzziah.
26 Ezri mwana wa Kelubi alikuwa juu ya mashamba, hao walio lima ardhi.
And over them that worked in the field for tillage of the ground was Ezri the son of Chelub.
27 Shimei kutoka Rama alikuwa juu ya mashamba ya mizabibu, na Zabdi kutoka Shefamu alikuwa juu ya mizabibu na mhifadhi wa mvinyo.
And over the vineyards was Shimei the Ramathite; and over what was in the vineyards of stores of wine was Zabdi the Shiphmite:
28 Mwangalizi wa miti mizeituni na miti ya mikuyu iliyo kuwa bondeni alikuwa Baali Hanani kutoka Gederi, na juu ya nyumba za ghala za mafuta alikuwa Yoashi.
and over the olive-trees and the sycamore-trees that were in the lowland was Baal-hanan the Gederite; and over the cellars of oil was Joash.
29 Juu ya mifugo iliyo kuwa inalishwa huko Sharoni alikuwa Shitrai kutoka Sharoni, na juu ya mifugo iliyo kuwa mabondeni alikuwa Shafati mwana wa Adlai.
And over the herds that fed in Sharon was Shitrai the Sharonite; and over the herds in the valleys was Shaphat the son of Adlai.
30 Msimamizi wa ngamia alikuwa Obili Mishimaeli, na juu ya punda wakike alikuwa Yehideia kutoka Meronothi. Juu ya mifugo alikuwa Yazizi Mhagri.
And over the camels was Obil the Ishmaelite; and over the asses was Jehdiah the Meronothite.
31 Hawa wote walikuwa wasimamizi wa mali za Mfalme Daudi.
And over the flocks was Jaziz the Hagarite. All these were comptrollers of the substance which was king David's.
32 Yonathani, mjomba wake Daudi alikuwa mshauri, sababu alikuwa na busara na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakimoni aliwajali watoto wa mfalme.
And Jonathan, David's uncle, was counsellor, a wise man, and a scribe; and Jehiel the son of Hachmoni was with the king's sons;
33 Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme, na Hushai kutoka watu wa Waariki alikuwa mshauri wake wa siri.
and Ahithophel was the king's counsellor; and Hushai the Archite was the king's friend;
34 Nafasi ya Ahithofeli ilichukuliwa na Yehoiada mwana wa Benaia, na Abiathari. Yoabu alikuwa mkuu wa jeshi la mfalme.
and after Ahithophel was Jehoiada the son of Benaiah, and Abiathar; and Joab was captain of the king's army.

< 1 Nyakati 27 >