< 1 Nyakati 25 >

1 Daudi na viongozi wa wafanyakazi wa hema la kuabudia walichaguliwa kwa kazi baadhi walikuwa wana wa Asafu, Hemani, na Yeduthuni. Wanaume hawa walitabiri kwa vinubi, vifaa vya uzi, na upatu. Hii ni orodha ya wanaume walioifanya hii kazi:
Then David and the magistrates of the army set apart, for the ministry, the sons of Asaph, and of Heman, and of Jeduthun, who were to prophesy with harps and psalteries and cymbals, in accord with their number, having been dedicated to their appointed office.
2 Kutoka wana wa Asafu: Zakuri, Yosefu, Nethania, na Asharela, wana wa Asafu, chini ya mwongozo wa Asafu, ambaye alitabiri chini ya uwangalizi wa mfalme.
From the sons of Asaph: Zaccur, and Joseph, and Nethaniah, and Asharelah, the sons of Asaph, under the hand of Asaph, prophesying beside the king.
3 Kutoka wana wa Yeduthuni: Gedalia, Zeri, Yeshaia, Shimei, Hashabia, na Matithia, sita kwa ujumla, chini ya mwongozo wa baba yao Yeduthuni, ambaye alipiga kinubi kwa kutoa shukurani na kumsifu Yahweh.
Then of Jeduthun, the sons of Jeduthun: Gedaliah, Zeri, Jeshaiah, and Hashabiah, and Mattithiah, six, under the hand of their father Jeduthun, who was prophesying with stringed instruments, while confessing and praising the Lord.
4 Kutoka wana wa Hemani: Bukia, Matania, Uzieli, Shebueli, na yerimothi, Hanania, Hanani, Eliatha, Gidalti, Romamti Ezeri, yoshibekasha, Mallothi, Hothiri, na Mahaziothi.
Also, of Heman, the sons of Heman: Bukkiah, Mattaniah, Uzziel, Shebuel, and Jerimoth, Hananiah, Hanani, Eliathah, Giddalti, and Romamtiezer, and Joshbekashah, Mallothi, Hothir, Mahazioth.
5 Hawa wote walikuwa wana wa Hemani mfalme wa manabii. Mungu alimpa Hemani wana kumi na nne na mabinti watatu kwa ajili ya kumpa heshima.
All these were the sons of Heman, the seer of the king in the words of God, in order to lift up the horn. And God gave to Heman fourteen sons and three daughters.
6 Hawa wote walikuwa chini ya mwongozo wa baba yao. Walikuwa ni waimbaji katika nyumba ya Yahweh, pamoja na upatu na vifaa vya uzi walivyohudumu katika nyumba ya Mungu. Asafu, Yeduthuni, na Hemani walikuwa chini ya uwangalizi wa mfalme.
All these, under their father’s hand, were distributed in order to sing in the temple of the Lord, with cymbals and psalteries and harps, in the ministry of the house of the Lord beside the king, specifically, Asaph, and Jeduthun, and Heman.
7 Wao na kaka zao walikuwa na uwelewa na walifundishwa kutengeneza muziki kwa Yahweh walikuwa na idadi ya 288.
Now the number of these, with their brothers, who were instructing in the song of the Lord, all the teachers, were two hundred eighty-eight.
8 Walirusha kura kwa majukumu yao, wote sawa, sawa kwa vijana na kwa wazee, kwa walimua na kwa wanafunzi.
And they cast lots in their turns, the elder equally with the younger, the learned together with the unlearned.
9 Sasa kuhusu wana wa Asafu: kura ya kwanza iliangukia katika familia ya Yusufu; ya pili iliangukia katika familia ya Gedalia, idadi ya watu kumi na mbili;
And the first lot went forth to Joseph, who was of Asaph; the second went forth to Gedaliah, to him and his sons and his brothers, twelve.
10 ya tatu iliangukia kwa Zakuri, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The third went to Zaccur, to his sons and brothers, twelve.
11 ya nne iliangukia kwa Izri, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The fourth went to Izri, to his sons and brothers, twelve.
12 ya tano iliangukia kwa Nethania, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The fifth went to Nethaniah, to his sons and brothers, twelve.
13 ya sita iliangukia kwa Bukia, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The sixth went to Bukkiah, to his sons and brothers, twelve.
14 ya saba iliangukia kwa Yesharela, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The seventh went to Jesharelah, to his sons and brothers, twelve.
15 ya nane iliangukia kwa Yeshaia, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The eighth went to Jeshaiah, to his sons and brothers, twelve.
16 ya tisa iliangukia kwa Matania, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The ninth went to Mattaniah, to his sons and brothers, twelve.
17 ya kumi iliangukia kwa Shimei, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The tenth went to Shimei, to his sons and brothers, twelve.
18 ya kumi na moja iliangukia kwa Azareli, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The eleventh went to Azarel, to his sons and brothers, twelve.
19 ya kumi na mbili iliangukia kwa Hashabia, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The twelfth went to Hashabiah, to his sons and brothers, twelve.
20 ya kumi na tatu iliangukia kwa Shubaeli, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The thirteenth went to Shubael, to his sons and brothers, twelve.
21 ya kumi na nne iliangukia kwa Matithia, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The fourteenth went to Mattithiah, to his sons and brothers, twelve.
22 ya kumi na tano iliangukia kwa Yeromothi, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The fifteenth went to Jeremoth, to his sons and brothers, twelve.
23 ya kumi na sita iliangukia kwa Hanania, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The sixteenth went to Hananiah, to his sons and brothers, twelve.
24 ya kumi na saba iliangukia kwa Yoshibekasha, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The seventeenth went to Joshbekashah, to his sons and brothers, twelve.
25 ya kumi na nane iliangukia kwa Hanani, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The eighteenth went to Hanani, to his sons and brothers, twelve.
26 ya kumi na tisa iliangukia kwa Malothi, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The nineteenth went to Mallothi, to his sons and his brothers, twelve.
27 ya ishirini iliangukia kwa Eliatha, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The twentieth went to Eliathah, to his sons and brothers, twelve.
28 ya ishirini na moja iliangukia kwa Hothiri, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The twenty-first went to Hothir, to his sons and brothers, twelve.
29 ya ishirini na mbili iliangukia kwa Gidalti, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The twenty-second went to Giddalti, to his sons and brothers, twelve.
30 ya ishirini na tatu iliangukia kwa Mahaziothi, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili;
The twenty-third went to Mahazioth, to his sons and brothers, twelve.
31 ya ishirini na nne iliangukia kwa Romamti Eza, wana wake na ndugu zake, idadi ya watu kumi na mbili.
The twenty-fourth went to Romamtiezer, to his sons and brothers, twelve.

< 1 Nyakati 25 >