< 1 Nyakati 24 >
1 Makundi vya kazi kulingana na uzao wa Aroni yalikuwa haya: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
Los hijos de Aarón fueron colocados en divisiones de la siguiente manera. Los hijos de Aarón eran Nadab, Abiú, Eleazar e Itamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao kufa. Walikuwa hawana watoto, kwahiyo Eleazari na Ithamari walitumika kama makuhani.
Pero Nadab y Abiú murieron antes que su padre, y no tuvieron hijos. Sólo Eleazar e Itamar continuaron como sacerdotes.
3 Daudi pamoja na Zadoki, uzao wa Eleazari, na Ahimeleki, uzao wa Ithamari, waliwagawanya katika makundi yao ya kazi kama makuhani.
Con la ayuda de Sadoc, descendiente de Eleazar, y de Itamar, descendiente de Ahimelec, David los colocó en divisiones según sus funciones asignadas.
4 Kulikuwa na wanaume viongozi zaidi kati ya uzao wa Eleazari kuliko kati ya uzao wa Ithamari, kwahiyo waligawanya uzao wa Eleazari katika makundi kumi na sita. Walifanya hivyo na viongozi wa ukoo na uzao wa Ithamari. Magawanyo haya yalikuwa nane kwa idadi, sambamba na koo zao.
Como los descendientes de Eleazar tenían más jefes que los de Itamar, se dividieron así: dieciséis jefes de familia de los descendientes de Eleazar, y ocho de los descendientes de Itamar.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kura, kwa kuwa walikuwa waamuzi watakatifu na waamuzi wa Mungu, kutoka pande zote uzao wa Eleazari na uzao wa Ithamari.
Se dividieron echando suertes, sin preferencia, porque había oficiales del santuario y oficiales de Dios tanto de los hijos de Eleazar como de los hijos de Itamar.
6 Shemaia mwana wa Nethaneli mwandishi, Mlawi, aliandika majina yao mbele ya mfalme, muamuzi, kuhani Zadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa makuhani na familia za Walawi. Ukoo mmoja ulichaguliwa kwa kura kutoka uzao wa Eleazari, na kisha uliofata utachaguliwa kutoka uzao wa Ithhamari.
Semaías hijo de Netanel, un levita, era el secretario. Anotó los nombres y las asignaciones en presencia del rey, de los funcionarios, del sacerdote Sadoc, de Ahimelec hijo de Abiatar y de los jefes de familia de los sacerdotes y levitas. Una familia de Eleazar y otra de Itamar fueron elegidas por turno.
7 Kura ya kwanza ilienda kwa Yehoiaribu, ya pili kwa Yedaia,
La primera suerte recayó en Joiarib. El segundo a Jedaías.
8 ya tatu kwa Harimu, ya nne kwa Seorimu,
La tercera a Harim. El cuarto a Seorim.
9 ya tano kwa Malikija, ya sita kwa Mijamini,
La quinta a Malquías. La sexta a Mijamín.
10 ya saba kwa Hakozi, ya nane kwa Abija,
La séptima a Cos. La octava a Abías.
11 ya tisa kwa Yeshua, ya kumi kwa Shekania,
La novena a Jesúa. La décima por Secanías.
12 ya kumi na moja kwa Eliashibu, ya kumi na mbili kwa Yakimu,
La undécima por Eliasib. La duodécima a Jacim.
13 ya kumi na tatu kwa Hupa, ya kumi na nne kwa Yesheheabu,
La decimotercera por Hupah. La decimocuarta por Jeshebeab.
14 ya kumi na tano kwa Biliga, ya kumi na sita kwa Imma,
La decimoquinta por Bilga. El decimosexto a Immer.
15 ya kumi na saba kwa Heziri, ya kumi na nane kwa Hapizezi,
El decimoséptimo a Hezir. El decimoctavo a Afisés.
16 ya kumi na tisa kwa Pethaia, ya ishirini kwa Yehezikeli,
La decimonovena a Petaías. El vigésimo a Hezequiel.
17 ya ishirini na moja kwa Yakini, ya ishirini na mbili kwa Gamuli,
El vigésimo primero a Jaquín. El vigésimo segundo a Gamul.
18 ya ishirini na tatu kwa Delaia, na ya ishirini na nne kwa Maazia.
El vigésimo tercero a Delaía. El vigésimo cuarto a Maazías.
19 Hii ilikuwa taratibu ya utumishi wao, walipo kuja kwenye nyumba ya Yahweh, wakifuata utaratibu waliopewa na Aruni babu yao, kama Yahweh, Mungu wa Israeli, alivyo waagiza.
Este era el orden en que cada grupo debía servir cuando entraba en la casa del Señor, siguiendo el procedimiento que les había definido su antepasado Aarón, según las instrucciones del Señor, el Dios de Israel.
20 Hawa walikuwa Walawi waliobakia: Wana wa Amiramu, Shebueli; wana wa Shebaeli, Yedeia.
Estos fueron el resto de los hijos de Leví: de Los hijos de Amram: Shubael; de Los hijos de Shubael: Jehdeiah.
21 Wana wa Rehabia: wana wa Rehabia, Ishia kiongozi.
Para Rehabía, de sus hijos Isías (el primogénito).
22 Wa Waizari, Shelomothi; mwana wa Shelomothi, Yahathi.
De los Izharitas: Shelomoth; de Los hijos de Shelomoth: Jahat.
23 Wana wa Hebroni: Yeria kiongozi, Amaria wapili, Yahazieli watatu, na Yekameamu wanne.
Los hijos de Hebrón: Jeriah (el mayor), Amariah (el segundo), Jahaziel (el tercero) y Jecamán (el cuarto).
24 Wana wa uzao wa Uzieli ulimjumuisha Mika. Uzao wa Mika ulimjumuisha Shamiri.
El hijo de Uziel: Miqueas; de Los hijos de Miqueas: Shamir.
25 Kaka wa Mika alikuwa Ishia. Wana wa Ishia akijumuishwa Zakaria.
El hermano de Micaías: Isías; de Los hijos de Isías: Zacarías.
26 Wana na Merari: Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia, Beno.
Los hijos de Merari: Mahli y Musi. El hijo de Jaaziah: Beno.
27 Wana wa Merari: Yaazia, Beno, Shohamu, Zakuri, na Ibrri.
Los hijos de Merari: de Jaaziah: Beno, Shoham, Zaccur e Ibri.
28 Wana wa Mahili: eleazari, ambaye alikuwa hana wana.
De Mahli: Eleazar, que no tuvo hijos.
29 Wana wa Kishi: Yerameli
De Cis: el hijo de Cis, Jerajmeel.
30 wana wa Mushi: Mahli, Eda, na yerimothi. Walikuwa walawi, walio orodheshwa na familia zao.
Los hijos de Musi: Mahli, Eder y Jerimot. Estos eran los hijos de los levitas, según sus familias.
31 Wanaume hawa ambao walikuwa vichwa katika nyumba za baba zao na kila wadogo zao, walipiga kura katika uwepo wa Mfalme Daudi, na Zadoki na Ahimeleki, pamoja na viongozi wa familia wa makuhani na Walawi. Walirusha kura kama uzao wa Aroni walivyofanya.
También echaron suertes de la misma manera que sus parientes los descendientes de Aarón. Lo hicieron en presencia del rey David, de Sadoc, de Ahimelec y de los jefes de familia de los sacerdotes y de los levitas, tanto de los jefes de familia como de sus hermanos menores.