< 1 Nyakati 24 >

1 Makundi vya kazi kulingana na uzao wa Aroni yalikuwa haya: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
A [oto] podział synów Aarona. Synami Aarona [byli]: Nedab, Abihu, Eleazar i Itamar;
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao kufa. Walikuwa hawana watoto, kwahiyo Eleazari na Ithamari walitumika kama makuhani.
Ale Nadab i Abihu umarli przed swoim ojcem i nie mieli synów, dlatego Eleazar i Itamar sprawowali urząd kapłański.
3 Daudi pamoja na Zadoki, uzao wa Eleazari, na Ahimeleki, uzao wa Ithamari, waliwagawanya katika makundi yao ya kazi kama makuhani.
I Dawid podzielił ich, [to jest] Sadoka z synów Eleazara i Achimeleka z synów Itamara, według ich urzędu w ich służbie.
4 Kulikuwa na wanaume viongozi zaidi kati ya uzao wa Eleazari kuliko kati ya uzao wa Ithamari, kwahiyo waligawanya uzao wa Eleazari katika makundi kumi na sita. Walifanya hivyo na viongozi wa ukoo na uzao wa Ithamari. Magawanyo haya yalikuwa nane kwa idadi, sambamba na koo zao.
I okazało się, że spośród synów Eleazara było więcej naczelników niż spośród synów Itamara. Tak więc ich podzielono: spośród synów Eleazara [było] szesnastu naczelników według rodów, a spośród synów Itamara według rodów – ośmiu.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kura, kwa kuwa walikuwa waamuzi watakatifu na waamuzi wa Mungu, kutoka pande zote uzao wa Eleazari na uzao wa Ithamari.
A zostali podzieleni przez losowanie, zarówno jedni, jak i drudzy, gdyż przełożeni świątyni i przełożeni domu Bożego byli spośród synów Eleazara, jak i spośród synów Itamara.
6 Shemaia mwana wa Nethaneli mwandishi, Mlawi, aliandika majina yao mbele ya mfalme, muamuzi, kuhani Zadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa makuhani na familia za Walawi. Ukoo mmoja ulichaguliwa kwa kura kutoka uzao wa Eleazari, na kisha uliofata utachaguliwa kutoka uzao wa Ithhamari.
A Szemajasz, syn Netaneela, pisarz z [pokolenia] Lewiego, spisał ich wobec króla i książąt, kapłana Sadok, Achimeleka, syna Abiatara, oraz naczelników rodów kapłańskich i lewickich. Losowano [na przemian] jeden dom z rodu Eleazara, drugi – z Itamara.
7 Kura ya kwanza ilienda kwa Yehoiaribu, ya pili kwa Yedaia,
Pierwszy los padł na Jehojariba, drugi na Jedajasza;
8 ya tatu kwa Harimu, ya nne kwa Seorimu,
Trzeci na Charima, czwarty na Seorima;
9 ya tano kwa Malikija, ya sita kwa Mijamini,
Piąty na Malkiasza, szósty na Mijamina;
10 ya saba kwa Hakozi, ya nane kwa Abija,
Siódmy na Hakkosa, ósmy na Abiasza;
11 ya tisa kwa Yeshua, ya kumi kwa Shekania,
Dziewiąty na Jeszuę, dziesiąty na Szekaniasza;
12 ya kumi na moja kwa Eliashibu, ya kumi na mbili kwa Yakimu,
Jedenasty na Eliasziba, dwunasty na Jakima;
13 ya kumi na tatu kwa Hupa, ya kumi na nne kwa Yesheheabu,
Trzynasty na Chuppę, czternasty na Jeszebaba;
14 ya kumi na tano kwa Biliga, ya kumi na sita kwa Imma,
Piętnasty na Bilgę, szesnasty na Immera;
15 ya kumi na saba kwa Heziri, ya kumi na nane kwa Hapizezi,
Siedemnasty na Chezira, osiemnasty na Happisesa;
16 ya kumi na tisa kwa Pethaia, ya ishirini kwa Yehezikeli,
Dziewiętnasty na Petachiasza, dwudziesty na Ezechiela;
17 ya ishirini na moja kwa Yakini, ya ishirini na mbili kwa Gamuli,
Dwudziesty pierwszy na Jachina, dwudziesty drugi na Gamula;
18 ya ishirini na tatu kwa Delaia, na ya ishirini na nne kwa Maazia.
Dwudziesty trzeci na Delajasza, dwudziesty czwarty na Maazjasza.
19 Hii ilikuwa taratibu ya utumishi wao, walipo kuja kwenye nyumba ya Yahweh, wakifuata utaratibu waliopewa na Aruni babu yao, kama Yahweh, Mungu wa Israeli, alivyo waagiza.
Taka [była] kolejność w służbie, aby wchodzili do domu PANA zgodnie z ustaleniem, jakie pochodziło od ich ojca Aarona, jak mu rozkazał PAN, Bóg Izraela.
20 Hawa walikuwa Walawi waliobakia: Wana wa Amiramu, Shebueli; wana wa Shebaeli, Yedeia.
A pozostali z synów Lewiego to: z synów Amrama – Szubael; z synów Szubaela – Jechdejasz.
21 Wana wa Rehabia: wana wa Rehabia, Ishia kiongozi.
Z Rechabiasza: z synów Rechabiasza pierwszym [był] Jisziasz.
22 Wa Waizari, Shelomothi; mwana wa Shelomothi, Yahathi.
Z Ishara – Szelomit; z synów Szelomita – Jachat.
23 Wana wa Hebroni: Yeria kiongozi, Amaria wapili, Yahazieli watatu, na Yekameamu wanne.
A synowie Chebrona: pierwszy Jeriasz, drugi Amariasz, trzeci Jachaziel, czwarty Jekameam.
24 Wana wa uzao wa Uzieli ulimjumuisha Mika. Uzao wa Mika ulimjumuisha Shamiri.
Synowie Uzziela: Mika; z synów Miki – Szamir.
25 Kaka wa Mika alikuwa Ishia. Wana wa Ishia akijumuishwa Zakaria.
Brat Miki: Jisziasz; z synów Jisziasza – Zachariasz.
26 Wana na Merari: Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia, Beno.
Synowie Merariego: Machli i Muszi; synowie Jaazjasza: Beno.
27 Wana wa Merari: Yaazia, Beno, Shohamu, Zakuri, na Ibrri.
Synowie Merariego z Jaazjasza: Beno, Szoham, Zakkur i Ibri.
28 Wana wa Mahili: eleazari, ambaye alikuwa hana wana.
Z Machliego: Eleazar, który nie miał synów.
29 Wana wa Kishi: Yerameli
Z Kisza, synowie Kisza: Jerachmeel.
30 wana wa Mushi: Mahli, Eda, na yerimothi. Walikuwa walawi, walio orodheshwa na familia zao.
A synowie Musziego: Machli, Eder i Jerimot. Ci [byli] synami Lewitów według ich rodów.
31 Wanaume hawa ambao walikuwa vichwa katika nyumba za baba zao na kila wadogo zao, walipiga kura katika uwepo wa Mfalme Daudi, na Zadoki na Ahimeleki, pamoja na viongozi wa familia wa makuhani na Walawi. Walirusha kura kama uzao wa Aroni walivyofanya.
Oni również rzucali losy tak samo jak ich bracia, synowie Aarona, przed królem Dawidem, Sadokiem, Achimelekiem oraz naczelnikami rodów kapłańskich i lewickich – naczelnicy rodów na równi z młodszymi ich braćmi.

< 1 Nyakati 24 >