< 1 Nyakati 24 >

1 Makundi vya kazi kulingana na uzao wa Aroni yalikuwa haya: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
And to [the] descendants of Aaron divisions their [the] sons of Aaron Nadab and Abihu Eleazar and Ithamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao kufa. Walikuwa hawana watoto, kwahiyo Eleazari na Ithamari walitumika kama makuhani.
And he died Nadab and Abihu before father their and sons not they belonged to them and they served as priests Eleazar and Ithamar.
3 Daudi pamoja na Zadoki, uzao wa Eleazari, na Ahimeleki, uzao wa Ithamari, waliwagawanya katika makundi yao ya kazi kama makuhani.
And he divided them David and Zadok one of [the] descendants of Eleazar and Ahimelech one of [the] descendants of Ithamar to group their by service their.
4 Kulikuwa na wanaume viongozi zaidi kati ya uzao wa Eleazari kuliko kati ya uzao wa Ithamari, kwahiyo waligawanya uzao wa Eleazari katika makundi kumi na sita. Walifanya hivyo na viongozi wa ukoo na uzao wa Ithamari. Magawanyo haya yalikuwa nane kwa idadi, sambamba na koo zao.
And they were found [the] descendants of Eleazar many to [the] chiefs of the men more than [the] descendants of Ithamar and they divided them [belonged] to [the] descendants of Eleazar heads of a house of ancestors six-teen and [belonged] to [the] descendants of Ithamar of [the] house of ancestors their eight.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kura, kwa kuwa walikuwa waamuzi watakatifu na waamuzi wa Mungu, kutoka pande zote uzao wa Eleazari na uzao wa Ithamari.
And they divided them by lots these with these for they were officials of holiness and [the] officials of God from [the] descendants of Eleazar and among [the] descendants of Ithamar.
6 Shemaia mwana wa Nethaneli mwandishi, Mlawi, aliandika majina yao mbele ya mfalme, muamuzi, kuhani Zadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa makuhani na familia za Walawi. Ukoo mmoja ulichaguliwa kwa kura kutoka uzao wa Eleazari, na kisha uliofata utachaguliwa kutoka uzao wa Ithhamari.
And he recorded them Shemaiah [the] son of Nethanel the scribe one of the Levite[s] before the king and the officials and Zadok the priest and Ahimelech [the] son of Abiathar and [the] heads of the fathers of the priests and of the Levites a house of a father one drawn for Eleazar and drawn - drawn for Ithamar.
7 Kura ya kwanza ilienda kwa Yehoiaribu, ya pili kwa Yedaia,
And it went out the lot first to Jehoiarib to Jedaiah the second.
8 ya tatu kwa Harimu, ya nne kwa Seorimu,
To Harim the third to Seorim the fourth.
9 ya tano kwa Malikija, ya sita kwa Mijamini,
To Malkijah the fifth to Mijamin the sixth.
10 ya saba kwa Hakozi, ya nane kwa Abija,
To Hakkoz the seventh to Abijah the eighth.
11 ya tisa kwa Yeshua, ya kumi kwa Shekania,
To Jeshua the ninth to Shecaniah the tenth.
12 ya kumi na moja kwa Eliashibu, ya kumi na mbili kwa Yakimu,
To Eliashib one [plus] ten to Jakim two [plus] ten.
13 ya kumi na tatu kwa Hupa, ya kumi na nne kwa Yesheheabu,
To Huppah thir-teen to Jeshebeab four-teen.
14 ya kumi na tano kwa Biliga, ya kumi na sita kwa Imma,
To Bilgah fif-teen to Immer six-teen.
15 ya kumi na saba kwa Heziri, ya kumi na nane kwa Hapizezi,
To Hezir seven-teen to Happizzez eight-teen.
16 ya kumi na tisa kwa Pethaia, ya ishirini kwa Yehezikeli,
To Pethahiah nine-teen to Jehezkel the twenty.
17 ya ishirini na moja kwa Yakini, ya ishirini na mbili kwa Gamuli,
To Jakin one and twenty to Gamul two and twenty.
18 ya ishirini na tatu kwa Delaia, na ya ishirini na nne kwa Maazia.
To Delaiah three and twenty to Maaziah four and twenty.
19 Hii ilikuwa taratibu ya utumishi wao, walipo kuja kwenye nyumba ya Yahweh, wakifuata utaratibu waliopewa na Aruni babu yao, kama Yahweh, Mungu wa Israeli, alivyo waagiza.
These [were] group[s] their for service their to go to [the] house of Yahweh according to ordinance their by [the] hand of Aaron ancestor their just as he had commanded him Yahweh [the] God of Israel.
20 Hawa walikuwa Walawi waliobakia: Wana wa Amiramu, Shebueli; wana wa Shebaeli, Yedeia.
And to [the] sons of Levi which remained of [the] sons of Amram Shubael of [the] sons of Shubael Jehdeiah.
21 Wana wa Rehabia: wana wa Rehabia, Ishia kiongozi.
For Rehabiah of [the] sons of Rehabiah the chief Isshiah.
22 Wa Waizari, Shelomothi; mwana wa Shelomothi, Yahathi.
For the Izharite[s] Shelomoth of [the] sons of Shelomoth Jahath.
23 Wana wa Hebroni: Yeria kiongozi, Amaria wapili, Yahazieli watatu, na Yekameamu wanne.
And [the] sons Jeriah Amariah the second Jahaziel the third Jekameam the fourth.
24 Wana wa uzao wa Uzieli ulimjumuisha Mika. Uzao wa Mika ulimjumuisha Shamiri.
[the] sons of Uzziel Micah of [the] sons of Micah (Shamir. *Q(K)*)
25 Kaka wa Mika alikuwa Ishia. Wana wa Ishia akijumuishwa Zakaria.
[the] brother of Micah Isshiah of [the] sons of Isshiah Zechariah.
26 Wana na Merari: Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia, Beno.
[the] sons of Merari Mahli and Mushi [the] sons of Jaaziah (Beno. *L(F)*)
27 Wana wa Merari: Yaazia, Beno, Shohamu, Zakuri, na Ibrri.
[the] sons of Merari of Jaaziah (Beno *L(F)*) and Shoham and Zaccur and Ibri.
28 Wana wa Mahili: eleazari, ambaye alikuwa hana wana.
For [the] Mahlite[s] Eleazar and not it belonged to him sons.
29 Wana wa Kishi: Yerameli
For Kish [the] sons of Kish Jerahmeel.
30 wana wa Mushi: Mahli, Eda, na yerimothi. Walikuwa walawi, walio orodheshwa na familia zao.
And [the] sons of Mushi Mahli and Eder and Jerimoth these [were] [the] sons of the Levites to [the] house of ancestors their.
31 Wanaume hawa ambao walikuwa vichwa katika nyumba za baba zao na kila wadogo zao, walipiga kura katika uwepo wa Mfalme Daudi, na Zadoki na Ahimeleki, pamoja na viongozi wa familia wa makuhani na Walawi. Walirusha kura kama uzao wa Aroni walivyofanya.
And they cast also they lots corresponding to - relatives their [the] descendants of Aaron before David the king and Zadok and Ahimelech and [the] heads of the fathers of the priests and of the Levites fathers the chief corresponding to brother his young.

< 1 Nyakati 24 >