< 1 Nyakati 24 >

1 Makundi vya kazi kulingana na uzao wa Aroni yalikuwa haya: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
Men for Arons Børn vare Skifterne disse: Arons Sønner vare Nadab og Abihu, Eleasar og Ithamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao kufa. Walikuwa hawana watoto, kwahiyo Eleazari na Ithamari walitumika kama makuhani.
Men Nadab og Abihu døde for deres Faders Ansigt, og de havde ingen Børn; og Eleasar og Ithamar gjorde Præstetjeneste.
3 Daudi pamoja na Zadoki, uzao wa Eleazari, na Ahimeleki, uzao wa Ithamari, waliwagawanya katika makundi yao ya kazi kama makuhani.
Og David tillige med Zadok af Eleasars Børn og Akimelek af Ithamars Børn inddelte dem til deres Embede i deres Tjeneste.
4 Kulikuwa na wanaume viongozi zaidi kati ya uzao wa Eleazari kuliko kati ya uzao wa Ithamari, kwahiyo waligawanya uzao wa Eleazari katika makundi kumi na sita. Walifanya hivyo na viongozi wa ukoo na uzao wa Ithamari. Magawanyo haya yalikuwa nane kwa idadi, sambamba na koo zao.
Og der blev flere fundne af Eleasars Børn, som vare Øverster for Mændene, end af Ithamars Børn, da de delte dem; af Eleasars Børn var der seksten Øverster for deres Fædrenehuse, men af Ithamars Børn for deres Fædrenehuse var der otte.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kura, kwa kuwa walikuwa waamuzi watakatifu na waamuzi wa Mungu, kutoka pande zote uzao wa Eleazari na uzao wa Ithamari.
Og de inddelte dem efter Lodkastning, disse med hine; thi der havde været Helligdommens Fyrster og Guds Fyrster saavel af Eleasars Børn som af Ithamars Børn.
6 Shemaia mwana wa Nethaneli mwandishi, Mlawi, aliandika majina yao mbele ya mfalme, muamuzi, kuhani Zadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa makuhani na familia za Walawi. Ukoo mmoja ulichaguliwa kwa kura kutoka uzao wa Eleazari, na kisha uliofata utachaguliwa kutoka uzao wa Ithhamari.
Og Semaja, Nethaneels Søn, Skriveren, en af Leviterne, opskrev dem i Paasyn af Kongen og Fyrsterne, og Zadok, Præsten, og Akimelek, Abjathars Søn, og Øversterne for Fædrenehusene blandt Præsterne og Leviterne; et Fædrenehus blev udtrukket for Eleasar, et andet blev skiftevis udtrukket for Ithamar.
7 Kura ya kwanza ilienda kwa Yehoiaribu, ya pili kwa Yedaia,
Den første Lod kom ud for Jojarib, den anden for Jedaja,
8 ya tatu kwa Harimu, ya nne kwa Seorimu,
den tredje for Harim, den fjerde for Seorim,
9 ya tano kwa Malikija, ya sita kwa Mijamini,
den femte for Malkia, den sjette for Mijamin,
10 ya saba kwa Hakozi, ya nane kwa Abija,
den syvende for Hakkoz, den ottende for Abia,
11 ya tisa kwa Yeshua, ya kumi kwa Shekania,
den niende for Jesua, den tiende for Sekania,
12 ya kumi na moja kwa Eliashibu, ya kumi na mbili kwa Yakimu,
den ellevte for Eljasib, den tolvte for Jakim,
13 ya kumi na tatu kwa Hupa, ya kumi na nne kwa Yesheheabu,
den trettende for Hufa, den fjortende for Jesebab,
14 ya kumi na tano kwa Biliga, ya kumi na sita kwa Imma,
den femtende for Bilga, den sekstende for Immer,
15 ya kumi na saba kwa Heziri, ya kumi na nane kwa Hapizezi,
den syttende for Hesir, den attende for Hafizez,
16 ya kumi na tisa kwa Pethaia, ya ishirini kwa Yehezikeli,
den nittende for Petakia, den tyvende for Ezekiel,
17 ya ishirini na moja kwa Yakini, ya ishirini na mbili kwa Gamuli,
den en og tyvende for Jakin, den to og tyvende for Gamul,
18 ya ishirini na tatu kwa Delaia, na ya ishirini na nne kwa Maazia.
den tre og tyvende for Delaja, den fire og tyvende for Maaseja.
19 Hii ilikuwa taratibu ya utumishi wao, walipo kuja kwenye nyumba ya Yahweh, wakifuata utaratibu waliopewa na Aruni babu yao, kama Yahweh, Mungu wa Israeli, alivyo waagiza.
Disses Embedsgerning var det at gaa ind i Herrens Hus, som deres Vis var, efter deres Faders, Arons, Anvisning, saaledes som Herren, Israels Gud havde budt ham.
20 Hawa walikuwa Walawi waliobakia: Wana wa Amiramu, Shebueli; wana wa Shebaeli, Yedeia.
Og hvad de øvrige af Levis Børn angaar, da var der af Amrams Sønner Subael, af Subaels Sønner Jedeja.
21 Wana wa Rehabia: wana wa Rehabia, Ishia kiongozi.
Hvad Rehabia angaar, da var af Rehabias Sønner Jissija den første.
22 Wa Waizari, Shelomothi; mwana wa Shelomothi, Yahathi.
Af Jizehariterne var der Selomoth, af Selomoths Sønner var der Jahath;
23 Wana wa Hebroni: Yeria kiongozi, Amaria wapili, Yahazieli watatu, na Yekameamu wanne.
og Jerijas Sønner: Amaria var den anden, Jehasiel den tredje, Jekameam den fjerde.
24 Wana wa uzao wa Uzieli ulimjumuisha Mika. Uzao wa Mika ulimjumuisha Shamiri.
Af Ussiels Sønner var der Mika, af Mikas Sønner var der Samir.
25 Kaka wa Mika alikuwa Ishia. Wana wa Ishia akijumuishwa Zakaria.
Jissija var Mikas Broder; af Jissijas Sønner var der Sakaria.
26 Wana na Merari: Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia, Beno.
Meraris Sønner vare: Maheli og Musi, Børn af hans Søn Jasia.
27 Wana wa Merari: Yaazia, Beno, Shohamu, Zakuri, na Ibrri.
Meraris Børn af hans Søn Jasia vare baade Skoam og Sakur og Ibri.
28 Wana wa Mahili: eleazari, ambaye alikuwa hana wana.
Af Maheli var der Eleasar, og han havde ingen Sønner.
29 Wana wa Kishi: Yerameli
Hvad Kis angaar, Kis's Sønner vare Jeramel.
30 wana wa Mushi: Mahli, Eda, na yerimothi. Walikuwa walawi, walio orodheshwa na familia zao.
Og Musis Sønner vare: Maheli og Eder og Jerimoth; disse ere Leviternes Børn efter deres Fædres Hus.
31 Wanaume hawa ambao walikuwa vichwa katika nyumba za baba zao na kila wadogo zao, walipiga kura katika uwepo wa Mfalme Daudi, na Zadoki na Ahimeleki, pamoja na viongozi wa familia wa makuhani na Walawi. Walirusha kura kama uzao wa Aroni walivyofanya.
Ogsaa de kastede Lod ligesom deres Brødre, Arons Børn, i Paasyn af Kong David og Zadok og Akimelek, og Øversterne for Fædrenehusene iblandt Præsterne og Leviterne, Øversten for Fædrenehuset saavel som hans yngste Broder.

< 1 Nyakati 24 >