< 1 Nyakati 23 >

1 Daudi alipo kuwa mzee na kukaribia mwisho wa maisha yake, alimfanya Sulemani mwanae mfalme juu ya Israeli.
And David was old and satisfied with days, and he causes his son Solomon to reign over Israel,
2 Aliwakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, na makuhani na Walawi.
and gathers all the heads of Israel, and the priests, and the Levites;
3 Walawi walio kuwa miaka thelathini na zaidi walihesabiwa. Idadi ya elfu thelathini na nane.
and the Levites are numbered from a son of thirty years and upward, and their number, for their counted heads, is of thirty-eight thousand mighty men.
4 Kwa hawa, elfu ishirini na nne walikuwa kusimamia kazi ya nyumba ya Yahweh, na elfu sita walikuwa maaskari na waamuzi.
Of these, twenty-four thousand [are] to preside over the work of the house of YHWH, and six thousand officers and judges,
5 Elfu nne walikuwa walinzi wa lango, na elfu nne walikuwa wamsifu Yahweh na vyombo nilivyo vitengeneza vya kusifu.” Daudi akasema.
and four thousand gatekeepers, and four thousand giving praise to YHWH, “with instruments that I made for praising,” [says David.]
6 Akawatenganisha kwenye vikundi kulingana na wana wa Levi: Gerishoni, Kohathi, na Merari.
And David distributes them into divisions of the sons of Levi—of Gershon, Kohath, and Merari.
7 Kwa koo za uzao wa Gerishoni, kulilkuwa na Ladani na Shimei.
Of the Gershonite: Laadan and Shimei.
8 Palikuwa na watatu wa wana wa Ladani: Yehieli kiongozi, Zethami, na Yoeli.
Sons of Laadan: the head [is] Jehiel, and Zetham, and Joel—three.
9 Palikuwa na watatu wa wana wa Shimei: Shelomothi, Hazieli, na Harani. Hawa walikuwa viongozi wa koo ya Ladani.
Sons of Shimei: Shelomith, and Haziel, and Haran—three; these [are] heads of the fathers of Laadan.
10 Palikuwa na wanne wa wana wa Shimei: Yahathi, Ziza, Yeushi, na Beria.
And sons of Shimei: Jahath, Zina, and Jeush, and Beriah; these [are] the four sons of Shimei.
11 Yahathi alikuwa mkubwa, Ziza wapili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi, hivyo walihesabiwa kama ukoo mmoja na kupangiwa kazi sawa.
And Jahath is the head, and Zizah the second, and Jeush and Beriah have not multiplied sons, and they become the house of a father by one numbering.
12 Palikuwa na wanne wa wana wa Kohathi: Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
Sons of Kohath: Amram, Izhar, Hebron, and Uzziel—four.
13 Hawa walikuwa wana wa Amramu: Aruni na Musa. Aruni alichaguliwa kuandaa vitu vitakatifu, yeye na uzao wake watatoa uvumba kwa Yahweh, kumtumikia na kumpa baraka kwa jina lake.
Sons of Amram: Aaron and Moses; and Aaron is separated for his sanctifying the Holy of Holies, he and his sons, for all time, to make incense before YHWH, to serve Him, and to bless in His Name for all time.
14 Lakini kwa Musa mtu wa Mungu, wana wake walihesabiwa kuwa Walawi.
As for Moses, the man of God, his sons are called after the tribe of Levi.
15 Wana wa Musa walikuwa Gerishomu na Eliezeri.
Sons of Moses: Gershom and Eliezer.
16 Uzao wa Gerishomu ulikuwa Shebueli mkubwa.
Sons of Gershom: Shebuel the head.
17 Uzao wa Eliezeri alikuwa Rehabia. Eliezeri hakuwa na wana wengine, lakini Rehabia alikuwa na uzao mkubwa.
And sons of Eliezer are Rehabiah the head, and Eliezer had no other sons, and the sons of Rehabiah have multiplied exceedingly.
18 Mwana wa Izihari alikuwa Shelomithi kiongonzi.
Sons of Izhar: Shelomith the head.
19 Uzao wa Hebroni ulikuwa Yeria, mkubwa, Amaria wapili, Yahazieli watatu, na Yekameamu wanne.
Sons of Hebron: Jeriah the head, Amariah the second, Jahaziel the third, and Jekameam the fourth.
20 Wana wa Uzieli walikuwa Mika mkubwa, na Ishia wapili.
Sons of Uzziel: Micah the head, and Ishshiah the second.
21 Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Wana wa Mahili walikuwa Eleazari na Kishi.
Sons of Merari: Mahli and Mushi; sons of Mahli: Eleazar and Kish.
22 Eleazari alikufa bila mtoto wa kiume. Alikuwa na mabinti tu. Wana wa Kishi waliwaoa.
And Eleazar dies, and he had no sons, but daughters, and their brothers, sons of Kish, take them.
23 Wana wa Mushi watatu walikuwa Mahili, Ederi, na Yeremothi.
Sons of Mushi: Mahli, and Eder, and Jerimoth—three.
24 Hawa walikuwa uzao wa Lawi kuligana na koo zao. Walikuwa viongozi, wamehesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, kuanzia koo zilizo fanya kazi katika nyumba ya Yahweh, kutoka miaka ishirini na zaidi.
These [are] sons of Levi, by the house of their fathers, heads of the fathers, by their appointments, in the number of names, by their counted heads, doing the work for the service of the house of YHWH, from a son of twenty years and upward,
25 Kwa kuwa Daudi alisema, “Yahweh, Mungu wa Israeli, amewapa pumziko watu wake. Anafanya makao yake Yerusalemu milele.
for David said, “YHWH, God of Israel, has given rest to His people, and He dwells in Jerusalem for all time”;
26 Walawi hawataitaji kubeba hema la kuabuadia na vifaa vyake vinavyo tumika kwenye utumishi wake.”
and also of the Levites, “None [are] to carry the Dwelling Place and all its vessels for its service”;
27 Kwa maneno ya Daudi ya mwisho Walawi walihesabiwa, miaka ishirini na kuendelea.
for by the last words of David they [took] the number of the sons of Levi from a son of twenty years and upward,
28 Wajibu wao ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aruni katika utumishi wa nyumba ya Yahweh. Walikuwa washughulikie nyuani, vyumbani, utakasaji wa vitu vyote vya Yahweh, na kazi zingine katika utumishi wa nyumba ya Mungu.
for their station [is] at the side of the sons of Aaron, for the service of the house of YHWH, over the courts, and over the chambers, and over the cleansing of every holy thing, and the work of the service of the house of God,
29 Pia walishughulikia mkate wa uwepo, unga safi wa mbegu za sadaka, maandazi ya siotiwa chachu, sadaka za ngano, sadaka ziliochanganywa na mafuta, na vipimo vyote vya idadi n a ukubwa wa vitu.
and for the bread of the arrangement, and for fine flour for present, and for the thin unleavened cakes, and for [the work of] the pan, and for that which is stirred, and for all [liquid] measure and [solid] measure;
30 Pia walisimama kila asubui kumshukuru na kumsifu Yahweh. Pia walifanya hivi jioni
and to stand, morning by morning, to give thanks, and to give praise to YHWH, and so at evening;
31 na kila wakati sadaka ya kuteketezwa ilipo tolewa kwa Yahweh, siku ya Sabato na sherehe za mwezi mpya na siku za maakuli. Idadi iliyo pangwa, iliyo tolewa kwa amri, ilipaswa kuwa mbele ya Yahweh.
and for all the burnt-offerings—burnt-offerings to YHWH for Sabbaths, for new moons, and for appointed times, by number, according to the ordinance on them continually, before YHWH.
32 Walikuwa viongozi wa hema la kukutania, patakatifu, na kuwasaidia ndugu zao wa uzao wa Aruni katika utumishi wa nyumba ya Yahweh.
And they have kept the charge of the Tent of Meeting, and the charge of the holy place, and the charge of their brothers, the sons of Aaron, for the service of the house of YHWH.

< 1 Nyakati 23 >