< 1 Nyakati 22 >

1 Kisha Daudi akasema, “Hapo ndipo nyumba ya Yahweh Mungu itakuwepo, na madhabahu ya sadaka za kuteketezwa za Israeli.”
Then David said, “This is where the house of Yahweh God will be, with the altar for the burnt offerings of Israel.”
2 Hivyo Daudi akaagiza watumishi wake wawakusanye pamoja wageni wote wanao ishi katika nchi ya Israeli. Aliwapangia kuwa wachonga mawe, kuchonga matofali ya mawe, ilikuweza kujenga nyumba ya Mungu.
So David ordered his servants to gather together the foreigners living in the land of Israel. He assigned them to be stonecutters, to cut stone blocks, in order to build God's house.
3 Daudi alisambaza idadi kubwa ya chuma kwa ajili ya misumari na vitasa vya kuweka kwenye malango. Pia alitoa shaba zaidi kushinda kipimo,
David supplied a large amount of iron for the nails for the doors to go in the gateways, and for braces. He also supplied more bronze than could be weighed,
4 na miti ya mierezi zaidi ya kipimo. (Wasidoni na Watiria walileta mboa nyingi za mierezi kwa Daudi azihesabu.)
and more cedar trees than could be counted. (The Sidonians and the Tyrians brought too many cedar logs to David to count.)
5 Daudi akasema, “Mwanangu Sulemani ni mdogo na hana uzoefu, na nyumba itayo jengwa kwa Yahweh lazima iwe maridadi, ilikwamba iwe maarufu na ya utukufu kwa nchi zingine. Hivyo nitaanda ujenzi wake.” Hivyo Daudi akafanya maandalizi ya kina kabla ya mauti yake.
David said, “My son Solomon is young and inexperienced, and the house that is to be built for Yahweh must be especially magnificent, so that it will be famous and glorious in all other lands. So I will prepare for its building.” So David made extensive preparations before his death.
6 Akaagiza Sulemani mwanae kuitwa na kumuamuru ajenge nyumba ya Yahweh, Mungu wa Israeli.
Then he called for Solomon his son and commanded him to build a house for Yahweh, the God of Israel.
7 Daudi akasema kwa Sulemani, “Mwanangu, ilikuwa dhamira yangu kujenga nyumba mwenyewe, kwa ajili ya jina la Yahweh Mungu wangu.
David said to Solomon, “My son, it was my intention to build a house myself, for the name of Yahweh my God.
8 Lakini Yahweh alikuja kwangu na kusema, 'Wewe umemwaga damu nyingi na umepigana mapambono mengi. Hauta jenga nyumba kwa jina langu, kwasababu umemwaga damu nyingi kwenye ardhi machoni pangu.
But Yahweh came to me and said, 'You have shed much blood and have fought many battles. You will not build a house for my name, because you have shed much blood on the earth in my sight.
9 Walakini, utapata mwana ambaye atakuwa mtu wa amani. Nitampa kupumzika na maadui zake kwa kila upande. Kwa kuwa jina lake litaitwa Sulemani, na nitatoa amani na utulivu kwa Israeli katika siku zake.
However, you will have a son who will be a peaceful man. I will give him rest from all his enemies on every side. For his name will be Solomon, and I will give peace and quiet to Israel in his days.
10 Ata jenga nyumba kwa jina langu. Ata kuwa mwana wangu, na nitakuwa baba yake. Nitaimarisha kiti cha enzi cha ufalme wake juu ya Israeli.
He will build a house for my name. He will be my son, and I will be his father. I will establish the throne of his kingdom over Israel forever.'
11 Sasa, mwanangu, Yahweh awe nawe na kukuwezesha kufanikiwa. Uweze kujenga nyumba ya Yahweh Mungu wako, kama alivyo sema utajenga.
Now, my son, may Yahweh be with you and enable you to succeed. May you build the house of Yahweh your God, as he said you would.
12 Yahweh tu akupe uwelewa na ufahamu, ili utii sheria ya Yahweh Mungu wako, ata kapokuweka kiongozi juu ya Israeli.
Only may Yahweh give you insight and understanding, so that you may obey the law of Yahweh your God, when he places you in charge over Israel.
13 Kisha utafanikiwa, kama tu ukitii maagizo na amri Yahweh alizo mpa Musa kuhusu Israeli. Kuwa hodari na mshujaa. Usiogope wala kufadhaika.
Then you will succeed, if you carefully obey the statutes and the decrees that Yahweh gave to Moses concerning Israel. Be strong and courageous. Do not fear or be discouraged.
14 Sasa, ona, kwa bidii kubwa nimeandaa kwa ajili ya nyumba ya Yahweh talanta 100, 000 za dhahabu, talanta milioni moja za fedha, na shaba na chuma katika idadi kubwa. Pia nimetoa mbao na mawe. Lazima uongeze zaidi katika haya.
Now, see, at great effort I have prepared for Yahweh's house 100,000 talents of gold, one million talents of silver, and bronze and iron in large quantities. I have also provided timber and stone. You must add more to all this.
15 Una wafanya kazi wengi: wachonga mawe, maseremala, wanaume wenye ujuzi mbali mbali,
You have many workmen with you: stonecutters, masons, carpenters, and skillful craftsmen without number of every kind,
16 wenye uwezo wa kufanya kazi na dhahabu, fedha, shaba, na nishati. Hivyo anza kufanya kazi, na Yahweh awe nawe.
who can work with gold, silver, bronze, and iron. Arise and begin the work, and may Yahweh be with you.”
17 Daudi akawaagiza viongozi wote Waisraeli wamsaidie Sulemani mwanae, akisema,
David also ordered all the leaders of Israel to help Solomon his son, saying,
18 “Yahweh Mungu wenu yupo nanyi na amewapa amani kila pande. Amewakabidhi mikononi mwangu wenyeji wote mkoa. Mkoa umetiishwa mbele za Yahweh na watu wake.
“Yahweh your God is with you and has given you peace on every side. He has given the region's inhabitants into my hand. The region is subdued before Yahweh and his people.
19 Sasa mtafuteni Yahweh Mungu wenu kwa moyo wenu wote na nafsi. Simameni na mjenge sehemu takatifu ya Yahweh Mungu. Kisha mwaweza kuleta sanduku la agano la Yahweh na vitu vya Mungu ndani ya nyumba iliyo jengwa kwa ajili ya jina la Yahweh.
Now seek Yahweh your God with all your heart and your soul. Get up and build the holy place of Yahweh God. Then you can bring the ark of the covenant of Yahweh and the things that belong to God into the house built for Yahweh's name.”

< 1 Nyakati 22 >