< 1 Nyakati 22 >

1 Kisha Daudi akasema, “Hapo ndipo nyumba ya Yahweh Mungu itakuwepo, na madhabahu ya sadaka za kuteketezwa za Israeli.”
Then David said, “Here, [at the edge of Jerusalem, ] is where [we will build] the temple for our God Yahweh, and where [we will make] the altar for burning the offerings that the Israeli [people will bring].”
2 Hivyo Daudi akaagiza watumishi wake wawakusanye pamoja wageni wote wanao ishi katika nchi ya Israeli. Aliwapangia kuwa wachonga mawe, kuchonga matofali ya mawe, ilikuweza kujenga nyumba ya Mungu.
So David commanded that the foreigners who lived in Israel must gather together. [When they did that, ] he appointed [some of those] men to [cut huge] stones [from the quarries] and to smooth their surfaces, to be used to build the temple of God.
3 Daudi alisambaza idadi kubwa ya chuma kwa ajili ya misumari na vitasa vya kuweka kwenye malango. Pia alitoa shaba zaidi kushinda kipimo,
David provided a large amount of iron for making nails and hinges for the doors in the gates of the temple. He also provided so much bronze [for making the altar and various utensils], that no one could weigh it all.
4 na miti ya mierezi zaidi ya kipimo. (Wasidoni na Watiria walileta mboa nyingi za mierezi kwa Daudi azihesabu.)
He also provided [money for buying] a large amount of cedar logs. Because there was a huge number of them, no one was able to count them. Those were logs that men from Tyre and Sidon [cities] sent to David.
5 Daudi akasema, “Mwanangu Sulemani ni mdogo na hana uzoefu, na nyumba itayo jengwa kwa Yahweh lazima iwe maridadi, ilikwamba iwe maarufu na ya utukufu kwa nchi zingine. Hivyo nitaanda ujenzi wake.” Hivyo Daudi akafanya maandalizi ya kina kabla ya mauti yake.
David [provided all those things because he] thought, “My son Solomon is still young and he does not know what he needs to know [about building], and the temple of Yahweh must be (magnificent/very beautiful). It must be a glorious building that will become famous, and people throughout the world must consider it to be glorious/splendid. So now I will begin to prepare for it to be built, [and Solomon will be responsible for building it].” So David collected a great amount of building materials before he died.
6 Akaagiza Sulemani mwanae kuitwa na kumuamuru ajenge nyumba ya Yahweh, Mungu wa Israeli.
[When] David [was old, he] summoned his son Solomon, and told him that he should arrange for a temple to be built for Yahweh, the God whom the Israelis [worshiped].
7 Daudi akasema kwa Sulemani, “Mwanangu, ilikuwa dhamira yangu kujenga nyumba mwenyewe, kwa ajili ya jina la Yahweh Mungu wangu.
He said to him, “I wanted [IDM] to build a temple to honor [MTY] Yahweh, my God.
8 Lakini Yahweh alikuja kwangu na kusema, 'Wewe umemwaga damu nyingi na umepigana mapambono mengi. Hauta jenga nyumba kwa jina langu, kwasababu umemwaga damu nyingi kwenye ardhi machoni pangu.
But Yahweh told [a prophet to tell] me, ‘You have killed many men [MTY] in the battles that you have fought. I have seen the blood of all the people whom you killed, so you will not be the one who will arrange for a temple to be built to honor me [MTY].
9 Walakini, utapata mwana ambaye atakuwa mtu wa amani. Nitampa kupumzika na maadui zake kwa kila upande. Kwa kuwa jina lake litaitwa Sulemani, na nitatoa amani na utulivu kwa Israeli katika siku zake.
But you will have a son [who will be king of Israel after you die]. He will be a man who is peaceful and quiet, [not a man who kills others]. And I will cause that there will be peace between him and his enemies who are in all the nearby lands. His name will be Solomon, [which sounds like the word for peace]. During the time that he is king, people in Israel will be peaceful and safe.
10 Ata jenga nyumba kwa jina langu. Ata kuwa mwana wangu, na nitakuwa baba yake. Nitaimarisha kiti cha enzi cha ufalme wake juu ya Israeli.
He is the one who will arrange for a temple to be built to honor me [MTY]. He will be [like] a son to me, and I will cause some of his descendants to rule [MTY] over Israel forever [HYP].’
11 Sasa, mwanangu, Yahweh awe nawe na kukuwezesha kufanikiwa. Uweze kujenga nyumba ya Yahweh Mungu wako, kama alivyo sema utajenga.
“So now, my son, I hope/wish that Yahweh will help you, and enable you to be successful in arranging for building the temple of Yahweh, your God, which is what he said that you would do.
12 Yahweh tu akupe uwelewa na ufahamu, ili utii sheria ya Yahweh Mungu wako, ata kapokuweka kiongozi juu ya Israeli.
I also hope/wish that he will enable you to be wise and to understand what you need to know, and enable you to obey his laws while you rule over Israel.
13 Kisha utafanikiwa, kama tu ukitii maagizo na amri Yahweh alizo mpa Musa kuhusu Israeli. Kuwa hodari na mshujaa. Usiogope wala kufadhaika.
If you carefully obey all the laws and regulations/commands that Yahweh gave to Moses to give to us Israeli people, you will be successful. So be steadfast/strong and courageous. Do not be afraid of anything, and do not become discouraged!
14 Sasa, ona, kwa bidii kubwa nimeandaa kwa ajili ya nyumba ya Yahweh talanta 100, 000 za dhahabu, talanta milioni moja za fedha, na shaba na chuma katika idadi kubwa. Pia nimetoa mbao na mawe. Lazima uongeze zaidi katika haya.
“I have tried hard to provide [materials] for [building] the temple of Yahweh. I have provided nearly 4,000 tons of gold, and nearly 40,000 tons of silver. I have also provided a very large amount of iron and bronze; no one has been able to weigh it all. I have also gathered/provided lumber and stone [for the walls of the temple], but you may need to get some more of those things.
15 Una wafanya kazi wengi: wachonga mawe, maseremala, wanaume wenye ujuzi mbali mbali,
There are many men [in Israel] who have good ability to cut big stones for making stone walls, and carpenters, and men who are very skilled at making various kinds of things.
16 wenye uwezo wa kufanya kazi na dhahabu, fedha, shaba, na nishati. Hivyo anza kufanya kazi, na Yahweh awe nawe.
There are many men who know how to make things from gold and silver and bronze and iron. So now [I say to you], begin the work [of building the temple], and I hope/wish that Yahweh will help/be with you.”
17 Daudi akawaagiza viongozi wote Waisraeli wamsaidie Sulemani mwanae, akisema,
Then David commanded that all the Israeli leaders must assist Solomon. He said to them,
18 “Yahweh Mungu wenu yupo nanyi na amewapa amani kila pande. Amewakabidhi mikononi mwangu wenyeji wote mkoa. Mkoa umetiishwa mbele za Yahweh na watu wake.
“Yahweh our God is certainly with/helping you [RHQ]. He has allowed you to have peace with all the nearby nations [RHQ]. He has enabled my [army] to conquer [IDM] them, so now Yahweh and my people control them.
19 Sasa mtafuteni Yahweh Mungu wenu kwa moyo wenu wote na nafsi. Simameni na mjenge sehemu takatifu ya Yahweh Mungu. Kisha mwaweza kuleta sanduku la agano la Yahweh na vitu vya Mungu ndani ya nyumba iliyo jengwa kwa ajili ya jina la Yahweh.
Now you must obey Yahweh completely. Help Solomon to arrange for building the temple for Yahweh God, in order that you can bring the Sacred Chest that contains the Ten Commandments and the other sacred items that belong to God into the temple that you will build to honor Yahweh.”

< 1 Nyakati 22 >