< 1 Nyakati 21 >

1 Adui akainuka dhidi ya Israeli na kumchochea Daudi kuhesabu Israeli.
Then Satan stands up against Israel, and persuades David to number Israel,
2 Daudi akamwabia Yoabu na kwa wakuu wa Jeshi, “Nenda, wahesabu watu wa Israeli kutoka Beerisheba mpaka Dani na uniletee taarifa, ilinijue idadi yao.”
and David says to Joab and to the heads of the people, “Go, number Israel from Beer-Sheba even to Dan, and bring [the account] to me, and I know their number.”
3 Yoabu akasema, “Yahweh na afanya jeshi lake mara mia zaidi ya lilivyo. Lakini bwana wangu mfalme, kwani wote hawamtumikii bwana wangu? kwa nini bwana wangu anataka hili? Kwa nini ulete hatia kwa Israeli?”
And Joab says, “YHWH adds to His people as they are one hundred times; are they not, my lord, O king, all of them for servants to my lord? Why does my lord seek this? Why is he for a cause of guilt to Israel?”
4 Lakini neno la mfalme halikubadilika kwa Yoabu. Hivyo Yoabu akaondoka na kwenda Israeli yote. Kisha akarudi Yerusalemu.
And the word of the king [is] severe against Joab, and Joab goes out, and goes up and down in all Israel, and comes to Jerusalem.
5 Yoabu akatoa taarifa ya idadi ya jumla ya wanaume wa mapambano kwa Daudi. Kulikuwa ndani ya Israeli wanaume 1, 100, 000 walio beba upanga. Yuda peke yake kulikuwa na wanajeshi 470, 000.
And Joab gives the account of the numbering of the people to David, and all Israel is one million and one hundred thousand, each drawing sword, and Judah [is] four hundred and seventy thousand, each drawing sword.
6 Lakini Levi na Benjamini hawaku hesabiwa miongoni mwao, kwa kuwa amri ya mfalme ilimuudhi Yoabu.
And he has not numbered Levi and Benjamin in their midst, for the word of the king was abominable with Joab.
7 Mungu alikwazika na hili tendo, akashambulia Israeli.
And it is evil in the eyes of God concerning this thing, and He strikes Israel,
8 Daudi akamwambia Mungu, “Nimetenda dhambi kubwa kwa kufanya hili. Sasa chukua hatia ya mtumishi wako, nimetenda kwa ujinga sana.”
and David says to God, “I have sinned exceedingly in that I have done this thing; and now, please cause the iniquity of Your servant to pass away, for I have acted very foolishly.”
9 Yahweh akamwambia Gadi, nabii wa Daudi,
And YHWH speaks to Gad, seer of David, saying,
10 “Nenda useme kwa Daudi, “Hili ndilo Yahweh anasema: Ninakupa maamuzi matatu. Chagua moja wapo.”
“Go, and you have spoken to David, saying, Thus said YHWH: I am extending three [choices] to you; choose one of these for yourself, and I do [it] to you.”
11 Hivyo Gadi akaenda kwa Daudi na kusema, “Yahweh anasema hivi, 'Chagua moja ya haya:
And Gad comes to David and says to him, “Thus said YHWH: Take for yourself—
12 kati ya miaka mitatu ya ukame, miezi mitatu unakimbizwa na adui zako na kupatwa na upanga wao, au siku tatu za upanga wa Yahweh, yani, pigo katika nchi, malaika wa Yahweh akiharibu nchi yote ya Israeli.' Hivyo sasa, amua jibu gani ni mpelekee yeye aliye nituma.”
either famine for three years, or three months to be consumed from the face of your adversaries (even [for] the sword of your enemies to overtake), or three days of the sword of YHWH (even pestilence in the land, and a messenger of YHWH destroying in all the border of Israel); and now, see; what word do I return to Him who is sending me?”
13 Kisha Daudi akamwambia Gadi, “Nipo katika shida kubwa sana. Acha nianguke katika mikono ya Yahweh kuliko kuangukia mikono ya mwanadamu, sababu matendo yake ya rehema ni makubwa mno.”
And David says to Gad, “I am greatly distressed, please let me fall into the hand of YHWH, for His mercies [are] very many, and do not let me fall into the hand of man.”
14 Hivyo Yahweh akatuma pigo Israeli, na watu elfu sabini wakafa.
And YHWH gives a pestilence in Israel, and there falls from Israel seventy thousand men,
15 Mungu akatuma malaika Yerusalemu kuiharibu. Wakati alipo taka kuiharibu, Yahweh akatazama na kubadili nia yake kuhusu shambulio. Akasema kwa malaika wa uharibifu, “Imetosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Yahweh alikua amesimama eneo la kupeta la Orinani Myebusi.
and God sends a messenger to Jerusalem to destroy it, and as he is destroying, YHWH has seen, and is comforted concerning the calamity, and says to the messenger who [is] destroying, “Enough now, cease your hand.” And the messenger of YHWH is standing by the threshing-floor of Ornan the Jebusite,
16 Daudi akatazama juu na kuona malaika wa Yahweh amesimama kati ya nchi na mbingu, akiwa na upanga mkonono mwake akiuelekeza Yerusalemu. Kisha Daudi na wazee, wakiwa wamevaa magunia, wakalala chini uso ukiwa kwenye ardhi.
and David lifts up his eyes, and sees the messenger of YHWH standing between the earth and the heavens, and his sword [is] drawn in his hand, stretched out over Jerusalem, and David falls, and the elderly, covered with sackcloth, on their faces.
17 Daudi akamwambia Mungu, “Sio mimi niliye amuru jeshi kuhesabiwa? Nimefanya hichi kitu kiovu. Lakini hawa kondoo, wamefanya nini? Yahweh Mungu wangu! Acha mkono wako unipige mimi na familia yangu, lakini usiache pigo iliendelee kubaki kwa watu wako.”
And David says to God, “Did I not command to number the people? Indeed, it [is] I who have sinned, and done great evil: and these, the flock, what did they do? O YHWH, my God, please let Your hand be on me, and on the house of my father, and not on Your people—to be plagued.”
18 Hivyo malaika wa Yahweh akamuamuru Gadi kusema kwa Daudi, kwamba Daudi aende juu na kujenga madhabahu ya Yahweh katika eneo la kupeta la Oranani Myebusi.
And the messenger of YHWH commanded to Gad to say to David, “Surely David goes up to raise an altar to YHWH in the threshing-floor of Ornan the Jebusite.”
19 Daudi akaenda kama Gadi alivyo muelekeza cha kufanya kwa jina la Yahweh.
And David goes up by the word of Gad, that he spoke in the Name of YHWH.
20 Wakati Orinani akipepeta ngano, aligeuka na kumuona malaika. Yeye na wana wake wanne wakajificha.
And Ornan turns back and sees the messenger, and his four sons [are] with him hiding themselves, and Ornan is threshing wheat.
21 Wakati Daudi alipo kuja kwa Orinani, Orinani akatazama na kumuona Daudi. Aliacha eneo la kupeta na akamuinamia Daudi uso wake ukiwa kwenye ardhi.
And David comes to Ornan, and Ornan looks attentively and sees David, and goes out from the threshing-floor, and bows himself to David—face to the earth.
22 Kisha Daudi akasema kwa Orinani, “Niuzie hili eneo la kupeta, iliniweze kumjenga Yahweh madhabahu. Nitalipa gharama yote, ili pigo liondolewe kwa watu.”
And David says to Ornan, “Give the place of the threshing-floor to me, and I build an altar to YHWH in it; give it to me for full price, and the plague is restrained from the people.”
23 Orinani wakwambia Daudi, “Chukuwa kama lako, bwana wangu mfalme. Fanya nalo linalo kupendeza. Tazama, nitakupa ng'ombe kwa sadaka ya kuteketeza, vifaa vya kupeta kwa ajili ya mbao, na ngano kwa sadaka ya mbegu; nitakupa yote wewe.”
And Ornan says to David, “Take [it] to yourself, and my lord the king does that which is good in his eyes; see, I have given the oxen for burnt-offerings, and the threshing instruments for wood, and the wheat for a present; I have given the whole.”
24 Mfalme Daudi akamwambia Orinani, “Hapana, nina sisitiza kununua kwa bei yote. Sitachukua kilicho chako na kutoa kama sadaka ya kuteketeza kwa Yahweh kama haitanighramu chochote.”
And King David says to Ornan, “No, for I surely buy [it] for full price; for I do not lift up that which is yours to YHWH, so as to offer a burnt-offering without cost.”
25 Hivyo Daudi akalipa shekeli mia sita ya dhahabu kwa hilo eneo.
And David gives to Ornan six hundred shekels of gold [in] weight for the place;
26 Daudi akajenga madhabahu ya Yahweh pale na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za ushirika. Akamuita Yahweh, aliye mjibu kwa moto kutoka mbinguni kwenye madhabahu ya sadaka za kuteketezwa.
and David builds an altar to YHWH there, and offers burnt-offerings and peace-offerings, and calls to YHWH, and He answers him from the heavens with fire on the altar of the burnt-offering.
27 Kisha Yahweh akampa agizo malaika, na malaika akarudisha upanga kwenye mfuko wake.
And YHWH speaks to the messenger, and he turns back his sword to its sheath.
28 Daudi alipo ona kuwa Yahweh amemjibu kwenye eneo la kupeta la Orinani Myebusi, alitoa dhabihu pale pale kwa wakati huo.
At that time, when David sees that YHWH has answered him in the threshing-floor of Ornan the Jebusite, then he sacrifices there;
29 Sasa kwa wakati huo, hema la kuabudia la Yahweh, ambalo Musa alilitengeneza nyikani, na madhabahu ya sadaka za kuteketezwa, zilikuwa sehemu ya juu huko Gibeoni.
and the Dwelling Place of YHWH that Moses made in the wilderness, and the altar of the burnt-offering, [are] at that time at a high place in Gibeon;
30 Walakini, Daudi hakuweza kwenda huko kumuliza Mungu muelekeo, kwa kuwa alikuwa anaogopa upanga wa malaika wa Yahweh.
and David is not able to go before it to seek God, for he has been afraid because of the sword of the messenger of YHWH.

< 1 Nyakati 21 >