< 1 Nyakati 21 >

1 Adui akainuka dhidi ya Israeli na kumchochea Daudi kuhesabu Israeli.
And the Accuser stood up against Israel, and incited David to count Israel.
2 Daudi akamwabia Yoabu na kwa wakuu wa Jeshi, “Nenda, wahesabu watu wa Israeli kutoka Beerisheba mpaka Dani na uniletee taarifa, ilinijue idadi yao.”
And David said to Joab, and to the princes of the people, Go, number Israel from Beer-sheba' even to Dan, and bring their number to me, that I may know it.
3 Yoabu akasema, “Yahweh na afanya jeshi lake mara mia zaidi ya lilivyo. Lakini bwana wangu mfalme, kwani wote hawamtumikii bwana wangu? kwa nini bwana wangu anataka hili? Kwa nini ulete hatia kwa Israeli?”
Then said Joab, May the Lord add unto his people, how many soever they be, a hundred-fold more: are they not all, my lord the king, my lord's servants? why then will my lord require this thing? why shall it be a cause of guiltiness for Israel?
4 Lakini neno la mfalme halikubadilika kwa Yoabu. Hivyo Yoabu akaondoka na kwenda Israeli yote. Kisha akarudi Yerusalemu.
Nevertheless the king's word remained firm against Joab; and Joab went out, and moved about throughout all Israel, and came [back] to Jerusalem.
5 Yoabu akatoa taarifa ya idadi ya jumla ya wanaume wa mapambano kwa Daudi. Kulikuwa ndani ya Israeli wanaume 1, 100, 000 walio beba upanga. Yuda peke yake kulikuwa na wanajeshi 470, 000.
And Joab gave up the sum of the number of the people unto David: and there were [in] all Israel a thousand times thousand and one hundred thousand men that drew the sword: and [of] Judah were four hundred and seventy thousand men that drew the sword.
6 Lakini Levi na Benjamini hawaku hesabiwa miongoni mwao, kwa kuwa amri ya mfalme ilimuudhi Yoabu.
But Levi and Benjamin did he not count among them: for the king's word was abominable to Joab.
7 Mungu alikwazika na hili tendo, akashambulia Israeli.
And this thing was displeasing in the eyes of God, and he smote Israel.
8 Daudi akamwambia Mungu, “Nimetenda dhambi kubwa kwa kufanya hili. Sasa chukua hatia ya mtumishi wako, nimetenda kwa ujinga sana.”
And David said unto God, I have sinned greatly, because I have done this thing; but now, I beseech thee, cause the iniquity of thy servant to pass away; for I have acted very foolishly.
9 Yahweh akamwambia Gadi, nabii wa Daudi,
And the Lord spoke unto Gad, David's seer, saying,
10 “Nenda useme kwa Daudi, “Hili ndilo Yahweh anasema: Ninakupa maamuzi matatu. Chagua moja wapo.”
Go and speak unto David, saying, Thus hath said the Lord, Three things do I offer thee: choose for thyself one of them, and I will do it unto thee.
11 Hivyo Gadi akaenda kwa Daudi na kusema, “Yahweh anasema hivi, 'Chagua moja ya haya:
So Gad came to David, and said unto him, Thus hath said the Lord, Select for thyself,
12 kati ya miaka mitatu ya ukame, miezi mitatu unakimbizwa na adui zako na kupatwa na upanga wao, au siku tatu za upanga wa Yahweh, yani, pigo katika nchi, malaika wa Yahweh akiharibu nchi yote ya Israeli.' Hivyo sasa, amua jibu gani ni mpelekee yeye aliye nituma.”
Whether there shall be three years famine; or three months, to be destroyed before thy adversaries, so that the sword of thy enemies overtake thee; or that during three days the sword of the Lord, even the pestilence, shall be in the land, and an angel of the Lord destroying throughout all the boundaries of Israel? And now reflect what word I shall bring back to him that hath sent me.
13 Kisha Daudi akamwambia Gadi, “Nipo katika shida kubwa sana. Acha nianguke katika mikono ya Yahweh kuliko kuangukia mikono ya mwanadamu, sababu matendo yake ya rehema ni makubwa mno.”
And David said unto Gad, I am in a great strait: let me fall then into the hand of the Lord; for his mercies are very great; but let me not fall into the hand of man.
14 Hivyo Yahweh akatuma pigo Israeli, na watu elfu sabini wakafa.
So the Lord sent a pestilence in Israel, and there fell of Israel seventy thousand men.
15 Mungu akatuma malaika Yerusalemu kuiharibu. Wakati alipo taka kuiharibu, Yahweh akatazama na kubadili nia yake kuhusu shambulio. Akasema kwa malaika wa uharibifu, “Imetosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Yahweh alikua amesimama eneo la kupeta la Orinani Myebusi.
And God sent an angel unto Jerusalem to destroy it; but as he was destroying, the Lord looked on, and he bethought himself of the evil, and said to the angel that destroyed, It is enough: now stay thy hand. And the angel of the Lord was standing by the threshing-floor of Ornan the Jebusite.
16 Daudi akatazama juu na kuona malaika wa Yahweh amesimama kati ya nchi na mbingu, akiwa na upanga mkonono mwake akiuelekeza Yerusalemu. Kisha Daudi na wazee, wakiwa wamevaa magunia, wakalala chini uso ukiwa kwenye ardhi.
And David lifted up his eyes, and saw the angel of the Lord standing between the earth and the heavens, with his sword drawn in his hand, stretched out over Jerusalem. Then fell David, with the elders wrapt in sackcloth, upon their faces.
17 Daudi akamwambia Mungu, “Sio mimi niliye amuru jeshi kuhesabiwa? Nimefanya hichi kitu kiovu. Lakini hawa kondoo, wamefanya nini? Yahweh Mungu wangu! Acha mkono wako unipige mimi na familia yangu, lakini usiache pigo iliendelee kubaki kwa watu wako.”
And David said unto God, Was it not I that ordered to count the people? and I am the one that have sinned and have done evil indeed; but these sheep, what have they done? O Lord my God, let thy hand, I pray thee, be against me, and against my father's house, but not against thy people, that there should be a plague.
18 Hivyo malaika wa Yahweh akamuamuru Gadi kusema kwa Daudi, kwamba Daudi aende juu na kujenga madhabahu ya Yahweh katika eneo la kupeta la Oranani Myebusi.
And the angel of the Lord spoke to Gad to say to David, that David should go up, to erect an altar unto the Lord on the threshing-floor of Ornan the Jebusite.
19 Daudi akaenda kama Gadi alivyo muelekeza cha kufanya kwa jina la Yahweh.
And David went up by the word of Gad, which he had spoken in the name of the Lord.
20 Wakati Orinani akipepeta ngano, aligeuka na kumuona malaika. Yeye na wana wake wanne wakajificha.
And when Ornan turned back, and saw the angel, then did he and his four sons with him hide themselves. Now Ornan was threshing wheat.
21 Wakati Daudi alipo kuja kwa Orinani, Orinani akatazama na kumuona Daudi. Aliacha eneo la kupeta na akamuinamia Daudi uso wake ukiwa kwenye ardhi.
And as David came up to Ornan, Ornan looked up and saw David; and he went out of the threshing-floor, and bowed himself to David with his face to the ground.
22 Kisha Daudi akasema kwa Orinani, “Niuzie hili eneo la kupeta, iliniweze kumjenga Yahweh madhabahu. Nitalipa gharama yote, ili pigo liondolewe kwa watu.”
Then said David to Ornan, “Grant me the site of this threshing-floor, that I may build thereon an altar unto the Lord: for the full price shalt thou give it unto me, so that the plague may be stayed from the people.”
23 Orinani wakwambia Daudi, “Chukuwa kama lako, bwana wangu mfalme. Fanya nalo linalo kupendeza. Tazama, nitakupa ng'ombe kwa sadaka ya kuteketeza, vifaa vya kupeta kwa ajili ya mbao, na ngano kwa sadaka ya mbegu; nitakupa yote wewe.”
And Ornan said unto David, Take it for thyself, and let my lord the king do what is good in his eyes: lo, I give the oxen for burnt-offerings, and the threshing-rollers for wood, and the wheat for the meat-offering; the whole do I give [thee].
24 Mfalme Daudi akamwambia Orinani, “Hapana, nina sisitiza kununua kwa bei yote. Sitachukua kilicho chako na kutoa kama sadaka ya kuteketeza kwa Yahweh kama haitanighramu chochote.”
And king David said to Ornan, No: but I will surely buy it at the full value; for I will not take what is thine for the Lord, so as to offer burnt-offerings without paying therefore.
25 Hivyo Daudi akalipa shekeli mia sita ya dhahabu kwa hilo eneo.
So David gave to Ornan for the place six hundred shekels of gold by weight.
26 Daudi akajenga madhabahu ya Yahweh pale na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za ushirika. Akamuita Yahweh, aliye mjibu kwa moto kutoka mbinguni kwenye madhabahu ya sadaka za kuteketezwa.
And David built there an altar unto the Lord, and offered burnt-offerings and peace-offerings, and he called on the Lord: and he answered him from heaven by fire upon the altar of burnt-offering.
27 Kisha Yahweh akampa agizo malaika, na malaika akarudisha upanga kwenye mfuko wake.
And the Lord spoke to the angel, and he put back his sword into its sheath.
28 Daudi alipo ona kuwa Yahweh amemjibu kwenye eneo la kupeta la Orinani Myebusi, alitoa dhabihu pale pale kwa wakati huo.
At that time when David saw that the Lord had answered him on the threshing-floor of Ornan the Jebusite, then did he sacrifice there.
29 Sasa kwa wakati huo, hema la kuabudia la Yahweh, ambalo Musa alilitengeneza nyikani, na madhabahu ya sadaka za kuteketezwa, zilikuwa sehemu ya juu huko Gibeoni.
But the tabernacle of the Lord, which Moses had made in the wilderness, and the altar of the burnt-offering, were at that time in the high-place at Gib'on.
30 Walakini, Daudi hakuweza kwenda huko kumuliza Mungu muelekeo, kwa kuwa alikuwa anaogopa upanga wa malaika wa Yahweh.
But David was not able to go before it to inquire of God; for he was afraid because of the sword of the angel of the Lord.

< 1 Nyakati 21 >