< 1 Nyakati 21 >

1 Adui akainuka dhidi ya Israeli na kumchochea Daudi kuhesabu Israeli.
Now Satan rose up against Israel, and he incited David so that he would number Israel.
2 Daudi akamwabia Yoabu na kwa wakuu wa Jeshi, “Nenda, wahesabu watu wa Israeli kutoka Beerisheba mpaka Dani na uniletee taarifa, ilinijue idadi yao.”
And David said to Joab and to the leaders of the people: “Go, and number Israel, from Beersheba even to Dan. And bring me the number, so that I may know it.”
3 Yoabu akasema, “Yahweh na afanya jeshi lake mara mia zaidi ya lilivyo. Lakini bwana wangu mfalme, kwani wote hawamtumikii bwana wangu? kwa nini bwana wangu anataka hili? Kwa nini ulete hatia kwa Israeli?”
And Joab responded: “May the Lord increase his people a hundred times more than they are. But, my lord the king, are they not all your servants? Why would my lord seek this thing, which may be imputed as a sin to Israel?”
4 Lakini neno la mfalme halikubadilika kwa Yoabu. Hivyo Yoabu akaondoka na kwenda Israeli yote. Kisha akarudi Yerusalemu.
But the word of the king prevailed instead. And Joab went away, and he traveled around, through all of Israel. And he returned to Jerusalem.
5 Yoabu akatoa taarifa ya idadi ya jumla ya wanaume wa mapambano kwa Daudi. Kulikuwa ndani ya Israeli wanaume 1, 100, 000 walio beba upanga. Yuda peke yake kulikuwa na wanajeshi 470, 000.
And he gave to David the number of those whom he had surveyed. And the entire number of Israel was found to be one million and one hundred thousand men who could draw the sword; but from Judah, there were four hundred and seventy thousand men of war.
6 Lakini Levi na Benjamini hawaku hesabiwa miongoni mwao, kwa kuwa amri ya mfalme ilimuudhi Yoabu.
But Levi and Benjamin he did not number. For Joab executed the orders of the king unwillingly.
7 Mungu alikwazika na hili tendo, akashambulia Israeli.
Then God was displeased with what had been ordered, and so he struck Israel.
8 Daudi akamwambia Mungu, “Nimetenda dhambi kubwa kwa kufanya hili. Sasa chukua hatia ya mtumishi wako, nimetenda kwa ujinga sana.”
And David said to God: “I have sinned exceedingly in doing this. I beg you take away the iniquity of your servant. For I have acted unwisely.”
9 Yahweh akamwambia Gadi, nabii wa Daudi,
And the Lord spoke to Gad, the seer of David, saying:
10 “Nenda useme kwa Daudi, “Hili ndilo Yahweh anasema: Ninakupa maamuzi matatu. Chagua moja wapo.”
“Go, and speak to David, and tell him: Thus says the Lord: I give to you the option of three things. Choose the one that you will want, and I will do it to you.”
11 Hivyo Gadi akaenda kwa Daudi na kusema, “Yahweh anasema hivi, 'Chagua moja ya haya:
And when Gad had gone to David, he said to him: “Thus says the Lord: Choose what you will want:
12 kati ya miaka mitatu ya ukame, miezi mitatu unakimbizwa na adui zako na kupatwa na upanga wao, au siku tatu za upanga wa Yahweh, yani, pigo katika nchi, malaika wa Yahweh akiharibu nchi yote ya Israeli.' Hivyo sasa, amua jibu gani ni mpelekee yeye aliye nituma.”
Either three years of famine, or three months for you to flee from your enemies, unable to escape from their sword, or three days for the sword of the Lord and a pestilence to turn within the land, with the Angel of the Lord killing in every part of Israel. Now therefore, see what I should respond to him who sent me.”
13 Kisha Daudi akamwambia Gadi, “Nipo katika shida kubwa sana. Acha nianguke katika mikono ya Yahweh kuliko kuangukia mikono ya mwanadamu, sababu matendo yake ya rehema ni makubwa mno.”
And David said to Gad: “There are difficulties pressing upon me from every side. But it is better for me to fall into the hands of the Lord, for his mercies are many, than into the hands of men.”
14 Hivyo Yahweh akatuma pigo Israeli, na watu elfu sabini wakafa.
Therefore, the Lord sent a pestilence upon Israel. And there fell from Israel seventy thousand men.
15 Mungu akatuma malaika Yerusalemu kuiharibu. Wakati alipo taka kuiharibu, Yahweh akatazama na kubadili nia yake kuhusu shambulio. Akasema kwa malaika wa uharibifu, “Imetosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Yahweh alikua amesimama eneo la kupeta la Orinani Myebusi.
Also, he sent an Angel to Jerusalem, so that he might strike it. And while he was striking, the Lord saw and took pity over the magnitude of the harm. And he commanded the Angel who was striking: “It is enough. Now let your hand cease.” And the Angel of the Lord was standing beside the threshing floor of Ornan the Jebusite.
16 Daudi akatazama juu na kuona malaika wa Yahweh amesimama kati ya nchi na mbingu, akiwa na upanga mkonono mwake akiuelekeza Yerusalemu. Kisha Daudi na wazee, wakiwa wamevaa magunia, wakalala chini uso ukiwa kwenye ardhi.
And David, lifting up his eyes, saw the Angel of the Lord, standing between heaven and earth with a drawn sword in his hand, turned toward Jerusalem. And both he and those greater by birth, being clothed in haircloth, fell prone upon the ground.
17 Daudi akamwambia Mungu, “Sio mimi niliye amuru jeshi kuhesabiwa? Nimefanya hichi kitu kiovu. Lakini hawa kondoo, wamefanya nini? Yahweh Mungu wangu! Acha mkono wako unipige mimi na familia yangu, lakini usiache pigo iliendelee kubaki kwa watu wako.”
And David said to God: “Am I not the one who ordered that the people be numbered? It is I who sinned; it is I who did evil. This flock, what does it deserve? O Lord my God, I beg you to let your hand be turned against me and against the house of my father. But let not your people be struck down.”
18 Hivyo malaika wa Yahweh akamuamuru Gadi kusema kwa Daudi, kwamba Daudi aende juu na kujenga madhabahu ya Yahweh katika eneo la kupeta la Oranani Myebusi.
Then the Angel of the Lord instructed Gad to tell David that he should ascend and build an altar to the Lord God on the threshing floor of Ornan the Jebusite.
19 Daudi akaenda kama Gadi alivyo muelekeza cha kufanya kwa jina la Yahweh.
Therefore, David ascended, in accord with the word of Gad, which he had spoken to him in the name of the Lord.
20 Wakati Orinani akipepeta ngano, aligeuka na kumuona malaika. Yeye na wana wake wanne wakajificha.
Now when Ornan had looked up and seen the Angel, he and his four sons hid themselves. For at that time, he was threshing wheat upon the floor.
21 Wakati Daudi alipo kuja kwa Orinani, Orinani akatazama na kumuona Daudi. Aliacha eneo la kupeta na akamuinamia Daudi uso wake ukiwa kwenye ardhi.
Then, as David was approaching Ornan, Ornan saw him, and he went out from the threshing floor to meet him. And he reverenced him prone on the ground.
22 Kisha Daudi akasema kwa Orinani, “Niuzie hili eneo la kupeta, iliniweze kumjenga Yahweh madhabahu. Nitalipa gharama yote, ili pigo liondolewe kwa watu.”
And David said to him: “Give this place of your threshing floor to me, so that I may build an altar to the Lord upon it. And you shall accept from me as much money as it is worth, so that the plague may cease from the people.”
23 Orinani wakwambia Daudi, “Chukuwa kama lako, bwana wangu mfalme. Fanya nalo linalo kupendeza. Tazama, nitakupa ng'ombe kwa sadaka ya kuteketeza, vifaa vya kupeta kwa ajili ya mbao, na ngano kwa sadaka ya mbegu; nitakupa yote wewe.”
But Ornan said to David: “Take it, and may my lord the king do whatever pleases him. Moreover, I give the oxen also as a holocaust, and the plow for wood, and the wheat for a sacrifice. I will offer all freely.”
24 Mfalme Daudi akamwambia Orinani, “Hapana, nina sisitiza kununua kwa bei yote. Sitachukua kilicho chako na kutoa kama sadaka ya kuteketeza kwa Yahweh kama haitanighramu chochote.”
And king David said to him: “By no means shall it be so. Instead, I will give money to you, as much as it is worth. For I must not take it from you, and thereby offer to the Lord holocausts that cost nothing.”
25 Hivyo Daudi akalipa shekeli mia sita ya dhahabu kwa hilo eneo.
Therefore, David gave Ornan, for the place, the very just weight of six hundred shekels of gold.
26 Daudi akajenga madhabahu ya Yahweh pale na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za ushirika. Akamuita Yahweh, aliye mjibu kwa moto kutoka mbinguni kwenye madhabahu ya sadaka za kuteketezwa.
And he built an altar to the Lord there. And he offered holocausts and peace offerings, and he called upon the Lord. And he heeded him by sending fire from heaven upon the altar of the holocaust.
27 Kisha Yahweh akampa agizo malaika, na malaika akarudisha upanga kwenye mfuko wake.
And the Lord instructed the Angel, and he turned his sword back into its sheath.
28 Daudi alipo ona kuwa Yahweh amemjibu kwenye eneo la kupeta la Orinani Myebusi, alitoa dhabihu pale pale kwa wakati huo.
Then, seeing that the Lord had heeded him at the threshing floor of Ornan the Jebusite, David immediately immolated victims there.
29 Sasa kwa wakati huo, hema la kuabudia la Yahweh, ambalo Musa alilitengeneza nyikani, na madhabahu ya sadaka za kuteketezwa, zilikuwa sehemu ya juu huko Gibeoni.
But the tabernacle of the Lord, which Moses had made in the desert, and the altar of holocausts, were at that time on the high place of Gibeon.
30 Walakini, Daudi hakuweza kwenda huko kumuliza Mungu muelekeo, kwa kuwa alikuwa anaogopa upanga wa malaika wa Yahweh.
And David was unable to go to the altar, so that he might pray to God there. For he had been struck with an exceedingly great fear, seeing the sword of the Angel of the Lord.

< 1 Nyakati 21 >