< 1 Nyakati 2 >
1 Hawa ndio wana wa Israeli: Reubeni, Simioni, Lawi, Yuda, Isakari, Zebuloni,
Вот сыновья Израиля: Рувим, Симеон, Левий, Иуда, Иссахар, Завулон,
2 Dani, Yusufu, Benyamini, Naftali, Gadi, na Asheri.
Дан, Иосиф, Вениамин, Неффалим, Гад и Асир.
3 Wana wa Yuda walikuwa Eri, Onani, na Shela, ambao walizaliwa na binti wa Shua, Wakanaani. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa muovu katika macho ya Yahweh, na Yahweh akamwua.
Сыновья Иуды: Ир, Онан и Силом, - трое родились у него от дочери Шуевой, Хананеянки. И был Ир, первенец Иудин, не благоугоден в очах Господа, и Он умертвил его.
4 Tamari, mkwe wake, alimzalia Peresi na Zera. Yuda alikuwa na wana wa kiume wa tano.
И Фамарь, невестка его, родила ему Фареса и Зару. Всех сыновей у Иуды было пятеро.
5 Wana wa Peresi walikuwa Hesroni na Hamuli.
Сыновья Фареса: Есром и Хамул.
6 Wana wa Zera walikuwa Zimri, Ethani, Hemani, Kalikoli na Darda, wote kwa jumla ni watano.
Сыновья Зары: Зимри, Ефан, Еман, Халкол и Дара; всех их пятеро.
7 Mwana wa Karmi alikuwa ni Akani, aliye leta taabu katika Israeli alipo iba kile kilicho hifadhiwa kwa ajili ya Mungu.
Сыновья Харми: Ахар, наведший беду на Израиля, нарушив заклятие.
8 Mwana wa Ethani alikuwa Azaria.
Сын Ефана: Азария.
9 Wana wa Hezroni walikuwa ni Yerameeli, Ramu, na Kalebu.
Сыновья Есрома, которые родились у него: Иерахмеил, Арам и Хелувай.
10 Ramu akawa baba wa Aminadabu, na Aminadabu akawa baba wa Nashoni, kiongozi miongoni uzao wa Yuda.
Арам же родил Аминадава; Аминадав родил Наассона, князя сынов Иудиных;
11 Nashoni akawa baba wa Salmoni, na Salmon akawa baba wa Boazi.
Наассон родил Салмона, Салмон родил Вооза;
12 Boazi akawa baba wa Obedi, na Obedi akawa baba wa Yese.
Вооз родил Овида, Овид родил Иессея;
13 Yese akawa baba wa mzaliwa wake wa kwanza Eliabu, wa pili Abinadabu, wa tatu Shama.
Иессей родил первенца своего Елиава, второго - Аминадава, третьего - Самму,
14 Nethaneli wa nne, Radai wa tano.
четвертого - Нафанаила, пятого - Раддая,
15 Ozemu wa sita, na Daudi wa saba.
шестого - Оцема, седьмого - Давида.
16 Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa Abishai, Yoabu, na Asaheli, jumla watatu.
Сестры их: Саруия и Авигея. Сыновья Саруии: Авесса, Иоав и Азаил, трое.
17 Abigali akamzaa Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri Mwishmaeli.
Авигея родила Амессу; отец же Амессы - Иефер, Измаильтянин.
18 Kalebu mwana wa Hesroni akawa baba wa watoto wa Azubu mkewe, na Yeriothi. Wanawe walikuwa Yesheri, Shobabu, na Ardoni.
Халев, сын Есрома, родил от Азувы, жены своей, и от Иериофы, и вот сыновья его: Иешер, Шовав и Ардон.
19 Azuba akafa, na Kalebu akamuoa Efrathi, aliye mzalia Huri.
И умерла Азува; и взял себе Халев жену Ефрафу, и она родила ему Хура.
20 Huri akawa baba wa Uri, na Uri akawa baba wa Besaleli.
Хур родил Урия, Урий родил Веселиила.
21 Baadae Hesroni (alipo kuwa na miaka sitini) akamuoa binti wa Makiri, baba wa Gileadi. Akamzalia Segubu.
После Есром вошел к дочери Махира, отца Галаадова, и взял ее, будучи шестидесяти лет, и она родила ему Сегува.
22 Segubu akawa baba wa Yairi, aliye miliki miji ishirini na mitatu katika nchi ya Gileadi.
Сегув родил Иаира, и было у него двадцать три города в земле Галаадской.
23 Geshuri na Aramu wakawapokonya miji ya Yairi na Kenathi, pamoja na miji sitini iliyo zunguka. Hawa wakazi wote walikuwa ni uzao wa Makiri, baba wa Gileadi.
Но Гессуряне и Сирияне взяли у них селения Иаира, Кенаф и зависящие от него города, - шестьдесят городов. Все эти города сыновей Махира, отца Галаадова.
24 Baada ya kifo cha Hesroni, Kalebu akalala na Efrata, mke wa baba yake Hesroni. Akamzalia Ashuri, baba wa Tekoa.
По смерти Есрома в Халев-Ефрафе, жена Есромова, Авия, родила ему Ашхура, отца Фекои.
25 Wana wa Yerameeli, mzaliwa wa kwanza wa Hesroni, walikuwa ni Ramu mzaliwa wa kwanza, Buna, Oreni, Ozemu, na Ahiya.
Сыновья Иерахмеила, первенца Есромова, были: первенец Рам, за ним Вуна, Орен, Оцем и Ахия.
26 Yerameeli alikuwa na mke mwingine, Jina lake lilikuwa Atara. Yeye alikuwa mama wa Onamu.
Была у Иерахмеила и другая жена, имя ее Афара; она мать Онама.
27 Wana wa Ramu, mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli, walikuwa Maasi, Yamini, na Ekeri.
Сыновья Рама, первенца Иерахмеилова, были: Маац, Иамин и Екер.
28 Wana wa Onamu walikuwa ni Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa ni Nadabu na Abishuri.
Сыновья Онама были: Шаммай и Иада. Сыновья Шаммая: Надав и Авишур.
29 Jina la mke wa Abishuri lilikuwa Abihaili, na akamzalia Abani na Molidi.
Имя жене Авишуровой Авихаиль, и она родила ему Ахбана и Молида.
30 Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa pasipo watoto.
Сыновья Надава: Селед и Афаим. И умер Селед бездетным.
31 Mwana wa Apaimu alikuwa Ishi. Mwana wa Ishi alikuwa Sheshani. Mwana wa Sheshani alikuwa Alai.
Сын Афаима: Иший. Сын Ишия: Шешан. Сын Шешана: Ахлай.
32 Wana wa Yada, kaka yake Shamai, walikuwa Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa pasipo mtoto.
Сыновья Иады, брата Шаммаева: Иефер и Ионафан. Иефер умер бездетным.
33 Wana wa Yonathani walikuwa Pelethi na Zaza. Hawa ndio uzao wa Yerameeli.
Сыновья Ионафана: Пелеф и Заза. Это сыновья Иерахмеила.
34 Sasa Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, bali wa kike pekee. Sheshani alikuwa na mtumishi, wa Kimisri, ambaye jina lake lilikuwa Yariha.
У Шешана не было сыновей, а только дочери. У Шешана был раб, Египтянин, имя его Иарха;
35 Sheshani alimkabidhi binti yake kwa Yariha mtumishi wake kama mke wake. Akamzalia Atai.
Шешан отдал дочь свою Иархе рабу своему в жену: и она родила ему Аттая.
36 Atai akawa baba wa Nathani, na Nathani akawa baba wa Zabadi.
Аттай родил Нафана, Нафан родил Завада;
37 Zabadi akawa baba wa Efalali, na Afalali akawa baba wa Obedi.
Завад родил Ефлала, Ефлал родил Овида;
38 Obedi akawa baba wa Yehu, na Yehu akawa baba wa Azaria.
Овид родил Иеуя, Иеуй родил Азарию;
39 Azaria akawa baba wa Helesi, na Helesi akawa baba wa Eleasa.
Азария родил Хелеца, Хелец родил Елеасу;
40 Eleasa akawa baba wa Sismai, na Sismai akawa baba wa Shalumu.
Елеаса родил Сисмая, Сисмай родил Саллума;
41 Shalumu akawa baba wa Yekamia, na Yekamia akawa baba wa Elishama.
Саллум родил Иекамию, Иекамия родил Елишаму.
42 Wana wa Kalebu, kaka yake Yerameeli, walikuwa ni Mesha mzaliwa wake wa kwanza, aliye kuwa baba wa Zifu. Mwanae wa pili, Maresha, allikuwa baba wa Hebroni.
Сыновья Халева, брата Иерахмеилова: Меша, первенец его, - он отец Зифа; и сыновья Мареши, отца Хеврона.
43 Wana wa Hebroni walikuwa Kora, Tapua, Rekemu, na Shema.
Сыновья Хеврона: Корей и Таппуах, и Рекем и Шема.
44 Shema akawa baba wa Rahamu, baba wa Yorkeamu. Rekemu akawa baba wa Shamai.
Шема родил Рахама, отца Иоркеамова, а Рекем родил Шаммая.
45 Mwana wa Shamai alikuwa Maoni, na Maoni alikuwa baba wa Bethsuri.
Сын Шаммая Маон, а Маон - отец Беф-Цура.
46 Efa, suria wa Kalebu, alimza Harani, Mosa, na Gazezi. Harani akawa baba wa Gazezi.
И Ефа, наложница Халевова, родила Харана, Моцу и Газеза. И Харан родил Газеза.
47 Wana wa Yadai walikuwa Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa, na Shaafa.
Сыновья Иегдая: Регем, Иофам, Гешан, Пелет, Ефа и Шааф.
48 Maaka, suria wa Kalebu, alimza Sheberi na Tirhana.
Наложница Халевова, Мааха, родила Шевера и Фирхану;
49 Pia akamza Shaafu baba wa Madmana, Sheva baba wa Makbena na baba wa Gibea. Binti wa Kalebu alikuwa Aksa. Hawa walikuwa uzao wa Kalebu.
она же родила Шаафа, отца Мадманны, Шеву, отца Махбены и отца Гивеи. Дочь же Халева - Ахса.
50 Hawa walikuwa wana wa Huri, mzaliwa wake wa kwanza kwa Efratha: Shobali baba wa Kiriath-Yearimu.
Вот сыновья Халева: сын Хур, первенец Ефрафы; Шовал, отец Кириаф-Иарима;
51 Salma baba wa Bethlehemu, na Harefu baba wa Beth-gaderi.
Салма, отец Вифлеема; Хареф, отец Бефгадера.
52 Shobali baba wa kiriath-Yearimu alikuwa na uzao: Haroe, nusu ya watu Wamenuthite,
У Шовала, отца Кириаф-Иарима, были сыновья: Гарое, Хаци, Галменюхот.
53 na ukoo wa Kiriath-Yearimu: Waithri, Waputhi, Washumathi, na Wamishrai. Wasorathi na Waeshtaoli walitoka huku.
Племена Кириаф-Иарима: Ифрияне, Футияне, Шумафане и Мидраитяне. От сих произошли Цоряне и Ештаоляне.
54 Ukoo wa Salma ulikuwa kama ufatao: Bethlehemu, Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, na nusu ya Wamenuhothi na Wazori,
Сыновья Салмы: Вифлеемляне и Нетофафяне, венец дома Иоавова и половина Менухотян - Цоряне,
55 ukoo wa waandishi walio ishi Yabesi: Watirathi, Washimeathi, na Wasukathi. Hawa walikuwa Wakeni walio toka katika uzao wa Hamathi, babu wa Warekabu.
и племена Соферийцев, живших в Иабеце, Тирейцы, Шимейцы, Сухайцы: это Кинеяне, происшедшие от Хамафа, отца Бетрехава.