< 1 Nyakati 2 >

1 Hawa ndio wana wa Israeli: Reubeni, Simioni, Lawi, Yuda, Isakari, Zebuloni,
Or les fils d’Israël sont: Ruben, Siméon, Lévi, Juda, Issachar et Zabulon,
2 Dani, Yusufu, Benyamini, Naftali, Gadi, na Asheri.
Dan, Joseph, Benjamin, Nephthali, Gad et Aser.
3 Wana wa Yuda walikuwa Eri, Onani, na Shela, ambao walizaliwa na binti wa Shua, Wakanaani. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa muovu katika macho ya Yahweh, na Yahweh akamwua.
Les fils de Juda: Her, Onan et Séla; ces trois lui naquirent de la fille de Sué, Ghananéenne. Mais Her, le premier-né de Juda, fut méchant devant le Seigneur, qui le frappa de mort.
4 Tamari, mkwe wake, alimzalia Peresi na Zera. Yuda alikuwa na wana wa kiume wa tano.
Or Thamar, belle-fille de Juda, lui enfanta Pharès et Zara. Tous les fils de Juda furent au nombre de cinq.
5 Wana wa Peresi walikuwa Hesroni na Hamuli.
Pharès eut deux fils: Hesron et Hamul.
6 Wana wa Zera walikuwa Zimri, Ethani, Hemani, Kalikoli na Darda, wote kwa jumla ni watano.
Et les fils de Zara furent Zamri, Ethan, Eman, ainsi que Chalchal et Dara; cinq en tout.
7 Mwana wa Karmi alikuwa ni Akani, aliye leta taabu katika Israeli alipo iba kile kilicho hifadhiwa kwa ajili ya Mungu.
Les fils de Charmi: Achar, qui troubla Israël, et pécha par le larcin de l’anathème;
8 Mwana wa Ethani alikuwa Azaria.
Les fils d’Ethan, Azarias;
9 Wana wa Hezroni walikuwa ni Yerameeli, Ramu, na Kalebu.
Mais les fils d’Hesron, qui lui naquirent: Jéraméel, Ram, et Calubi.
10 Ramu akawa baba wa Aminadabu, na Aminadabu akawa baba wa Nashoni, kiongozi miongoni uzao wa Yuda.
Or Ram engendra Aminadab; Aminadab engendra Nahasson, prince des fils de Juda.
11 Nashoni akawa baba wa Salmoni, na Salmon akawa baba wa Boazi.
Nahasson aussi engendra Salma, duquel est né Booz.
12 Boazi akawa baba wa Obedi, na Obedi akawa baba wa Yese.
Or Booz engendra Obed, qui lui-même engendra Isaï.
13 Yese akawa baba wa mzaliwa wake wa kwanza Eliabu, wa pili Abinadabu, wa tatu Shama.
Mais Isaï engendra son premier-né Eliab; le second, Abinabad; le troisième, Simmaa;
14 Nethaneli wa nne, Radai wa tano.
Le quatrième, Nathanaël; le cinquième, Raddaï;
15 Ozemu wa sita, na Daudi wa saba.
Le sixième, Asom; le septième, David;
16 Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa Abishai, Yoabu, na Asaheli, jumla watatu.
Dont les sœurs furent Sarvia et Abigaïl; les fils de Sarvia, trois: Abisaï, Joab et Asaël.
17 Abigali akamzaa Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri Mwishmaeli.
Or Abigaïl enfanta Amasa, dont le père fut Jéther, l’Ismahélite.
18 Kalebu mwana wa Hesroni akawa baba wa watoto wa Azubu mkewe, na Yeriothi. Wanawe walikuwa Yesheri, Shobabu, na Ardoni.
Or Caleb, fils d’Hesron, prit une femme du nom d’Azuba, dont il engendra Jérioth; et ses fils furent Jaser, Sobab et Ardon.
19 Azuba akafa, na Kalebu akamuoa Efrathi, aliye mzalia Huri.
Mais lorsque Azuba fut morte, Caleb prit pour femme Ephratha, qui lui enfanta Hur.
20 Huri akawa baba wa Uri, na Uri akawa baba wa Besaleli.
Or Hur engendra Uri; et Uri engendra Bézéléel.
21 Baadae Hesroni (alipo kuwa na miaka sitini) akamuoa binti wa Makiri, baba wa Gileadi. Akamzalia Segubu.
Après cela, Hesron s’unit à la fille de Machir, père de Galaad; et il la prit, lorsqu’il avait soixante ans: elle lui enfanta Ségub.
22 Segubu akawa baba wa Yairi, aliye miliki miji ishirini na mitatu katika nchi ya Gileadi.
Mais Ségub aussi engendra Jaïr; et il posséda vingt-trois villes dans la terre de Galaad.
23 Geshuri na Aramu wakawapokonya miji ya Yairi na Kenathi, pamoja na miji sitini iliyo zunguka. Hawa wakazi wote walikuwa ni uzao wa Makiri, baba wa Gileadi.
Et Gessur et Aram prirent les villes de Jaïr, et Canath, et ses bourgades, soixante villes. Tous ceux-là étaient les fils de Machir, père de Galaad.
24 Baada ya kifo cha Hesroni, Kalebu akalala na Efrata, mke wa baba yake Hesroni. Akamzalia Ashuri, baba wa Tekoa.
Mais après qu’Hesron fut mort, Caleb s’unit à Ephratha; Hesron eut encore pour femme Abia, qui lui enfanta Ashur, père de Thécua.
25 Wana wa Yerameeli, mzaliwa wa kwanza wa Hesroni, walikuwa ni Ramu mzaliwa wa kwanza, Buna, Oreni, Ozemu, na Ahiya.
Or il naquit des fils à Jéraméel, premier-né d’Hesron: Ram, son premier-né, ensuite Buna, Aram, Asom et Achia.
26 Yerameeli alikuwa na mke mwingine, Jina lake lilikuwa Atara. Yeye alikuwa mama wa Onamu.
Et Jéraméel prit encore une autre femme: Atara, qui fut mère d’Onam.
27 Wana wa Ramu, mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli, walikuwa Maasi, Yamini, na Ekeri.
Mais, de plus, les fils de Ram, fils aîné de Jéraméel, furent Moos, Jamin et Achar.
28 Wana wa Onamu walikuwa ni Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa ni Nadabu na Abishuri.
Or Onam eut pour fils Séméi et Jada. Les fils de Séméi sont Nadab et Abisur.
29 Jina la mke wa Abishuri lilikuwa Abihaili, na akamzalia Abani na Molidi.
Et le nom de la femme d’Abisur était Abihaïl, laquelle lui enfanta Ahobban et Molid.
30 Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa pasipo watoto.
Or les fils de Nadab furent Saled et Apphaïm. Quant à Saled, il mourut sans enfants.
31 Mwana wa Apaimu alikuwa Ishi. Mwana wa Ishi alikuwa Sheshani. Mwana wa Sheshani alikuwa Alai.
Mais le fils d’Apphaïm fut Jési; lequel Jési engendra Sésan. Or Sésan engendra Oholaï.
32 Wana wa Yada, kaka yake Shamai, walikuwa Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa pasipo mtoto.
Et les fils de Jada, frère de Séméi, furent Jéther et Jonathan. Mais Jéther aussi mourut sans enfants.
33 Wana wa Yonathani walikuwa Pelethi na Zaza. Hawa ndio uzao wa Yerameeli.
Or Jonathan engendra Phaleth et Ziza. Voilà quels ont été les fils de Jéraméel.
34 Sasa Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, bali wa kike pekee. Sheshani alikuwa na mtumishi, wa Kimisri, ambaye jina lake lilikuwa Yariha.
Pour Sésan, il n’eut point de fils, mais des filles, et un esclave égyptien nommé Jéraa,
35 Sheshani alimkabidhi binti yake kwa Yariha mtumishi wake kama mke wake. Akamzalia Atai.
Et il lui donna sa fille pour femme, laquelle lui enfanta Ethéi.
36 Atai akawa baba wa Nathani, na Nathani akawa baba wa Zabadi.
Or Ethéi engendra Nathan, et Nathan engendra Zabad.
37 Zabadi akawa baba wa Efalali, na Afalali akawa baba wa Obedi.
Zabad aussi engendra Ophlal, et Ophlal engendra Obed.
38 Obedi akawa baba wa Yehu, na Yehu akawa baba wa Azaria.
Obed engendra Jéhu, Jéhu engendra Azarias.
39 Azaria akawa baba wa Helesi, na Helesi akawa baba wa Eleasa.
Azarias engendra Hellès, et Hellès engendra Elasa.
40 Eleasa akawa baba wa Sismai, na Sismai akawa baba wa Shalumu.
Elasa engendra Sisamoï; Sisamoï engendra Sellum.
41 Shalumu akawa baba wa Yekamia, na Yekamia akawa baba wa Elishama.
Sellum engendra Icamia, mais Icamia engendra Elisama.
42 Wana wa Kalebu, kaka yake Yerameeli, walikuwa ni Mesha mzaliwa wake wa kwanza, aliye kuwa baba wa Zifu. Mwanae wa pili, Maresha, allikuwa baba wa Hebroni.
Or les fils de Caleb, frère de Jéraméel, furent Mésa, son premier-né; c’est le père de Ziph, et les fils de Marésa, père d’Hébron;
43 Wana wa Hebroni walikuwa Kora, Tapua, Rekemu, na Shema.
Et les fils d’Hébron furent Coré, Taphua, Récem et Samma.
44 Shema akawa baba wa Rahamu, baba wa Yorkeamu. Rekemu akawa baba wa Shamai.
Or Samma engendra Rahani, père de Jercaam, et Récem engendra Sammaï.
45 Mwana wa Shamai alikuwa Maoni, na Maoni alikuwa baba wa Bethsuri.
Le fils de Sammaï fut Maon, et Maon fut père de Bethsur.
46 Efa, suria wa Kalebu, alimza Harani, Mosa, na Gazezi. Harani akawa baba wa Gazezi.
Or Epha, femme du second rang de Caleb, enfanta Haran, Mosa et Gézez. Et Haran engendra Gézez.
47 Wana wa Yadai walikuwa Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa, na Shaafa.
Mais les fils de Jahaddaï furent Régom, Joathan, Gésan, Phalet, Epha et Saaph.
48 Maaka, suria wa Kalebu, alimza Sheberi na Tirhana.
Maacha, femme du second rang de Caleb, enfanta Saber, et Tharana.
49 Pia akamza Shaafu baba wa Madmana, Sheva baba wa Makbena na baba wa Gibea. Binti wa Kalebu alikuwa Aksa. Hawa walikuwa uzao wa Kalebu.
Mais Saaph, père de Madména, engendra Sué, père de Machbéna, et père de Gabaa. Or la fille de Caleb fut Achsa,
50 Hawa walikuwa wana wa Huri, mzaliwa wake wa kwanza kwa Efratha: Shobali baba wa Kiriath-Yearimu.
Voici quels furent les fils de Caleb, fils d’Hur, premier-né d’Ephratha: Sobal, père de Cariathiarim;
51 Salma baba wa Bethlehemu, na Harefu baba wa Beth-gaderi.
Salma, père de Bethléhem; Hariph, père de Bethgader.
52 Shobali baba wa kiriath-Yearimu alikuwa na uzao: Haroe, nusu ya watu Wamenuthite,
Or Sobal, père de Cariathiarim, eut des fils. Il voyait la moitié des lieux de repos.
53 na ukoo wa Kiriath-Yearimu: Waithri, Waputhi, Washumathi, na Wamishrai. Wasorathi na Waeshtaoli walitoka huku.
Et des familles de Cariathiarim sont venus les Jéthréens, les Aphuthéens, les Sémathéens, les Maséréens. C’est d’eux que sont sortis les Saraïtes et les Esthaolites.
54 Ukoo wa Salma ulikuwa kama ufatao: Bethlehemu, Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, na nusu ya Wamenuhothi na Wazori,
Les fils de Salma, Bethléhem et Nétophathi, les Couronnes de la maison de Joab, et la Moitié du lieu de repos de Saraï.
55 ukoo wa waandishi walio ishi Yabesi: Watirathi, Washimeathi, na Wasukathi. Hawa walikuwa Wakeni walio toka katika uzao wa Hamathi, babu wa Warekabu.
Et les familles des scribes habitant à Jabès, chantant et jouant des instruments, et demeurant dans des tabernacles. Ce sont les Cinéens, qui sont venus de Calor, père de la maison de Réchab.

< 1 Nyakati 2 >