< 1 Nyakati 2 >
1 Hawa ndio wana wa Israeli: Reubeni, Simioni, Lawi, Yuda, Isakari, Zebuloni,
Voici les noms des fils d'Israël: Ruben, Siméon, Lévi, Juda, Issachar, Zabulon,
2 Dani, Yusufu, Benyamini, Naftali, Gadi, na Asheri.
Dan, Joseph, Benjamin, Nephthali, Gad, Aser.
3 Wana wa Yuda walikuwa Eri, Onani, na Shela, ambao walizaliwa na binti wa Shua, Wakanaani. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa muovu katika macho ya Yahweh, na Yahweh akamwua.
Fils de Juda: Her, Onan, Sela; tous trois naquirent de la fille de Savas (Sué), la Chananéenne; et Her, le premier-né de Juda, fit le mal devant le Seigneur, qui le tua.
4 Tamari, mkwe wake, alimzalia Peresi na Zera. Yuda alikuwa na wana wa kiume wa tano.
Et Thamar, bru de Juda, enfanta Pharès et Zara; en tout: cinq fils de Juda.
5 Wana wa Peresi walikuwa Hesroni na Hamuli.
Fils de Pharès: Esron et Jemuhel.
6 Wana wa Zera walikuwa Zimri, Ethani, Hemani, Kalikoli na Darda, wote kwa jumla ni watano.
Fils de Zara: Zambri, Etham, Aimuan, Calchal et Darad; en tout: cinq.
7 Mwana wa Karmi alikuwa ni Akani, aliye leta taabu katika Israeli alipo iba kile kilicho hifadhiwa kwa ajili ya Mungu.
Fils de Charmi: Achar, le perturbateur d'Israël, qui désobéit au sujet de l'anathème.
8 Mwana wa Ethani alikuwa Azaria.
Fils d'Etham: Azarias.
9 Wana wa Hezroni walikuwa ni Yerameeli, Ramu, na Kalebu.
Fils d'Esron, qui lui furent enfantés: Jeraméel, Aram et Caleb.
10 Ramu akawa baba wa Aminadabu, na Aminadabu akawa baba wa Nashoni, kiongozi miongoni uzao wa Yuda.
Aram engendra Aminadab; Aminadab engendra Nahasson, chef de la maison de Juda.
11 Nashoni akawa baba wa Salmoni, na Salmon akawa baba wa Boazi.
Nahasson engendra Salmon; Salmon engendra Booz;
12 Boazi akawa baba wa Obedi, na Obedi akawa baba wa Yese.
Booz engendra Obed; Obed engendra Jessé;
13 Yese akawa baba wa mzaliwa wake wa kwanza Eliabu, wa pili Abinadabu, wa tatu Shama.
Jessé engendra son premier-né Eliab, le second Aminadab, le troisième Samaa,
14 Nethaneli wa nne, Radai wa tano.
Nathanael le quatrième, Zabdé le cinquième,
15 Ozemu wa sita, na Daudi wa saba.
Azam le sixième, et David le septième.
16 Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa Abishai, Yoabu, na Asaheli, jumla watatu.
Et leurs sœurs furent: Sarvia et Abigaïl. Les fils de Sarvia furent: Abessa, Joab et Asaël; trois.
17 Abigali akamzaa Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri Mwishmaeli.
Abagaïl enfanta Amessab, et le père d'Amessab fut Jolhor l'Ismaélite.
18 Kalebu mwana wa Hesroni akawa baba wa watoto wa Azubu mkewe, na Yeriothi. Wanawe walikuwa Yesheri, Shobabu, na Ardoni.
Caleb, fils d'Esron, prit pour femmes Gazuba et Jerioth; voici ses fils: Jasar, Subab et Ardon.
19 Azuba akafa, na Kalebu akamuoa Efrathi, aliye mzalia Huri.
Et Gazuba mourut, et Caleb prit pour femme Ephratha, et elle lui enfanta Hur.
20 Huri akawa baba wa Uri, na Uri akawa baba wa Besaleli.
Hur engendra Urias; Urias engendra Beseléel.
21 Baadae Hesroni (alipo kuwa na miaka sitini) akamuoa binti wa Makiri, baba wa Gileadi. Akamzalia Segubu.
Après cela, Esron eut commerce avec la fille de Machir, père de Galaad, et il la prit pour femme; il avait alors soixante-cinq ans, et elle lui enfanta Seruch.
22 Segubu akawa baba wa Yairi, aliye miliki miji ishirini na mitatu katika nchi ya Gileadi.
Seruch engendra Jaïr; il possédait vingt-trois villes en Galaad.
23 Geshuri na Aramu wakawapokonya miji ya Yairi na Kenathi, pamoja na miji sitini iliyo zunguka. Hawa wakazi wote walikuwa ni uzao wa Makiri, baba wa Gileadi.
Il prit de plus Gessur et Aram, villes de Jaïr, parmi les siennes, et la terre de Canath avec ses villes: soixante villes; toutes appartenaient aux fils de Machir, père de Galaad.
24 Baada ya kifo cha Hesroni, Kalebu akalala na Efrata, mke wa baba yake Hesroni. Akamzalia Ashuri, baba wa Tekoa.
Après la mort d'Esron, Caleb épousa Ephratha; or, Abia, femme d'Esron, lui avait enfanté Ascho, père de Thécoé.
25 Wana wa Yerameeli, mzaliwa wa kwanza wa Hesroni, walikuwa ni Ramu mzaliwa wa kwanza, Buna, Oreni, Ozemu, na Ahiya.
Les fils de Jeraméel, premier-né d'Esron, furent: Ram, premier-né; puis, Banaa, Aram et Asan, son frère.
26 Yerameeli alikuwa na mke mwingine, Jina lake lilikuwa Atara. Yeye alikuwa mama wa Onamu.
Et Jeraméel avait une autre femme qui se nommait Atara; celle-ci fut la mère d'Ozom.
27 Wana wa Ramu, mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli, walikuwa Maasi, Yamini, na Ekeri.
Les fils de Ram, premier-né de Jeraméel, furent: Mass, Jamin et Acor.
28 Wana wa Onamu walikuwa ni Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa ni Nadabu na Abishuri.
Les fils d'Ozom furent: Samaï et Jadaé, et les fils de Samaï: Nadab et Abisur.
29 Jina la mke wa Abishuri lilikuwa Abihaili, na akamzalia Abani na Molidi.
La femme d'Abisur se nommait Abihaïl, et elle lui enfanta Achobor et Moêl.
30 Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa pasipo watoto.
Fils de Nadab: Salad et Aphaïn; Salad mourut sans enfants.
31 Mwana wa Apaimu alikuwa Ishi. Mwana wa Ishi alikuwa Sheshani. Mwana wa Sheshani alikuwa Alai.
Fils d'Aphaïn: Iséuniel; fils d'Isémiel: Sosan; fils de Sosan: Dadaï.
32 Wana wa Yada, kaka yake Shamai, walikuwa Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa pasipo mtoto.
Fils de Dadaï: Achisamas, Jéther, Jonatham; Jéther mourut sans enfants.
33 Wana wa Yonathani walikuwa Pelethi na Zaza. Hawa ndio uzao wa Yerameeli.
Fils de Jonathan: Phaleth et Ozam; voilà les fils de Jonathan.
34 Sasa Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, bali wa kike pekee. Sheshani alikuwa na mtumishi, wa Kimisri, ambaye jina lake lilikuwa Yariha.
Sosan n'eut pas de fils, mais des filles; or, il avait un serviteur égyptien qui se nommait Johel.
35 Sheshani alimkabidhi binti yake kwa Yariha mtumishi wake kama mke wake. Akamzalia Atai.
Et Sosan donna sa fille, pour femme, à son serviteur Johel; elle lui enfanta Ethi.
36 Atai akawa baba wa Nathani, na Nathani akawa baba wa Zabadi.
Et Ethi engendra Nathan, et Nathan engendra Zabed.
37 Zabadi akawa baba wa Efalali, na Afalali akawa baba wa Obedi.
Zabed engendra Aphamel, et Aphamel engendra Obed.
38 Obedi akawa baba wa Yehu, na Yehu akawa baba wa Azaria.
Obed engendra Jéhu, et Jéhu engendra Azarias.
39 Azaria akawa baba wa Helesi, na Helesi akawa baba wa Eleasa.
Azarias engendra Hellès, et Hellès engendra Eléaza.
40 Eleasa akawa baba wa Sismai, na Sismai akawa baba wa Shalumu.
Eléaza engendra Sosomaï, et Sosomaï engendra Salum.
41 Shalumu akawa baba wa Yekamia, na Yekamia akawa baba wa Elishama.
Salum engendra Jéhémie; Jéhémie engendra Elisama, et Elisama engendra Ismaël.
42 Wana wa Kalebu, kaka yake Yerameeli, walikuwa ni Mesha mzaliwa wake wa kwanza, aliye kuwa baba wa Zifu. Mwanae wa pili, Maresha, allikuwa baba wa Hebroni.
Fils de Caleb, frère de Jeraméel Marisa, premier-né; c'est le père de Siph; Marisa eut encore des fils, il fut le père d'Hébron.
43 Wana wa Hebroni walikuwa Kora, Tapua, Rekemu, na Shema.
Fils d'Hébron: Coré, Thaphus, Rhicom et Samaa.
44 Shema akawa baba wa Rahamu, baba wa Yorkeamu. Rekemu akawa baba wa Shamai.
Samaa engendra Rahem, père de Jéclan, et Jéclan engendra Samaï.
45 Mwana wa Shamai alikuwa Maoni, na Maoni alikuwa baba wa Bethsuri.
Mahon fut son fils, et Mahon fut le père de Bethsur.
46 Efa, suria wa Kalebu, alimza Harani, Mosa, na Gazezi. Harani akawa baba wa Gazezi.
Gaïpha, concubine de Caleb, enfanta Aram, et Mosa et Gézué.
47 Wana wa Yadai walikuwa Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa, na Shaafa.
Fils d'Adaï: Rahem, Joatham, Sagar, Phalec, Gaïpha et Sagaé.
48 Maaka, suria wa Kalebu, alimza Sheberi na Tirhana.
Mocha, concubine de Caleb, enfanta Saber et Tharam.
49 Pia akamza Shaafu baba wa Madmana, Sheva baba wa Makbena na baba wa Gibea. Binti wa Kalebu alikuwa Aksa. Hawa walikuwa uzao wa Kalebu.
Sagaé engendra le père de Madmena, et Sahu, père de Mahabena, et le père de Gébal; la fille de Caleb s'appelait Ascha.
50 Hawa walikuwa wana wa Huri, mzaliwa wake wa kwanza kwa Efratha: Shobali baba wa Kiriath-Yearimu.
Voilà les fils de Caleb. Voici les fils d'Hur, premier-né d'Ephratha: Sobal, père de Cariathiarim,
51 Salma baba wa Bethlehemu, na Harefu baba wa Beth-gaderi.
Salomon, père de Bétha, Lammon, père de Béthalaem, et Arim, père de Bethgedor.
52 Shobali baba wa kiriath-Yearimu alikuwa na uzao: Haroe, nusu ya watu Wamenuthite,
Fils de Sobal, père de Cariathiarim: Araa, Aïsi, Ammanith
53 na ukoo wa Kiriath-Yearimu: Waithri, Waputhi, Washumathi, na Wamishrai. Wasorathi na Waeshtaoli walitoka huku.
Et Umasphaé; villes de Jdir: Ethalim, Miphitim, Hésamathim et Hémasaraïm, d'où sont sortis les Sarathéens et les fils d'Esthaam.
54 Ukoo wa Salma ulikuwa kama ufatao: Bethlehemu, Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, na nusu ya Wamenuhothi na Wazori,
Fils de Salomon: Béthalaem le Netophatite, Ataroth de la maison de Joab, la moitié de Manathi, et Esari.
55 ukoo wa waandishi walio ishi Yabesi: Watirathi, Washimeathi, na Wasukathi. Hawa walikuwa Wakeni walio toka katika uzao wa Hamathi, babu wa Warekabu.
Familles de lettrés, demeurant en Jabis: Thargathiim, et Samathiim et Sohathim. Ce sont les Cinéens, issus d'Emath, père de la maison de Rhéchab.