< 1 Nyakati 2 >

1 Hawa ndio wana wa Israeli: Reubeni, Simioni, Lawi, Yuda, Isakari, Zebuloni,
Voici les fils d'Israël: Ruben, Siméon, Lévi, Juda, Issacar, Zabulon,
2 Dani, Yusufu, Benyamini, Naftali, Gadi, na Asheri.
Dan, Joseph, Benjamin, Nephtali, Gad et Asher.
3 Wana wa Yuda walikuwa Eri, Onani, na Shela, ambao walizaliwa na binti wa Shua, Wakanaani. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa muovu katika macho ya Yahweh, na Yahweh akamwua.
Fils de Juda: Er, Onan et Schéla, qui lui naquirent tous trois de la fille de Shua, la Cananéenne. Er, premier-né de Juda, était méchant aux yeux de Yahvé, qui le fit mourir.
4 Tamari, mkwe wake, alimzalia Peresi na Zera. Yuda alikuwa na wana wa kiume wa tano.
Tamar, sa belle-fille, lui enfanta Pérets et Zérach. Tous les fils de Juda étaient au nombre de cinq.
5 Wana wa Peresi walikuwa Hesroni na Hamuli.
Fils de Pérets: Hetsron et Hamul.
6 Wana wa Zera walikuwa Zimri, Ethani, Hemani, Kalikoli na Darda, wote kwa jumla ni watano.
Fils de Zérach: Zimri, Éthan, Héman, Calcol et Dara, au nombre de cinq en tout.
7 Mwana wa Karmi alikuwa ni Akani, aliye leta taabu katika Israeli alipo iba kile kilicho hifadhiwa kwa ajili ya Mungu.
Fils de Carmi: Acar, le perturbateur d'Israël, qui commit une infidélité dans la chose consacrée.
8 Mwana wa Ethani alikuwa Azaria.
Fils d'Éthan: Azaria.
9 Wana wa Hezroni walikuwa ni Yerameeli, Ramu, na Kalebu.
Les fils de Hetsron, qui lui sont nés, sont les suivants: Jerahmeel, Ram, et Chelubai.
10 Ramu akawa baba wa Aminadabu, na Aminadabu akawa baba wa Nashoni, kiongozi miongoni uzao wa Yuda.
Ram engendra Amminadab, et Amminadab engendra Nachschon, prince des fils de Juda;
11 Nashoni akawa baba wa Salmoni, na Salmon akawa baba wa Boazi.
et Nachschon engendra Salma, et Salma engendra Boaz;
12 Boazi akawa baba wa Obedi, na Obedi akawa baba wa Yese.
et Boaz engendra Obed, et Obed engendra Isaï;
13 Yese akawa baba wa mzaliwa wake wa kwanza Eliabu, wa pili Abinadabu, wa tatu Shama.
et Jessé engendra son premier-né Éliab, Abinadab le second, Shimea le troisième,
14 Nethaneli wa nne, Radai wa tano.
Nethanel le quatrième, Raddaï le cinquième,
15 Ozemu wa sita, na Daudi wa saba.
Ozem le sixième, et David le septième;
16 Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa Abishai, Yoabu, na Asaheli, jumla watatu.
et leurs sœurs étaient Séruia et Abigaïl. Fils de Séruia: Abischaï, Joab et Asaël, au nombre de trois.
17 Abigali akamzaa Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri Mwishmaeli.
Abigaïl enfanta Amasa; le père d'Amasa était Jéther, l'Ismaélite.
18 Kalebu mwana wa Hesroni akawa baba wa watoto wa Azubu mkewe, na Yeriothi. Wanawe walikuwa Yesheri, Shobabu, na Ardoni.
Caleb, fils de Hetsron, engendra des enfants d'Azuba, sa femme, et de Jerioth; voici ses fils: Jesher, Shobab et Ardon.
19 Azuba akafa, na Kalebu akamuoa Efrathi, aliye mzalia Huri.
Azuba mourut, et Caleb épousa Ephrath, qui lui donna naissance à Hur.
20 Huri akawa baba wa Uri, na Uri akawa baba wa Besaleli.
Hur engendra Uri, et Uri engendra Bezalel.
21 Baadae Hesroni (alipo kuwa na miaka sitini) akamuoa binti wa Makiri, baba wa Gileadi. Akamzalia Segubu.
Ensuite, Hetsron alla vers la fille de Makir, père de Galaad, qu'il prit pour femme à l'âge de soixante ans; et elle lui enfanta Segub.
22 Segubu akawa baba wa Yairi, aliye miliki miji ishirini na mitatu katika nchi ya Gileadi.
Segub engendra Jaïr, qui eut vingt-trois villes dans le pays de Galaad.
23 Geshuri na Aramu wakawapokonya miji ya Yairi na Kenathi, pamoja na miji sitini iliyo zunguka. Hawa wakazi wote walikuwa ni uzao wa Makiri, baba wa Gileadi.
Geshur et Aram leur prirent les villes de Jaïr, avec Kenath et ses villages, soit soixante villes. Tous ceux-là étaient les fils de Makir, père de Galaad.
24 Baada ya kifo cha Hesroni, Kalebu akalala na Efrata, mke wa baba yake Hesroni. Akamzalia Ashuri, baba wa Tekoa.
Après la mort de Hetsron à Caleb Ephrata, Abija, femme de Hetsron, lui enfanta Ashhur, père de Tekoa.
25 Wana wa Yerameeli, mzaliwa wa kwanza wa Hesroni, walikuwa ni Ramu mzaliwa wa kwanza, Buna, Oreni, Ozemu, na Ahiya.
Les fils de Jerahmeel, premier-né de Hezron, étaient Ram, premier-né, Bunah, Oren, Ozem et Ahijah.
26 Yerameeli alikuwa na mke mwingine, Jina lake lilikuwa Atara. Yeye alikuwa mama wa Onamu.
Jerahmeel avait une autre femme, dont le nom était Atarah. Elle était la mère d'Onam.
27 Wana wa Ramu, mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli, walikuwa Maasi, Yamini, na Ekeri.
Les fils de Ram, premier-né de Jerahmeel, étaient Maaz, Jamin et Eker.
28 Wana wa Onamu walikuwa ni Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa ni Nadabu na Abishuri.
Les fils d'Onam étaient: Shammai et Jada. Fils de Schammaï: Nadab et Abischur.
29 Jina la mke wa Abishuri lilikuwa Abihaili, na akamzalia Abani na Molidi.
Le nom de la femme d'Abischur était Abihail; elle lui enfanta Ahban et Molid.
30 Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa pasipo watoto.
Fils de Nadab: Seled et Appaïm; mais Seled mourut sans enfants.
31 Mwana wa Apaimu alikuwa Ishi. Mwana wa Ishi alikuwa Sheshani. Mwana wa Sheshani alikuwa Alai.
Fils d'Appaïm: Ishi. Fils d'Ishi: Sheshan. Fils de Sheshan: Ahlaï.
32 Wana wa Yada, kaka yake Shamai, walikuwa Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa pasipo mtoto.
Fils de Jada, frère de Schammaï: Jéther et Jonathan; Jéther mourut sans enfants.
33 Wana wa Yonathani walikuwa Pelethi na Zaza. Hawa ndio uzao wa Yerameeli.
Fils de Jonathan: Peleth et Zaza. Ce sont là les fils de Jerahmeel.
34 Sasa Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, bali wa kike pekee. Sheshani alikuwa na mtumishi, wa Kimisri, ambaye jina lake lilikuwa Yariha.
Or Sheshan n'avait pas de fils, mais seulement des filles. Sheshan avait un serviteur, un Égyptien, dont le nom était Jarha.
35 Sheshani alimkabidhi binti yake kwa Yariha mtumishi wake kama mke wake. Akamzalia Atai.
Sheshan donna sa fille pour femme à son serviteur Jarha, qui lui enfanta Attaï.
36 Atai akawa baba wa Nathani, na Nathani akawa baba wa Zabadi.
Attaï engendra Nathan; Nathan engendra Zabad;
37 Zabadi akawa baba wa Efalali, na Afalali akawa baba wa Obedi.
Zabad engendra Ephlal; Ephlal engendra Obed;
38 Obedi akawa baba wa Yehu, na Yehu akawa baba wa Azaria.
Obed engendra Jéhu; Jéhu engendra Azaria,
39 Azaria akawa baba wa Helesi, na Helesi akawa baba wa Eleasa.
Azaria engendra Hélez, et Hélez engendra Éleasa,
40 Eleasa akawa baba wa Sismai, na Sismai akawa baba wa Shalumu.
Éleasa engendra Sismaï, et Sismaï engendra Shallum,
41 Shalumu akawa baba wa Yekamia, na Yekamia akawa baba wa Elishama.
Shallum engendra Jekamia, et Jekamia engendra Élishama.
42 Wana wa Kalebu, kaka yake Yerameeli, walikuwa ni Mesha mzaliwa wake wa kwanza, aliye kuwa baba wa Zifu. Mwanae wa pili, Maresha, allikuwa baba wa Hebroni.
Fils de Caleb, frère de Jerahmeel: Mesha, son premier-né, père de Ziph, et les fils de Marescha, père d'Hébron.
43 Wana wa Hebroni walikuwa Kora, Tapua, Rekemu, na Shema.
Fils d'Hébron: Koré, Tappuach, Rékem et Schéma.
44 Shema akawa baba wa Rahamu, baba wa Yorkeamu. Rekemu akawa baba wa Shamai.
Shema engendra Raham, père de Jorkeam; et Rekem engendra Shammai.
45 Mwana wa Shamai alikuwa Maoni, na Maoni alikuwa baba wa Bethsuri.
Le fils de Shammaï était Maon; et Maon était le père de Beth Tsur.
46 Efa, suria wa Kalebu, alimza Harani, Mosa, na Gazezi. Harani akawa baba wa Gazezi.
Epha, concubine de Caleb, enfanta Haran, Moza et Gazez; et Haran engendra Gazez.
47 Wana wa Yadai walikuwa Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa, na Shaafa.
Fils de Jahdaï: Regem, Jothan, Geshan, Pelet, Épha et Shaaph.
48 Maaka, suria wa Kalebu, alimza Sheberi na Tirhana.
Maaca, concubine de Caleb, enfanta Shéber et Tirhana.
49 Pia akamza Shaafu baba wa Madmana, Sheva baba wa Makbena na baba wa Gibea. Binti wa Kalebu alikuwa Aksa. Hawa walikuwa uzao wa Kalebu.
Elle enfanta aussi Shaaph, père de Madmanna, Sheva, père de Machbena et père de Gibea; et la fille de Caleb était Acsa.
50 Hawa walikuwa wana wa Huri, mzaliwa wake wa kwanza kwa Efratha: Shobali baba wa Kiriath-Yearimu.
Voici les fils de Caleb, fils de Hur, premier-né d'Éphrata: Schobal, père de Kiriath Jearim,
51 Salma baba wa Bethlehemu, na Harefu baba wa Beth-gaderi.
Salma, père de Bethléhem, et Hareph, père de Beth Gader.
52 Shobali baba wa kiriath-Yearimu alikuwa na uzao: Haroe, nusu ya watu Wamenuthite,
Shobal, père de Kiriath Jearim, eut des fils: Harœh, la moitié des Menuhoth.
53 na ukoo wa Kiriath-Yearimu: Waithri, Waputhi, Washumathi, na Wamishrai. Wasorathi na Waeshtaoli walitoka huku.
Familles de Kiriath Jearim: les Ithrites, les Puthites, les Shumathites et les Mishraites; d'eux vinrent les Zorathites et les Eshtaolites.
54 Ukoo wa Salma ulikuwa kama ufatao: Bethlehemu, Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, na nusu ya Wamenuhothi na Wazori,
Fils de Salma: Bethléem, les Netophathes, Atroth Beth Joab, la moitié des Manahathes, les Zorathes.
55 ukoo wa waandishi walio ishi Yabesi: Watirathi, Washimeathi, na Wasukathi. Hawa walikuwa Wakeni walio toka katika uzao wa Hamathi, babu wa Warekabu.
Familles de scribes qui habitaient à Jabez: les Tirathites, les Shimeathites et les Sucathites. Ce sont les Kénites qui sont venus de Hammath, père de la maison de Réchab.

< 1 Nyakati 2 >