< 1 Nyakati 19 >
1 Ikajakuwa baadae kwamba Nahashi, mfalme wa watu wa Amoni, akafa, na mwanae akawa mfalme baada yake.
And it came to pass after this, that Nachash the king of the children of 'Ammon died, and his son became king in his stead.
2 Daudi akasema, “Nitaonyesha ukarimu kwa mwana wa Hanuni wa Nahashi, kwasababu baba yake alionyesha ukarimu kwangu.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe kumfariji kuhusu baba yake. Watumishi wa Daudi wakaingia nchi ya Waamoni na kumfuata Hanuni, ilikumfariji.
And David said, I will show kindness unto Chanun the son of Nachash, because his father showed kindness unto me. And David sent messengers to comfort him concerning his father. And the servants of David came unto the land of the children of 'Ammon to Chanun, to comfort him.
3 Lakini viongozi wakamwambia Hanuni, “Unadhani Daudi anamheshimu baba yako sababu ametuma watu kukufaraji? Je watumishi wake hawajaja kutadhimini nchi iliwaipindue?
And the princes of the children of 'Ammon said unto Chanun, Doth David honor thy father in thy eyes, that he hath sent comforters unto thee? are not his servants come unto thee in order to search out, and to overthrow, and to spy out the land?
4 Hanuni akawakamata watumishi wa Daudi, akawanyoa, akakata mavazi ya nusu kwenye kiuno kushuka, na kuwarudisha.
Chanun thereupon took David's servants, and shaved them, and cut off their garments in the middle as far as the hip-bone, and sent them away.
5 Walipo eleza haya kwa Daudi, alienda kukutana nao, kwa kuwa walifedheeka sana. Mfalme akasema, “Bakini Yeriko hadi ndevu zenu ziote tena, kisha mrudi.”
And some people went and told David concerning these men. And he sent [persons] to meet them: because the men were greatly ashamed; and the king said, Tarry at Jericho until your beard be grown, and then return.
6 Waamoni walipoona wamekuwa kikwazo kwa Daudi, Hanuni na Waamoni walituma talanta elfu moja za fedha kukodisha magari ya farasi kwa Waaremei na wanaume wa farasi kutoka Naharaimu, Maka, na Zoba.
And when the children of 'Ammon saw that they were become in bad odor with David, Chanun and the children of 'Ammon sent a thousand talents of silver to hire for themselves from Mesopotamia, and from Syria-ma'achah, and from Zobah, chariots and horsemen.
7 Waliwakodishia magari ya farasi elfu thelathini na mbili pamoja na mfalme wa Maka na watu wake, walio kuja na kueka kambi mbele ya Medeba. Waamoni walijikusanya pamoja kutoka miji yao, na wakaja kwa vita.
And they hired for themselves thirty and two thousand [warriors in] chariots, and the king of Ma'achah and his people: and they came and encamped before Medeba. And the children of 'Ammon gathered themselves together out of their cities, and came to the battle.
8 Daudi alipo sikia, alimtuma Yoabu na wanajeshi wake wote.
And when David heard of it, he sent Joab, and all the army [and] the mighty men.
9 Watu wa Amoni walikuja na kupanga mstari kwa ajili ya pambano katika lango la mji, wafalme waliokuja walikuwa peke yao katika shamba.
And the children of 'Ammon came out, and put themselves in battle array at the entrance of the city: and the kings that were come were by themselves in the field.
10 Yoabu alipoona mistari ya pambano imemzunguka mbele na nyuma, alichagua wapambanaji shupavu wa Israeli na kuwa panga dhidi ya Waaremi.
When now Joab saw that the front of battle was against him before and behind, he made a selection from all the chosen men of Israel, and arrayed himself against the Syrians.
11 Wanajeshi wengine wote, aliwaeka chini ya Abishai kaka yake, akawapanga kwa mstari dhidi ya Amoni.
And the rest of the people he delivered into the hand of Abshai his brother, and they arrayed themselves against the children of 'Ammon.
12 Yoabu akasema, “Kama Waaremi wananguvu kunizidi, kisha wewe, Abishai, lazima uniokoe. Lakini kama jeshi la Waamoni lina nguvu kukuzidi, nitakuja kukuokoa.
And he said, If the Syrians be too strong for me, then shalt thou bring me help; but if the children of 'Ammon be too strong for thee, then will I help thee.
13 Kuwa thabiti, natujionyeshe kwa watu wetu kuwa ni wenye nguvu na kwa miji ya Mungu wetu, kwa kuwa Yahweh ata fanya lililo jema kwa kusudi lake.”
Be strong, and let us strengthen ourselves in behalf of our people, and in behalf of the cities of our God, and may the Lord do that which seemeth good in his eyes.
14 Hivyo Yoabu na wanajeshi wasogea kwenye pambano dhidi ya Waaremi, walio lazimika kukimbia mbele ya jeshi la Waisraeli.
And Joab drew nigh and the people that were with him in front of the Syrians unto the battle, and they fled from before him.
15 Jeshi la Waamoni walipoona kuwa Waaremi wamekimbia, wao pia wakamkimbia kaka yake Yoabu Abishai na kurudi mjini. Kisha Yoabu akarudi kutoka kwa watu wa Amoni na kurudi Yerusalemu.
And when the children of 'Ammon saw that the Syrians were fled, then did they also fly before Abshai his brother, and entered into the city. And Joab went back to Jerusalem.
16 Waaremi walipoona kuwa wanashindwa na Waisraeli, wakatuma msaada nyuma ya Mto Frati, na Shofaki mkuu wajeshi la Hadadezeri.
And when the Syrians saw that they were smitten before Israel, they sent messengers, and brought out the Syrians that were beyond the river: and Shophach the captain of the army of Hadar'ezer went before them.
17 Daudi alipo ambiwa haya, akakusanya Israeli yote, akuvuka Yordani, na kuja juu yao. Alipanga jeshi kwa ajili ya pambano dhidi ya Waaremi, na wakapigana nao.
And when it was told to David, he gathered all Israel together, and passed over the Jordan, and came up with them, and arrayed himself against them. So when David had arrayed himself against the Syrians [for] battle, they fought with him.
18 Waaremi waliwakimbia Waisraeli, na Daudi akaua waendesha magari ya farasi ya Waaremi elfu saba na wanajeshi wa miguu elfu arobaini. Pia alimuua Shopaki, mkuu wa jeshi.
And the Syrians fled from before Israel: and David slew of the Syrians [the men of] seven thousand chariots, and forty thousand men on foot, and Shophach the captain of the army he put to death.
19 Wafalme wote walio kuwa watumishi wa Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, walifanya amani na Daudi na kumtumikia. Hivyo watu wa Aramu hawakuwa tayari kuwasaidia Waamoni.
And when the vassals of Hadar'ezer saw that they were smitten before Israel, they made peace with David, and served him: and the Syrians would not help the children of 'Ammon any more.