< 1 Nyakati 18 >

1 Baada ya haya Daudi akawashambulia Wafilisti na kuwashinda. Alichukuwa Gathi na vijiji vyake katika utawala wa Wafilisti.
Il advint, après cela, que David battit les Philistins et qu'il les mit en fuite; et il leur enleva Geth avec ses bourgs.
2 Kisha akamshinda Moabu, na Wamoabu wakawa watumishi wa Daudi na wakamlipa ushuru maalumu.
Il vainquit Moab, et les fils de Moab lui furent asservis; et ils lui payèrent un tribut.
3 Daudi kisha akamshinda Hadadezeri, mfalme wa Zoba huko Hamathi, wakati Hadadezeri alipo kuwa akisafiri kuimarisha utawala wake kwa Mto wa Frati.
David vainquit aussi, dans le pays d'Hémath, Adraazar, roi de Suba, qui s'était mis en campagne pour se rendre maître des rives de l'Euphrate.
4 Daudi akateka magari ya farasi elfu, wanaume wa farasi elfu saba, na wanajeshi wa miguu elfu ishirini. Daudi aliwajeruhi farasi wote wagari, lakini akahifadhi baadhi kwa ajili ya magari ya farasi mia moja.
Et David prit aux vaincus mille chars, sept mille chevaux et vingt mille piétons; puis, il énerva les attelages de tous les chars, et n'en garda que cent.
5 Waaramia wa Damasko walipo kuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Zoba, Daudi aliua wanaume elfu ishirini na mbili wa Kiaramia.
Et le Syrien de Damas marcha au secours d'Adraazar, roi de Suba, et David tua au Syrien vingt-deux mille hommes.
6 Kisha Daudi akaweka vikosi huko Aramu ya Damasko, na Waaramia wakawa watumishi wake na wakamletea ushuru maalaumu. Yahweh alimpatia Daudi ushindi popote alipoenda.
Et David mit une garnison dans la Syrie de Damas, et les Syriens lui furent asservis; ils lui payèrent un tribut. Et le Seigneur protégea David partout où il porta ses armes.
7 Daudi alichukua ngao za dhahabu zilizo kuwa kwa watumishi wa Hadadezeri na kuleta Yerusalemu.
Et David prit les colliers d'or que portaient les serviteurs d'Adraazar, et il les consacra dans Jérusalem.
8 Kutoka Tibhathi na Kuni, miji ya Hadadezeri, Daudi alichukuwa shaba nyingi sana. Ilikuwa shaba hii ambayo baadae Sulemani alifanya saani ya shaba, nguzo, na vifaa vya shaba.
Et David recueillit à Mathabeth (Métébac), et dans les principales villes d'Adraazar, une prodigieuse quantité d'airain, dont Salomon se servit pour fabriquer la mer d'airain, et les colonnes et tous les vases d'airain.
9 Wakati Toi, mfalme wa Hamathi, alipo sikia kuwa Daudi ameshinda majeshi yote ya Hadadezeri mfalme wa Zoba,
Cependant Thoa (Thu), roi d'Hémath, apprit que David avait taillé en pièces toute l'armée d'Adraazar.
10 Toi akamtuma Hadoramu mwanae kwa Mfalme Daudi kumsalimia na kumbariki, kwasababu Daudi amepigana na Hadadezeri na kumshinda, na kwasababu Hadadezeri alifanya vita na Toi. Hadoramu alipeleka vifaa vya fedha, dhahabu, na shaba.
Et il envoya vers David son fils Aduram (Jedduram), pour lui demander la paix et le bénir à cause de sa victoire sur Adraazar; car Thoa était ennemi d'Adraazar. Et tous les vases d'or, d'argent et d'airain,
11 Mfalme Daudi alivitenga hivi vitu kwa ajili ya Yahweh, pamoja na fedha na dhahabu aliyo ibeba kutoka kwa mataifa yote: Edomu, Moabu, watu wa Amoni, Wafilisti, na Waamaleki.
Le roi David les consacra au Seigneur de même que l'argent et l'or qu'il avait pris à toutes les nations: à l'Idumée, à Moab, aux fils d'Ammon, aux Philistins et aux fils d'Amalec.
12 Abishai mwana wa Zeruia akawaua Waedomi elfu kumi na nane katika Bonde la Chumvi.
Et Abessa, fils de Sarvia, tailla en pièces quatre-vingt mille Philistins dans le val d'Aïlon.
13 Alieka vikosi huko Edomu, na Waedomi wote wakawa watumishi wa Daudi. Yahweh alimpa Daudi ushindi pote alipoenda.
Et il mit dans la vallée une garnison, et tous les Iduméens furent asservis à David, et le Seigneur protégea David partout où il porta ses armes.
14 Daudi alitawala Israeli yote, na alitenda haki na utaua kwa watu wote.
Ainsi, David régna sur tout Israël, et il jugea tout son peuple selon l'équité.
15 Yoabu mwana wa Zeruia walikuwa mkuu wa jeshi, na Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mtunza kumbukumbu.
Joab, fils de Sarvia, commandait l'armée; Josaphat, fils d'Achilud, recueillait les actes publics.
16 Zadoki mwana wa Ahitubi na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Shavisha alikuwa mwandishi.
Sadoc, fils d'Achitob, et Achimélech, fils d'Abiathar, étaient prêtres, et Susa (Sasa), scribe.
17 Benaia mwana wa Yehoiada alikuwa mwangalizi wa Wakerethi na Wapelethi, na wana wa Daudi walikuwa washauri wakuu wa mfalme.
Et Banaïas, fils de Joad, commandait Chéléthi et Phéléthi, et les fils de David étaient les premiers lieutenants du roi.

< 1 Nyakati 18 >