< 1 Nyakati 18 >

1 Baada ya haya Daudi akawashambulia Wafilisti na kuwashinda. Alichukuwa Gathi na vijiji vyake katika utawala wa Wafilisti.
And it came to pass afterwards, that David struck the Philistines, and routed them, and took Geth and its villages out of the hand of the Philistines.
2 Kisha akamshinda Moabu, na Wamoabu wakawa watumishi wa Daudi na wakamlipa ushuru maalumu.
And he struck Moab; and the Moabites became servants to David, [and] tributaries.
3 Daudi kisha akamshinda Hadadezeri, mfalme wa Zoba huko Hamathi, wakati Hadadezeri alipo kuwa akisafiri kuimarisha utawala wake kwa Mto wa Frati.
And David struck Adraazar king of Suba of Emath, as he was going to establish power towards the river Euphrates.
4 Daudi akateka magari ya farasi elfu, wanaume wa farasi elfu saba, na wanajeshi wa miguu elfu ishirini. Daudi aliwajeruhi farasi wote wagari, lakini akahifadhi baadhi kwa ajili ya magari ya farasi mia moja.
And David took of them a thousand chariots, and seven thousand horsemen, and twenty thousand infantry: and David houghed all the chariot [horses], but there were reserved of them a hundred chariots.
5 Waaramia wa Damasko walipo kuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Zoba, Daudi aliua wanaume elfu ishirini na mbili wa Kiaramia.
And the Syrian came from Damascus to help Adraazar king of Suba; and David struck of the Syrian [army] twenty and two thousand men.
6 Kisha Daudi akaweka vikosi huko Aramu ya Damasko, na Waaramia wakawa watumishi wake na wakamletea ushuru maalaumu. Yahweh alimpatia Daudi ushindi popote alipoenda.
And David put a garrison in Syria near Damascus; and they became tributary servants to David: and the Lord delivered David wherever he went.
7 Daudi alichukua ngao za dhahabu zilizo kuwa kwa watumishi wa Hadadezeri na kuleta Yerusalemu.
And David took the golden collars that were on the servants of Adraazar, and brought them to Jerusalem.
8 Kutoka Tibhathi na Kuni, miji ya Hadadezeri, Daudi alichukuwa shaba nyingi sana. Ilikuwa shaba hii ambayo baadae Sulemani alifanya saani ya shaba, nguzo, na vifaa vya shaba.
And David took out of Matabeth, and out of the chief cities of Adraazar very much brass: of this Solomon made the brazen sea, and the pillars, and the brazen vessels.
9 Wakati Toi, mfalme wa Hamathi, alipo sikia kuwa Daudi ameshinda majeshi yote ya Hadadezeri mfalme wa Zoba,
And Thoa king of Emath heard that David had struck the whole force of Adraazar king of Suba.
10 Toi akamtuma Hadoramu mwanae kwa Mfalme Daudi kumsalimia na kumbariki, kwasababu Daudi amepigana na Hadadezeri na kumshinda, na kwasababu Hadadezeri alifanya vita na Toi. Hadoramu alipeleka vifaa vya fedha, dhahabu, na shaba.
And he sent Aduram his son to king David to ask how he was, and to congratulate him because he had fought against Adraazar, and struck him; for Thoa was the enemy of Adraazar.
11 Mfalme Daudi alivitenga hivi vitu kwa ajili ya Yahweh, pamoja na fedha na dhahabu aliyo ibeba kutoka kwa mataifa yote: Edomu, Moabu, watu wa Amoni, Wafilisti, na Waamaleki.
And all the golden and silver and brazen vessels, even these king David consecrated to the Lord, with the silver and the gold which he took from all the nations; from Idumaea, and Moab, and from the children of Ammon, and from the Philistines, and from Amalec.
12 Abishai mwana wa Zeruia akawaua Waedomi elfu kumi na nane katika Bonde la Chumvi.
And Abesa son of Saruia struck the Idumeans in the valley of Salt, eighteen thousand.
13 Alieka vikosi huko Edomu, na Waedomi wote wakawa watumishi wa Daudi. Yahweh alimpa Daudi ushindi pote alipoenda.
And he put garrisons in the valley; and all the Idumaeans became David's servants: and the Lord delivered David wherever he went.
14 Daudi alitawala Israeli yote, na alitenda haki na utaua kwa watu wote.
So David reigned over all Israel; and he executed judgement and justice to all his people.
15 Yoabu mwana wa Zeruia walikuwa mkuu wa jeshi, na Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mtunza kumbukumbu.
And Joab the son of Saruia [was] over the army, and Josaphat the son of Achilud [was] recorder.
16 Zadoki mwana wa Ahitubi na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Shavisha alikuwa mwandishi.
And Sadoc son of Achitob, and Achimelech son of Abiathar, [were] the priests; and Susa [was] the scribe;
17 Benaia mwana wa Yehoiada alikuwa mwangalizi wa Wakerethi na Wapelethi, na wana wa Daudi walikuwa washauri wakuu wa mfalme.
and Banaeas the son of Jodae [was] over the Cherethite and the Phelethite, and the sons of David were the chief deputies of the king.

< 1 Nyakati 18 >