< 1 Nyakati 16 >

1 Wakaleta ndani Sanduku la Mungu na kuweka katika ya hema ambalo Daudi aliandaa. Kisha wakatoa sadaka ya kuteketeza na sadaka ya ushirika mbele ya Mungu.
Entraron el Arca de Dios y la colocaron en medio del Tabernáculo que David había erigido para ella; y ofrecieron ante Dios holocaustos y sacrificios pacíficos.
2 Daudi alipo maliza kutoa dhabiu ya kuteketeza na sadaka za ushirika, aliwabariki watu kwa jina la Yahweh.
Cuando David hubo acabado de ofrecer los holocaustos y los sacrificios pacíficos, bendijo al pueblo en nombre de Yahvé,
3 Alisambaza kwa kila Misraeli, mwanaume na mwanamke, kipande cha mkate, na kipande cha nyama, na keki ya mzabibu.
y distribuyó a toda la gente de Israel, hombres y mujeres, a cada uno, una torta de pan, una porción de carne y un pastel de uvas pasas.
4 Daudi aliewapangia baadhi ya Walawi kutumika mbele ya sanduku la Yahweh, na kusheherekea, kushukuru na kumsifu Yahweh, Mungu wa Israeli.
Y puso levitas que habían de hacer el servicio delante del Arca de Yahvé, invocando, alabando y ensalzando a Yahvé, el Dios de Israel.
5 Hawa Walawi walikuwa Asafu kiongozi, wa pili kutoka kwake Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaia, Obedi Edomu, na Yeieli. Hawa walikuwa wacheze na vyombo vya uzi na vinubi. Asafu alikuwa apige upatu, kwa kelele.
Asaf era el jefe; después de él, Zacarías, Jeiel, Semiramot, Jehiel, Matatías, Eliab, Banaías, Obededom y Jeiel, que tenían salterios y cítaras. Asaf hacía sonar los címbalos.
6 Benaia na Yahazieli walikuwa wakupiga tarumbeta kila mara, mbele sanduku la agano la Mungu.
Los sacerdotes Banaías y Jahaziel estaban con trompetas continuamente delante del Arca de la Alianza de Yahvé.
7 Kisha katika hiyo siku Daudi akawachagua Asafu na kaka zake kuimba hii nyimbo ya shukurani kwa Yahweh.
Entonces, en aquel día, David dio por primera vez (este himno) en manos de Asaf y de sus hermanos para que alabasen a Yahvé:
8 Mpeni shukurani Yahweh, liitieni jina lake; fahamisheni mataifa matendo yake.
“¡Alabad a Yahvé, invocad su nombre; pregonad a las naciones sus proezas!
9 Mwiimbieni, imbeni sifa kwake; semeni matendo yake ya ajabu.
¡Cantadle, tañed salmos en su honor; narrad todas sus maravillas!
10 Jisifuni katika jina lake takatifu; mioyo ya wanao mtafuta Yahweh ishangilie.
¡Gloriaos en su santo Nombre; alégrese el corazón de los que buscan a Yahvé!
11 Mtafute Yahweh na nguvu zake; tafuteni uwepo wake siku zote.
¡Buscad a Yahvé y su fortaleza; buscad de continuo su Rostro!
12 Kumbukeni matendo aliyo ya fanya kwenu, miujiza yake na amri za kinywa chake,
¡Acordaos de las maravillas que Él ha hecho, de sus prodigios y de los juicios de su boca,
13 enyi uzao wa Israeli mtumishi wake, enyi watu wa Yakobo, wateule wake.
oh hijos de Israel, su siervo, descendientes de Jacob, sus elegidos!
14 Yeye ni Yahweh, Mungu wetu. Amri zake zipo duniani kote.
Él es Yahvé, Dios nuestro; Él es quien juzga toda la tierra.
15 Tunzeni agano lake akilini mwenu milele, neno alilo liamuru kwa vizazi elfu moja.
Recordad para siempre su Alianza, la palabra valedera para mil generaciones;
16 Anakumbuka agano alilo lifanya na Ibrahimu, na nadhiri yake kwake Isaka.
el pacto que firmó con Abrahán, y el juramento que prestó a Isaac.
17 Hili ndilo alilo lithibitisha kwa Yakobo kama amri maalumu, na kwa Israeli kama agano la milele.
Lo estableció para Jacob como ley, y para Israel como alianza eterna;
18 Alisema, “Nitakupa nchi ya Kanani kama sehemu ya urithi wako.”
diciendo: “Te daré el país de Canaán, como parte de vuestra herencia.”
19 Nilisema hili mlipo kuwa wachache kwa idadi, wachache sana, mlipo kuwa wageni katika nchi.
Cuando erais escasa gente, poco numerosos, y extranjeros en el país;
20 Walienda taifa hadi taifa, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
cuando iban de una nación a otra, y de un reino a otro pueblo,
21 Hakuwaruhusu yeyote awatese; aliwahadhibu wafalme kwa ajili yao.
no permitió que nadie los oprimiese. Por amor de ellos castigó a reyes;
22 Alisema, “Msiwaguse wapakwa mafuta wangu, na msiwadhuru manabii wangu.”
“¡No toquéis a mis ungidos, ni hagáis mal a mis profetas!”
23 Imbeni kwa Yahweh, dunia yote; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
Cantad a Yahvé, oh tierra toda, anunciad de día en día su salvación.
24 Kirini utukufu wake kwa mataifa, matendo yake makuu kwa mataifa yote.
Narrad entre las naciones su gloria, sus maravillas a todos los pueblos.
25 Kwa kuwa Yahweh ni mkuu na ni wakusifiwa sana, na ni wakuogopewa kuliko miungu yote.
Pues grande es Yahvé, y digno de toda alabanza; y más temible que todos los dioses.
26 Kwa kuwa miungu ya mataifa ni sanamu, lakini ni Yahweh aliye umba mbingu.
Porque ídolos son todos los dioses de los pueblos. Yahvé ha creado los cielos;
27 Uzuri wa ajabu na utukufu upo uweponi mwake. Uwezo na furaha upo kwake.
gloria y majestad están ante Él, fortaleza y alegría, en su Morada.
28 Mpeni sifa Yahweh, enyi koo za watu, mpeni sifa Yahweh utukufu na uwezo;
Tributad a Yahvé, oh familias de los pueblos, dad a Yahvé la gloria y el poder!
29 Mpeni Yahweh utukufu upasao jina lake. Leta sadaka na mje kwake. Muinamieni Yahweh katika utakatifu wa uzuri wake.
¡Tributad a Yahvé la gloria de su Nombre! ¡Traed ofrendas, y presentaos delante de Él! ¡Adorad a Yahvé con adorno sagrado!
30 Mtetemeke mbele zake, dunia yote. Dunia imeimarishwa; haiwezi kutikisika.
¡Conmuévase ante Él toda la tierra! Firme está el orbe, y no será conmovido.
31 Mbingu nazo ziwe nafuraha, na dunia ifurahi; na wasema kwa mataifa yote, “Yahweh anatawala.”
¡Regocíjense los cielos, y alégrese la tierra; digan los gentiles: “¡Yahvé es rey!”
32 Bahari na ingurume, na inayo ijaza ipige kelele kwa furaha. Mashamba yawe na furaha tele, na vyote vilivyomo ndani yake.
¡Brame el mar, y cuanto lo llena! ¡Salten de júbilo los campos, y cuanto en ellos existe!
33 Na miti iliyopo misituni ipige kelele kwa Yahweh, kwa kuwa anakuja kuhukumu dunia.
Prorrumpan en gritos de alegría los árboles de la selva, ante Yahvé; pues viene a juzgar la tierra.
34 Toeni shukurani kwa Yahweh, kwa kuwa ni mwema, uaminifu wa agano lake la dumu ata milele.
¡Alabad a Yahvé, porque Él es bueno, porque es eterna su misericordia!
35 Kisha sema, “Tuokoe, Mungu wa wokovu wetu. Tukusanye pamoja na utuokoe kutoka kwa mataifa mengine, ilikwamba tutoe shukurani kwa jina lako takatifu na tufurahi katika sifa zako.”
Y decid: “¡Sálvanos, oh Dios de nuestra salvación; reúnenos y líbranos de las naciones, para que celebremos tu santo Nombre, y nos gloriemos, cantando tus alabanzas!
36 Na Yahweh, Mungu wa Israeli, asifiwe kutoka milele na milele. Watu wote wakasema, “Amina” na wakamsifu Yahweh.
Bendito sea Yahvé, el Dios de Israel, por eternidad de eternidades.” Y todo el pueblo dijo: “Amén”, y alabó a Yahvé.
37 Hivyo Daudi akamwacha Asafu na kaka zake pale mbele ya sanduku la Yahweh, kutumika daima mbele ya sanduku, kama kazi za kila siku zilivyo itaji. Obedi Edomu pamoja na ndugu sitini na nane walijumuishwa.
Entonces dejó (David) allí, delante del Arca de la Alianza de Yahvé, a Asaf y sus hermanos, para el servicio continuo delante del Arca, según el reglamento de cada día;
38 Obedi Edomu mwana wa Yeduthuni, pamoja na Hosa, walikuwa wawe walinzi wa lango.
y a Obededom, con sus hermanos, en número de sesenta y ocho; y a Obededom, hijo de Iditún, y a Hosá, como porteros;
39 Zadoki kuhani na makuhani wenzake walikuwa watumike mbele ya hema la Yahweh katika mahali pa juu huko Gibeoni.
asimismo a Sadoc, el sacerdote, y sus hermanos, los sacerdotes, delante de la Morada de Yahvé, en la altura de Gabaón,
40 Walikuwa watoe sadaka za kuteketeza kwa Yahweh kwenye madhabahu ya sadaka za kuteketeza daima asubui na jioni, kwa mujibu wa yote yalio andikwa katika amri za Yahweh, aliyo wapa Waisraeli kama sheria.
para que ofreciesen continuamente holocaustos a Yahvé en el altar del holocausto, por la mañana y por la tarde, según todo lo dispuesto en la Ley de Yahvé, que Él había prescrito a Israel.
41 Hemani na Yeduthuni walikuwa nao, pamoja na walio chaguliwa kwa jina, kumpa shukurani Yahweh, kwasababu uaminifu wa agano lake la dumu ata milele
Con ellos (estableció) a Hemán y a Iditún, y a los otros escogidos y nominalmente designados, para alabar a Yahvé: “Porque su misericordia es eterna.”
42 Hemani na Yeduthuni walikuwa viongozi wa wao waliopiga tarumbeta, upatu, na vyombo vingine kwa muziki wa kumuabudu Mungu. Wana wa Yeduthuni walilinda lango.
Con ellos estaban, pues, Hemán e Iditún, que tenían las trompetas y los címbalos para cuantos los tocaban, y los instrumentos para los cánticos de Dios. Los hijos de Iditún eran porteros.
43 Kisha watu wote walirudi nyumbani, na Daudi akarudi kubariki nyumba yake.
Luego todo el pueblo se fue, cada cual a su casa; también David se volvió para bendecir su casa.

< 1 Nyakati 16 >