< 1 Nyakati 16 >

1 Wakaleta ndani Sanduku la Mungu na kuweka katika ya hema ambalo Daudi aliandaa. Kisha wakatoa sadaka ya kuteketeza na sadaka ya ushirika mbele ya Mungu.
adtulerunt igitur arcam Dei et constituerunt eam in medio tabernaculi quod tetenderat ei David et obtulerunt holocausta et pacifica coram Deo
2 Daudi alipo maliza kutoa dhabiu ya kuteketeza na sadaka za ushirika, aliwabariki watu kwa jina la Yahweh.
cumque conplesset David offerens holocausta et pacifica benedixit populo in nomine Domini
3 Alisambaza kwa kila Misraeli, mwanaume na mwanamke, kipande cha mkate, na kipande cha nyama, na keki ya mzabibu.
et divisit universis per singulos a viro usque ad mulierem tortam panis et partem assae carnis bubulae et frixam oleo similam
4 Daudi aliewapangia baadhi ya Walawi kutumika mbele ya sanduku la Yahweh, na kusheherekea, kushukuru na kumsifu Yahweh, Mungu wa Israeli.
constituitque coram arca Domini de Levitis qui ministrarent et recordarentur operum eius et glorificarent atque laudarent Dominum Deum Israhel
5 Hawa Walawi walikuwa Asafu kiongozi, wa pili kutoka kwake Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaia, Obedi Edomu, na Yeieli. Hawa walikuwa wacheze na vyombo vya uzi na vinubi. Asafu alikuwa apige upatu, kwa kelele.
Asaph principem et secundum eius Zacchariam porro Iahihel et Semiramoth et Ieihel et Matthathiam et Eliab et Banaiam et Obededom et Ieihel super organa psalterii et lyras Asaph autem ut cymbalis personaret
6 Benaia na Yahazieli walikuwa wakupiga tarumbeta kila mara, mbele sanduku la agano la Mungu.
Banaiam vero et Azihel sacerdotes canere tuba iugiter coram arca foederis Domini
7 Kisha katika hiyo siku Daudi akawachagua Asafu na kaka zake kuimba hii nyimbo ya shukurani kwa Yahweh.
in illo die fecit David principem ad confitendum Domino Asaph et fratres eius
8 Mpeni shukurani Yahweh, liitieni jina lake; fahamisheni mataifa matendo yake.
confitemini Domino invocate nomen eius notas facite in populis adinventiones illius
9 Mwiimbieni, imbeni sifa kwake; semeni matendo yake ya ajabu.
canite ei et psallite et narrate omnia mirabilia eius
10 Jisifuni katika jina lake takatifu; mioyo ya wanao mtafuta Yahweh ishangilie.
laudate nomen sanctum eius laetetur cor quaerentium Dominum
11 Mtafute Yahweh na nguvu zake; tafuteni uwepo wake siku zote.
quaerite Dominum et virtutem eius quaerite faciem eius semper
12 Kumbukeni matendo aliyo ya fanya kwenu, miujiza yake na amri za kinywa chake,
recordamini mirabilium eius quae fecit signorum illius et iudiciorum oris eius
13 enyi uzao wa Israeli mtumishi wake, enyi watu wa Yakobo, wateule wake.
semen Israhel servi eius filii Iacob electi illius
14 Yeye ni Yahweh, Mungu wetu. Amri zake zipo duniani kote.
ipse Dominus Deus noster in universa terra iudicia eius
15 Tunzeni agano lake akilini mwenu milele, neno alilo liamuru kwa vizazi elfu moja.
recordamini in sempiternum pacti eius sermonis quem praecepit in mille generationes
16 Anakumbuka agano alilo lifanya na Ibrahimu, na nadhiri yake kwake Isaka.
quem pepigit cum Abraham et iuramenti illius cum Isaac
17 Hili ndilo alilo lithibitisha kwa Yakobo kama amri maalumu, na kwa Israeli kama agano la milele.
et constituit illud Iacob in praeceptum et Israhel in pactum sempiternum
18 Alisema, “Nitakupa nchi ya Kanani kama sehemu ya urithi wako.”
dicens tibi dabo terram Chanaan funiculum hereditatis vestrae
19 Nilisema hili mlipo kuwa wachache kwa idadi, wachache sana, mlipo kuwa wageni katika nchi.
cum essent pauci numero parvi et coloni eius
20 Walienda taifa hadi taifa, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
et transierunt de gente in gentem et de regno ad populum alterum
21 Hakuwaruhusu yeyote awatese; aliwahadhibu wafalme kwa ajili yao.
non dimisit quemquam calumniari eos sed increpuit pro eis reges
22 Alisema, “Msiwaguse wapakwa mafuta wangu, na msiwadhuru manabii wangu.”
nolite tangere christos meos et in prophetis meis nolite malignari
23 Imbeni kwa Yahweh, dunia yote; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
canite Domino omnis terra adnuntiate ex die in diem salutare eius
24 Kirini utukufu wake kwa mataifa, matendo yake makuu kwa mataifa yote.
narrate in gentibus gloriam eius in cunctis populis mirabilia illius
25 Kwa kuwa Yahweh ni mkuu na ni wakusifiwa sana, na ni wakuogopewa kuliko miungu yote.
quia magnus Dominus et laudabilis nimis et horribilis super omnes deos
26 Kwa kuwa miungu ya mataifa ni sanamu, lakini ni Yahweh aliye umba mbingu.
omnes enim dii populorum idola Dominus autem caelos fecit
27 Uzuri wa ajabu na utukufu upo uweponi mwake. Uwezo na furaha upo kwake.
confessio et magnificentia coram eo fortitudo et gaudium in loco eius
28 Mpeni sifa Yahweh, enyi koo za watu, mpeni sifa Yahweh utukufu na uwezo;
adferte Domino familiae populorum adferte Domino gloriam et imperium
29 Mpeni Yahweh utukufu upasao jina lake. Leta sadaka na mje kwake. Muinamieni Yahweh katika utakatifu wa uzuri wake.
date Domino gloriam nomini eius levate sacrificium et venite in conspectu eius et adorate Dominum in decore sancto
30 Mtetemeke mbele zake, dunia yote. Dunia imeimarishwa; haiwezi kutikisika.
commoveatur a facie illius omnis terra ipse enim fundavit orbem inmobilem
31 Mbingu nazo ziwe nafuraha, na dunia ifurahi; na wasema kwa mataifa yote, “Yahweh anatawala.”
laetentur caeli et exultet terra et dicant in nationibus Dominus regnavit
32 Bahari na ingurume, na inayo ijaza ipige kelele kwa furaha. Mashamba yawe na furaha tele, na vyote vilivyomo ndani yake.
tonet mare et plenitudo eius exultent agri et omnia quae in eis sunt
33 Na miti iliyopo misituni ipige kelele kwa Yahweh, kwa kuwa anakuja kuhukumu dunia.
tunc laudabunt ligna saltus coram Domino quia venit iudicare terram
34 Toeni shukurani kwa Yahweh, kwa kuwa ni mwema, uaminifu wa agano lake la dumu ata milele.
confitemini Domino quoniam bonus quoniam in aeternum misericordia eius
35 Kisha sema, “Tuokoe, Mungu wa wokovu wetu. Tukusanye pamoja na utuokoe kutoka kwa mataifa mengine, ilikwamba tutoe shukurani kwa jina lako takatifu na tufurahi katika sifa zako.”
et dicite salva nos Deus salvator noster et congrega nos et erue de gentibus ut confiteamur nomini sancto tuo et exultemus in carminibus tuis
36 Na Yahweh, Mungu wa Israeli, asifiwe kutoka milele na milele. Watu wote wakasema, “Amina” na wakamsifu Yahweh.
benedictus Dominus Deus Israhel ab aeterno usque in aeternum et dicat omnis populus amen et hymnus Domino
37 Hivyo Daudi akamwacha Asafu na kaka zake pale mbele ya sanduku la Yahweh, kutumika daima mbele ya sanduku, kama kazi za kila siku zilivyo itaji. Obedi Edomu pamoja na ndugu sitini na nane walijumuishwa.
dereliquit itaque ibi coram arca foederis Domini Asaph et fratres eius ut ministrarent in conspectu arcae iugiter per singulos dies et vices suas
38 Obedi Edomu mwana wa Yeduthuni, pamoja na Hosa, walikuwa wawe walinzi wa lango.
porro Obededom et fratres eius sexaginta octo et Obededom filium Idithun et Osa constituit ianitores
39 Zadoki kuhani na makuhani wenzake walikuwa watumike mbele ya hema la Yahweh katika mahali pa juu huko Gibeoni.
Sadoc autem sacerdotem et fratres illius sacerdotes coram tabernaculo Domini in excelso quod erat in Gabaon
40 Walikuwa watoe sadaka za kuteketeza kwa Yahweh kwenye madhabahu ya sadaka za kuteketeza daima asubui na jioni, kwa mujibu wa yote yalio andikwa katika amri za Yahweh, aliyo wapa Waisraeli kama sheria.
ut offerrent holocausta Domino super altare holocaustomatis iugiter mane et vespere iuxta omnia quae scripta sunt in lege Domini quam praecepit Israheli
41 Hemani na Yeduthuni walikuwa nao, pamoja na walio chaguliwa kwa jina, kumpa shukurani Yahweh, kwasababu uaminifu wa agano lake la dumu ata milele
et post eum Heman et Idithun et reliquos electos unumquemque vocabulo suo ad confitendum Domino quoniam in aeternum misericordia eius
42 Hemani na Yeduthuni walikuwa viongozi wa wao waliopiga tarumbeta, upatu, na vyombo vingine kwa muziki wa kumuabudu Mungu. Wana wa Yeduthuni walilinda lango.
Heman quoque et Idithun canentes tuba et quatientes cymbala et omnia musicorum organa ad canendum Deo filios autem Idithun fecit esse portarios
43 Kisha watu wote walirudi nyumbani, na Daudi akarudi kubariki nyumba yake.
reversusque est omnis populus in domum suam et David ut benediceret etiam domui suae

< 1 Nyakati 16 >