< 1 Nyakati 16 >

1 Wakaleta ndani Sanduku la Mungu na kuweka katika ya hema ambalo Daudi aliandaa. Kisha wakatoa sadaka ya kuteketeza na sadaka ya ushirika mbele ya Mungu.
Attulerunt igitur arcam Dei, et constituerunt eam in medio tabernaculi quod tetenderat ei David: et obtulerunt holocausta et pacifica coram Deo.
2 Daudi alipo maliza kutoa dhabiu ya kuteketeza na sadaka za ushirika, aliwabariki watu kwa jina la Yahweh.
Cumque complesset David offerens holocausta et pacifica, benedixit populo in nomine Domini.
3 Alisambaza kwa kila Misraeli, mwanaume na mwanamke, kipande cha mkate, na kipande cha nyama, na keki ya mzabibu.
Et divisit universis per singulos, a viro usque ad mulierem, tortam panis, et partem assæ carnis bubalæ, et frixam oleo similam.
4 Daudi aliewapangia baadhi ya Walawi kutumika mbele ya sanduku la Yahweh, na kusheherekea, kushukuru na kumsifu Yahweh, Mungu wa Israeli.
Constituitque coram arca Domini de Levitis, qui ministrarent, et recordarentur operum ejus, et glorificarent atque laudarent Dominum Deum Israël:
5 Hawa Walawi walikuwa Asafu kiongozi, wa pili kutoka kwake Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaia, Obedi Edomu, na Yeieli. Hawa walikuwa wacheze na vyombo vya uzi na vinubi. Asafu alikuwa apige upatu, kwa kelele.
Asaph principem, et secundum ejus Zachariam: porro Jahiel, et Semiramoth, et Jehiel, et Mathathiam, et Eliab, et Banaiam, et Obededom: Jehiel super organa psalterii et lyras: Asaph autem ut cymbalis personaret:
6 Benaia na Yahazieli walikuwa wakupiga tarumbeta kila mara, mbele sanduku la agano la Mungu.
Banaiam vero et Jaziel sacerdotes canere tuba jugiter coram arca fœderis Domini.
7 Kisha katika hiyo siku Daudi akawachagua Asafu na kaka zake kuimba hii nyimbo ya shukurani kwa Yahweh.
In illo die fecit David principem ad confitendum Domino Asaph et fratres ejus:
8 Mpeni shukurani Yahweh, liitieni jina lake; fahamisheni mataifa matendo yake.
Confitemini Domino, et invocate nomen ejus: notas facite in populis adinventiones ejus.
9 Mwiimbieni, imbeni sifa kwake; semeni matendo yake ya ajabu.
Cantate ei, et psallite ei, et narrate omnia mirabilia ejus.
10 Jisifuni katika jina lake takatifu; mioyo ya wanao mtafuta Yahweh ishangilie.
Laudate nomen sanctum ejus: lætetur cor quærentium Dominum.
11 Mtafute Yahweh na nguvu zake; tafuteni uwepo wake siku zote.
Quærite Dominum, et virtutem ejus: quærite faciem ejus semper.
12 Kumbukeni matendo aliyo ya fanya kwenu, miujiza yake na amri za kinywa chake,
Recordamini mirabilium ejus quæ fecit; signorum illius, et judiciorum oris ejus,
13 enyi uzao wa Israeli mtumishi wake, enyi watu wa Yakobo, wateule wake.
semen Israël servi ejus, filii Jacob electi ejus.
14 Yeye ni Yahweh, Mungu wetu. Amri zake zipo duniani kote.
Ipse Dominus Deus noster: in universa terra judicia ejus.
15 Tunzeni agano lake akilini mwenu milele, neno alilo liamuru kwa vizazi elfu moja.
Recordamini in sempiternum pacti ejus: sermonis quem præcepit in mille generationes,
16 Anakumbuka agano alilo lifanya na Ibrahimu, na nadhiri yake kwake Isaka.
quem pepigit cum Abraham, et juramenti illius cum Isaac.
17 Hili ndilo alilo lithibitisha kwa Yakobo kama amri maalumu, na kwa Israeli kama agano la milele.
Et constituit illud Jacob in præceptum, et Israël in pactum sempiternum,
18 Alisema, “Nitakupa nchi ya Kanani kama sehemu ya urithi wako.”
dicens: Tibi dabo terram Chanaan, funiculum hæreditatis vestræ:
19 Nilisema hili mlipo kuwa wachache kwa idadi, wachache sana, mlipo kuwa wageni katika nchi.
cum essent pauci numero, parvi et coloni ejus.
20 Walienda taifa hadi taifa, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
Et transierunt de gente in gentem, et de regno ad populum alterum.
21 Hakuwaruhusu yeyote awatese; aliwahadhibu wafalme kwa ajili yao.
Non dimisit quemquam calumniari eos, sed increpavit pro eis reges.
22 Alisema, “Msiwaguse wapakwa mafuta wangu, na msiwadhuru manabii wangu.”
Nolite tangere christos meos, et in prophetis meis nolite malignari.
23 Imbeni kwa Yahweh, dunia yote; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
Cantate Domino omnis terra; annuntiate ex die in diem salutare ejus:
24 Kirini utukufu wake kwa mataifa, matendo yake makuu kwa mataifa yote.
narrate in gentibus gloriam ejus; in cunctis populis mirabilia ejus.
25 Kwa kuwa Yahweh ni mkuu na ni wakusifiwa sana, na ni wakuogopewa kuliko miungu yote.
Quia magnus Dominus, et laudabilis nimis, et horribilis super omnes deos.
26 Kwa kuwa miungu ya mataifa ni sanamu, lakini ni Yahweh aliye umba mbingu.
Omnes enim dii populorum idola: Dominus autem cælos fecit.
27 Uzuri wa ajabu na utukufu upo uweponi mwake. Uwezo na furaha upo kwake.
Confessio et magnificentia coram eo: fortitudo et gaudium in loco ejus.
28 Mpeni sifa Yahweh, enyi koo za watu, mpeni sifa Yahweh utukufu na uwezo;
Afferte Domino, familiæ populorum: afferte Domino gloriam et imperium.
29 Mpeni Yahweh utukufu upasao jina lake. Leta sadaka na mje kwake. Muinamieni Yahweh katika utakatifu wa uzuri wake.
Date Domino gloriam; nomini ejus levate sacrificium, et venite in conspectu ejus: et adorate Dominum in decore sancto.
30 Mtetemeke mbele zake, dunia yote. Dunia imeimarishwa; haiwezi kutikisika.
Commoveatur a facie ejus omnis terra: ipse enim fundavit orbem immobilem.
31 Mbingu nazo ziwe nafuraha, na dunia ifurahi; na wasema kwa mataifa yote, “Yahweh anatawala.”
Lætentur cæli, et exultet terra, et dicant in nationibus: Dominus regnavit.
32 Bahari na ingurume, na inayo ijaza ipige kelele kwa furaha. Mashamba yawe na furaha tele, na vyote vilivyomo ndani yake.
Tonet mare et plenitudo ejus; exultent agri, et omnia quæ in eis sunt.
33 Na miti iliyopo misituni ipige kelele kwa Yahweh, kwa kuwa anakuja kuhukumu dunia.
Tunc laudabunt ligna saltus coram Domino: quia venit judicare terram.
34 Toeni shukurani kwa Yahweh, kwa kuwa ni mwema, uaminifu wa agano lake la dumu ata milele.
Confitemini Domino, quoniam bonus: quoniam in æternum misericordia ejus.
35 Kisha sema, “Tuokoe, Mungu wa wokovu wetu. Tukusanye pamoja na utuokoe kutoka kwa mataifa mengine, ilikwamba tutoe shukurani kwa jina lako takatifu na tufurahi katika sifa zako.”
Et dicite: Salva nos, Deus salvator noster, et congrega nos, et erue de gentibus: ut confiteamur nomini sancto tuo, et exultemus in carminibus tuis.
36 Na Yahweh, Mungu wa Israeli, asifiwe kutoka milele na milele. Watu wote wakasema, “Amina” na wakamsifu Yahweh.
Benedictus Dominus Deus Israël, ab æterno usque in æternum. Et dicat omnis populo: Amen, et hymnum Domino.
37 Hivyo Daudi akamwacha Asafu na kaka zake pale mbele ya sanduku la Yahweh, kutumika daima mbele ya sanduku, kama kazi za kila siku zilivyo itaji. Obedi Edomu pamoja na ndugu sitini na nane walijumuishwa.
Reliquit itaque ibi coram arca fœderis Domini Asaph et fratres ejus, ut ministrarent in conspectu arcæ jugiter per singulos dies, et vices suas.
38 Obedi Edomu mwana wa Yeduthuni, pamoja na Hosa, walikuwa wawe walinzi wa lango.
Porro Obededom, et fratres ejus sexaginta octo: et Obededom filium Idithun, et Hosa, constituit janitores;
39 Zadoki kuhani na makuhani wenzake walikuwa watumike mbele ya hema la Yahweh katika mahali pa juu huko Gibeoni.
Sadoc autem sacerdotem, et fratres ejus sacerdotes, coram tabernaculo Domini in excelso quod erat in Gabaon,
40 Walikuwa watoe sadaka za kuteketeza kwa Yahweh kwenye madhabahu ya sadaka za kuteketeza daima asubui na jioni, kwa mujibu wa yote yalio andikwa katika amri za Yahweh, aliyo wapa Waisraeli kama sheria.
ut offerrent holocausta Domino super altare holocautomatis jugiter, mane et vespere, juxta omnia quæ scripta sunt in lege Domini, quam præcepit Israëli.
41 Hemani na Yeduthuni walikuwa nao, pamoja na walio chaguliwa kwa jina, kumpa shukurani Yahweh, kwasababu uaminifu wa agano lake la dumu ata milele
Et post eum Heman, et Idithun, et reliquos electos, unumquemque vocabulo suo ad confitendum Domino, quoniam in æternum misericordia ejus.
42 Hemani na Yeduthuni walikuwa viongozi wa wao waliopiga tarumbeta, upatu, na vyombo vingine kwa muziki wa kumuabudu Mungu. Wana wa Yeduthuni walilinda lango.
Heman quoque et Idithun canentes tuba, et quatientes cymbala et omnia musicorum organa ad canendum Deo: filios autem Idithun fecit esse portarios.
43 Kisha watu wote walirudi nyumbani, na Daudi akarudi kubariki nyumba yake.
Reversusque est omnis populus in domum suam: et David, ut benediceret etiam domui suæ.

< 1 Nyakati 16 >