< 1 Nyakati 16 >
1 Wakaleta ndani Sanduku la Mungu na kuweka katika ya hema ambalo Daudi aliandaa. Kisha wakatoa sadaka ya kuteketeza na sadaka ya ushirika mbele ya Mungu.
So they brought the ark of God, and set it in the midst of the tent, which David had pitched for it: and they offered holocausts, and peace offerings before God.
2 Daudi alipo maliza kutoa dhabiu ya kuteketeza na sadaka za ushirika, aliwabariki watu kwa jina la Yahweh.
And when David had made an end of offering holocausts, and peace offerings, he blessed the people in the name of the Lord.
3 Alisambaza kwa kila Misraeli, mwanaume na mwanamke, kipande cha mkate, na kipande cha nyama, na keki ya mzabibu.
And he divided to all and every one, both men and women, a loaf of bread, and a piece of roasted beef, and flour fried with oil.
4 Daudi aliewapangia baadhi ya Walawi kutumika mbele ya sanduku la Yahweh, na kusheherekea, kushukuru na kumsifu Yahweh, Mungu wa Israeli.
And he appointed Levites to minister before the ark of the Lord, and to remember his works, and to glorify, and praise the Lord God of Israel.
5 Hawa Walawi walikuwa Asafu kiongozi, wa pili kutoka kwake Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaia, Obedi Edomu, na Yeieli. Hawa walikuwa wacheze na vyombo vya uzi na vinubi. Asafu alikuwa apige upatu, kwa kelele.
Asaph the chief, and next after him Zacharias: moreover Jahiel, and Semiramoth, and Jehiel, and Mathathias, and Eliab, and Banaias, and Obededom: and Jehiel over the instruments of psaltery, and harps: and Asaph sounded with cymbals:
6 Benaia na Yahazieli walikuwa wakupiga tarumbeta kila mara, mbele sanduku la agano la Mungu.
But Banaias, and Jaziel the priests, to sound the trumpet continually before the ark of the covenant of the Lord.
7 Kisha katika hiyo siku Daudi akawachagua Asafu na kaka zake kuimba hii nyimbo ya shukurani kwa Yahweh.
In that day David made Asaph the chief to give praise to the Lord with his brethren.
8 Mpeni shukurani Yahweh, liitieni jina lake; fahamisheni mataifa matendo yake.
Praise ye the Lord, and call upon his name: make known his doings among the nations.
9 Mwiimbieni, imbeni sifa kwake; semeni matendo yake ya ajabu.
Sing to him, yea, sing praises to him: and relate all his wondrous works.
10 Jisifuni katika jina lake takatifu; mioyo ya wanao mtafuta Yahweh ishangilie.
Praise ye his holy name: let the heart I of them rejoice, that seek the Lord.
11 Mtafute Yahweh na nguvu zake; tafuteni uwepo wake siku zote.
Seek ye the Lord, and his power: seek ye his face evermore.
12 Kumbukeni matendo aliyo ya fanya kwenu, miujiza yake na amri za kinywa chake,
Remember his wonderful works, which he hath done: his signs, and the judgments of his mouth.
13 enyi uzao wa Israeli mtumishi wake, enyi watu wa Yakobo, wateule wake.
O ye seed of Israel his servants, ye children of Jacob his chosen.
14 Yeye ni Yahweh, Mungu wetu. Amri zake zipo duniani kote.
He is the Lord our God: his judgments are in all the earth.
15 Tunzeni agano lake akilini mwenu milele, neno alilo liamuru kwa vizazi elfu moja.
Remember for ever his covenant: the word, which he commanded to a thousand generations.
16 Anakumbuka agano alilo lifanya na Ibrahimu, na nadhiri yake kwake Isaka.
The covenant which he made with Abraham: and his oath to Isaac.
17 Hili ndilo alilo lithibitisha kwa Yakobo kama amri maalumu, na kwa Israeli kama agano la milele.
And he appointed the same to Jacob for a precept: and to Israel for an everlasting covenant:
18 Alisema, “Nitakupa nchi ya Kanani kama sehemu ya urithi wako.”
Saying: To thee will I give the land of Chanaan: the lot of your inheritance.
19 Nilisema hili mlipo kuwa wachache kwa idadi, wachache sana, mlipo kuwa wageni katika nchi.
When they were but a small number: very few and sojourners in it.
20 Walienda taifa hadi taifa, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
And they passed from nation to nation: and from a kingdom to another people.
21 Hakuwaruhusu yeyote awatese; aliwahadhibu wafalme kwa ajili yao.
He suffered no man to do them wrong: and reproved kings for their sake.
22 Alisema, “Msiwaguse wapakwa mafuta wangu, na msiwadhuru manabii wangu.”
Touch not my anointed: and do no evil to my prophets.
23 Imbeni kwa Yahweh, dunia yote; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
Sing ye to the Lord, all the earth: shew forth from day to day his salvation.
24 Kirini utukufu wake kwa mataifa, matendo yake makuu kwa mataifa yote.
Declare his glory among the Gentiles: his wonders among all people.
25 Kwa kuwa Yahweh ni mkuu na ni wakusifiwa sana, na ni wakuogopewa kuliko miungu yote.
For the Lord is great and exceedingly to be praised: and he is to be feared above all gods.
26 Kwa kuwa miungu ya mataifa ni sanamu, lakini ni Yahweh aliye umba mbingu.
For all the gods of the nations are idols: but the Lord made the heavens.
27 Uzuri wa ajabu na utukufu upo uweponi mwake. Uwezo na furaha upo kwake.
Praise and magnificence are before him: strength and joy in his place.
28 Mpeni sifa Yahweh, enyi koo za watu, mpeni sifa Yahweh utukufu na uwezo;
Bring ye to the Lord, O ye families of the nations: bring ye to the Lord glory and empire.
29 Mpeni Yahweh utukufu upasao jina lake. Leta sadaka na mje kwake. Muinamieni Yahweh katika utakatifu wa uzuri wake.
Give to the Lord glory to his name, bring up sacrifice, and come ye in his sight: and adore the Lord in holy becomingness.
30 Mtetemeke mbele zake, dunia yote. Dunia imeimarishwa; haiwezi kutikisika.
Let all the earth be moved at his presence: for he hath founded the world immoveable.
31 Mbingu nazo ziwe nafuraha, na dunia ifurahi; na wasema kwa mataifa yote, “Yahweh anatawala.”
Let the heavens rejoice, and the earth be glad: and let them say among the nations: The Lord hath reigned.
32 Bahari na ingurume, na inayo ijaza ipige kelele kwa furaha. Mashamba yawe na furaha tele, na vyote vilivyomo ndani yake.
Let the sea roar, and the fulness thereof: let the fields rejoice, and all things that are in them.
33 Na miti iliyopo misituni ipige kelele kwa Yahweh, kwa kuwa anakuja kuhukumu dunia.
Then shall the trees of the wood give praise before the Lord: because he is come to judge the earth.
34 Toeni shukurani kwa Yahweh, kwa kuwa ni mwema, uaminifu wa agano lake la dumu ata milele.
Give ye glory to the Lord, for he is good: for his mercy endureth for ever.
35 Kisha sema, “Tuokoe, Mungu wa wokovu wetu. Tukusanye pamoja na utuokoe kutoka kwa mataifa mengine, ilikwamba tutoe shukurani kwa jina lako takatifu na tufurahi katika sifa zako.”
And say ye: Save us, O God our saviour: and gather us together, and deliver us from the nations, that we may give glory to thy holy name, and may rejoice in singing thy praises.
36 Na Yahweh, Mungu wa Israeli, asifiwe kutoka milele na milele. Watu wote wakasema, “Amina” na wakamsifu Yahweh.
Blessed be the Lord the God of Israel from eternity to eternity: and let all the people say Amen, and a hymn to God.
37 Hivyo Daudi akamwacha Asafu na kaka zake pale mbele ya sanduku la Yahweh, kutumika daima mbele ya sanduku, kama kazi za kila siku zilivyo itaji. Obedi Edomu pamoja na ndugu sitini na nane walijumuishwa.
So he left there before the ark of the covenant of the Lord, Asaph and his brethren to minister in the presence of the ark continually day by day, and in their courses.
38 Obedi Edomu mwana wa Yeduthuni, pamoja na Hosa, walikuwa wawe walinzi wa lango.
And Obededom, with his brethren sixty-eight: and Obededom the son of Idithun, and Hosa he appointed to be porters.
39 Zadoki kuhani na makuhani wenzake walikuwa watumike mbele ya hema la Yahweh katika mahali pa juu huko Gibeoni.
And Sadoc the priest, and his brethren priests, before the tabernacle of the Lord in the high place, which was in Gabaon.
40 Walikuwa watoe sadaka za kuteketeza kwa Yahweh kwenye madhabahu ya sadaka za kuteketeza daima asubui na jioni, kwa mujibu wa yote yalio andikwa katika amri za Yahweh, aliyo wapa Waisraeli kama sheria.
That they should offer holocausts to the Lord upon the altar of holocausts continually, morning and evening, according to all that is written in the law of the Lord, which he commanded Israel.
41 Hemani na Yeduthuni walikuwa nao, pamoja na walio chaguliwa kwa jina, kumpa shukurani Yahweh, kwasababu uaminifu wa agano lake la dumu ata milele
And after him Heman, and Idithun, and the rest that were chosen, every one by his name to give praise to the Lord: because his mercy endureth for ever.
42 Hemani na Yeduthuni walikuwa viongozi wa wao waliopiga tarumbeta, upatu, na vyombo vingine kwa muziki wa kumuabudu Mungu. Wana wa Yeduthuni walilinda lango.
And Heman and Idithun sounded the trumpet, and played on the cymbals, and all kinds of musical instruments to sing praises to God: and the sons of Idithun he made porters.
43 Kisha watu wote walirudi nyumbani, na Daudi akarudi kubariki nyumba yake.
And all the people returned to their houses: and David to bless also his own house.