< 1 Nyakati 16 >
1 Wakaleta ndani Sanduku la Mungu na kuweka katika ya hema ambalo Daudi aliandaa. Kisha wakatoa sadaka ya kuteketeza na sadaka ya ushirika mbele ya Mungu.
And so they took the ark of God, and they set it in the midst of the tabernacle, which David had pitched for it. And they offered holocausts and peace offerings before God.
2 Daudi alipo maliza kutoa dhabiu ya kuteketeza na sadaka za ushirika, aliwabariki watu kwa jina la Yahweh.
And when David had completed offering holocausts and peace offerings, he blessed the people in the name of the Lord.
3 Alisambaza kwa kila Misraeli, mwanaume na mwanamke, kipande cha mkate, na kipande cha nyama, na keki ya mzabibu.
And he divided to every single one, from men even to women, a twist of bread, and a piece of roasted beef, and fine wheat flour fried with oil.
4 Daudi aliewapangia baadhi ya Walawi kutumika mbele ya sanduku la Yahweh, na kusheherekea, kushukuru na kumsifu Yahweh, Mungu wa Israeli.
And he appointed some from the Levites who would minister before the ark of the Lord, and commemorate his works, and glorify and praise the Lord, the God of Israel.
5 Hawa Walawi walikuwa Asafu kiongozi, wa pili kutoka kwake Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaia, Obedi Edomu, na Yeieli. Hawa walikuwa wacheze na vyombo vya uzi na vinubi. Asafu alikuwa apige upatu, kwa kelele.
Asaph was the leader, and second to him was Zechariah. In addition, there were Jeiel, and Shemiramoth, and Jehiel, and Mattithiah, and Eliab, and Benaiah, and Obededom. And Jeiel was over the instruments of the psaltery and the harps. But Asaph sounded out with the cymbals.
6 Benaia na Yahazieli walikuwa wakupiga tarumbeta kila mara, mbele sanduku la agano la Mungu.
Truly, the priests, Benaiah and Jahaziel, were to sound the trumpet continually before the ark of the covenant of the Lord.
7 Kisha katika hiyo siku Daudi akawachagua Asafu na kaka zake kuimba hii nyimbo ya shukurani kwa Yahweh.
In that day, David made Asaph the leader, in order to confess to the Lord with his brothers:
8 Mpeni shukurani Yahweh, liitieni jina lake; fahamisheni mataifa matendo yake.
“Confess to the Lord, and invoke his name. Make known his endeavors among the peoples.
9 Mwiimbieni, imbeni sifa kwake; semeni matendo yake ya ajabu.
Sing to him, and sing psalms to him, and describe all his miracles.
10 Jisifuni katika jina lake takatifu; mioyo ya wanao mtafuta Yahweh ishangilie.
Praise his holy name! Let the heart of those who seek the Lord rejoice!
11 Mtafute Yahweh na nguvu zake; tafuteni uwepo wake siku zote.
Seek the Lord and his virtue. Seek his face always.
12 Kumbukeni matendo aliyo ya fanya kwenu, miujiza yake na amri za kinywa chake,
Remember his miracles, which he has accomplished, his signs, and the judgments of his mouth.
13 enyi uzao wa Israeli mtumishi wake, enyi watu wa Yakobo, wateule wake.
O offspring of Israel, his servants! O sons of Jacob, his elect!
14 Yeye ni Yahweh, Mungu wetu. Amri zake zipo duniani kote.
He is the Lord our God. His judgments are throughout all the earth.
15 Tunzeni agano lake akilini mwenu milele, neno alilo liamuru kwa vizazi elfu moja.
Remember forever his covenant, the word that he instructed unto a thousand generations,
16 Anakumbuka agano alilo lifanya na Ibrahimu, na nadhiri yake kwake Isaka.
the covenant that he formed with Abraham, and his oath with Isaac.
17 Hili ndilo alilo lithibitisha kwa Yakobo kama amri maalumu, na kwa Israeli kama agano la milele.
And he appointed the same to Jacob as a precept, and to Israel as an everlasting pact,
18 Alisema, “Nitakupa nchi ya Kanani kama sehemu ya urithi wako.”
saying: ‘To you, I will give the land of Canaan, the lot of your inheritance.’
19 Nilisema hili mlipo kuwa wachache kwa idadi, wachache sana, mlipo kuwa wageni katika nchi.
At that time, they were small in number, they were few and were settlers there.
20 Walienda taifa hadi taifa, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
And they passed through, from nation to nation, and from one kingdom to another people.
21 Hakuwaruhusu yeyote awatese; aliwahadhibu wafalme kwa ajili yao.
He did not permit anyone to falsely accuse them. Instead, he reproved kings on their behalf:
22 Alisema, “Msiwaguse wapakwa mafuta wangu, na msiwadhuru manabii wangu.”
‘Do not touch my Christ. And do not malign my prophets.’
23 Imbeni kwa Yahweh, dunia yote; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
Sing to the Lord, all the earth! Announce his salvation, from day to day.
24 Kirini utukufu wake kwa mataifa, matendo yake makuu kwa mataifa yote.
Describe his glory among the Gentiles, his miracles among all the peoples.
25 Kwa kuwa Yahweh ni mkuu na ni wakusifiwa sana, na ni wakuogopewa kuliko miungu yote.
For the Lord is great and exceedingly praiseworthy. And he is terrible, above all gods.
26 Kwa kuwa miungu ya mataifa ni sanamu, lakini ni Yahweh aliye umba mbingu.
For all the gods of the peoples are idols. But the Lord made the heavens.
27 Uzuri wa ajabu na utukufu upo uweponi mwake. Uwezo na furaha upo kwake.
Confession and magnificence are before him. Strength and gladness are in his place.
28 Mpeni sifa Yahweh, enyi koo za watu, mpeni sifa Yahweh utukufu na uwezo;
Bring to the Lord, O families of the peoples, bring to the Lord glory and dominion.
29 Mpeni Yahweh utukufu upasao jina lake. Leta sadaka na mje kwake. Muinamieni Yahweh katika utakatifu wa uzuri wake.
Give glory to the Lord, to his name. Lift up sacrifice, and approach before his sight. And adore the Lord in holy attire.
30 Mtetemeke mbele zake, dunia yote. Dunia imeimarishwa; haiwezi kutikisika.
Let all the earth be moved before his face. For he founded the globe immoveable.
31 Mbingu nazo ziwe nafuraha, na dunia ifurahi; na wasema kwa mataifa yote, “Yahweh anatawala.”
Let the heavens rejoice, and let the earth exult. And let them say among the nations, ‘The Lord has reigned.’
32 Bahari na ingurume, na inayo ijaza ipige kelele kwa furaha. Mashamba yawe na furaha tele, na vyote vilivyomo ndani yake.
Let the sea roar, with all its plenitude. Let the fields exult, with all that is in them.
33 Na miti iliyopo misituni ipige kelele kwa Yahweh, kwa kuwa anakuja kuhukumu dunia.
Then the trees of the forest will give praise before the Lord. For he comes to judge the earth.
34 Toeni shukurani kwa Yahweh, kwa kuwa ni mwema, uaminifu wa agano lake la dumu ata milele.
Confess to the Lord, for he is good. For his mercy is eternal.
35 Kisha sema, “Tuokoe, Mungu wa wokovu wetu. Tukusanye pamoja na utuokoe kutoka kwa mataifa mengine, ilikwamba tutoe shukurani kwa jina lako takatifu na tufurahi katika sifa zako.”
And say: ‘Save us, O God our savior! And gather us together, and rescue us from the nations, so that we may confess to your holy name, and may exult in your songs.
36 Na Yahweh, Mungu wa Israeli, asifiwe kutoka milele na milele. Watu wote wakasema, “Amina” na wakamsifu Yahweh.
Blessed be the Lord, the God of Israel, from eternity to eternity.’ And let all the people say, ‘Amen,’ and let them sing a hymn to the Lord.”
37 Hivyo Daudi akamwacha Asafu na kaka zake pale mbele ya sanduku la Yahweh, kutumika daima mbele ya sanduku, kama kazi za kila siku zilivyo itaji. Obedi Edomu pamoja na ndugu sitini na nane walijumuishwa.
And so, there before the ark of the covenant of the Lord, he left Asaph and his brothers, so that they might minister in the sight of the ark continually, throughout each day, and in their turns.
38 Obedi Edomu mwana wa Yeduthuni, pamoja na Hosa, walikuwa wawe walinzi wa lango.
Now Obededom and his brothers were sixty-eight. And he appointed Obededom, the son of Jeduthun, and Hosah to be porters.
39 Zadoki kuhani na makuhani wenzake walikuwa watumike mbele ya hema la Yahweh katika mahali pa juu huko Gibeoni.
But Zadok the priest, and his brothers the priests, were before the tabernacle of the Lord in the high place, which was in Gibeon,
40 Walikuwa watoe sadaka za kuteketeza kwa Yahweh kwenye madhabahu ya sadaka za kuteketeza daima asubui na jioni, kwa mujibu wa yote yalio andikwa katika amri za Yahweh, aliyo wapa Waisraeli kama sheria.
so that they could offer holocausts to the Lord upon the altar of holocausts continually, morning and evening, according to all that was written in the law of the Lord, which he instructed to Israel.
41 Hemani na Yeduthuni walikuwa nao, pamoja na walio chaguliwa kwa jina, kumpa shukurani Yahweh, kwasababu uaminifu wa agano lake la dumu ata milele
And after him, Heman, and Jeduthun, and the remainder of the elect, each one by his name, were appointed to confess to the Lord: “For his mercy endures forever.”
42 Hemani na Yeduthuni walikuwa viongozi wa wao waliopiga tarumbeta, upatu, na vyombo vingine kwa muziki wa kumuabudu Mungu. Wana wa Yeduthuni walilinda lango.
Also Heman and Jeduthun sounded the trumpet, and they played upon the cymbals, and upon every kind of musical instrument, in order to sing praises to God. But the sons of Jeduthun he made to be porters.
43 Kisha watu wote walirudi nyumbani, na Daudi akarudi kubariki nyumba yake.
And all the people returned to their houses, and David also, so that he might bless his own house too.