< 1 Nyakati 15 >

1 Daudi akajingea nyumba zake katika mji wa Daudi. Akaanda sehemu kwa ajili ya sanduku la Mungu na hema lake.
And he makes houses for himself in the City of David, and prepares a place for the Ark of God, and stretches out a tent for it.
2 Kisha Daudi akasema, “Walawi pekee ndio watabeba sanduku la Mungu, kwa kuwa walichaguliwa na Yahweh kubeba sanduku la Yahweh, na kumtumikia milele.”
Then David said, “None [are] to carry the Ark of God, except the Levites, for YHWH has fixed on them to carry the Ark of God and to serve Him for all time.”
3 Kisha Daudi akakusanya Israeli yote Yerusalemu, kuleta sanduku la Yahweh sehemu aliyo iandaa.
And David assembles all Israel to Jerusalem, to bring up the Ark of YHWH to its place that he had prepared for it.
4 Daudi akakusanya uzao wa Aruni na Walawi pamoja.
And David gathers the sons of Aaron and the Levites—
5 Kutoka uzao wa Kohathi, palikuwa na Urieli kiongozi na ndugu zake, wanaume 120.
of sons of Kohath: Uriel the chief and one hundred and twenty of his brothers;
6 Kutoka uzao wa Merari, palikuwa na Asaia kiongozi na ndugu zake, wanaume 220.
of sons of Merari: Asaiah the chief and two hundred and twenty of his brothers;
7 Kutoka uzao wa Gerishomu, palikuwa na Yoeli kiongozi na ndugu zake, wanaume 130.
of sons of Gershom: Joel the chief and one hundred and thirty of his brothers;
8 Kutoka uzao wa Elizafani, palikuwa na Shemaia kiongozi na ndugu zake, wanaume 200.
of sons of Elizaphan: Shemaiah the chief and two hundred of his brothers;
9 Kutoka uzao wa Hebroni, palikuwa na Elieli kiongozi na ndugu zake, wanaume themanini.
of sons of Hebron: Eliel the chief and eighty of his brothers;
10 Kutoka uzao wa Uzieli, palikuwa na Aminadabu kiongozi na ndugu zake, wanaume 112.
of sons of Uzziel: Amminadab the chief and one hundred and twelve of his brothers.
11 Daudi akaagiza Zadoki kuitwa na Abiathari kuhuani, na Walawi Urieli, Asaia, Yoeli, Shemaia, Elieli, na Aminadabu.
And David calls to Zadok and to Abiathar the priests, and to the Levites, to Uriel, Asaiah, and Joel, Shemaiah, and Eliel, and Amminadab,
12 Akasema, “Nyinyi ni viongozi wa familia za Kilawi. Jiwekeni wakfu, nyie na ndugu zenu, ilikwamba mlete sanduku la Yahweh, Mungu wa Israeli, kwenye sehemu niliyo iandaa.
and says to them, “You [are] heads of the fathers of the Levites; sanctify yourselves, you and your brothers, and you have brought up the Ark of YHWH, God of Israel, to [the place] I have prepared for it;
13 Mara ya kwanza hamkubeba. Ndio maana Yahweh Mungu wetu akawa na hasira kwetu, kwa kuwa hatuku mtafuta wala kutii amri yake.”
because you [did] not [do it] at the first, our God YHWH made a breach on us, because we did not seek Him according to the ordinance.”
14 Hivyo makuhani na Walawi waka jiweka wakfu iliwaweze kuleta sanduku la Yahweh, Mungu wa Israeli.
And the priests and the Levites sanctify themselves to bring up the Ark of YHWH, God of Israel;
15 Walawi wakabeba sanduku la Mungu katika mabega yao na nguzo, kama Musa alivyo amuru-kwa kufuata sheria zilizo tolewa na Yahweh.
and sons of the Levites carry the Ark of God, as Moses commanded, according to the word of YHWH, above them with poles on their shoulder.
16 Daudi akazungumza na viongozi wa Walawi kuwapangia ndugu zao kuwa wana muziki wenye vyombo vya muziki, vyombo vya uzi, vinubi na upatu, kwa kupiga kwa sauti na furaha wakipaza sauti zao.
And David says to the heads of the Levites to appoint their brothers the singers, with instruments of song, psalteries, and harps, and cymbals, sounding, to lift up with the voice for joy.
17 Hivyo Walawi wakamchagua Hemani mwana wa Yoeli na mmoja wa kaka zake, Asafu mwana wa Berekia. Pia walimchagua ndugu wa uzao wa Merari na Ethani mwana wa Kushaia.
And the Levites appoint Heman son of Joel, and of his brothers, Asaph son of Berechiah, and of the sons of Merari their brothers, Ethan son of Kushaiah;
18 Pamoja nao walikuwa ndugu wa daraja la pili: Zekarai, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaia, Maasaeia, Matithia, Elifelehu, Mikineaia, Obedi Edomu, na Yeieli, mlinzi wa lango.
and with them their brothers, the seconds [in rank]: Zechariah, Ben, and Jaaziel, and Shemiramoth, and Jehiel, and Unni, Eliab, and Benaiah, and Maaseiah, and Mattithiah, and Elipheleh, and Mikneiah; and Obed-Edom and Jeiel the gatekeepers;
19 Wanamuziki Hemani, Asafu, na Ethani walichaguliwa kupiga upatu wa shaba.
and the singers, Heman, Asaph, and Ethan, [are] to sound with cymbals of bronze;
20 Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni Eliabu, Maaseia, na Benaia walicheza vyombo vya uzi.
and Zechariah, and Aziel, and Shemiramoth, and Jeheil, and Unni, and Eliab, and Maaseiah, and Benaiah, with psalteries over the girls’ [voices],
21 Matithia, Elifelehu, Mikineia, Obedi Edomu, Yeieli, na Azazia waliongoza njia na vinubi.
and Mattithiah, and Elipheleh, and Mikneiah, and Obed-Edom, and Jeiel, and Azaziah, to oversee with harps on the eighth.
22 Kenania, kiongozi wa Walawi, aliongoza uimbaji sababu alikuwa mwalimu wa muziki.
And Chenaniah, head of the Levites, [is] over the burden; he instructs about the burden, for he [is] intelligent.
23 Berekia na Elikana walikuwa walinzi wa sanduku.
And Berechiah and Elkanah [are] gatekeepers for the Ark.
24 Shebania, Yoshafati, Nethanieli, Amasai, Zekaria, Benaia, na Eliezeri, makuhani, walikuwa wa kupuliza matarumbeta mbele ya sanduku la Mungu. Obedi Edomu na Yehia walikuwa walinzi wa sanduku.
And Shebaniah, and Joshaphat, and Nethaneel, and Amasai, and Zechariah, and Benaiah, and Eliezer the priests, are blowing with trumpets before the Ark of God; and Obed-Edom and Jehiah [are] gatekeepers for the Ark.
25 Hivyo Daudi, wazee wa Israeli, na wakuu wa maelfu wakaenda kuchukua sanduku la agano la Yahweh kutoka nyumba ya Obedi Edomu kwa shangwe.
And it is David, and [the] elderly of Israel, and the heads of the thousands, who are going to bring up the Ark of the Covenant of YHWH from the house of Obed-Edom with joy;
26 Wakati Mungu alipo wasaidia Walawi kubeba sanduku la agano la Yahweh, walitoa ng'ombe saba na mbuzi
and it comes to pass, in God’s helping the Levites carrying the Ark of the Covenant of YHWH, that they sacrifice seven bullocks and seven rams.
27 Daudi alivishwa joho safi la maridadi, pamoja na Walawi walio beba sanduku, waimbaji, na Kenania, kiongozi wa nyimbo na waimbaji. Daudi alivaa juu ya joho lake naivera.
And David is wrapped in an upper robe of fine linen, and all the Levites who are carrying the Ark, and the singers, and Chenaniah head of the burden of the singers; and an Ephod of linen [is] on David.
28 Hivyo Israeli yote wakaleta sanduku la agano la Yahweh na kelele za shangwe, na sauti za tarumbeta, ngoma za saani, na vyombo vya uzi na vinubi.
And all of Israel is bringing up the Ark of the Covenant of YHWH with shouting, and with the sound of a horn, and with trumpets, and with cymbals, sounding with psalteries and harps,
29 Lakini sanduku la Yahweh lilivyokuja kwa mji wa Daudi, Mikali binti wa Sauli, alitazama nje ya dirisha, Akamuona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea. Kisha akamdharau moyoni mwake.
and it comes to pass, the Ark of the Covenant of YHWH is entering into the City of David, and Michal daughter of Saul is looking through the window, and sees King David dancing and playing, and despises him in her heart.

< 1 Nyakati 15 >