< 1 Nyakati 15 >
1 Daudi akajingea nyumba zake katika mji wa Daudi. Akaanda sehemu kwa ajili ya sanduku la Mungu na hema lake.
Also, he made houses for himself in the City of David. And built a place for the ark of God, and he set up a tent for it.
2 Kisha Daudi akasema, “Walawi pekee ndio watabeba sanduku la Mungu, kwa kuwa walichaguliwa na Yahweh kubeba sanduku la Yahweh, na kumtumikia milele.”
Then David said: “It is illicit for anyone to carry the ark of God except the Levites, whom the Lord chose to carry it and to minister to himself, even unto eternity.”
3 Kisha Daudi akakusanya Israeli yote Yerusalemu, kuleta sanduku la Yahweh sehemu aliyo iandaa.
And he gathered all of Israel in Jerusalem, so that the ark of God might be brought into its place, which he had prepared for it.
4 Daudi akakusanya uzao wa Aruni na Walawi pamoja.
Certainly, there were both the sons of Aaron and the Levites:
5 Kutoka uzao wa Kohathi, palikuwa na Urieli kiongozi na ndugu zake, wanaume 120.
From the sons of Kohath, Uriel was the leader, and his brothers were one hundred twenty.
6 Kutoka uzao wa Merari, palikuwa na Asaia kiongozi na ndugu zake, wanaume 220.
From the sons of Merari: Asaiah was the leader, and his brothers were two hundred twenty.
7 Kutoka uzao wa Gerishomu, palikuwa na Yoeli kiongozi na ndugu zake, wanaume 130.
From the sons of Gershom: Joel was the leader, and his brothers were one hundred thirty.
8 Kutoka uzao wa Elizafani, palikuwa na Shemaia kiongozi na ndugu zake, wanaume 200.
From the sons of Elizaphan: Shemaiah was the leader, and his brothers were two hundred.
9 Kutoka uzao wa Hebroni, palikuwa na Elieli kiongozi na ndugu zake, wanaume themanini.
From the sons of Hebron: Eliel was the leader, and his brothers were eighty.
10 Kutoka uzao wa Uzieli, palikuwa na Aminadabu kiongozi na ndugu zake, wanaume 112.
From the sons of Uzziel: Amminadab was the leader, and his brothers were one hundred twelve.
11 Daudi akaagiza Zadoki kuitwa na Abiathari kuhuani, na Walawi Urieli, Asaia, Yoeli, Shemaia, Elieli, na Aminadabu.
And David summoned the priests, Zadok and Abiathar, and the Levites: Uriel, Asaiah, Joel, Shemaiah, Eliel, and Amminadab.
12 Akasema, “Nyinyi ni viongozi wa familia za Kilawi. Jiwekeni wakfu, nyie na ndugu zenu, ilikwamba mlete sanduku la Yahweh, Mungu wa Israeli, kwenye sehemu niliyo iandaa.
And he said to them: “You who are the leaders of the Levitical families, be sanctified with your brothers, and bring the ark of the Lord God of Israel to the place that has been prepared for it.
13 Mara ya kwanza hamkubeba. Ndio maana Yahweh Mungu wetu akawa na hasira kwetu, kwa kuwa hatuku mtafuta wala kutii amri yake.”
Otherwise, as it was before, when the Lord struck us because you were not present, so also it might be now, if we do what is illicit.”
14 Hivyo makuhani na Walawi waka jiweka wakfu iliwaweze kuleta sanduku la Yahweh, Mungu wa Israeli.
Therefore, the priests and the Levites were sanctified, so that they might carry the ark of the Lord God of Israel.
15 Walawi wakabeba sanduku la Mungu katika mabega yao na nguzo, kama Musa alivyo amuru-kwa kufuata sheria zilizo tolewa na Yahweh.
And the sons of Levi took the ark of God, just as Moses had instructed, in accord with the word of the Lord, upon their shoulders by the bars.
16 Daudi akazungumza na viongozi wa Walawi kuwapangia ndugu zao kuwa wana muziki wenye vyombo vya muziki, vyombo vya uzi, vinubi na upatu, kwa kupiga kwa sauti na furaha wakipaza sauti zao.
And David spoke to the leaders of the Levites, so that they might appoint, from their brothers, singers with musical instruments, specifically, psalteries, and harps, and cymbals, so that a joyful noise might resound on high.
17 Hivyo Walawi wakamchagua Hemani mwana wa Yoeli na mmoja wa kaka zake, Asafu mwana wa Berekia. Pia walimchagua ndugu wa uzao wa Merari na Ethani mwana wa Kushaia.
And they appointed from the Levites: Heman, the son of Joel; and from his brothers, Asaph, the son of Berechiah; and truly, from their brothers, the sons of Merari: Ethan, the son of Kushaiah.
18 Pamoja nao walikuwa ndugu wa daraja la pili: Zekarai, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaia, Maasaeia, Matithia, Elifelehu, Mikineaia, Obedi Edomu, na Yeieli, mlinzi wa lango.
And with them were their brothers in the second rank: Zechariah, and Ben, and Jaaziel, and Shemiramoth, and Jahiel, and Unni, and Eliab, and Benaiah, and Maaseiah, and Mattithiah, and Eliphelehu, and Mikneiah, and Obededom, and Jeiel, who were gatekeepers.
19 Wanamuziki Hemani, Asafu, na Ethani walichaguliwa kupiga upatu wa shaba.
Now the singers, Heman, Asaph, and Ethan, were sounding out with cymbals of brass.
20 Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni Eliabu, Maaseia, na Benaia walicheza vyombo vya uzi.
And Zechariah, and Aziel, and Shemiramoth, and Jehiel, and Unni, and Eliab, and Maaseiah, and Benaiah were singing mysteries with the psalteries.
21 Matithia, Elifelehu, Mikineia, Obedi Edomu, Yeieli, na Azazia waliongoza njia na vinubi.
Then Mattithiah, and Eliphelehu, and Mikneiah and Obededom, and Jeiel and Azaziah were singing a song of victory with the harps, for the octave.
22 Kenania, kiongozi wa Walawi, aliongoza uimbaji sababu alikuwa mwalimu wa muziki.
Now Chenaniah, the leader of the Levites, was foremost over the prophecies, in order to mark out in advance the melodies. For indeed, he was very skillful.
23 Berekia na Elikana walikuwa walinzi wa sanduku.
And Berechiah and Elkanah were porters of the ark.
24 Shebania, Yoshafati, Nethanieli, Amasai, Zekaria, Benaia, na Eliezeri, makuhani, walikuwa wa kupuliza matarumbeta mbele ya sanduku la Mungu. Obedi Edomu na Yehia walikuwa walinzi wa sanduku.
And the priests, Shebaniah, and Joshaphat, and Nethanel, and Amasai, and Zechariah, and Benaiah, and Eliezer, were sounding the trumpets before the ark of God. And Obededom and Jehiah were porters of the ark.
25 Hivyo Daudi, wazee wa Israeli, na wakuu wa maelfu wakaenda kuchukua sanduku la agano la Yahweh kutoka nyumba ya Obedi Edomu kwa shangwe.
Therefore, David, and all those greater by birth of Israel, and the tribunes, went to carry the ark of the covenant of the Lord from the house of Obededom with rejoicing.
26 Wakati Mungu alipo wasaidia Walawi kubeba sanduku la agano la Yahweh, walitoa ng'ombe saba na mbuzi
And when God had assisted the Levites, who were carrying the ark of the covenant of the Lord, they immolated seven bulls and seven rams.
27 Daudi alivishwa joho safi la maridadi, pamoja na Walawi walio beba sanduku, waimbaji, na Kenania, kiongozi wa nyimbo na waimbaji. Daudi alivaa juu ya joho lake naivera.
Now David was clothed with a robe of fine linen, as were all the Levites who were carrying the ark, and the singers, and Chenaniah, the leader of the prophecy among the singers. But David was also clothed with a linen ephod.
28 Hivyo Israeli yote wakaleta sanduku la agano la Yahweh na kelele za shangwe, na sauti za tarumbeta, ngoma za saani, na vyombo vya uzi na vinubi.
And all of Israel were leading back the ark of the covenant of the Lord with jubilation, sounding out with the noise of horns, and trumpets, and cymbals, and psalteries, and harps.
29 Lakini sanduku la Yahweh lilivyokuja kwa mji wa Daudi, Mikali binti wa Sauli, alitazama nje ya dirisha, Akamuona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea. Kisha akamdharau moyoni mwake.
And when the ark of the covenant of the Lord had arrived in the City of David, Michal, the daughter of Saul, gazing through a window, saw king David dancing and playing, and she despised him in her heart.