< 1 Nyakati 14 >

1 Kisha Hiramu mfalme wa Tire alituma wajumbe kwa Daudi, na miti ya mierezi, maseremala, na wajenzi. Walijenga nyumba kwa ajili yake.
וישלח חירם מלך צר מלאכים אל דויד ועצי ארזים וחרשי קיר וחרשי עצים לבנות לו בית׃
2 Daudi alijua kuwa Yahweh alimfanya kuwa mfalme juu ya Waisraeli, na hivyo ufalme wake ulitukuzwa juu sana kwa ajili ya watu wa Israeli
וידע דויד כי הכינו יהוה למלך על ישראל כי נשאת למעלה מלכותו בעבור עמו ישראל׃
3 Ndani ya Yerusalemu, Daudi aliongeza wake, na akawa baba wa wana wengi na mabinti.
ויקח דויד עוד נשים בירושלם ויולד דויד עוד בנים ובנות׃
4 Haya yalikuwa majina ya watoto waliozaliwa nae huko yerusalemu: Shammua, Shobabu, nathani, Solimoni,
ואלה שמות הילודים אשר היו לו בירושלם שמוע ושובב נתן ושלמה׃
5 Ibhari, Elishama, Elpeleti,
ויבחר ואלישוע ואלפלט׃
6 Noga, Nefegi, Jafia,
ונגה ונפג ויפיע׃
7 Elishama, Beliada, na Elifeleti.
ואלישמע ובעלידע ואליפלט׃
8 Sasa tangu Wafilisti waliposikia Daudi amepakwa mafuta kama mfalme juu ya Waisraeli, wote walitoka nje kwenda kumtafuta. Lakini Daudi alisikia kuhusu hilo nae akaenda nje kinyume nao.
וישמעו פלשתים כי נמשח דויד למלך על כל ישראל ויעלו כל פלשתים לבקש את דויד וישמע דויד ויצא לפניהם׃
9 Sasa wafilisti walikuja na kufanya shambulio katika bonde la Refaimu.
ופלשתים באו ויפשטו בעמק רפאים׃
10 Kisha Daudi akaomba msaada kwa Mungu. Akasema, “Je niwashambulie Wafilisti? Utanipa ushindi juu yao?” Yahweh akamwambia, “Shambulia, kwa uhakika nitawakabidhi kwako.”
וישאל דויד באלהים לאמר האעלה על פלשתיים ונתתם בידי ויאמר לו יהוה עלה ונתתים בידך׃
11 Kwa hivyo wakaja Baali Perazimu na akawashinda. Akasema, “Yahweh kapasua maadui zangu kwa mkono wangu kama vile mpasuko wa mafuriko ya maji.” Hivyo jina la sehemu ile likawa Baali Perazimu.
ויעלו בבעל פרצים ויכם שם דויד ויאמר דויד פרץ האלהים את אויבי בידי כפרץ מים על כן קראו שם המקום ההוא בעל פרצים׃
12 Wafilisti walitelekeza miungu yao pale, na Daudi akatoa amri wateketezwe kwa moto.
ויעזבו שם את אלהיהם ויאמר דויד וישרפו באש׃
13 Kisha Wafilisti wakavamia kwa mara nyingine tena.
ויסיפו עוד פלשתים ויפשטו בעמק׃
14 Hivyo Daudi akaomba msaada kwa Mungu tena. Mungu akamwambia, “Usiwashambulie kwa mbele, lakini wazunguke kwa nyuma yao na uwajie kupitia misitu ya balisamu.
וישאל עוד דויד באלהים ויאמר לו האלהים לא תעלה אחריהם הסב מעליהם ובאת להם ממול הבכאים׃
15 Utakaposikia sauti ya wanajeshi wanatembea kwenye upepo uvumao kutoka juu ya miti ya balisamu, kisha shambulia kwa nguvu. Fanya hivyo kwasababu Mungu atakutangulia kwenda kuwashambulia majeshi ya wafilisti.”
ויהי כשמעך את קול הצעדה בראשי הבכאים אז תצא במלחמה כי יצא האלהים לפניך להכות את מחנה פלשתים׃
16 Hivyo Daudi alifanya kama Mungu alivyo muamuru. Aliwashinda jeshi la Wafilisti kutoka Gibeoni mpaka Gezeri.
ויעש דויד כאשר צוהו האלהים ויכו את מחנה פלשתים מגבעון ועד גזרה׃
17 Kisha umaarufu wa Daudi ukaenda katika nchi zote, na Yahweh akasababisha mataifa yote kumuhofia.
ויצא שם דויד בכל הארצות ויהוה נתן את פחדו על כל הגוים׃

< 1 Nyakati 14 >