< 1 Nyakati 14 >

1 Kisha Hiramu mfalme wa Tire alituma wajumbe kwa Daudi, na miti ya mierezi, maseremala, na wajenzi. Walijenga nyumba kwa ajili yake.
Hiram, roi de Tyr, envoya des messagers à David avec des cèdres, des maçons et des charpentiers, pour lui construire une maison.
2 Daudi alijua kuwa Yahweh alimfanya kuwa mfalme juu ya Waisraeli, na hivyo ufalme wake ulitukuzwa juu sana kwa ajili ya watu wa Israeli
David s'aperçut que Yahvé l'avait établi roi sur Israël, car son royaume était très élevé, à cause de son peuple Israël.
3 Ndani ya Yerusalemu, Daudi aliongeza wake, na akawa baba wa wana wengi na mabinti.
David prit d'autres femmes à Jérusalem, et il engendra d'autres fils et d'autres filles.
4 Haya yalikuwa majina ya watoto waliozaliwa nae huko yerusalemu: Shammua, Shobabu, nathani, Solimoni,
Voici les noms des enfants qu'il eut à Jérusalem: Shammua, Shobab, Nathan, Salomon,
5 Ibhari, Elishama, Elpeleti,
Ibhar, Elishua, Elpelet,
6 Noga, Nefegi, Jafia,
Nogah, Nepheg, Japhia,
7 Elishama, Beliada, na Elifeleti.
Elishama, Beeliada et Eliphelet.
8 Sasa tangu Wafilisti waliposikia Daudi amepakwa mafuta kama mfalme juu ya Waisraeli, wote walitoka nje kwenda kumtafuta. Lakini Daudi alisikia kuhusu hilo nae akaenda nje kinyume nao.
Lorsque les Philistins apprirent que David avait été oint roi sur tout Israël, tous les Philistins montèrent à la recherche de David; David l'apprit et sortit à leur rencontre.
9 Sasa wafilisti walikuja na kufanya shambulio katika bonde la Refaimu.
Les Philistins étaient venus et avaient fait un raid dans la vallée des Rephaïm.
10 Kisha Daudi akaomba msaada kwa Mungu. Akasema, “Je niwashambulie Wafilisti? Utanipa ushindi juu yao?” Yahweh akamwambia, “Shambulia, kwa uhakika nitawakabidhi kwako.”
David consulta Dieu, en disant: Monterai-je contre les Philistins? Les livreras-tu entre mes mains? » Yahvé lui dit: « Monte, car je vais les livrer entre tes mains. »
11 Kwa hivyo wakaja Baali Perazimu na akawashinda. Akasema, “Yahweh kapasua maadui zangu kwa mkono wangu kama vile mpasuko wa mafuriko ya maji.” Hivyo jina la sehemu ile likawa Baali Perazimu.
Ils montèrent donc à Baal Perazim, et David les battit là. David dit: Dieu a brisé mes ennemis par ma main, comme des eaux qui jaillissent. C'est pourquoi on donna à ce lieu le nom de Baal Perazim.
12 Wafilisti walitelekeza miungu yao pale, na Daudi akatoa amri wateketezwe kwa moto.
Ils y laissèrent leurs dieux; David donna un ordre, et ils furent brûlés par le feu.
13 Kisha Wafilisti wakavamia kwa mara nyingine tena.
Les Philistins firent un autre raid dans la vallée.
14 Hivyo Daudi akaomba msaada kwa Mungu tena. Mungu akamwambia, “Usiwashambulie kwa mbele, lakini wazunguke kwa nyuma yao na uwajie kupitia misitu ya balisamu.
David consulta de nouveau Dieu, et Dieu lui dit: « Tu ne monteras pas après eux. Détourne-toi d'eux, et tombe sur eux en face des mûriers.
15 Utakaposikia sauti ya wanajeshi wanatembea kwenye upepo uvumao kutoka juu ya miti ya balisamu, kisha shambulia kwa nguvu. Fanya hivyo kwasababu Mungu atakutangulia kwenda kuwashambulia majeshi ya wafilisti.”
Quand tu entendras le bruit de la marche dans les cimes des mûriers, alors tu sortiras pour combattre, car Dieu est sorti devant toi pour frapper l'armée des Philistins. »
16 Hivyo Daudi alifanya kama Mungu alivyo muamuru. Aliwashinda jeshi la Wafilisti kutoka Gibeoni mpaka Gezeri.
David fit ce que Dieu lui avait ordonné, et ils attaquèrent l'armée des Philistins depuis Gabaon jusqu'à Guézer.
17 Kisha umaarufu wa Daudi ukaenda katika nchi zote, na Yahweh akasababisha mataifa yote kumuhofia.
La renommée de David se répandit dans tous les pays, et Yahvé fit craindre sa présence à toutes les nations.

< 1 Nyakati 14 >