< 1 Nyakati 13 >

1 Daudi akashuriana na wakuu wa jeshi la maelfu na mamia, na kila kiongozi.
And David consulted with the captains of thousands and of hundreds, even with every leader.
2 Daudi akasema kwa kusanyiko la Isaraeli, “Kama itakuwa vyema, na kama hii inatoka kwa Yahweh Mungu wetu, na tutume wajumbe kila sehemu kwa ndugu zetu walio baki maeneo yote ya Israeli, na kwa makuhani na Walawi walio kwenye miji yao. Waambiwe wajiunge nasi.
And David said to all the assembly of Israel, If it seems good to you, and if it be of Jehovah our God, let us send abroad everywhere to our brothers who are left in all the land of Israel, with whom the priests and Levites are in their cities that have suburbs, that they may gather themselves to us.
3 Na tulete sanduku la Mungu wetu, kwa kuwa hatukutafuta mapenzi yake katika siku za Sauli.”
And let us bring again the ark of our God to us, for we did not inquire from it in the days of Saul.
4 Kusanyiko lote liliafiki kufanya haya yote, kwa kuwa yalionekana sawa machoni pa watu wote.
And all the assembly said that they would do so, for the thing was right in the eyes of all the people.
5 Kwaiyo Daudi akakusanya Israeli yote, kutoka mto Shihori ulio Misri hadi Lebo Hamathi, kuleta sandaku la Mungu kutoka Kiriathi Yearimu.
So David assembled all Israel together, from the Shihor the brook of Egypt even to the entrance of Hamath, to bring the ark of God from Kiriath-jearim.
6 Daudi na Israeli yote walienda mpaka Baala, ambayo ni, Kiriathi Yearimu, ambao ni ya Yuda, kuleta sanduku la Mungu, ambalo linaitwa kwa jina la Yahweh, Yahweh, ambaye ameketi juu ya makerubi.
And David went up, and all Israel, to Baalah, that is to Kiriath-jearim, which belonged to Judah, to bring up from there the ark of God, Jehovah who sits above the cherubim that is called by the Name.
7 Kwaiyo wakaketisha sanduku la Mungu juu ya chombo kipya cha matairi. Wakaleta nje ya nyumba ya Abinadabu. Uza na Ahio walikuwa wakilinda hicho chombo.
And they carried the ark of God upon a new cart, and brought it out of the house of Abinadab. And Uzza and Ahio drove the cart.
8 Daudi na Israeli yote walikuwa wakishangilia mbele za Mungu kwa nguvu zao zote. Walikuwa wakiimba na vyombo vya uzi, vinubi, upatu, na tarumbeta.
And David and all Israel played before God with all their might, even with songs, and with harps, and with psalteries, and with timbrels, and with cymbals, and with trumpets.
9 Walipo kuja eneo la kupeta mazao huko Kidoni, Uza alinyoosha mkono wake kuzuia sandaku, sababu ng'ombe aliyekuwa amebeba sanduku aliyumba.
And when they came to the threshing-floor of Chidon, Uzza put forth his hand to hold the ark, for the oxen stumbled.
10 Hasira ya Yahweh ikawaka juu ya Uza, na Yahweh akamua kwasababu Uza alishika na mkono wake sanduku. Akafa pale mbele za Mungu.
And the anger of Jehovah was kindled against Uzza, and he smote him because he put forth his hand to the ark. And there he died before God.
11 Daudi alipatwa na hasira kwa kuwa Yahweh alimshambulia Uza. Hiyo sehemu inaitwa Perezi Uza hadi leo.
And David was displeased, because Jehovah had broken forth upon Uzza. And he called that place Perez-uzza, to this day.
12 Daudi alimuogopa Mungu hiyo siku. Akasema, “Nawezaje kuleta sanduku la Mungu nyumbani mwangu?”
And David was afraid of God that day, saying, How shall I bring the ark of God home to me?
13 Kwaiyo Daudi hakuleta sanduku kwenye mji wa Daudi, lakini aliweka pembeni mwa nyumba ya Obedi Edomu Mgiti.
So David did not move the ark to him into the city of David, but carried it aside into the house of Obed-edom the Gittite.
14 Sanduku la Mungu lilibaki nyumbani mwa Obedi Edomu kwa miezi mitatu. Kwaiyo Yahweh akabariki nyumba yake na yote aliyo miliki.
And the ark of God remained with the family of Obed-edom in his house three months. And Jehovah blessed the house of Obed-edom, and all that he had.

< 1 Nyakati 13 >