< 1 Nyakati 12 >

1 Hawa walikuwa wanaume walio kuja kwa Daudi huko Zikilagi, wakati akiwa bado amefukuzwa katika uwepo wa Sauli mwana wa Kishi. Walikuwa miongoni mwa wanajeshi, wasaidizi wake katika mapambano.
These were the men who came to David to Ziklag, while he was still banished from the presence of Saul son of Kish. They were among the soldiers, his helpers in battle.
2 Walikuwa wana upinde na waliweza kutumia mkono wa kuume na wakushoto kurusha mawe na manati na kupiga mishale kutoka kwenye upinde. Walikuwa Wabenjamini, ndugu wa kabila moja na Sauli.
They were armed with bows and could use both the right hand and the left in slinging stones and in shooting arrows from the bow. They were Benjamites, Saul's fellow tribesmen.
3 Kiongozi alikuwa Ahi Eza, halafu Yoashi, Wana wote wa Shemaa Mgibeathi. Kulikuwa na Yezieli na Peleti, wana wa Azimavethi. Kulikuwa pia na Beraka, Yehu Waanathothi,
The chief was Ahiezer, then Joash, both sons of Shemaah the Gibeathite. There were Jeziel and Pelet, sons of Azmaveth. There were also Berakah, Jehu the Anathothite,
4 Ishimaia Mgibeoni, mwanajeshi kati ya wale thelathini ( na kiongozi wa wale thelathini); Yeremia, Yahazieli, Yohana, Yozabadi Wagederathi,
Ishmaiah the Gibeonite, a soldier among the thirty (and in command of the thirty); Jeremiah, Jahaziel, Johanan, Jozabad the Gederathite,
5 Eluzai, Yerimothi, Bealia, Shemaria, Shefatia Waharufi,
Eluzai, Jerimoth, Bealiah, Shemariah, Shephatiah the Haruphite,
6 Wakorahi ni Elkana, Ishia, Azareli, Yoeza, Yashobeamu, na
the Korahites Elkanah, Isshiah, Azarel, Joezer, Jashobeam, and
7 Yoela na Zebadia, wana wa Yeroham wa Gedori.
Joelah and Zebadiah, sons of Jeroham of Gedor.
8 Baadhi ya Wagadi walijiunga na Daudi katika ngome iliyo nyikani. Walikuwa wanaume wapiganaji, waliofundishwa kwa mapambano, walioweza kumudu ngao na mkuki; ambao nyuso zao zilikuwa kali kama za simba. Walikuwa wepesi kwenye milima kama swala.
Some Gadites joined David at the stronghold in the wilderness. They were fighting men, men trained for battle, who could handle shield and spear; whose faces were as fierce as the faces of lions. They were as swift as gazelles on the mountains.
9 Kulikuwa na Eza kiongozi, Obadia wapili, Eliabu watatu,
There were Ezer the leader, Obadiah the second, Eliab the third,
10 Mishimana wanne, Yeremia watano,
Mishmannah the fourth, Jeremiah the fifth,
11 Atai wasita, Elieli wasaba,
Attai the sixth, Eliel the seventh,
12 Yohana wanane, Elizabadi watisa,
Johanan the eighth, Elzabad the ninth,
13 Yeremia wakumi, Makibanai wakumi na moja.
Jeremiah the tenth, Makbannai the eleventh.
14 Wana wa Gadi walikuwa viongozi wa jeshi. Wamwisho aliongoza mia moja, na mkubwa aliongoza elfu moja.
These sons of Gad were leaders of the army. The least led a hundred, and the greatest led a thousand.
15 Walikatisha Yordani kwa mwezi wa kwanza, wakati vijito vyake vilipofurika, na kuwafukuza wote wanaoishi katika mabonde, pande zote za mashariki na magharibi.
They crossed the Jordan in the first month, when it overflowed its banks, and chased away all those living in the valleys, both toward the east and toward the west.
16 Baadhi ya wanaume wa Benjamini na Yuda walikuja kwenye ngome kwa Daudi.
Some of the men of Benjamin and Judah came to the stronghold to David.
17 Daudi alienda nje kuwasalimu na kuwahutubia: “kama mmekuja kwa amani kunisaidia, mnaweza kujiunga nami. Lakini kama mmekuja kunisaliti kwa maadui zangu, Ee Mungu wa mababu zetu awaone na kuwakemea, tangu sijafanya kosa.”
David went out to meet them and addressed them: “If you have come in peace to me to help me, you may join me. But if you have come to betray me to my adversaries, may the God of our ancestors see and rebuke you, since I have done no wrong.”
18 Kisha roho ikaja juu ya Amasai, ambaye alikuwa kiongozi wa wale thelathini. Amasai alisema, “Sisi ni wako, Daudi. Sisi tupo upande wako, mwana wa Yesse. na amani iwe juu ya yeyote atakaye kusaidia. Kuwa Mungu wako anakusaidia.” Kisha Daudi akawapokea na kuwafanya wakuu wa watu wake.
Then the Spirit came on Amasai, who was chief of the thirty. Amasai said, “We are yours, David. We are on your side, son of Jesse. Peace, may peace be to whoever helps you. May peace be to your helpers, for your God is helping you.” Then David received them and made them commanders over his men.
19 Baadhi kutoka kwa Manase pia wakamwendea Daudi alipokuja na Wafilisti dhidi ya Sauli katika pambano. Lakini hawakuwasaidia Wafilisti kwasababu mabwana wa Wafilisti walishauriana na wakamfukuza Daudi. Walisema, “Atamwendea Bwana wake Sauli na kuhatarisha maisha yetu.”
Some from Manasseh also deserted to David when he came with the Philistines against Saul to battle. Yet they did not help the Philistines, because the Philistine lords consulted with each other and sent David away. They said, “He will desert to his master Saul at the risk of our lives.”
20 Alipokwenda kwa Zikilagi, wanaume wa Manase walioungana nae walikuwa Adina, Yozabadi, Yediaeli, Yozabadi, Elihu, na Zilethai, viongozi wa maelfu wa Manase.
When he went to Ziklag, the men of Manasseh who joined him were Adnah, Jozabad, Jediael, Michael, Jozabad, Elihu, and Zillethai, captains over thousands of Manasseh.
21 Walimsaidia Daudi kupigana na kikundi cha wezi, maana walikuwa wanaume wa mapambano. Baadae walikuwa wakuu katika jeshi.
They helped David fight against the roving bands, for they were fighting men. Later they became commanders in the army.
22 Siku hadi siku, wanaume walikuja kwa Daudi kumsaidia, mpaka wakawa jeshi kubwa, kama jeshi la Mungu.
Day after day, men came to David to help him, until there was a great army, like the army of God.
23 Hii ni kumbukumbu ya wanajeshi wa vita, walio kuja kwa Daudi Hebroni, kuupindua ufalme wa Sauli kwake, ilikutimiza neno la Yahweh.
This is the record of the armed soldiers for war, who came to David to Hebron, to turn the kingdom of Saul over to him, which carried out Yahweh's word.
24 Kutoka Yuda walio beba ngao na mkuki ni 6, 800, tayari kwa vita.
From Judah those who carried shield and spear were 6,800, armed for war.
25 Kutoka kwa Wasimeoni walikuwa 7, 100 wanaume wa mapambano.
From the Simeonites there were 7,100 fighting men.
26 Kutoka kwa Walawi kulikuwa na wanaume wa mapambano 4, 600.
From the Levites there were 4,600 fighting men.
27 Yehoiada alikuwa kiongozi wa uzao wa Aruni, na kwa yeye walikuwa 3, 700.
Jehoiada was the leader of Aaron's descendants, and with him were 3,700.
28 Kwa Zadoki, kijana, mwenye nguvu, na mjasiri, walikuwa viongozi ishirini na mbili kwa familia ya baba yake.
With Zadok, a young, strong, and courageous man, were twenty-two leaders from his father's family.
29 Kutoka kwa Benjamini, kabila la Sauli, walikuwa elfu tatu. Wengi wao walibaki waaminifu kwa Sauli mpaka muda huu.
From Benjamin, Saul's tribe, were three thousand. Most of them had remained loyal to Saul until this time.
30 Kutoka kwa Waefraimu palikuwa na wanume wa mapambano 20, 800, wanaume maharufu kwenye familia za baba zao.
From the Ephraimites there were 20,800 fighting men, men who were famous in their fathers' houses.
31 Kutoka kabila nusu la Manase palikuwa na wanaume elfu kumi na nane maharufu walio kuja kufanya Daudi mfalme.
From the half tribe of Manasseh there were eighteen thousand famous men who came to make David king.
32 Kutoka kwa Isakari, palikuwa na viongozi mia mbili walio kuwa na ufahamu wa nyakati na walijua nini Israeli ya paswa kufanya. Ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.
From Issachar, there were two hundred leaders who had understanding of the times and knew what Israel ought to do. All their relatives were under their command.
33 Kutoka Zebuloni palikuwa na wanaume elfu hamsini wa mapambano, tayari kwa vita, na silaha zote za vita, na tayari kutoa uwaminifu usio pungua.
From Zebulun there were fifty thousand fighting men, prepared for battle, with all the weapons of war, and ready to give undivided loyalty.
34 Kutoka kwa Naftali palikuwa na askari elfu moja, na pamoja nao wanaume elfu thelathini na saba wenye ngao na mikuki.
From Naphtali there were one thousand officers, and with them thirty-seven thousand men with shields and spears.
35 Kutoka kwa Wadani palikuwa na wanaume 28, 600 wameandaliwa kwa ajili ya pambano.
From the Danites there were 28,600 men prepared for battle.
36 Kutoka kwa Asheri palikuwa na wanaume elfu arobaini wameandaliwa kwa pambano.
From Asher there were forty thousand men prepared for battle.
37 Kutoka upande wa pili wa Yordani, kutoka kwa Warubeni, Wagadi, na nusu kabila la Manase, palikuwa na wanaume 120, 000 wameandaliwa na silaha za kila namna kwa ajili ya pambano.
From the other side of the Jordan, from the Reubenites, Gadites, and the half tribe of Manasseh, there were 120,000 men armed with all kinds of weapons for battle.
38 Wanajeshi hawa wote, waliandaliwa kwa pambano, kuja Hebroni kwa dhumuni maalumu la kumfanya Daudi mfalme wa Israeli yote. Israeli yote ilikubaliana na kumfanya Daudi mfalme.
All these soldiers, equipped for battle, came to Hebron with firm intentions to make David king over all Israel. All the rest of Israel were in agreement to make David king also.
39 Walikuwa na Daudi siku tatu, kula na kunywa, kwa kuwa ndugu zao waliwapa mahitaji ya kwenda nayo.
They were there with David three days, eating and drinking, for their relatives had sent them with provisions.
40 Kwa kuongezea, wao walio kuwa karibu nao, kwa umbali wa Isakari na Zebuloni na Naftali, walileta mkate kwa punda, ngamia, ng'ombe, na keki, mvinyo, mafuta, ng'ombe, na kondoo, kwa kuwa Israeli walikuwa wana sherehekea
In addition, those who were near to them, as far as Issachar and Zebulun and Naphtali, brought bread on donkeys, camels, mules, and oxen, and cakes of figs, clusters of raisins, wine, oil, oxen, and sheep, for Israel was celebrating.

< 1 Nyakati 12 >