< 1 Nyakati 12 >

1 Hawa walikuwa wanaume walio kuja kwa Daudi huko Zikilagi, wakati akiwa bado amefukuzwa katika uwepo wa Sauli mwana wa Kishi. Walikuwa miongoni mwa wanajeshi, wasaidizi wake katika mapambano.
David went to Ziklag [town] to escape from [King] Saul. While he was there, many warriors came and joined him, and they helped him when he fought battles.
2 Walikuwa wana upinde na waliweza kutumia mkono wa kuume na wakushoto kurusha mawe na manati na kupiga mishale kutoka kwenye upinde. Walikuwa Wabenjamini, ndugu wa kabila moja na Sauli.
They carried bows [and arrows]. They were able to shoot arrows and to sling stones. They could use either their right arms or their left arms to do that. They were relatives of Saul from the tribe of Benjamin.
3 Kiongozi alikuwa Ahi Eza, halafu Yoashi, Wana wote wa Shemaa Mgibeathi. Kulikuwa na Yezieli na Peleti, wana wa Azimavethi. Kulikuwa pia na Beraka, Yehu Waanathothi,
Their leader was Ahiezer. Next in command was Joash. They were both sons of Shemaah from Gibeah [city]. [These are the names of some of those warriors: ] Jeziel and Pelet, the sons of Azmaveth; Beracah; Jehu from Anathoth [town];
4 Ishimaia Mgibeoni, mwanajeshi kati ya wale thelathini ( na kiongozi wa wale thelathini); Yeremia, Yahazieli, Yohana, Yozabadi Wagederathi,
Ishmaiah from the Gibeon [city], who was a leader of the thirty mighty warriors; Jeremiah, Jahaziel, Johanan, and Jozabad from Gederah [town];
5 Eluzai, Yerimothi, Bealia, Shemaria, Shefatia Waharufi,
Eluzai, Jerimoth, Bealiah, Shemariah, and Shephatiah from Haruph [town];
6 Wakorahi ni Elkana, Ishia, Azareli, Yoeza, Yashobeamu, na
Elkanah, Isshiah, Azarel, Joezer and Jashobeam, who were descendants of Korah;
7 Yoela na Zebadia, wana wa Yeroham wa Gedori.
Joelah and Zebadiah, who were sons of Jeroham, from Gedor [town].
8 Baadhi ya Wagadi walijiunga na Daudi katika ngome iliyo nyikani. Walikuwa wanaume wapiganaji, waliofundishwa kwa mapambano, walioweza kumudu ngao na mkuki; ambao nyuso zao zilikuwa kali kama za simba. Walikuwa wepesi kwenye milima kama swala.
Some men from the tribe of Gad [east of the Jordan River] joined David when he was at his fortress in [the caves in] the desert. They were brave warriors who were trained for fighting battles and able to use shields and spears well. They [SYN] were as fierce as [SIM, MTY] lions, and they could run as fast as [HYP, SIM] deer/gazelles on the hills/mountains.
9 Kulikuwa na Eza kiongozi, Obadia wapili, Eliabu watatu,
Ezer was their leader. Next in command was Obadiah. Next was Eliab.
10 Mishimana wanne, Yeremia watano,
Next was Mishmannah. Next was Jeremiah.
11 Atai wasita, Elieli wasaba,
Next was Attai. Next was Eliel.
12 Yohana wanane, Elizabadi watisa,
Next was Johanan. Next was Elzabad.
13 Yeremia wakumi, Makibanai wakumi na moja.
Next was [another man whose name was] Jeremiah. The last was Macbannai.
14 Wana wa Gadi walikuwa viongozi wa jeshi. Wamwisho aliongoza mia moja, na mkubwa aliongoza elfu moja.
Those men from the tribe of Gad were all army officers. Some of them commanded 1,000 soldiers, and some of them commanded 100 soldiers.
15 Walikatisha Yordani kwa mwezi wa kwanza, wakati vijito vyake vilipofurika, na kuwafukuza wote wanaoishi katika mabonde, pande zote za mashariki na magharibi.
They crossed [to the west side of] the Jordan [River] during March, [at the time of the year] when the river was flooded. They chased from there all the people who lived in the valleys on both sides of the river.
16 Baadhi ya wanaume wa Benjamini na Yuda walikuja kwenye ngome kwa Daudi.
Some other men from the tribe of Benjamin and from Judah also came to David in his fortress.
17 Daudi alienda nje kuwasalimu na kuwahutubia: “kama mmekuja kwa amani kunisaidia, mnaweza kujiunga nami. Lakini kama mmekuja kunisaliti kwa maadui zangu, Ee Mungu wa mababu zetu awaone na kuwakemea, tangu sijafanya kosa.”
David went out [of the cave] to meet them and said to them, “If you have come peacefully to help me, I am eager to have you join with me. But if you have come to enable my enemies to capture me, even though I [SYN] have not done anything to harm you, I hope/wish that the God whom our ancestors (worshiped/belonged to) will see it and condemn/punish you.”
18 Kisha roho ikaja juu ya Amasai, ambaye alikuwa kiongozi wa wale thelathini. Amasai alisema, “Sisi ni wako, Daudi. Sisi tupo upande wako, mwana wa Yesse. na amani iwe juu ya yeyote atakaye kusaidia. Kuwa Mungu wako anakusaidia.” Kisha Daudi akawapokea na kuwafanya wakuu wa watu wake.
Then [God’s] Spirit came upon Amasai, who was another leader of the thirty [greatest warriors], and he said, “David, we want to be with you; you who are the son of Jesse, we will join you. We know that things will go very well [DOU] for you and for those who are with you, because your God is helping you.”
19 Baadhi kutoka kwa Manase pia wakamwendea Daudi alipokuja na Wafilisti dhidi ya Sauli katika pambano. Lakini hawakuwasaidia Wafilisti kwasababu mabwana wa Wafilisti walishauriana na wakamfukuza Daudi. Walisema, “Atamwendea Bwana wake Sauli na kuhatarisha maisha yetu.”
So David welcomed those men, and he appointed them to be leaders of his soldiers. Some men from the tribe of Manasseh also joined David when he went with the soldiers of Philistia to fight against Saul’s [army]. But David and his men did not really help the army of Philistia. After the leaders of Philistia talked [about David and his soldiers], they sent David away. They said, “If David joins his master Saul again, we will all be killed {his army will kill all of us}!”
20 Alipokwenda kwa Zikilagi, wanaume wa Manase walioungana nae walikuwa Adina, Yozabadi, Yediaeli, Yozabadi, Elihu, na Zilethai, viongozi wa maelfu wa Manase.
When David went to Ziklag, these were the men from the tribe of Manasseh who went with him: Adnah, Jozabad, Jediael, Michael, [another man whose name was] Jozabad, Elihu, and Zillethai. Each of them had been a commander of 1,000 men [in Saul’s army].
21 Walimsaidia Daudi kupigana na kikundi cha wezi, maana walikuwa wanaume wa mapambano. Baadae walikuwa wakuu katika jeshi.
They were all brave soldiers, and they helped David to fight against the groups of men who roamed throughout the country, robbing people. So those men became commanders in David’s army.
22 Siku hadi siku, wanaume walikuja kwa Daudi kumsaidia, mpaka wakawa jeshi kubwa, kama jeshi la Mungu.
Every day more men joined David’s men, and his army became large, like [SIM] the army of God (OR, a very huge army).
23 Hii ni kumbukumbu ya wanajeshi wa vita, walio kuja kwa Daudi Hebroni, kuupindua ufalme wa Sauli kwake, ilikutimiza neno la Yahweh.
These are the numbers of soldiers who were ready for battle who joined David at Hebron [city]. They came to help him to become the king of Israel to replace Saul, as Yahweh had promised would happen.
24 Kutoka Yuda walio beba ngao na mkuki ni 6, 800, tayari kwa vita.
There were 6,800 men from Judah, who carried shields and spears.
25 Kutoka kwa Wasimeoni walikuwa 7, 100 wanaume wa mapambano.
There were 7,100 men from the tribe of Simeon. They were all strong warriors trained to fight battles.
26 Kutoka kwa Walawi kulikuwa na wanaume wa mapambano 4, 600.
There were 4,600 men from the tribe of Levi.
27 Yehoiada alikuwa kiongozi wa uzao wa Aruni, na kwa yeye walikuwa 3, 700.
Jehoiada, who was a leader descended from Aaron, was in that group of descendants of Levi, and there were 3,700 men with him.
28 Kwa Zadoki, kijana, mwenye nguvu, na mjasiri, walikuwa viongozi ishirini na mbili kwa familia ya baba yake.
Zadok, a strong young soldier, was also in that group, and there were 22 other leaders from his clan who came with him.
29 Kutoka kwa Benjamini, kabila la Sauli, walikuwa elfu tatu. Wengi wao walibaki waaminifu kwa Sauli mpaka muda huu.
There were 3,000 men from the tribe of Benjamin who were Saul’s relatives. Most of them had previously wanted one of Saul’s descendants to be the king.
30 Kutoka kwa Waefraimu palikuwa na wanume wa mapambano 20, 800, wanaume maharufu kwenye familia za baba zao.
There were 20,800 men from the tribe of Ephraim who were all brave warriors and trained for fighting battles and famous in their own clans.
31 Kutoka kabila nusu la Manase palikuwa na wanaume elfu kumi na nane maharufu walio kuja kufanya Daudi mfalme.
There were 18,000 men from the half of the tribe of Manasseh [that lived west of the Jordan River]. They were all chosen to go and help David become the king.
32 Kutoka kwa Isakari, palikuwa na viongozi mia mbili walio kuwa na ufahamu wa nyakati na walijua nini Israeli ya paswa kufanya. Ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.
There were 200 men who were leaders from the tribe of Issachar, along with their relatives. Those leaders always knew what the Israelis should do, and they knew the right time to do it.
33 Kutoka Zebuloni palikuwa na wanaume elfu hamsini wa mapambano, tayari kwa vita, na silaha zote za vita, na tayari kutoa uwaminifu usio pungua.
There were 55,000 men from the tribe of Zebulun. They were all experienced warriors and knew how to use all kinds of weapons well. They were completely loyal to David.
34 Kutoka kwa Naftali palikuwa na askari elfu moja, na pamoja nao wanaume elfu thelathini na saba wenye ngao na mikuki.
There were 1,000 officers from the tribe of Naphtali. With them were 37,000 soldiers, each carrying shields and spears.
35 Kutoka kwa Wadani palikuwa na wanaume 28, 600 wameandaliwa kwa ajili ya pambano.
There were 28,600 soldiers from the tribe of Dan, all trained to fight battles.
36 Kutoka kwa Asheri palikuwa na wanaume elfu arobaini wameandaliwa kwa pambano.
There were 47,000 experienced soldiers from the tribe of Asher, all trained to fight battles.
37 Kutoka upande wa pili wa Yordani, kutoka kwa Warubeni, Wagadi, na nusu kabila la Manase, palikuwa na wanaume 120, 000 wameandaliwa na silaha za kila namna kwa ajili ya pambano.
There were also 120,000 soldiers from the area east of the Jordan [River who joined David]. They were from the tribes of Reuben, Gad, and the eastern half of the tribe of Manasseh. They had all kinds of weapons.
38 Wanajeshi hawa wote, waliandaliwa kwa pambano, kuja Hebroni kwa dhumuni maalumu la kumfanya Daudi mfalme wa Israeli yote. Israeli yote ilikubaliana na kumfanya Daudi mfalme.
All those men were soldiers who volunteered to be in David’s army. They came to Hebron wanting very much to enable David to be the king of all of the Israeli people.
39 Walikuwa na Daudi siku tatu, kula na kunywa, kwa kuwa ndugu zao waliwapa mahitaji ya kwenda nayo.
The men spent three days there with David, eating and drinking, because their families had given them food to take with them.
40 Kwa kuongezea, wao walio kuwa karibu nao, kwa umbali wa Isakari na Zebuloni na Naftali, walileta mkate kwa punda, ngamia, ng'ombe, na keki, mvinyo, mafuta, ng'ombe, na kondoo, kwa kuwa Israeli walikuwa wana sherehekea
Also, their fellow Israelis came from as far away as the area where the tribes of Issachar, Zebulun, and Naphtali lived, bringing food on donkeys, camels, mules, and oxen. They brought a lot of flour, fig cakes, raisins, wine, [olive] oil, cattle and sheep. And throughout Israel, the people were very joyful.

< 1 Nyakati 12 >