< 1 Nyakati 12 >
1 Hawa walikuwa wanaume walio kuja kwa Daudi huko Zikilagi, wakati akiwa bado amefukuzwa katika uwepo wa Sauli mwana wa Kishi. Walikuwa miongoni mwa wanajeshi, wasaidizi wake katika mapambano.
These also are they that came to Dauid to Ziklag, while he was yet kept close, because of Saul the sonne of Kish: and they were among the valiant and helpers of the battel.
2 Walikuwa wana upinde na waliweza kutumia mkono wa kuume na wakushoto kurusha mawe na manati na kupiga mishale kutoka kwenye upinde. Walikuwa Wabenjamini, ndugu wa kabila moja na Sauli.
They were weaponed with bowes, and could vse the right and the left hand with stones and with arrowes and with bowes, and were of Sauls brethren, euen of Beniamin.
3 Kiongozi alikuwa Ahi Eza, halafu Yoashi, Wana wote wa Shemaa Mgibeathi. Kulikuwa na Yezieli na Peleti, wana wa Azimavethi. Kulikuwa pia na Beraka, Yehu Waanathothi,
The chiefe were Ahiezer, and Ioash the sonnes of Shemaah a Gibeathite, and Ieziel, and Pelet the sonnes of Asinaueth, Berachah and Iehu the Antothite,
4 Ishimaia Mgibeoni, mwanajeshi kati ya wale thelathini ( na kiongozi wa wale thelathini); Yeremia, Yahazieli, Yohana, Yozabadi Wagederathi,
And Ishmaiah the Gibeonite, a valiant man among thirtie, and aboue the thirtie, and Ieremiah, and Iehaziel, and Iohanan, and Ioshabad the Gederathite,
5 Eluzai, Yerimothi, Bealia, Shemaria, Shefatia Waharufi,
Eluzai, and Ierimoth, and Bealiah, and Shemariah, and Shephatiah the Haruphite,
6 Wakorahi ni Elkana, Ishia, Azareli, Yoeza, Yashobeamu, na
Elkanah, and Ishiah, and Azariel, and Ioezer, Iashobeam of Hakorehim,
7 Yoela na Zebadia, wana wa Yeroham wa Gedori.
And Ioelah, and Zebadiah, the sonnes of Ieroham of Gedor,
8 Baadhi ya Wagadi walijiunga na Daudi katika ngome iliyo nyikani. Walikuwa wanaume wapiganaji, waliofundishwa kwa mapambano, walioweza kumudu ngao na mkuki; ambao nyuso zao zilikuwa kali kama za simba. Walikuwa wepesi kwenye milima kama swala.
And of the Gadites there separated them selues some vnto Dauid into the holde of the wildernesse, valiant men of warre, and men of armes, and apt for battel, which coulde handle speare and shielde, and their faces were like the faces of lyons, and were like the roes in the mountaines in swiftnesse,
9 Kulikuwa na Eza kiongozi, Obadia wapili, Eliabu watatu,
Ezer the chiefe, Obadiah the second, Eliab the third,
10 Mishimana wanne, Yeremia watano,
Mishmanah the fourth, Ieremiah the fift,
11 Atai wasita, Elieli wasaba,
Attai the sixt, Eliel the seuenth,
12 Yohana wanane, Elizabadi watisa,
Iohanan the eight, Elzabad the ninth,
13 Yeremia wakumi, Makibanai wakumi na moja.
Ieremiah the tenth, Macbannai the eleuenth.
14 Wana wa Gadi walikuwa viongozi wa jeshi. Wamwisho aliongoza mia moja, na mkubwa aliongoza elfu moja.
These were the sonnes of Gad, captaines of the hoste: one of the least could resist an hundreth, and the greatest a thousand.
15 Walikatisha Yordani kwa mwezi wa kwanza, wakati vijito vyake vilipofurika, na kuwafukuza wote wanaoishi katika mabonde, pande zote za mashariki na magharibi.
These are they that went ouer Iorden in the first moneth when he had filled ouer all his bankes, and put to flight all them of the valley, toward the East and the West.
16 Baadhi ya wanaume wa Benjamini na Yuda walikuja kwenye ngome kwa Daudi.
And there came of the children of Beniamin, and Iudah to the hold vnto Dauid,
17 Daudi alienda nje kuwasalimu na kuwahutubia: “kama mmekuja kwa amani kunisaidia, mnaweza kujiunga nami. Lakini kama mmekuja kunisaliti kwa maadui zangu, Ee Mungu wa mababu zetu awaone na kuwakemea, tangu sijafanya kosa.”
And Dauid went out to meete them, and answered and sayde vnto them, If yee be come peaceably vnto me to helpe me, mine heart shall be knit vnto you, but if you come to betray me to mine aduersaries, seeing there is no wickednes in mine handes, the God of our fathers beholde it, and rebuke it.
18 Kisha roho ikaja juu ya Amasai, ambaye alikuwa kiongozi wa wale thelathini. Amasai alisema, “Sisi ni wako, Daudi. Sisi tupo upande wako, mwana wa Yesse. na amani iwe juu ya yeyote atakaye kusaidia. Kuwa Mungu wako anakusaidia.” Kisha Daudi akawapokea na kuwafanya wakuu wa watu wake.
And the spirit came vpon Amasai, which was the chiefe of thirtie, and he said, Thine are we, Dauid, and with thee, O sonne of Ishai. Peace, peace be vnto thee, and peace be vnto thine helpers: for thy God helpeth thee. Then Dauid receiued them, and made them captaines of the garison.
19 Baadhi kutoka kwa Manase pia wakamwendea Daudi alipokuja na Wafilisti dhidi ya Sauli katika pambano. Lakini hawakuwasaidia Wafilisti kwasababu mabwana wa Wafilisti walishauriana na wakamfukuza Daudi. Walisema, “Atamwendea Bwana wake Sauli na kuhatarisha maisha yetu.”
And of Manasseh some fell to Dauid, when he came with the Philistims against Saul to battell, but they helped them not: for the Princes of the Philistims by aduisement sent him away, saying, He will fall to his master Saul for our heads.
20 Alipokwenda kwa Zikilagi, wanaume wa Manase walioungana nae walikuwa Adina, Yozabadi, Yediaeli, Yozabadi, Elihu, na Zilethai, viongozi wa maelfu wa Manase.
As he went to Ziklag, there fell to him of Manasseh, Adnah, and Iozabad, and Iediael, and Michael, and Iozabad, and Elihu, and Ziltai, heads of the thousands that were of Manasseh.
21 Walimsaidia Daudi kupigana na kikundi cha wezi, maana walikuwa wanaume wa mapambano. Baadae walikuwa wakuu katika jeshi.
And they helped Dauid against that bad: for they were all valiant men and were captaines in the hoste.
22 Siku hadi siku, wanaume walikuja kwa Daudi kumsaidia, mpaka wakawa jeshi kubwa, kama jeshi la Mungu.
For at that time day by day there came to Dauid to helpe him, vntill it was a great hoste, like the hoste of God.
23 Hii ni kumbukumbu ya wanajeshi wa vita, walio kuja kwa Daudi Hebroni, kuupindua ufalme wa Sauli kwake, ilikutimiza neno la Yahweh.
And these are the nombers of the captaines that were armed to battell, and came to Dauid to Hebron to turne the kingdome of Saul to him, according to the worde of the Lord.
24 Kutoka Yuda walio beba ngao na mkuki ni 6, 800, tayari kwa vita.
The children of Iudah that bare shield and speare, were sixe thousand and eight hundreth armed to the warre.
25 Kutoka kwa Wasimeoni walikuwa 7, 100 wanaume wa mapambano.
Of the children of Simeon valiant men of warre, seuen thousand and an hundreth.
26 Kutoka kwa Walawi kulikuwa na wanaume wa mapambano 4, 600.
Of the children of Leui foure thousande and sixe hundreth.
27 Yehoiada alikuwa kiongozi wa uzao wa Aruni, na kwa yeye walikuwa 3, 700.
And Iehoiada was the chiefe of them of Aaron: and with him three thousande and seuen hundreth.
28 Kwa Zadoki, kijana, mwenye nguvu, na mjasiri, walikuwa viongozi ishirini na mbili kwa familia ya baba yake.
And Zadok a yong man very valiant, and of his fathers housholde came two and twentie captaines.
29 Kutoka kwa Benjamini, kabila la Sauli, walikuwa elfu tatu. Wengi wao walibaki waaminifu kwa Sauli mpaka muda huu.
And of the children of Beniamin the brethren of Saul three thousande: for a great part of them vnto that time kept the warde of the house of Saul.
30 Kutoka kwa Waefraimu palikuwa na wanume wa mapambano 20, 800, wanaume maharufu kwenye familia za baba zao.
And of the children of Ephraim twentie thousande, and eight hundreth valiant men and famous men in the housholde of their fathers.
31 Kutoka kabila nusu la Manase palikuwa na wanaume elfu kumi na nane maharufu walio kuja kufanya Daudi mfalme.
And of the halfe tribe of Manasseh eighteene thousand, which were appointed by name to come and make Dauid King.
32 Kutoka kwa Isakari, palikuwa na viongozi mia mbili walio kuwa na ufahamu wa nyakati na walijua nini Israeli ya paswa kufanya. Ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.
And of the children of Issachar which were men that had vnderstanding of the times, to knowe what Israel ought to doe: the heades of them were two hundreth, and all their brethren were at their commandement.
33 Kutoka Zebuloni palikuwa na wanaume elfu hamsini wa mapambano, tayari kwa vita, na silaha zote za vita, na tayari kutoa uwaminifu usio pungua.
Of Zebulun that went out to battel, expert in warre, and in all instruments of warre, fiftie thousande which could set the battell in aray: they were not of a double heart.
34 Kutoka kwa Naftali palikuwa na askari elfu moja, na pamoja nao wanaume elfu thelathini na saba wenye ngao na mikuki.
And of Naphtali a thousand captaines, and with them with shielde and speare seuen and thirtie thousande.
35 Kutoka kwa Wadani palikuwa na wanaume 28, 600 wameandaliwa kwa ajili ya pambano.
And of Dan expert in battell, eyght and twentie thousande, and sixe hundreth.
36 Kutoka kwa Asheri palikuwa na wanaume elfu arobaini wameandaliwa kwa pambano.
And of Asher that went out to the battell and were trained in the warres, fourtie thousand.
37 Kutoka upande wa pili wa Yordani, kutoka kwa Warubeni, Wagadi, na nusu kabila la Manase, palikuwa na wanaume 120, 000 wameandaliwa na silaha za kila namna kwa ajili ya pambano.
And of the other side of Iorden of the Reubenites, and of the Gadites, and of the halfe tribe of Manasseh with all instruments of warre to fight with, an hundreth and twentie thousand.
38 Wanajeshi hawa wote, waliandaliwa kwa pambano, kuja Hebroni kwa dhumuni maalumu la kumfanya Daudi mfalme wa Israeli yote. Israeli yote ilikubaliana na kumfanya Daudi mfalme.
All these men of warre that coulde leade an armie, came with vpright heart to Hebron to make Dauid King ouer all Israel: and all the rest of Israel was of one accorde to make Dauid King:
39 Walikuwa na Daudi siku tatu, kula na kunywa, kwa kuwa ndugu zao waliwapa mahitaji ya kwenda nayo.
And there they were with Dauid three dayes, eating and drinking: for their brethren had prepared for them.
40 Kwa kuongezea, wao walio kuwa karibu nao, kwa umbali wa Isakari na Zebuloni na Naftali, walileta mkate kwa punda, ngamia, ng'ombe, na keki, mvinyo, mafuta, ng'ombe, na kondoo, kwa kuwa Israeli walikuwa wana sherehekea
Moreouer they that were neere them vntill Issachar, and Zebulun, and Naphtali brought bread vpon asses, and on camels, and on mules, and on oxen, euen meate, floure, figges, and reisins, and wine and oyle, and beeues and sheepe abundantly: for there was ioy in Israel.