< 1 Nyakati 12 >

1 Hawa walikuwa wanaume walio kuja kwa Daudi huko Zikilagi, wakati akiwa bado amefukuzwa katika uwepo wa Sauli mwana wa Kishi. Walikuwa miongoni mwa wanajeshi, wasaidizi wake katika mapambano.
Also, these went to David at Ziklag, while he was still fleeing from Saul, the son of Kish. And they were very strong and distinguished fighters,
2 Walikuwa wana upinde na waliweza kutumia mkono wa kuume na wakushoto kurusha mawe na manati na kupiga mishale kutoka kwenye upinde. Walikuwa Wabenjamini, ndugu wa kabila moja na Sauli.
bending the bow, and using either hand in casting stones with slings, and shooting arrows. From the brothers of Saul, out of Benjamin:
3 Kiongozi alikuwa Ahi Eza, halafu Yoashi, Wana wote wa Shemaa Mgibeathi. Kulikuwa na Yezieli na Peleti, wana wa Azimavethi. Kulikuwa pia na Beraka, Yehu Waanathothi,
the leader was Ahiezer, with Joash, sons of Shemaah from Gibeah, and Jeziel and Pelet, sons of Azmaveth, and Beracah and Jehu, from Anathoth.
4 Ishimaia Mgibeoni, mwanajeshi kati ya wale thelathini ( na kiongozi wa wale thelathini); Yeremia, Yahazieli, Yohana, Yozabadi Wagederathi,
Also, there was Ishmaiah, from Gibeon, the strongest among the thirty and over the thirty; Jeremiah, and Jahaziel, and Johanan, and Jozabad, from Gederah;
5 Eluzai, Yerimothi, Bealia, Shemaria, Shefatia Waharufi,
and Eluzai, and Jerimoth, and Bealiah, and Shemariah, and Shephatiah, the Haruphites;
6 Wakorahi ni Elkana, Ishia, Azareli, Yoeza, Yashobeamu, na
Elkanah, and Isshiah, and Azarel, and Joezer, and Jashobeam, from Carehim;
7 Yoela na Zebadia, wana wa Yeroham wa Gedori.
and also Joelah and Zebadiah, sons of Jeroham, from Gedor.
8 Baadhi ya Wagadi walijiunga na Daudi katika ngome iliyo nyikani. Walikuwa wanaume wapiganaji, waliofundishwa kwa mapambano, walioweza kumudu ngao na mkuki; ambao nyuso zao zilikuwa kali kama za simba. Walikuwa wepesi kwenye milima kama swala.
Then too, from Gad, there went over to David, when he was hiding in the desert, very robust men, who were excellent fighters, taking hold of shield and spear; their faces were like the faces of a lion, and they were swift like the roe deer upon the mountains.
9 Kulikuwa na Eza kiongozi, Obadia wapili, Eliabu watatu,
Ezer was the leader, Obadiah the second, Eliab the third,
10 Mishimana wanne, Yeremia watano,
Mishmannah the fourth, Jeremiah the fifth,
11 Atai wasita, Elieli wasaba,
Attai the sixth, Eliel the seventh,
12 Yohana wanane, Elizabadi watisa,
Johanan the eighth, Elzabad the ninth,
13 Yeremia wakumi, Makibanai wakumi na moja.
Jeremiah the tenth, Machbannai the eleventh.
14 Wana wa Gadi walikuwa viongozi wa jeshi. Wamwisho aliongoza mia moja, na mkubwa aliongoza elfu moja.
These were from the sons of Gad, leaders of the army. The least was in charge of one hundred soldiers, and the greatest was in charge of one thousand.
15 Walikatisha Yordani kwa mwezi wa kwanza, wakati vijito vyake vilipofurika, na kuwafukuza wote wanaoishi katika mabonde, pande zote za mashariki na magharibi.
These are the ones who crossed over the Jordan in the first month, when it is accustomed to overflow its banks. And they put to flight all those who were staying in the valleys, to the eastern region and to the west.
16 Baadhi ya wanaume wa Benjamini na Yuda walikuja kwenye ngome kwa Daudi.
Then some from Benjamin and from Judah also arrived at the stronghold where David was staying.
17 Daudi alienda nje kuwasalimu na kuwahutubia: “kama mmekuja kwa amani kunisaidia, mnaweza kujiunga nami. Lakini kama mmekuja kunisaliti kwa maadui zangu, Ee Mungu wa mababu zetu awaone na kuwakemea, tangu sijafanya kosa.”
And David went out to meet them, and he said: “If you have arrived peacefully, so as to be a help to me, may my heart be joined to you; but if to betray me to my adversaries, though I have no iniquity in my hands, may the God of our fathers see and judge.”
18 Kisha roho ikaja juu ya Amasai, ambaye alikuwa kiongozi wa wale thelathini. Amasai alisema, “Sisi ni wako, Daudi. Sisi tupo upande wako, mwana wa Yesse. na amani iwe juu ya yeyote atakaye kusaidia. Kuwa Mungu wako anakusaidia.” Kisha Daudi akawapokea na kuwafanya wakuu wa watu wake.
Truly, the Spirit clothed Amasai, the leader among the thirty, and he said: “O David, we are yours! O son of Jesse, we are for you! Peace, peace to you, and peace to your helpers. For your God helps you.” Therefore, David received them, and he appointed them as leaders of troops.
19 Baadhi kutoka kwa Manase pia wakamwendea Daudi alipokuja na Wafilisti dhidi ya Sauli katika pambano. Lakini hawakuwasaidia Wafilisti kwasababu mabwana wa Wafilisti walishauriana na wakamfukuza Daudi. Walisema, “Atamwendea Bwana wake Sauli na kuhatarisha maisha yetu.”
Moreover, some from Manasseh crossed over to David, when he went forth with the Philistines against Saul, so that he might fight. But he did not fight with them. For the leaders of the Philistines, taking counsel, sent him back, saying, “To the peril of our own heads, he will return to his lord, Saul.”
20 Alipokwenda kwa Zikilagi, wanaume wa Manase walioungana nae walikuwa Adina, Yozabadi, Yediaeli, Yozabadi, Elihu, na Zilethai, viongozi wa maelfu wa Manase.
And so, when he returned to Ziklag, some fled over to him from Manasseh: Adnah, and Jozabad, and Jediael, and Michael, and Adnah, and Jozabad, and Elihu, and Zillethai, leaders of thousands in Manasseh.
21 Walimsaidia Daudi kupigana na kikundi cha wezi, maana walikuwa wanaume wa mapambano. Baadae walikuwa wakuu katika jeshi.
These offered assistance to David against the robbers. For all were very strong men, and they became leaders in the army.
22 Siku hadi siku, wanaume walikuja kwa Daudi kumsaidia, mpaka wakawa jeshi kubwa, kama jeshi la Mungu.
Then, too, some came to David throughout each day, in order to help him, until they became a great number, like the army of God.
23 Hii ni kumbukumbu ya wanajeshi wa vita, walio kuja kwa Daudi Hebroni, kuupindua ufalme wa Sauli kwake, ilikutimiza neno la Yahweh.
Now this is the number of the leaders of the army who went to David when he was at Hebron, so that they might transfer the kingdom of Saul to him, in accord with the word of the Lord:
24 Kutoka Yuda walio beba ngao na mkuki ni 6, 800, tayari kwa vita.
the sons of Judah, carrying shield and spear, six thousand eight hundred, equipped for battle;
25 Kutoka kwa Wasimeoni walikuwa 7, 100 wanaume wa mapambano.
from the sons of Simeon, very strong men for the fight, seven thousand one hundred;
26 Kutoka kwa Walawi kulikuwa na wanaume wa mapambano 4, 600.
from the sons of Levi, four thousand six hundred;
27 Yehoiada alikuwa kiongozi wa uzao wa Aruni, na kwa yeye walikuwa 3, 700.
as well as Jehoiada, a leader from the stock of Aaron, and with him three thousand seven hundred;
28 Kwa Zadoki, kijana, mwenye nguvu, na mjasiri, walikuwa viongozi ishirini na mbili kwa familia ya baba yake.
and then Zadok, a youth of distinguished qualities, and the house of his father, twenty-two leaders;
29 Kutoka kwa Benjamini, kabila la Sauli, walikuwa elfu tatu. Wengi wao walibaki waaminifu kwa Sauli mpaka muda huu.
and from the sons of Benjamin, brothers of Saul, three thousand, for still a great part of them were following the house of Saul.
30 Kutoka kwa Waefraimu palikuwa na wanume wa mapambano 20, 800, wanaume maharufu kwenye familia za baba zao.
Then from the sons of Ephraim, there were twenty thousand eight hundred, very strong and robust men, renowned among their kindred.
31 Kutoka kabila nusu la Manase palikuwa na wanaume elfu kumi na nane maharufu walio kuja kufanya Daudi mfalme.
And out of the one half tribe of Manasseh, eighteen thousand, each by their names, went forth so that they might appoint David as king.
32 Kutoka kwa Isakari, palikuwa na viongozi mia mbili walio kuwa na ufahamu wa nyakati na walijua nini Israeli ya paswa kufanya. Ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.
Also, from the sons of Issachar, there were learned men, who knew each of the times, in order to anticipate what Israel ought to do, two hundred leaders. And all the remainder of the tribe were following their counsel.
33 Kutoka Zebuloni palikuwa na wanaume elfu hamsini wa mapambano, tayari kwa vita, na silaha zote za vita, na tayari kutoa uwaminifu usio pungua.
Then, from Zebulun, there were those who went forth to battle, and who were standing in a battle line, prepared with the weapons of warfare; these fifty thousand arrived to assist, without duplicity of heart.
34 Kutoka kwa Naftali palikuwa na askari elfu moja, na pamoja nao wanaume elfu thelathini na saba wenye ngao na mikuki.
And from Naphtali, there were one thousand leaders; and with them were thirty-seven thousand, prepared with shield and spear.
35 Kutoka kwa Wadani palikuwa na wanaume 28, 600 wameandaliwa kwa ajili ya pambano.
And then from Dan, there were twenty-eight thousand six hundred, ready for battle.
36 Kutoka kwa Asheri palikuwa na wanaume elfu arobaini wameandaliwa kwa pambano.
And from Asher, there were forty thousand, going forth to fight, and summoned to the battle line.
37 Kutoka upande wa pili wa Yordani, kutoka kwa Warubeni, Wagadi, na nusu kabila la Manase, palikuwa na wanaume 120, 000 wameandaliwa na silaha za kila namna kwa ajili ya pambano.
Then, across the Jordan, there were, from the sons of Reuben, and from Gad, and from the one half tribe of Manasseh, one hundred twenty thousand, prepared with the weapons of warfare.
38 Wanajeshi hawa wote, waliandaliwa kwa pambano, kuja Hebroni kwa dhumuni maalumu la kumfanya Daudi mfalme wa Israeli yote. Israeli yote ilikubaliana na kumfanya Daudi mfalme.
All these men of war, equipped for the fight, went with a perfect heart to Hebron, so that they might appoint David as king over all of Israel. Then, too, all the remainder of Israel were of one heart, so that they might make David king.
39 Walikuwa na Daudi siku tatu, kula na kunywa, kwa kuwa ndugu zao waliwapa mahitaji ya kwenda nayo.
And they were in that place with David for three days, eating and drinking. For their brothers had made preparations for them.
40 Kwa kuongezea, wao walio kuwa karibu nao, kwa umbali wa Isakari na Zebuloni na Naftali, walileta mkate kwa punda, ngamia, ng'ombe, na keki, mvinyo, mafuta, ng'ombe, na kondoo, kwa kuwa Israeli walikuwa wana sherehekea
Moreover, those who were near to them, even as far as Issachar, and Zebulun, and Naphtali, were bringing, on donkeys and camels and mules and oxen, bread for their provisions, with grain, dried figs, dried grapes, wine, oil, and oxen and sheep, with all abundance. For indeed, there was joy in Israel.

< 1 Nyakati 12 >