< 1 Nyakati 11 >

1 Kisha Waisraeli wote walikuja Hebroni kwa Daudi na kusema, “Angalia, sisi ni nyama na mifupa yako.
Then all Israel gathered themselves to David in Hebron, saying: We are thy bone, and thy flesh.
2 Katika wakati uliopita, Sauli alipoo kuwa mfalme juu yetu, ni wewe uliye ongoza jeshi la Israeli. Yahweh Mungu wako alisema kwako, 'utawachunga watu wangu wa Isaraeli, na utakuwa mtawala wa watu wangu wa Israeli”'.
Yesterday also, and the day before when Saul was king, thou wast he that leddest out and broughtest in Israel: for the Lord thy God said to thee: Thou shalt feed my people Israel, and thou shalt; be ruler over them.
3 Kwaiyo wazee wote wa Israeli wakamjia mfalme huko Hebroni, na Daudi akafanya agano nao mbele ya Yahweh. Wakampaka mafuta Daudi kuwa mfalme wa Israeli. Kwa namna hii, neno la Yahweh lilo nenwa na Samweli likawa kweli.
So all the ancients of Israel came to the king to Hebron, and David made a covenant with them before the Lord: and they anointed him king over Israel, according to the word of the Lord which he spoke in the hand of Samuel.
4 Daudi na Israeli yote wakaenda Yerusalemu (yani, Yebusi). Sasa Wayebusi, wakazi wa nchi, walikuwa pale.
And David and all Israel went to Jerusalem, which is Jebus, where the Jebusites were the inhabitants of the land.
5 Wakazi wa yebusi wakamwabia Daudi, “Hautakuja humu.” Lakini Daudi alichukuwa ngome ya Sayuni, mji wa Daudi.
And the inhabitants of Jebus said to David: Thou shalt not come in here. But David took the castle of Sion, which is the city of David.
6 Daudi alisema, “Yeyote atakaye washambulia Wayebusi wa kwanza atakuwa mkuu wa jeshi” kwaiyo Yoabu mwana wa Zeruia akashambulia wa kwanza, hivyo akafanywa mkuu wa jeshi.
And he said: Whosoever shall first strike the Jebusites, shall be the head and chief captain. And Joab the son of Sarvia went up first, and was made the general.
7 Daudi akaanza kuishi katika hiyo ngome. Kwaiyo wakaiita mji wa Daudi.
And David dwelt in the castle, and therefore it was called the city of David.
8 Akaimarisha mji kutoka Milo na hadi mpaka ukuta unao zunguka. Yoabu akaimairisha mji wote uliyo baki.
And he built the city round about from Mello all round, and Joab built the rest of the city.
9 Daudi akawa mkuu na mkuu kwa sababu Yahweh wa Majeshi alikuwa naye.
And David went on growing and increasing, and the Lord of hosts was with him.
10 Hawa walikuwa viongozi Daudi aliyo kuwa nao, waliyo jionyesha imara katika ufalme wake, pamoja na Israeli, kumfanya mfalme, kutii neno la Yahweh kuhusu Israeli.
These are the chief of the valiant men of David, who helped him to be made king over all Israel, according to the word of the Lord, which he spoke to Israel.
11 Hii ni orodha ya wanajeshi shupavu wa Daudi. Yashobeami, mwana wa Mhakimoni, alikuwa mkuu wa kikosi cha thelathini. Aliwaua wanaume mia tatu na mkuki wake katika sehemu moja.
And this is the number of the heroes of David: Jesbaam the son of Hachamoni the chief among the thirty: he lifted up his spear against three hundred wounded by him at one time.
12 Baada ya yeye alikuwa Eleazari mwana wa Dodo, Mahohi, aliyekuwa mmoja wa wanaume watatu hodari.
And after him was Eleazar his uncle’s son the Ahohite, who was one of the three mighties.
13 Alikuwa na Daudi huko Pasidamimu, na pale Wafilisti wakakusanyika pamoja kwa mapambano, ambapo palikuwa na uwanja wa ngano na jeshi liliwakimbia Wafilisti.
He was with David in Phesdomim, when the Philistines were gathered to that place to battle: and the field of that country was full of barley, and the people fled from before the Philistines.
14 Walisimama katikati ya uwanja. Wakautetea na kuwakata Wafilisti na Yahweh akawaokoa na ushindi mkubwa.
But these men stood in the midst of the field, and defended it: and they slew the Philistines, and the Lord gave a great deliverance to his people.
15 Kisha watatu wa viongozi thelathini wakashuka chini kwenye mwamba wa Daudi, katika pango la Adulamu. Jeshi la Wafilisti walieka kambi katika bonde la Refaim.
And three of the thirty captains went down to the rock, wherein David was, to the cave of Odollam, when the Philistines encamped in the valley of Raphaim.
16 Kwa wakati huo Daudi alikuwa katika ngome yake, pangoni, Wafilisti walikita kambi yao Bethilehemu.
And David was in a hold, and the garrison of the Philistines in Bethlehem.
17 Daudi alikuwa na kiu ya maji na akasema, “Laiti mtu akanipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho Bethilehemu, kisima kilicho pembeni mwa lango!”
And David longed, and said: O that some man would give me water of the cistern of Bethlehem, which is in the gate.
18 Hawa wanaume hodari watatu wakatoboa kupita jeshi la Wafilisti na kuchota maji kwenye kisima cha Bethilehemu, kisima pembeni mwa lango. Wakachukuwa maji na kumletea Daudi, lakini alikataa kunywa. Badala yake, akamwaga chini kwa Yahweh.
And these three broke through the midst of the camp of the Philistines, and drew water out of the cistern of Bethlehem, which was in the gate, and brought it to David to drink: and he would not drink of it, but rather offered it to the Lord,
19 Kisha akasema, “Yahweh, iwe mbali na mimi, kwamba ni yanywe haya maji. Je ninywe damu ya wanaume walio hatarisha maisha yao?” Kwa sababu wameeka maisha ya hatarini, akakataa kunywa. Haya ni mambo wanaume hodari watatu walio fanya.
Saying: God forbid that I should do this in the sight of my God, and should drink the blood of these men: for with the danger of their lives they have brought me the water. And therefore he would not drink. These things did the three most valiant.
20 Abishai kaka wa Yoabu, alikuwa kiongozi wa watatu. Alitumia mkuki wake dhidi ya watu mia tatu na kuwaua. Ametajwa pamoja na wale watatu.
And Abisai the brother of Joab, he was chief of three, and he lifted up his spear against three hundred whom he slew, and he was renowned among the three,
21 Kati ya wale watatu, yeye alipewa heshima mara mbili na akawa kiongozi wao. Japo hakuwa mmoja wa miongoni mwao.
And illustrious among the second three, and their captain: but yet he attained not to the first three.
22 Benaia mwana wa Yehoiada alikuwa mwanaume mwenye nguvu aliye fanya mambo makuu. Aliua wana wawili wa Arieli wa Moabu. Pia alishuka chini ya shimo na kumuua simba wakati theluji ikianguka.
Banaias the son of Joiada, a most valiant man, of Cabseel, who had done many acts: he slew the two ariels of Moab: and he went down, and killed a lion in the midst of a pit in the time of snow.
23 Alimua hadi Mmisri, mwanaume mwenye mita mbili na theluthi moja. Mmisri alikuwa na mkuki kama gongo la mshonaji, lakini alimfuata chini na fimbo tu. Akakamata mkuki katika mkono wa Mmisri na kumuua na mkuki wake.
And he slew an Egyptian, whose stature was of five cubits, and who had a spear like a weaver’s beam: and he went down to him with a staff, and plucked away the spear, that he held in his hand, and slew him with his own spear.
24 Benaia mwana wa Yehoiada alifanya haya matukio, na akatajwa miongoni mwa wale wanaume hodari watatu.
These things did Banaias the son of Joiada, who was renowned among the three valiant ones,
25 Alisifika zaidi ya wale wanajeshi thelathini kwa ujumla, lakini hakuwa pewa hadhi ya wale wanajeshi watatu hodari. Daudi alimueka kiongozi wa walinzi wake.
And the first among the thirty, but yet to the three he attained not: and David made him of his council.
26 Wanaume hodari walikuwa Asaheli kaka wa Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo wa Bethilehemu,
Moreover the most valiant men of the army, were Asahel brother of Joab, and Elchanan the son of his uncle of Bethlehem,
27 Shamothi Mherori, Helezi Mpeloni,
Sammoth an Arorite, Helles a Phalonite,
28 Ira mwana wa Ikeshi Mtekoi, Abi Eza Manathothi,
Ira the son of Acces a Thecuite, Abiezer an Anathothite,
29 Sibekai Mhushathite, Ilai Mahohite,
Sobbochai a Husathite, Ilai an Ahohite,
30 Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana Mnetofathite,
Maharai a Netophathite, Heled the son of Baana a Netophathite,
31 Itai mwana wa Ribai wa Gibea uzao wa Benjamini, Benaia Mpirathoni,
Ethai the son of Ribai of Gabaath of the sons of Benjamin, Banal a Pharathonite,
32 Hurai wa mabonde ya Gaashi, Abieli Marbathi,
Hurai of the torrent Gaas, Abiel an Arbathite, Azmoth a Bauramite, Eliaba a Salabonite,
33 Azmavethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
The sons of Assem a, Gezonite, Jonathan the son of Sage an Ararite,
34 Mwana wa Hashemu Mgizoni, Yonathani mwana wa Shagee Mhararite,
Ahiam the son of Sachar an Ararite,
35 Ahiamu mwana wa Sacari Mhararite, Elifali mwana wa Uri,
Eliphal the son of Ur,
36 Hefa Mmekarathi, Ahija Mpeloni,
Hepher a Mecherathite, Ahia a Phelonite,
37 Hezro Mcarmeli, Maarai mwana wa Ezibai,
Hesro a Carmelite, Naarai the son of Azbai,
38 Yoeli kaka wa Nathani, Mibhari mwana wa Hagiri,
Joel the brother of Nathan, Mibahar the son of Agarai.
39 Zeleki Mamoni, Naharai Mberothi ( mbeba ngao ya Yoabu mwana wa Zeruia),
Selec an Ammonite, Naharai a Berothite, the armourbearer of Joab the son of Sarvia.
40 Ira Mithire, Garebu Mithire,
Ira a Jethrite, Gareb a Jethrite,
41 Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Ahlai,
Urias a Hethite, Zabad the son of Oholi,
42 Adina mwana wa Shiza Mreubeni ( kiongozi wa Wareubeni) na thelathini pamoja nae,
Adina the son of Siza a Rubenite the prince of the Rubenites, and thirty with him:
43 Hanani mwana wa Maaka, na Yoshafati Mmithini,
Hanan the son of Maacha, and Josaphat a Mathanite,
44 Uzia Mashiterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Waaroeri,
Ozia an Astarothite, Samma, and Jehiel the sons of Hotham an Arorite,
45 Jediaeli mwana wa Shimri, Joha ( kaka yake Mtize),
Jedihel the son of Zamri, and Jobs his brother a Thosaite,
46 Elieli Mmahavi, Yeribai na Yoshavia mwana wa Elnaamu, Ithima Mmoabi,
Eliel a Mithumite, and Jeribai, and Josaia the sons of Elnaim, and Jethma a Moabite,
47 Elieli, Obedi, na Yaasieli Wamezobai.
Eliel, and Obed, and Jasiel of Masobia.

< 1 Nyakati 11 >