< Sefania 1 >

1 Neno la Bwana lililomjia Sefania mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amaria, mwana wa Hezekia, wakati wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda:
The word of the Lord, that was maad to Sofonye, sone of Chusi, sone of Godolie, sone of Amasie, sone of Ezechie, in the daies of Josie, the sone of Amon, king of Juda.
2 Bwana asema, “Nitafagia kila kitu kutoka kwenye uso wa dunia.”
Y gaderinge schal gadere alle thingis fro the face of erthe, seith the Lord;
3 “Nitafagilia mbali watu na wanyama; nitafagilia mbali ndege wa angani na samaki wa baharini. Wafanyao maovu watapata tu kokoto, nami nitamkatilia mbali mwanadamu atoke katika dunia,” asema Bwana.
Y gaderynge man and beeste, Y gaderynge volatils of heuene, and fischis of the see; and fallyngis of vnpitouse men schulen be, and Y schal leese men fro face of erthe, seith the Lord.
4 “Nitaiadhibu Yuda na wote wakaao Yerusalemu. Kutoka mahali hapa nitakatilia mbali kila mabaki ya Baali, majina ya wapagani na makuhani waabuduo sanamu:
And Y schal stretche out myn hond on Juda, and on alle dwellers of Jerusalem; and Y schal lese fro this place the relifs of Baal, and the names of keperis of housis, with prestis;
5 wale ambao husujudu juu ya mapaa kuabudu jeshi la vitu vya angani, wale ambao husujudu na kuapa kwa Bwana na ambao pia huapa kwa Malkamu,
and hem that worschipen on roouys the knyythod of heuene, and worschipen, and sweren in the Lord, and sweren in Melchon;
6 wale wanaoacha kumfuata Bwana, wala hawamtafuti Bwana wala kutaka shauri lake.
and whiche ben turned awei bihynde the bak of the Lord, and whiche `souyten not the Lord, nether enserchiden hym.
7 Nyamazeni mbele za Bwana Mwenyezi, kwa maana siku ya Bwana iko karibu. Bwana ameandaa dhabihu, amewaweka wakfu wale aliowaalika.
Be ye stille fro the face of the Lord God, for niy is the dai of the Lord; for the Lord made redi a sacrifice, halewide hise clepid men.
8 Katika siku ya dhabihu ya Bwana nitawaadhibu wakuu na wana wa mfalme na wale wote wanaovaa nguo za kigeni.
And it schal be, in the dai of sacrifice of the Lord, Y schal visite on princes, and on sones of the kyng, and on alle that ben clothid with pilgrimys, ether straunge, clothing.
9 Katika siku hiyo nitaadhibu wote ambao hukwepa kukanyaga kizingiti, ambao hujaza hekalu la miungu yao kwa dhuluma na udanganyifu.”
And Y schal visite on ech that proudli entrith on the threisfold in that dai, whiche fillen the hous of her Lord God with wickidnesse and gile.
10 Bwana asema, “Katika siku hiyo kilio kitapanda juu kutoka lango la Samaki, maombolezo kutoka mtaa wa pili, na mshindo mkubwa kutoka vilimani.
And ther schal be in that dai, seith the Lord, a vois of cry fro the yate of fischis, and yellynge fro the secounde yate, and greet defoulyng fro litle hillis.
11 Ombolezeni, ninyi mnaoishi katika eneo la sokoni; wafanyabiashara wenu wote wameangamizwa, wote ambao wanafanya biashara ya fedha wataangamizwa.
Yelle ye, dwelleris of Pila; al the puple of Canaan was stille togidere, alle men wlappid in siluer perischiden.
12 Wakati huo nitasaka mji wa Yerusalemu kwa taa, na kuwaadhibu wale ambao wanakaa katika hali ya kuridhika, ambao ni kama divai iliyobaki kwenye machicha, ambao hudhani, ‘Bwana hatafanya lolote, jema au baya.’
And it schal be, in that tyme Y schal seke Jerusalem with lanternes, and Y schal visite on alle men piyt in her darstis, whiche seien in her hertis, The Lord schal not do wel, and he schal not do yuele.
13 Utajiri wao utatekwa nyara, nyumba zao zitabomolewa. Watajenga nyumba, lakini hawataishi ndani yake; watapanda mizabibu lakini hawatakunywa divai yake.
And the strengthe of hem schal be in to rauyschyng, and the housis of hem in to desert; and thei schulen bilde housis, and schulen not enhabite; and thei schulen plaunte vyneyerdis, and thei schulen not drynke the wyn of hem.
14 “Siku kubwa ya Bwana iko karibu: iko karibu na inakuja haraka. Sikilizeni! Kilio katika siku ya Bwana kitakuwa kichungu, hata shujaa atapiga kelele.
Nyy is the greet dai of the Lord, niy and swift ful myche; the vois of the dai of the Lord is bittir, a strong man schal be in tribulacioun there.
15 Siku ile ni siku ya ghadhabu, siku ya fadhaa na dhiki, siku ya uharibifu na ukiwa, siku ya giza na utusitusi, siku ya mawingu na giza nene,
`The ilke dai is a dai of wraththe, dai of tribulacioun and angwisch, dai of nedynesse and wretchidnesse, dai of derknessis and myist, dai of cloude and whirlewynd,
16 siku ya tarumbeta na mlio wa vita dhidi ya miji yenye ngome na dhidi ya minara mirefu.
dai of trumpe and noise on strong citees and on hiye corneris.
17 Nitawaletea watu dhiki, nao watatembea kama vipofu, kwa sababu wametenda dhambi dhidi ya Bwana. Damu yao itamwagwa kama vumbi na matumbo yao kama taka.
And Y schal troble men, and thei schulen walke as blynde, for thei han synned ayens the Lord; and the blood of hem schal be sched out as erthe, and the bodies of hem schulen be as tordis.
18 Fedha yao wala dhahabu yao hazitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya ghadhabu ya Bwana. Katika moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa, kwa maana ataleta mwisho wa wote wanaoishi katika dunia ghafula.”
But and the siluer of hem, and gold of hem, schal not mowe delyuere hem in the dai of wraththe of the Lord; in fier of his feruour al erthe schal be deuourid, for he schal make ende with haastyng to alle men enhabitynge the erthe.

< Sefania 1 >