< Sefania 1 >

1 Neno la Bwana lililomjia Sefania mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amaria, mwana wa Hezekia, wakati wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda:
word LORD which to be to(wards) Zephaniah son: child Cushi son: child Gedaliah son: child Amariah son: child Hezekiah in/on/with day Josiah son: child Amon king Judah
2 Bwana asema, “Nitafagia kila kitu kutoka kwenye uso wa dunia.”
to gather to cease all from upon face: surface [the] land: planet utterance LORD
3 “Nitafagilia mbali watu na wanyama; nitafagilia mbali ndege wa angani na samaki wa baharini. Wafanyao maovu watapata tu kokoto, nami nitamkatilia mbali mwanadamu atoke katika dunia,” asema Bwana.
to cease man and animal to cease bird [the] heaven and fish [the] sea and [the] ruins with [the] wicked and to cut: eliminate [obj] [the] man from upon face: surface [the] land: planet utterance LORD
4 “Nitaiadhibu Yuda na wote wakaao Yerusalemu. Kutoka mahali hapa nitakatilia mbali kila mabaki ya Baali, majina ya wapagani na makuhani waabuduo sanamu:
and to stretch hand my upon Judah and upon all to dwell Jerusalem and to cut: cut from [the] place [the] this [obj] remnant [the] Baal [obj] name [the] pagan priest with [the] priest
5 wale ambao husujudu juu ya mapaa kuabudu jeshi la vitu vya angani, wale ambao husujudu na kuapa kwa Bwana na ambao pia huapa kwa Malkamu,
and [obj] [the] to bow upon [the] roof to/for army [the] heaven and [obj] [the] to bow [the] to swear to/for LORD and [the] to swear in/on/with Milcom
6 wale wanaoacha kumfuata Bwana, wala hawamtafuti Bwana wala kutaka shauri lake.
and [obj] [the] to turn from after LORD and which not to seek [obj] LORD and not to seek him
7 Nyamazeni mbele za Bwana Mwenyezi, kwa maana siku ya Bwana iko karibu. Bwana ameandaa dhabihu, amewaweka wakfu wale aliowaalika.
to silence from face: before Lord YHWH/God for near day LORD for to establish: prepare LORD sacrifice to consecrate: consecate to call: call to his
8 Katika siku ya dhabihu ya Bwana nitawaadhibu wakuu na wana wa mfalme na wale wote wanaovaa nguo za kigeni.
and to be in/on/with day sacrifice LORD and to reckon: punish upon [the] ruler and upon son: child [the] king and upon all [the] to clothe garment foreign
9 Katika siku hiyo nitaadhibu wote ambao hukwepa kukanyaga kizingiti, ambao hujaza hekalu la miungu yao kwa dhuluma na udanganyifu.”
and to reckon: punish upon all [the] to leap upon [the] threshold in/on/with day [the] he/she/it [the] to fill house: home lord their violence and deceit
10 Bwana asema, “Katika siku hiyo kilio kitapanda juu kutoka lango la Samaki, maombolezo kutoka mtaa wa pili, na mshindo mkubwa kutoka vilimani.
and to be in/on/with day [the] he/she/it utterance LORD voice cry from gate [the] Fish (Gate) and wailing from [the] Second [Quarter] and breaking great: large from [the] hill
11 Ombolezeni, ninyi mnaoishi katika eneo la sokoni; wafanyabiashara wenu wote wameangamizwa, wote ambao wanafanya biashara ya fedha wataangamizwa.
to wail to dwell [the] Mortar for to cease all people merchant to cut: eliminate all laden silver: money
12 Wakati huo nitasaka mji wa Yerusalemu kwa taa, na kuwaadhibu wale ambao wanakaa katika hali ya kuridhika, ambao ni kama divai iliyobaki kwenye machicha, ambao hudhani, ‘Bwana hatafanya lolote, jema au baya.’
and to be in/on/with time [the] he/she/it to search [obj] Jerusalem in/on/with lamp and to reckon: punish upon [the] human [the] to congeal upon dreg their [the] to say in/on/with heart their not be good LORD and not be evil
13 Utajiri wao utatekwa nyara, nyumba zao zitabomolewa. Watajenga nyumba, lakini hawataishi ndani yake; watapanda mizabibu lakini hawatakunywa divai yake.
and to be strength: rich their to/for plunder and house: home their to/for devastation and to build house: home and not to dwell and to plant vineyard and not to drink [obj] wine their
14 “Siku kubwa ya Bwana iko karibu: iko karibu na inakuja haraka. Sikilizeni! Kilio katika siku ya Bwana kitakuwa kichungu, hata shujaa atapiga kelele.
near day LORD [the] great: large near and quick much voice: sound day LORD bitter to cry there mighty man
15 Siku ile ni siku ya ghadhabu, siku ya fadhaa na dhiki, siku ya uharibifu na ukiwa, siku ya giza na utusitusi, siku ya mawingu na giza nene,
day fury [the] day [the] he/she/it day distress and distress day devastation and desolation day darkness and darkness day cloud and cloud
16 siku ya tarumbeta na mlio wa vita dhidi ya miji yenye ngome na dhidi ya minara mirefu.
day trumpet and shout upon [the] city [the] to gather/restrain/fortify and upon [the] corner [the] high
17 Nitawaletea watu dhiki, nao watatembea kama vipofu, kwa sababu wametenda dhambi dhidi ya Bwana. Damu yao itamwagwa kama vumbi na matumbo yao kama taka.
and to constrain to/for man and to go: walk like/as blind for to/for LORD to sin and to pour: pour blood their like/as dust and intestine their like/as dung
18 Fedha yao wala dhahabu yao hazitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya ghadhabu ya Bwana. Katika moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa, kwa maana ataleta mwisho wa wote wanaoishi katika dunia ghafula.”
also silver: money their also gold their not be able to/for to rescue them in/on/with day fury LORD and in/on/with fire jealousy his to eat all [the] land: country/planet for consumption surely to dismay to make with all to dwell [the] land: country/planet

< Sefania 1 >