< Sefania 1 >

1 Neno la Bwana lililomjia Sefania mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amaria, mwana wa Hezekia, wakati wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda:
The word of Jehovah, which came to Zephaniah, the son of Cushi, the son of Gedaliah, the son of Amariah, the son of Hizkiah, in the days of Josiah, the son of Amon, king of Judah.
2 Bwana asema, “Nitafagia kila kitu kutoka kwenye uso wa dunia.”
I will utterly consume all things from the face of the land, saith Jehovah;
3 “Nitafagilia mbali watu na wanyama; nitafagilia mbali ndege wa angani na samaki wa baharini. Wafanyao maovu watapata tu kokoto, nami nitamkatilia mbali mwanadamu atoke katika dunia,” asema Bwana.
I will consume man and beast; I will consume the birds of heaven, and the fishes of the sea, And the stumbling-blocks with the wicked; And I will cut off man from the face of the land, saith Jehovah.
4 “Nitaiadhibu Yuda na wote wakaao Yerusalemu. Kutoka mahali hapa nitakatilia mbali kila mabaki ya Baali, majina ya wapagani na makuhani waabuduo sanamu:
I will stretch out my hand over Judah, And over all the inhabitants of Jerusalem, And I will cut off from this place the residue of Baal, The name of the idol-sacrificers with the priests,
5 wale ambao husujudu juu ya mapaa kuabudu jeshi la vitu vya angani, wale ambao husujudu na kuapa kwa Bwana na ambao pia huapa kwa Malkamu,
And those who bow themselves on the house-tops to the host of heaven, And those who bow themselves and swear by Jehovah, And also swear by their idol,
6 wale wanaoacha kumfuata Bwana, wala hawamtafuti Bwana wala kutaka shauri lake.
And those that turn back from Jehovah, And those that seek not Jehovah, nor inquire for him.
7 Nyamazeni mbele za Bwana Mwenyezi, kwa maana siku ya Bwana iko karibu. Bwana ameandaa dhabihu, amewaweka wakfu wale aliowaalika.
Be silent before the Lord Jehovah! For the day of Jehovah is near; For Jehovah hath prepared a sacrifice; He hath appointed his guests.
8 Katika siku ya dhabihu ya Bwana nitawaadhibu wakuu na wana wa mfalme na wale wote wanaovaa nguo za kigeni.
And in the day of the sacrifice of Jehovah it shall come to pass That I will punish the princes and the sons of the king, And all that are clothed with foreign apparel.
9 Katika siku hiyo nitaadhibu wote ambao hukwepa kukanyaga kizingiti, ambao hujaza hekalu la miungu yao kwa dhuluma na udanganyifu.”
In that day also will I punish all that leap over the threshold, That fill the houses of their master with violence and deceit.
10 Bwana asema, “Katika siku hiyo kilio kitapanda juu kutoka lango la Samaki, maombolezo kutoka mtaa wa pili, na mshindo mkubwa kutoka vilimani.
And it shall come to pass in that day, saith Jehovah, That there shall be the noise of a cry from the fish-gate, And of a howling from the other part of the city, And of great destruction from the hills.
11 Ombolezeni, ninyi mnaoishi katika eneo la sokoni; wafanyabiashara wenu wote wameangamizwa, wote ambao wanafanya biashara ya fedha wataangamizwa.
Howl, ye inhabitants of Maktesh! For all the trafficking people are cut down; All they that bear silver are destroyed.
12 Wakati huo nitasaka mji wa Yerusalemu kwa taa, na kuwaadhibu wale ambao wanakaa katika hali ya kuridhika, ambao ni kama divai iliyobaki kwenye machicha, ambao hudhani, ‘Bwana hatafanya lolote, jema au baya.’
And it shall come to pass at that time, That I will search Jerusalem with lamps, And I will punish the men that are settled on their lees; That say in their hearts, “Jehovah doeth neither good nor evil.”
13 Utajiri wao utatekwa nyara, nyumba zao zitabomolewa. Watajenga nyumba, lakini hawataishi ndani yake; watapanda mizabibu lakini hawatakunywa divai yake.
Their substance shall become a spoil, And their houses a desolation; They shall also build houses, but not inhabit them; And shall plant vineyards, but not drink the wine thereof.
14 “Siku kubwa ya Bwana iko karibu: iko karibu na inakuja haraka. Sikilizeni! Kilio katika siku ya Bwana kitakuwa kichungu, hata shujaa atapiga kelele.
The day of Jehovah is near, the great day; It is near, and hasteth greatly; The day of Jehovah shall resound; Bitterly shall the mighty man cry for help.
15 Siku ile ni siku ya ghadhabu, siku ya fadhaa na dhiki, siku ya uharibifu na ukiwa, siku ya giza na utusitusi, siku ya mawingu na giza nene,
That day is a day of wrath, A day of distress and anguish, A day of destruction and desolation, A day of darkness and gloominess, A day of clouds and thick darkness,
16 siku ya tarumbeta na mlio wa vita dhidi ya miji yenye ngome na dhidi ya minara mirefu.
A day of the trumpet and the war-shout, Against the fenced cities, And against the high towers.
17 Nitawaletea watu dhiki, nao watatembea kama vipofu, kwa sababu wametenda dhambi dhidi ya Bwana. Damu yao itamwagwa kama vumbi na matumbo yao kama taka.
And I will distress the men, so that they shall walk like the blind, Because they have sinned against Jehovah. And their blood shall be poured out as dust, And their flesh as dung.
18 Fedha yao wala dhahabu yao hazitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya ghadhabu ya Bwana. Katika moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa, kwa maana ataleta mwisho wa wote wanaoishi katika dunia ghafula.”
Neither their silver nor their gold shall be able to deliver them in the day of the wrath of Jehovah, But by the fire of his indignation shall the whole land be devoured; For destruction, and that a speedy one, will he bring Upon all that dwell in the land.

< Sefania 1 >