< Sefania 2 >
1 Kusanyikeni pamoja, kusanyikeni pamoja, enyi taifa lisilo na aibu,
Congregae-vos, sim, congregae-vos, ó nação que não tem desejo,
2 kabla ya wakati ulioamriwa haujafika na siku ile inayopeperusha kama makapi, kabla hasira kali ya Bwana haijaja juu yenu, kabla siku ya ghadhabu ya Bwana haijaja juu yenu.
Antes que o decreto produza o seu effeito, antes que o dia passe como a pragana, antes que venha sobre vós a ira do Senhor, antes que venha sobre vós o dia da ira do Senhor.
3 Mtafuteni Bwana, enyi nyote wanyenyekevu wa nchi, ninyi ambao hufanya lile analoamuru. Tafuteni haki, tafuteni unyenyekevu; labda mtahifadhiwa siku ya hasira ya Bwana.
Buscae ao Senhor, vós todos os mansos da terra, que pondes em obra o seu juizo: buscae a justiça, buscae a mansidão; porventura sereis escondidos no dia da ira do Senhor.
4 Gaza utaachwa na Ashkeloni utaachwa magofu. Wakati wa adhuhuri Ashdodi utaachwa mtupu na Ekroni utangʼolewa.
Porque Gaza será desamparada, e Ascalon será assolada: Asdod ao meio dia será expellida, e Ekron será desarreigada.
5 Ole wenu ninyi ambao mnaishi kando ya bahari, enyi Wakerethi; neno la Bwana liko dhidi yenu, ee Kanaani, nchi ya Wafilisti. “Mimi nitawaangamiza, na hakuna atakayebaki.”
Ai dos habitantes da borda do mar, do povo dos chereteos! a palavra do Senhor será contra vós, ó Canaan, terra dos philisteos, e eu vos farei destruir, até que não haja morador.
6 Nchi kando ya bahari, mahali ambapo wanaishi Wakerethi, patakuwa mahali pa wachungaji na mazizi ya kondoo.
E a borda do mar será por cabanas, que cavam os pastores, e curraes dos rebanhos.
7 Itakuwa mali ya mabaki ya nyumba ya Yuda, hapo watapata malisho. Wakati wa jioni watajilaza chini katika nyumba za Ashkeloni. Bwana Mungu wao atawatunza, naye atawarudishia wafungwa wao.
E será a borda para o resto da casa de Judah, que n'ella apascentem: á tarde se assentarão nas casas de Ascalon, porque o Senhor seu Deus os visitará, e lhes tornará o seu captiveiro.
8 “Nimeyasikia matukano ya Moabu nazo dhihaka za Waamoni, ambao waliwatukana watu wangu na kutoa vitisho dhidi ya nchi yao.
Eu ouvi o escarneo de Moab, e as injuriosas palavras dos filhos de Ammon, com que escarneceram do meu povo, e se engrandeceram contra o seu termo.
9 Hakika, kama niishivyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, “hakika Moabu itakuwa kama Sodoma, Waamoni kama Gomora: mahali pa magugu na mashimo ya chumvi, nchi ya ukiwa milele. Mabaki ya watu wangu watawateka nyara; mabaki ya taifa langu watarithi nchi yao.”
Portanto, vivo eu, diz o Senhor dos Exercitos, o Deus de Israel, certamente Moab será como Sodoma, e os filhos de Ammon como Gomorrah, campo de ortigas e poços de sal, e assolação perpetua; o resto do meu povo os saqueará, e o restante do meu povo os possuirá.
10 Hiki ndicho watarudishiwa kwa ajili ya kiburi chao, kwa kutukana na kudhihaki watu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Isto terão em recompensa da sua soberba, porque escarneceram, e se engrandeceram contra o povo do Senhor dos Exercitos.
11 Bwana atakuwa wa kuhofisha kwao atakapoangamiza miungu yote ya nchi. Mataifa katika kila pwani yatamwabudu, kila moja katika nchi yake.
O Senhor será terrivel contra elles, porque emmagrecerá a todos os deuses da terra; e cada um se inclinará a elle desde o seu logar; todas as ilhas das nações.
12 “Ninyi pia, ee Wakushi, mtauawa kwa upanga wangu.”
Tambem vós, ó ethiopes, sereis mortos com a minha espada.
13 Mungu atanyoosha mkono wake dhidi ya kaskazini na kuangamiza Waashuru, akiiacha Ninawi ukiwa na pakame kama jangwa.
Estenderá tambem a sua mão contra o norte, e destruirá a Assyria; e fará de Ninive uma assolação, terra secca como o deserto.
14 Makundi ya kondoo na ngʼombe yatajilaza pale, viumbe vya kila aina. Bundi wa jangwani na bundi waliao kwa sauti nyembamba wataishi juu ya nguzo zake. Mwangwi wa kuita kwao utapita madirishani, kifusi kitakuwa milangoni, boriti za mierezi zitaachwa wazi.
E no meio d'ella repousarão os rebanhos, todos os animaes dos povos; e alojar-se-hão nos seus capiteis assim o pelicano como o ouriço: a voz do seu canto retinirá nas janellas, a assolação estará no umbral, quando tiver descoberto a sua obra de cedro.
15 Huu ndio mji uliotukuka na kuishi kwa furaha wakijisikia salama. Ulisema moyoni mwako, “Mimi ndimi, na wala hapana mwingine ila mimi.” Jinsi gani umekuwa gofu, mahali pa kulala wanyama pori! Wote wanaopita kando yake wanauzomea na kutikisa mkono kwa dharau.
Esta é a cidade que salta de alegria, que habita segura, que diz no seu coração: Eu sou, e não ha mais do que eu: como se tornou em assolação em pousada de animaes! qualquer que passar por ella assobiará, e meneará a sua mão