< Sefania 2 >

1 Kusanyikeni pamoja, kusanyikeni pamoja, enyi taifa lisilo na aibu,
Recueillez-vous, rentrez en vous-mêmes, race sans pudeur,
2 kabla ya wakati ulioamriwa haujafika na siku ile inayopeperusha kama makapi, kabla hasira kali ya Bwana haijaja juu yenu, kabla siku ya ghadhabu ya Bwana haijaja juu yenu.
avant que le décret ait enfanté, que le jour ait passé comme la paille; avant que vienne sur vous l’ardeur de la colère de Yahweh, avant que vienne sur vous le jour de la colère de Yahweh.
3 Mtafuteni Bwana, enyi nyote wanyenyekevu wa nchi, ninyi ambao hufanya lile analoamuru. Tafuteni haki, tafuteni unyenyekevu; labda mtahifadhiwa siku ya hasira ya Bwana.
Cherchez Yahweh, vous tous humbles du pays, qui avez pratiqué sa loi; recherchez la justice, recherchez l’humilité. Peut-être serez-vous à l’abri au jour de la colère de Yahweh!…
4 Gaza utaachwa na Ashkeloni utaachwa magofu. Wakati wa adhuhuri Ashdodi utaachwa mtupu na Ekroni utangʼolewa.
Car Gaza sera abandonnée, et Ascalon réduite en désert; on chassera Azot en plein midi, et Accaron sera déracinée.
5 Ole wenu ninyi ambao mnaishi kando ya bahari, enyi Wakerethi; neno la Bwana liko dhidi yenu, ee Kanaani, nchi ya Wafilisti. “Mimi nitawaangamiza, na hakuna atakayebaki.”
Malheur aux habitants de la région de la mer, à la nation des Crétois! La parole de Yahweh est prononcée contre vous, Chanaan, terre des Philistins: « Et je te détruirai en sorte qu’il ne te reste plus d’habitants. »
6 Nchi kando ya bahari, mahali ambapo wanaishi Wakerethi, patakuwa mahali pa wachungaji na mazizi ya kondoo.
La région de la mer deviendra des pâturages, des grottes de bergers et des parcs de moutons.
7 Itakuwa mali ya mabaki ya nyumba ya Yuda, hapo watapata malisho. Wakati wa jioni watajilaza chini katika nyumba za Ashkeloni. Bwana Mungu wao atawatunza, naye atawarudishia wafungwa wao.
Ce sera un territoire pour le reste de la maison de Juda, ils y paîtront leurs troupeaux; le soir, ils prendront leur gîte dans les maisons d’Ascalon, car Yahweh, leur Dieu, les visitera et les rétablira.
8 “Nimeyasikia matukano ya Moabu nazo dhihaka za Waamoni, ambao waliwatukana watu wangu na kutoa vitisho dhidi ya nchi yao.
J’ai entendu les insultes de Moab, et les outrages des fils d’Ammon, qui insultaient mon peuple, et s’agrandissaient aux dépens de ses frontières.
9 Hakika, kama niishivyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, “hakika Moabu itakuwa kama Sodoma, Waamoni kama Gomora: mahali pa magugu na mashimo ya chumvi, nchi ya ukiwa milele. Mabaki ya watu wangu watawateka nyara; mabaki ya taifa langu watarithi nchi yao.”
C’est pourquoi, je suis vivant, — oracle de Yahweh des armées, le Dieu d’Israël: Moab sera comme Sodome, et les fils d’Ammon comme Gomorrhe: un lieu livré aux orties, une carrière de sel, un désert à jamais. Le reste de mon peuple le pillera, et ce qui demeurera de ma nation, les aura en héritage.
10 Hiki ndicho watarudishiwa kwa ajili ya kiburi chao, kwa kutukana na kudhihaki watu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Cela leur arrivera pour leur orgueil, parce qu’ils ont été méprisants et insolents, contre le peuple de Yahweh des armées.
11 Bwana atakuwa wa kuhofisha kwao atakapoangamiza miungu yote ya nchi. Mataifa katika kila pwani yatamwabudu, kila moja katika nchi yake.
Yahweh sera un objet de terreur pour eux, car il anéantira tous les dieux de la terre; et devant lui se prosterneront, chacun de son lieu, les habitants de toutes les îles des nations.
12 “Ninyi pia, ee Wakushi, mtauawa kwa upanga wangu.”
Vous aussi, Éthiopiens!… Ils seront transpercés par mon épée.
13 Mungu atanyoosha mkono wake dhidi ya kaskazini na kuangamiza Waashuru, akiiacha Ninawi ukiwa na pakame kama jangwa.
Il étendra aussi sa main contre le nord, il détruira Assur, et il fera de Ninive une solitude, aride comme le désert.
14 Makundi ya kondoo na ngʼombe yatajilaza pale, viumbe vya kila aina. Bundi wa jangwani na bundi waliao kwa sauti nyembamba wataishi juu ya nguzo zake. Mwangwi wa kuita kwao utapita madirishani, kifusi kitakuwa milangoni, boriti za mierezi zitaachwa wazi.
Au milieu d’elle prendront leur gîte des troupeaux, des animaux de toute espèce; même le pélican, même le hérisson se logeront sur ses chapiteaux; on entendra des chants dans les fenêtres, la désolation sera sur le seuil, car on a mis à nu les boiseries de cèdres.
15 Huu ndio mji uliotukuka na kuishi kwa furaha wakijisikia salama. Ulisema moyoni mwako, “Mimi ndimi, na wala hapana mwingine ila mimi.” Jinsi gani umekuwa gofu, mahali pa kulala wanyama pori! Wote wanaopita kando yake wanauzomea na kutikisa mkono kwa dharau.
C’est là la ville joyeuse, assise avec assurance, qui disait en son cœur: « Moi, et rien que moi! » Comment est-elle devenue un désert, une demeure pour les bêtes? Quiconque passera sur elle sifflera et agitera la main.

< Sefania 2 >