< Sefania 2 >
1 Kusanyikeni pamoja, kusanyikeni pamoja, enyi taifa lisilo na aibu,
Be ashamed within yourselves, be ashamed,
2 kabla ya wakati ulioamriwa haujafika na siku ile inayopeperusha kama makapi, kabla hasira kali ya Bwana haijaja juu yenu, kabla siku ya ghadhabu ya Bwana haijaja juu yenu.
before you become as the drifting chaff, before the anger of the Lord comes upon you, before the day of the Lord’s wrath comes upon you.
3 Mtafuteni Bwana, enyi nyote wanyenyekevu wa nchi, ninyi ambao hufanya lile analoamuru. Tafuteni haki, tafuteni unyenyekevu; labda mtahifadhiwa siku ya hasira ya Bwana.
Seek the Lord all you meek of the earth, you who obey his law; Seek righteousness, seek meekness; perhaps you may be hidden in the day of the Lord’s wrath.
4 Gaza utaachwa na Ashkeloni utaachwa magofu. Wakati wa adhuhuri Ashdodi utaachwa mtupu na Ekroni utangʼolewa.
For Gaza will be forsaken; Ashkelon a desolation; Ashdod – by noon will they rout her and Ekron be torn up!
5 Ole wenu ninyi ambao mnaishi kando ya bahari, enyi Wakerethi; neno la Bwana liko dhidi yenu, ee Kanaani, nchi ya Wafilisti. “Mimi nitawaangamiza, na hakuna atakayebaki.”
Woe to those who live by the sea coast, people of the Cherethites! The word of the Lord is against you, Canaan, land of the Philistines! I will destroy you so that you will be without inhabitants,
6 Nchi kando ya bahari, mahali ambapo wanaishi Wakerethi, patakuwa mahali pa wachungaji na mazizi ya kondoo.
and you will become shepherds’ cots and folds for flocks.
7 Itakuwa mali ya mabaki ya nyumba ya Yuda, hapo watapata malisho. Wakati wa jioni watajilaza chini katika nyumba za Ashkeloni. Bwana Mungu wao atawatunza, naye atawarudishia wafungwa wao.
The sea coast will belong to the survivors of the house of Judah. They will pasture their flocks there. In the house of Ashkelon they will lie down at evening. The Lord their God will be with them and restore their fortunes.
8 “Nimeyasikia matukano ya Moabu nazo dhihaka za Waamoni, ambao waliwatukana watu wangu na kutoa vitisho dhidi ya nchi yao.
I have heard the taunts of Moab, and the revilings of the Ammonites, how they have taunted my people, and spoken boastfully concerning their border.
9 Hakika, kama niishivyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, “hakika Moabu itakuwa kama Sodoma, Waamoni kama Gomora: mahali pa magugu na mashimo ya chumvi, nchi ya ukiwa milele. Mabaki ya watu wangu watawateka nyara; mabaki ya taifa langu watarithi nchi yao.”
Therefore as I live, says the Lord of hosts, the God of Israel: Moab will be like Sodom, and the Ammonites like Gomorrah, a pile of nettles and saltpits, and a desolation, forever. The residue of my people will plunder them, and the survivors of my nation will inherit them.
10 Hiki ndicho watarudishiwa kwa ajili ya kiburi chao, kwa kutukana na kudhihaki watu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote.
This will they have for their pride, because they have taunted and spoken boastfully against the people of the Lord of hosts.
11 Bwana atakuwa wa kuhofisha kwao atakapoangamiza miungu yote ya nchi. Mataifa katika kila pwani yatamwabudu, kila moja katika nchi yake.
The Lord will terrify them; he will reduce all the gods of the earth; then all the peoples of the nations will worship him, each in their own land.
12 “Ninyi pia, ee Wakushi, mtauawa kwa upanga wangu.”
You, also, Ethiopians, slain by his sword are you!
13 Mungu atanyoosha mkono wake dhidi ya kaskazini na kuangamiza Waashuru, akiiacha Ninawi ukiwa na pakame kama jangwa.
And he will stretch out his hand against the north and destroy Assyria; And he will make Nineveh a desolation, dry as the wilderness.
14 Makundi ya kondoo na ngʼombe yatajilaza pale, viumbe vya kila aina. Bundi wa jangwani na bundi waliao kwa sauti nyembamba wataishi juu ya nguzo zake. Mwangwi wa kuita kwao utapita madirishani, kifusi kitakuwa milangoni, boriti za mierezi zitaachwa wazi.
Herds will lie down in it, every beast of the earth, Desert owl and screech owl will lodge in its capitals. The owl will hoot in the window, the raven on the doorstep, all stripped bare of cedar.
15 Huu ndio mji uliotukuka na kuishi kwa furaha wakijisikia salama. Ulisema moyoni mwako, “Mimi ndimi, na wala hapana mwingine ila mimi.” Jinsi gani umekuwa gofu, mahali pa kulala wanyama pori! Wote wanaopita kando yake wanauzomea na kutikisa mkono kwa dharau.
This is the exultant city which sat secure. The city who said to herself, I am and there is none else! How has she become a desolation! A lair of beasts! Every passerby hisses at her, shakes their hand.