< Sefania 2 >

1 Kusanyikeni pamoja, kusanyikeni pamoja, enyi taifa lisilo na aibu,
Gather yourselves together, yea, gather together, O shameless nation;
2 kabla ya wakati ulioamriwa haujafika na siku ile inayopeperusha kama makapi, kabla hasira kali ya Bwana haijaja juu yenu, kabla siku ya ghadhabu ya Bwana haijaja juu yenu.
Before the decree bring forth the day when one passeth as the chaff, before the fierce anger of the LORD come upon you, before the day of the LORD'S anger come upon you.
3 Mtafuteni Bwana, enyi nyote wanyenyekevu wa nchi, ninyi ambao hufanya lile analoamuru. Tafuteni haki, tafuteni unyenyekevu; labda mtahifadhiwa siku ya hasira ya Bwana.
Seek ye the LORD, all ye humble of the earth, that have executed His ordinance; seek righteousness, seek humility. It may be ye shall be hid in the day of the LORD'S anger.
4 Gaza utaachwa na Ashkeloni utaachwa magofu. Wakati wa adhuhuri Ashdodi utaachwa mtupu na Ekroni utangʼolewa.
For Gaza shall be forsaken, and Ashkelon a desolation; they shall drive out Ashdod at the noonday, and Ekron shall be rooted up.
5 Ole wenu ninyi ambao mnaishi kando ya bahari, enyi Wakerethi; neno la Bwana liko dhidi yenu, ee Kanaani, nchi ya Wafilisti. “Mimi nitawaangamiza, na hakuna atakayebaki.”
Woe unto the inhabitants of the sea-coast, the nation of the Cherethites! the word of the LORD is against you, O Canaan, the land of the Philistines; I will even destroy thee, that there shall be no inhabitant.
6 Nchi kando ya bahari, mahali ambapo wanaishi Wakerethi, patakuwa mahali pa wachungaji na mazizi ya kondoo.
And the sea-coast shall be pastures, even meadows for shepherds, and folds for flocks.
7 Itakuwa mali ya mabaki ya nyumba ya Yuda, hapo watapata malisho. Wakati wa jioni watajilaza chini katika nyumba za Ashkeloni. Bwana Mungu wao atawatunza, naye atawarudishia wafungwa wao.
And it shall be a portion for the remnant of the house of Judah, whereon they shall feed; in the houses of Ashkelon shall they lie down in the evening; for the LORD their God will remember them, and turn their captivity.
8 “Nimeyasikia matukano ya Moabu nazo dhihaka za Waamoni, ambao waliwatukana watu wangu na kutoa vitisho dhidi ya nchi yao.
I have heard the taunt of Moab, and the revilings of the children of Ammon, wherewith they have taunted My people, and spoken boastfully concerning their border.
9 Hakika, kama niishivyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, “hakika Moabu itakuwa kama Sodoma, Waamoni kama Gomora: mahali pa magugu na mashimo ya chumvi, nchi ya ukiwa milele. Mabaki ya watu wangu watawateka nyara; mabaki ya taifa langu watarithi nchi yao.”
Therefore as I live, saith the LORD of hosts, the God of Israel: Surely Moab shall be as Sodom, and the children of Ammon as Gomorrah, even the breeding-place of nettles, and saltpits, and a desolation, for ever; the residue of My people shall spoil them, and the remnant of My nation shall inherit them.
10 Hiki ndicho watarudishiwa kwa ajili ya kiburi chao, kwa kutukana na kudhihaki watu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote.
This shall they have for their pride, because they have taunted and spoken boastfully against the people of the LORD of hosts.
11 Bwana atakuwa wa kuhofisha kwao atakapoangamiza miungu yote ya nchi. Mataifa katika kila pwani yatamwabudu, kila moja katika nchi yake.
The LORD will be terrible unto them; for He will famish all the gods of the earth; then shall all the isles of the nations worship Him, every one from its place.
12 “Ninyi pia, ee Wakushi, mtauawa kwa upanga wangu.”
Ye Ethiopians also, ye shall be slain by My sword.
13 Mungu atanyoosha mkono wake dhidi ya kaskazini na kuangamiza Waashuru, akiiacha Ninawi ukiwa na pakame kama jangwa.
And He will stretch out His hand against the north, and destroy Assyria; and will make Nineveh a desolation, and dry like the wilderness.
14 Makundi ya kondoo na ngʼombe yatajilaza pale, viumbe vya kila aina. Bundi wa jangwani na bundi waliao kwa sauti nyembamba wataishi juu ya nguzo zake. Mwangwi wa kuita kwao utapita madirishani, kifusi kitakuwa milangoni, boriti za mierezi zitaachwa wazi.
And all beasts of every kind shall lie down in the midst of her in herds; both the pelican and the bittern shall lodge in the capitals thereof; voices shall sing in the windows; desolation shall be in the posts; for the cedar-work thereof shall be uncovered.
15 Huu ndio mji uliotukuka na kuishi kwa furaha wakijisikia salama. Ulisema moyoni mwako, “Mimi ndimi, na wala hapana mwingine ila mimi.” Jinsi gani umekuwa gofu, mahali pa kulala wanyama pori! Wote wanaopita kando yake wanauzomea na kutikisa mkono kwa dharau.
This is the joyous city that dwelt without care, that said in her heart: 'I am, and there is none else beside me'; how is she become a desolation, a place for beasts to lie down in! Every one that passeth by her shall hiss, and wag his hand.

< Sefania 2 >