< Sefania 2 >
1 Kusanyikeni pamoja, kusanyikeni pamoja, enyi taifa lisilo na aibu,
Saml jer, saml jer, I Folk, som ej kender Skam,
2 kabla ya wakati ulioamriwa haujafika na siku ile inayopeperusha kama makapi, kabla hasira kali ya Bwana haijaja juu yenu, kabla siku ya ghadhabu ya Bwana haijaja juu yenu.
før I endnu er blevet som flyvende Avner, før HERRENS glødende Harme kommer over eder, før HERRENS Vredes Dag kommer over eder.
3 Mtafuteni Bwana, enyi nyote wanyenyekevu wa nchi, ninyi ambao hufanya lile analoamuru. Tafuteni haki, tafuteni unyenyekevu; labda mtahifadhiwa siku ya hasira ya Bwana.
Søg HERREN, alle I ydmyge i Landet, som holder hans Bud, søg Retfærd, søg Ydmyghed! Maaske kan I skjule jer paa HERRENS Vredes Dag.
4 Gaza utaachwa na Ashkeloni utaachwa magofu. Wakati wa adhuhuri Ashdodi utaachwa mtupu na Ekroni utangʼolewa.
Thi Gaza skal ligge forladt og Askalon øde, Asdod drives bort ved Middag, Ekron udryddes.
5 Ole wenu ninyi ambao mnaishi kando ya bahari, enyi Wakerethi; neno la Bwana liko dhidi yenu, ee Kanaani, nchi ya Wafilisti. “Mimi nitawaangamiza, na hakuna atakayebaki.”
Ve dem, som bor ved Stranden, Kreternes Folk; HERRENS Ord over dig, Kana'an, Filisternes Land! Jeg gør dig til intet, saa ingen bor der.
6 Nchi kando ya bahari, mahali ambapo wanaishi Wakerethi, patakuwa mahali pa wachungaji na mazizi ya kondoo.
Du skal blive til Græsmark for Hyrder, til Folde for Smaakvæg.
7 Itakuwa mali ya mabaki ya nyumba ya Yuda, hapo watapata malisho. Wakati wa jioni watajilaza chini katika nyumba za Ashkeloni. Bwana Mungu wao atawatunza, naye atawarudishia wafungwa wao.
Og Stranden skal tilfalde Resten af Judas Hus; de skal græsse derpaa. Lejr skal de slaa ved Kvæld i Askalons Huse. Thi HERREN deres Gud ser til dem og vender deres Skæbne.
8 “Nimeyasikia matukano ya Moabu nazo dhihaka za Waamoni, ambao waliwatukana watu wangu na kutoa vitisho dhidi ya nchi yao.
Jeg hørte Moabs Spot, Ammoniternes haanende Ord, med hvilke de spotted mit Folk, hovmoded sig over deres Land.
9 Hakika, kama niishivyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, “hakika Moabu itakuwa kama Sodoma, Waamoni kama Gomora: mahali pa magugu na mashimo ya chumvi, nchi ya ukiwa milele. Mabaki ya watu wangu watawateka nyara; mabaki ya taifa langu watarithi nchi yao.”
Derfor, saa sandt jeg lever, lyder det fra Hærskarers HERRE, Israels Gud: Moab skal blive som Sodoma, Ammoniterne som Gomorra, Jord for Nælder, et Salthul, Ørken til evig Tid. Resten af mit Folk skal plyndre dem; hvad der levnes af mit Folk skal eje dem.
10 Hiki ndicho watarudishiwa kwa ajili ya kiburi chao, kwa kutukana na kudhihaki watu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Dette skal times dem for deres Hovmod, fordi de haanede Hærskarers HERRES Folk og gjorde sig store over for det.
11 Bwana atakuwa wa kuhofisha kwao atakapoangamiza miungu yote ya nchi. Mataifa katika kila pwani yatamwabudu, kila moja katika nchi yake.
Frygtelig er HERREN for dem; thi han udrydder alle Jordens Guder, og alle Hedningernes fjerne Strande skal tilbede ham, hver paa sit Sted.
12 “Ninyi pia, ee Wakushi, mtauawa kwa upanga wangu.”
Ogsaa I Ætiopere skal falde for HERRENS Sværd,
13 Mungu atanyoosha mkono wake dhidi ya kaskazini na kuangamiza Waashuru, akiiacha Ninawi ukiwa na pakame kama jangwa.
og han udrækker Haanden mod Nord og tilintetgør Assur, Nineve gør han til Ødemark, tørt som en Ørk;
14 Makundi ya kondoo na ngʼombe yatajilaza pale, viumbe vya kila aina. Bundi wa jangwani na bundi waliao kwa sauti nyembamba wataishi juu ya nguzo zake. Mwangwi wa kuita kwao utapita madirishani, kifusi kitakuwa milangoni, boriti za mierezi zitaachwa wazi.
Hjorde skal lejre sig deri, hvert Slettens Dyr; paa dets Søjlehoveder sover Pelikan og Rørdrum, i Vinduet skriger Uglen, Ravnen paa Tærsklen.
15 Huu ndio mji uliotukuka na kuishi kwa furaha wakijisikia salama. Ulisema moyoni mwako, “Mimi ndimi, na wala hapana mwingine ila mimi.” Jinsi gani umekuwa gofu, mahali pa kulala wanyama pori! Wote wanaopita kando yake wanauzomea na kutikisa mkono kwa dharau.
Det er den jublende By, som laa saa trygt, som sagde i sit Hjerte: »Jeg og ellers ingen.« Hvor er den dog blevet øde, et Raststed for Dyr! Enhver, som kommer forbi den, haaner med Fløjt og Haand.